.

.

Saturday, 20 June 2015

nabiielia 

Nabii Eliya

Wapendwa Shalom,

Ninaorodhesha machache ninayoyafahamu kuhusu Pool of Siloam Church ambalo lilianza mwaka 2003. (kwa maoni yangu walianza vizuri hadi ilipofika mwaka 2008 – ndipo U-Turn ilipotokea). Pia unaweza kusoma juu ya wanachokiamini kuhusiana na MWENENDO WA KANISA kwenye link hii; http://www.siloamgoshen.org/

MAMBO MACHACHE YA KANISA LA KIZAZI CHA NNE HAYA HAPA

1.   Pool of Siloam ilianzishwa rasmi 2003, na Mtumishi N. Munuo

2.   Mafunuo ya Nabii Eliya yanatambulika kuwa ni sahihi hutakiwi kuyahoji wala kuyaoanisha na Maandiko Matakatifu unapaswa kuyatii. Mojawapo ya ufunuo /maelezo ya ajabu ni hili Shetani aliuwawa na Nabii Eliya Novemba 2008. Hapa ndipo kwenye vile vitisho ya kuwa bubu, tasa kufa n.k.

3.   Imani yao imejengwa na kuongozwa katika ufunuo wa majira na nyakati na jambo hili ni muhimu sana. Hivi sasa wapo katika kizazi cha nne. Kizazi cha kwanza Adamu mpaka gharika, kizazi cha pili Nuhu hadi Yesu, kizazi cha tatu kutoka Yesu hadi Februari 2012. Kizazi cha nne kutoka Machi 2012 na kuendelea. Kwamba kwa kutumia Kalenda inayotumika sasa (Mwasisi wake akiwa ni Gregory – mwaka 1582) kanisa ilikuwa chini ya utumwa kwa miaka 430 kama Israel utumwani Misri. Kuanzia 2008 watu wa kizazi cha nne wana kalenda yao.

4.   Kanisa hivi sasa lipo katika kipindi cha miaka 1000 iliyoanza mwezi Machi 2012 (hii ni baada ya kupita kwa miaka 6000. Hesabu yao ni kuwa miezi yote (12) ina siku 28 na mwaka una siku 336). Yaani wenzetu tayari wamesha-spent mwaka mmoja katika ile miaka 1000 ya utawala wa Yesu hapa duniani, kama iliyoandikwa katika UFUNUO 20:1-5.

5.   Kwa kuwa Kristo anaishi na Kanisa hapa duniani hivyo hakuna magonjwa, dhiki, kudharauliwa na maonevu yote. Ni siku ya saba yaani miaka 1000 ya kustarehe na kutawala. Huenda hapa ndipo ile concept ya kutokufa inapokuja/ingia/ attach.

6.   Waumini wao hutakiwa kubadilisha hadi majina yao ya ukoo. Kwa sababu majina hayo yanabeba laana, kisha muumini hupewa familia nyingine (miongoni mwa washirika) na hutengwa na wazazi na ndugu wa kimwili.

7.   Maombi yao huomba kwa kushikamanisha na madhabahu ya Siloam /Mungu wa nabii Eliya.

8. Wanapomfanyia Deliverance mtu (mmoja wa wahudumu – huingiwa na pepo/mzimu ambao unamsumbua anayeombewa na kumweleza kilichokuwa kinamfunga). Biblically, mtu mwenye pepo/mizimu yeye ndiye hupagawa na kuongea, kisha huamuriwa kutoka ndani ya mtu.

Kila nilichokieleza hapo juu ina tafasiri yake ya ziada ambayo yeyote akipenda na akifunguka anaweza kutufafanulia.

–Mat

0 comments:

Post a Comment