.

.

Wednesday, 9 December 2015

Rais Dk John Magufuli.RAIS John Magufuli amegeuka gumzo kimataifa, kutokana na kasi ya mabadiliko ya kweli ya uongozi wake katika kipindi kifupi, hasa kudhibiti matumizi na kueleza fedha katika huduma za jamii.
Aidha, uongozi wake umeelezwa kuwa wa mfano, kwani miongoni mwa mambo anayoyafanya, yanagusa ulimwengu na anatekeleza yote bila kufanya safari yoyote ya nje ya nchi kama wanavyofanya viongozi wengine.
Tangu aingie madakarani mwezi mmoja na siku chache zilizopita, Dk Magufuli amedhibiti mabilioni ya fedha na kuwezesha fedha hizo kuboresha huduma za afya, ikiwamo kuongeza upatikanaji wa dawa za kupunguza makali ya Ukimwi (ARV’s), shule na miundombinu ya barabara.
Gazeti la The Sunday Independent linalochapishwa na chombo cha habari chenye nguvu nchini Afrika Kusini, liliandika katika tahariri yake hivi karibuni katika kichwa cha habari kisemacho, “Afrika ifuate mfano wa Tanzania.” Tahariri hiyo iliyochapishwa Jumapili iliyopita, ilisisitiza kuwa utekelezaji wa maazimio ya Mkutano wa Sita wa Mawaziri wa Baraza la Ushirikiano kati ya Afrika na China (FOCAC), unahitaji Rais kama Magufuli ambaye ameonesha kwa dhati nidhamu katika matumizi ya serikali.
Gazeti hilo limekuwa miongoni mwa vyombo vya habari vinavyosifu utendaji wa Dk Magufuli, ambaye anafanya kazi bila Baraza la Mawaziri kwa zaidi ya siku 30 tangu aapishwe. Baadhi ya waandishi wa habari kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika, walilieleza gazeti dada la gazeti hili, Daily News katika siku za mwisho wa mkutano wa FOCAC kwamba wameguswa kwa utendaji wa Dk Magufuli na kuwataka viongozi wengine wa Afrika kuiga.
Mwandishi wa gazeti la Daily Graphic la Ghana, Emmanuel Adu- Gyamerah alisema kazi anayofanya Dk Magufuli, ikiwamo kubadili sherehe za Uhuru ambazo mataifa mengi huzifanya kwa gharama kubwa, ni jambo ambalo viongozi wengi wa Afrika wameshindwa, lakini yeye amefanya kwa muda mfupi tangu aingie madarakani. “Hii hatua ya kupunguza matumizi inapaswa kufanywa na Waghana pia,” alisema Adu-Gyamerah.
Dk Magufuli alibadili namna ya kusherehekea sikukuu ya Uhuru na kuagiza Watanzania wote wafanye usafi katika maeneo yao ya kazi na makazi ili kupambana na magonjwa ya mlipuko, ikiwamo kipindupindu na kutunza mazingira. Baadhi ya wananchi wa Rwanda, walieleza kuwa hatua aliyochukua Dk Magufuli kuhusu sherehe za uhuru ni “ya Kinyarwanda” kwa kuwa kwao serikali ilifanya Jumamosi ya kwanza ya kila mwezi kuwa siku rasmi ya usafi nchi nzima.
Mtangazaji wa Televisheni ya China (CCTV) wa Kenya, alisema kufuta safari za nje ni moja ya hatua muhimu na alisema Wakenya wamekuwa wakizungumzia safari za Rais wao, Uhuru Kenyatta anazofaa nje ya nchi.
“Natamani hatua kama hizi zifanyike pia nchini mwangu,” alisema mtangazaji huyo huku akiionesha Daily News ujumbe wa twita unaoonesha sifa kemkem kwa Dk Magufuli. Gazeti la Sunday’s Paper of New Zimbabwe liliandika hivi, “Tanzania’s Magufuli: A new African” (Magufuli wa Tanzania: Mwafrika Mpya”, ikieleza kuwa Dk Magufuli ameleta mapinduzi na njia mpya katika kutawala.
Gazeti hilo lilieleza kuwa, uongozi wa Dk Magufuli umelenga kushughulika na wavivu na wala rushwa na kuandika, “Mpaka sasa mambo ni mazuri; hongera Magufuli.” Gazeti la mtandaoni la Nigeria, naij.com, lilieleza kuwa hatua ya kupunguza matumizi ni ya kuchukuliwa na serikali ya Nigeria vile vile. Naij.com ilimnukuu mhariri wake, Abang Mercy akitwiti hivi karibuni na kuandika ujumbe huu, “Tangu achaguliwe, Rais wa Tanzania, John Magufuli ametekeleza mabadiliko makubwa; na ndivyo ninavyotarajia kwa Rais Buhari (Rais wa Nigeria).”
Gazeti hilo la mtandaoni lilimfananisha Dk Magufuli na Baba wa Taifa wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere, mwasisi na mtu asiyekwepeka katika historia ya Tanzania. Gazeti la Daily Nation la Kenya limeripoti kuwa hatua ya Dk Magufuli kuzuia safari za nje, inapaswa kuchukuliwa pia nchini humo, hasa kutokana na wananchi kuonesha kutokupendezwa na safari za Rais Kenyatta nje ya nchi.
Aidha, suala la kupunguza matumizi kwa kuzuia kuchapisha kadi za sikukuu za Krismasi na Mwaka Mpya kwa taasisi na mashirika ya umma, limepongezwa pia na kumtaka Kenyatta kuiga mfano huo.

Rais Dk John Magufuli.RAIS John Magufuli amegeuka gumzo kimataifa, kutokana na kasi ya mabadiliko ya kweli ya uongozi wake katika kipindi kifupi, hasa kudhibiti matumizi na kueleza fedha katika huduma za jamii.
Aidha, uongozi wake umeelezwa kuwa wa mfano, kwani miongoni mwa mambo anayoyafanya, yanagusa ulimwengu na anatekeleza yote bila kufanya safari yoyote ya nje ya nchi kama wanavyofanya viongozi wengine.
Tangu aingie madakarani mwezi mmoja na siku chache zilizopita, Dk Magufuli amedhibiti mabilioni ya fedha na kuwezesha fedha hizo kuboresha huduma za afya, ikiwamo kuongeza upatikanaji wa dawa za kupunguza makali ya Ukimwi (ARV’s), shule na miundombinu ya barabara.
Gazeti la The Sunday Independent linalochapishwa na chombo cha habari chenye nguvu nchini Afrika Kusini, liliandika katika tahariri yake hivi karibuni katika kichwa cha habari kisemacho, “Afrika ifuate mfano wa Tanzania.” Tahariri hiyo iliyochapishwa Jumapili iliyopita, ilisisitiza kuwa utekelezaji wa maazimio ya Mkutano wa Sita wa Mawaziri wa Baraza la Ushirikiano kati ya Afrika na China (FOCAC), unahitaji Rais kama Magufuli ambaye ameonesha kwa dhati nidhamu katika matumizi ya serikali.
Gazeti hilo limekuwa miongoni mwa vyombo vya habari vinavyosifu utendaji wa Dk Magufuli, ambaye anafanya kazi bila Baraza la Mawaziri kwa zaidi ya siku 30 tangu aapishwe. Baadhi ya waandishi wa habari kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika, walilieleza gazeti dada la gazeti hili, Daily News katika siku za mwisho wa mkutano wa FOCAC kwamba wameguswa kwa utendaji wa Dk Magufuli na kuwataka viongozi wengine wa Afrika kuiga.
Mwandishi wa gazeti la Daily Graphic la Ghana, Emmanuel Adu- Gyamerah alisema kazi anayofanya Dk Magufuli, ikiwamo kubadili sherehe za Uhuru ambazo mataifa mengi huzifanya kwa gharama kubwa, ni jambo ambalo viongozi wengi wa Afrika wameshindwa, lakini yeye amefanya kwa muda mfupi tangu aingie madarakani. “Hii hatua ya kupunguza matumizi inapaswa kufanywa na Waghana pia,” alisema Adu-Gyamerah.
Dk Magufuli alibadili namna ya kusherehekea sikukuu ya Uhuru na kuagiza Watanzania wote wafanye usafi katika maeneo yao ya kazi na makazi ili kupambana na magonjwa ya mlipuko, ikiwamo kipindupindu na kutunza mazingira. Baadhi ya wananchi wa Rwanda, walieleza kuwa hatua aliyochukua Dk Magufuli kuhusu sherehe za uhuru ni “ya Kinyarwanda” kwa kuwa kwao serikali ilifanya Jumamosi ya kwanza ya kila mwezi kuwa siku rasmi ya usafi nchi nzima.
Mtangazaji wa Televisheni ya China (CCTV) wa Kenya, alisema kufuta safari za nje ni moja ya hatua muhimu na alisema Wakenya wamekuwa wakizungumzia safari za Rais wao, Uhuru Kenyatta anazofaa nje ya nchi.
“Natamani hatua kama hizi zifanyike pia nchini mwangu,” alisema mtangazaji huyo huku akiionesha Daily News ujumbe wa twita unaoonesha sifa kemkem kwa Dk Magufuli. Gazeti la Sunday’s Paper of New Zimbabwe liliandika hivi, “Tanzania’s Magufuli: A new African” (Magufuli wa Tanzania: Mwafrika Mpya”, ikieleza kuwa Dk Magufuli ameleta mapinduzi na njia mpya katika kutawala.
Gazeti hilo lilieleza kuwa, uongozi wa Dk Magufuli umelenga kushughulika na wavivu na wala rushwa na kuandika, “Mpaka sasa mambo ni mazuri; hongera Magufuli.” Gazeti la mtandaoni la Nigeria, naij.com, lilieleza kuwa hatua ya kupunguza matumizi ni ya kuchukuliwa na serikali ya Nigeria vile vile. Naij.com ilimnukuu mhariri wake, Abang Mercy akitwiti hivi karibuni na kuandika ujumbe huu, “Tangu achaguliwe, Rais wa Tanzania, John Magufuli ametekeleza mabadiliko makubwa; na ndivyo ninavyotarajia kwa Rais Buhari (Rais wa Nigeria).”
Gazeti hilo la mtandaoni lilimfananisha Dk Magufuli na Baba wa Taifa wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere, mwasisi na mtu asiyekwepeka katika historia ya Tanzania. Gazeti la Daily Nation la Kenya limeripoti kuwa hatua ya Dk Magufuli kuzuia safari za nje, inapaswa kuchukuliwa pia nchini humo, hasa kutokana na wananchi kuonesha kutokupendezwa na safari za Rais Kenyatta nje ya nchi.
Aidha, suala la kupunguza matumizi kwa kuzuia kuchapisha kadi za sikukuu za Krismasi na Mwaka Mpya kwa taasisi na mashirika ya umma, limepongezwa pia na kumtaka Kenyatta kuiga mfano huo.

Rais Magufuli akizoa takataka baada ya kumaliza kufanya usafi karibu na lango kuu la kuingilia Ikulu jijini Dar es Salaam.
Kama umefurahishwa na kitendo hiki, tupia neno lolote kumpongeza.

Rais Magufuli akizoa takataka baada ya kumaliza kufanya usafi karibu na lango kuu la kuingilia Ikulu jijini Dar es Salaam.
Kama umefurahishwa na kitendo hiki, tupia neno lolote kumpongeza.

Sunday, 6 December 2015

KOCHA wa Simba Dylan Kerr, amesema amefurahishwa na usajili wa mshambuliaji wa kimataifa wa Kenya, Paul Kiongera.
Kiongera ni mmoja wa wachezaji walioongezwa kwenye dirisha dogo la usajili na Simba baada ya timu hiyo kuonesha upungufu katika baadhi ya nafasi kwenye mechi tisa za mzunguko wa kwanza.
Akizungumza na gazeti hili, Kerr alisema anamhitaji mshambuliaji huyo ili aweze kumwelekeza namna na kucheza kwa kushirikiana na Hamisi Kiiza kwenye ushambuliaji. “Nimefurahi sana kwamba tayari amejiunga na sisi na sasa ni jukumu langu kuwaunganisha na wenzake,” alisema Kerr.
Alisema ujio wa mchezaji huyo ni fursa nzuri katika maandalizi kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Azam FC Jumamosi.
Alisema amekuwa akiweka mkazo mkubwa kwenye safu ya ushambuliaji kwa sababu kwake hiyo ndiyo sehemu muhimu ambayo inaweza kuwapa ubingwa msimu huu kama watafunga idadi kubwa ya mabao.
Alisema kuongezeka kwa Kiongera na Brian Majwega, ana uhakika atakuwa amemaliza tatizo la mabao lililojitokeza katika mechi za awali za ligi hiyo. Kocha huyo alisisitiza kuwa ujio wa wachezaji hao utabadilisha kikosi chake katika ushambuliaji na kuwa na safu inayotisha katika kufunga.
Kiongera alirudishwa KCB na Simba baada ya kupata majeraha makubwa ya goti msimu uliopita na timu hiyo kumpeleka India kwa ajili ya matibabu na baada ya hapo ilimruhusu acheze kwa mkopo kwa makubaliano ya kumrudisha atakapopona.K

KOCHA wa Simba Dylan Kerr, amesema amefurahishwa na usajili wa mshambuliaji wa kimataifa wa Kenya, Paul Kiongera.
Kiongera ni mmoja wa wachezaji walioongezwa kwenye dirisha dogo la usajili na Simba baada ya timu hiyo kuonesha upungufu katika baadhi ya nafasi kwenye mechi tisa za mzunguko wa kwanza.
Akizungumza na gazeti hili, Kerr alisema anamhitaji mshambuliaji huyo ili aweze kumwelekeza namna na kucheza kwa kushirikiana na Hamisi Kiiza kwenye ushambuliaji. “Nimefurahi sana kwamba tayari amejiunga na sisi na sasa ni jukumu langu kuwaunganisha na wenzake,” alisema Kerr.
Alisema ujio wa mchezaji huyo ni fursa nzuri katika maandalizi kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Azam FC Jumamosi.
Alisema amekuwa akiweka mkazo mkubwa kwenye safu ya ushambuliaji kwa sababu kwake hiyo ndiyo sehemu muhimu ambayo inaweza kuwapa ubingwa msimu huu kama watafunga idadi kubwa ya mabao.
Alisema kuongezeka kwa Kiongera na Brian Majwega, ana uhakika atakuwa amemaliza tatizo la mabao lililojitokeza katika mechi za awali za ligi hiyo. Kocha huyo alisisitiza kuwa ujio wa wachezaji hao utabadilisha kikosi chake katika ushambuliaji na kuwa na safu inayotisha katika kufunga.
Kiongera alirudishwa KCB na Simba baada ya kupata majeraha makubwa ya goti msimu uliopita na timu hiyo kumpeleka India kwa ajili ya matibabu na baada ya hapo ilimruhusu acheze kwa mkopo kwa makubaliano ya kumrudisha atakapopona.K

RC amsihi Yussuf Manji akubali kuachia Coco BeachMKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadiki amemuomba mmiliki wa Kampuni ya Q Consult inayomilikiwa na mfanyabiashara Yussuf Manji kutumia busara kukubali kuuachia ufukwe wa Coco jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Sadiki alisema Mahakama Kuu ya Tanzania, Kitengo cha Ardhi katika uamuzi wake imeiamuru Manispaa ya Kinondoni, kutekeleza mkataba wake na kampuni ya Q Consult kwa ajili ya kampuni hiyo kuendeleza ufukwe huo hata hivyo Manispaa ya Kinondoni imekata rufaa.
“Kampuni ya Q Consult kwa busara tu iachane na kesi, ikubali kurudisha ufukwe huo chini ya mamlaka ya Kinondoni ili iweze kuuendeleza ufukwe huo kwa manufaa ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam na sio kwa manufaa ya mtu mmoja kama anavyotaka mtu huyo,” alisema Sadiki.
Alisema wananchi wafahamu kuwa ufukwe huo wa Coco haujauzwa, kama watu wanavyodai na kwamba kesi hiyo iko mahakamani, ambapo Ofisi ya Manispaa ya Kinondoni kupitia Mwanasheria Mkuu wa Serikali wamekata rufaa.
Akielezea sakata hilo, Sadiki alisema kampuni ya Q Consult inayomilikiwa na Manji mwaka 2007 iliingia mkataba na Manispaa ya Kinondoni kuendeleza ufukwe huo.
Alisema, hata hivyo, baadaye Manispaa ya hiyo ilivunja mkataba huo baada ya Kampuni ya Q Consult kushindwa kutimiza masharti, jambo ambalo liliifanya kampuni hiyo kwenda mahakamani.
Mahakama Kuu ya Tanzania Kitengo cha Ardhi iliamuru Manispaa ya Kinondoni, kutekeleza mkataba wake na kampuni hiyo kwa ajili ya kuendeleza ufukwe huo.
“Kama nilivyosema kupitia mwanasheria mkuu wa Serikali tumekata rufaa katika uamuzi huo kwasababu tunaamini haukuwa sahihi, hata hivyo mwekezaji huyo namshauri tu anaweza kufanya maamuzi akaachana na kesi hiyo na kuamua kurudisha ufukwe huo uendelee kutumiwa na Watanzania wote,” alisema Sadiki.
Kwa kampuni hiyo kushinda kesi hiyo, inamaanisha kuwa mwekezaji huyo endapo ataendeleza eneo hilo, wananchi hawatakuwa na fursa hiyo tena, kama wanavyoutumia sasa.
Sadiki alisema tayari serikali imefanya mazungumzo na moja na benki hapa nchini kwa ajili ya kupata mkopo, ambao utasaidia kuendeleza eneo hilo ili liendelee kubaki chini ya Manispaa ya Kinondoni na kutumiwa na watu wote.






















RC amsihi Yussuf Manji akubali kuachia Coco BeachMKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadiki amemuomba mmiliki wa Kampuni ya Q Consult inayomilikiwa na mfanyabiashara Yussuf Manji kutumia busara kukubali kuuachia ufukwe wa Coco jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Sadiki alisema Mahakama Kuu ya Tanzania, Kitengo cha Ardhi katika uamuzi wake imeiamuru Manispaa ya Kinondoni, kutekeleza mkataba wake na kampuni ya Q Consult kwa ajili ya kampuni hiyo kuendeleza ufukwe huo hata hivyo Manispaa ya Kinondoni imekata rufaa.
“Kampuni ya Q Consult kwa busara tu iachane na kesi, ikubali kurudisha ufukwe huo chini ya mamlaka ya Kinondoni ili iweze kuuendeleza ufukwe huo kwa manufaa ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam na sio kwa manufaa ya mtu mmoja kama anavyotaka mtu huyo,” alisema Sadiki.
Alisema wananchi wafahamu kuwa ufukwe huo wa Coco haujauzwa, kama watu wanavyodai na kwamba kesi hiyo iko mahakamani, ambapo Ofisi ya Manispaa ya Kinondoni kupitia Mwanasheria Mkuu wa Serikali wamekata rufaa.
Akielezea sakata hilo, Sadiki alisema kampuni ya Q Consult inayomilikiwa na Manji mwaka 2007 iliingia mkataba na Manispaa ya Kinondoni kuendeleza ufukwe huo.
Alisema, hata hivyo, baadaye Manispaa ya hiyo ilivunja mkataba huo baada ya Kampuni ya Q Consult kushindwa kutimiza masharti, jambo ambalo liliifanya kampuni hiyo kwenda mahakamani.
Mahakama Kuu ya Tanzania Kitengo cha Ardhi iliamuru Manispaa ya Kinondoni, kutekeleza mkataba wake na kampuni hiyo kwa ajili ya kuendeleza ufukwe huo.
“Kama nilivyosema kupitia mwanasheria mkuu wa Serikali tumekata rufaa katika uamuzi huo kwasababu tunaamini haukuwa sahihi, hata hivyo mwekezaji huyo namshauri tu anaweza kufanya maamuzi akaachana na kesi hiyo na kuamua kurudisha ufukwe huo uendelee kutumiwa na Watanzania wote,” alisema Sadiki.
Kwa kampuni hiyo kushinda kesi hiyo, inamaanisha kuwa mwekezaji huyo endapo ataendeleza eneo hilo, wananchi hawatakuwa na fursa hiyo tena, kama wanavyoutumia sasa.
Sadiki alisema tayari serikali imefanya mazungumzo na moja na benki hapa nchini kwa ajili ya kupata mkopo, ambao utasaidia kuendeleza eneo hilo ili liendelee kubaki chini ya Manispaa ya Kinondoni na kutumiwa na watu wote.