KOCHA wa Simba Dylan Kerr, amesema amefurahishwa na usajili wa mshambuliaji wa kimataifa wa Kenya, Paul Kiongera.
Kiongera ni mmoja wa wachezaji walioongezwa kwenye dirisha dogo la
usajili na Simba baada ya timu hiyo kuonesha upungufu katika baadhi ya
nafasi kwenye mechi tisa za mzunguko wa kwanza.
Akizungumza na gazeti hili, Kerr alisema anamhitaji mshambuliaji huyo
ili aweze kumwelekeza namna na kucheza kwa kushirikiana na Hamisi Kiiza
kwenye ushambuliaji. “Nimefurahi sana kwamba tayari amejiunga na sisi
na sasa ni jukumu langu kuwaunganisha na wenzake,” alisema Kerr.
Alisema ujio wa mchezaji huyo ni fursa nzuri katika maandalizi kwenye
mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Azam FC Jumamosi.
Alisema amekuwa akiweka mkazo mkubwa kwenye safu ya ushambuliaji kwa
sababu kwake hiyo ndiyo sehemu muhimu ambayo inaweza kuwapa ubingwa
msimu huu kama watafunga idadi kubwa ya mabao.
Alisema kuongezeka kwa Kiongera na Brian Majwega, ana uhakika atakuwa
amemaliza tatizo la mabao lililojitokeza katika mechi za awali za ligi
hiyo. Kocha huyo alisisitiza kuwa ujio wa wachezaji hao utabadilisha
kikosi chake katika ushambuliaji na kuwa na safu inayotisha katika
kufunga.
Kiongera alirudishwa KCB na Simba baada ya kupata majeraha makubwa ya
goti msimu uliopita na timu hiyo kumpeleka India kwa ajili ya matibabu
na baada ya hapo ilimruhusu acheze kwa mkopo kwa makubaliano ya
kumrudisha atakapopona.K
Sunday, 6 December 2015
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment