*MANARA BLAA BLAA SITAKI KUSIKIA*
Kupitia Magic FM *Manara* aongea dhahabu....
1. Kuna taarifa zimesambaa mie naziita *black propaganda* ujue Hawa jamaa sijui wana nini wanapenda sana kuzusha vitu Mara ndanda wakate rufaa Mara wachezaj simba hawana vibali na Leo wanasema ya polisi dar.
2. Ni kawaida Yangu kutojibu blaablaa za mtandaoni. Ujue Yanga Hawa wanaangaika sana kazi yao *kuangaika angaika tu hawatulii sijajua nini kinawasumbua* watuache tu.
3. Umesikia sasa kabla ya hyo unayosema haijatokea asubuh walianza kusema " Ooonh simba wachezaji hawajapewa mishahara miezi miwili, sasa baada ya Mkude kuja kukanusha hizo taarifa basi wakaja na hilo la Lufunga.
4. Nawaambia hivi Yanga wasijfche nyuma waende tu TFF wakate wao Rufaa maana wanaumia kweli wajifanye tu Polisi Dar.
5. Niwaambie tu wanasimba wasiwe na wasiwasi simba inaenda hatua inayofuata na tupo fiti kuwavaa Azam fc.
6. Nakuuliza wew uwanja wa Jamhuri na uwanja wa Songea Majimaji una tofauti gani? Nijibu sasa mbona unatetemeka.
7. Kesho tunaandika barua na kuipeleka bodi ya Ligi kukataa kucheza kwenye uwanja wa songea kwa maana kuwa uwanja wa Jamhuri na uwanja wa Songea hakuna tofauti yeyote kama wamefunga kule wafunge na Songea.
8. Tusifanyane wajinga kwanini uwanja wa Jamhuri hawakuufunga kabla ya mechi yetu na Mtibwa ila wameona wanaenda kucheza Yanga ndio wanaufungia. Unagundua nini hapo???
9. Nasisitiza kwamba tunaandika barua na sisi hatuchezi uwanja wa Majimaji hata iweje.
10. Simba tupo vizuri kila idara na tumejipanga kwa hali madhubuti wala hatuyumbishwi na *Black propaganda*
Hongera msemaji makini..
Source Magic FM
*By Omary Dihile Jr*