MA B I N G W A wa Tanzania Bara, Yanga, jana walianza vibaya
mashindano ya Afrika Mashariki na Kati ya Kombe la Kagame, baada ya
kuchapwa mabao 2-1 katika mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa Taifa Dar es
Salaam.
Gor Mahia ambayo nusura ishindwe kushiriki mashindano hayo kutokana
na ukata na kuokolewa na serikali ya nchi yao, ilipata ushindi huo mbele
ya Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya, Raila Odinga.
Wenyeji Yanga ndio walikuwa wa kwanza kupata bao la kuongoza katika
dakika ya nne lililofungwa na mchezaji wa Gor Mahia, ambaye alitaka
kuokoa mpira uliopigwa na Donald Ngoma na kuujaza wavuni.
Gor Mahia ilicharuka na kusawazisha muda mfupi baadae kwa bao la
Michael Olunga alilofunga kwa kichwa baada ya kuruka kuwazidi mabeki wa
Yanga na kujaza mpira wavuni.
Yanga ilipata pigo katika dakika ya 11 baada ya kutolewa kwa mchezaji
wake Mzimbabwe Ngoma, kutokana na kumsukuma beki wa Gor Mahia.
Huku wakishangiliwa na mashabiki wanaodhaniwa kuwa ni wa Simba, Gor
Mahia walipata bao katika dakika ya 46 lililofungwa tena na Olunga baada
ya kuwatoka mabeki wa Yanga na kuujaza mpira wavuni kulia kwa kipa
Mustapha.
Wachezaji wa Gor Mahia waligoma kuingia katika vyumba vya
kubadilishia nguo, ambapo walitumia mlango tofauti. Yanga walipata
penalti baada ya mchezaji mmoja wa Gor Mahia kuunawa mpira lakini
nahodha wa Yanga,Nadir Haroub alipiga mpira na kuokolewa na kipa
Boniface Oluoch.
Yanga iko katika kundi A pamoja na Gor Mahia, Telecom (Djibout), KMKM
(Zanzibar) na Khartoum-N (Sudan) wakati Kundi B linaundwa na timu za
APR (Rwanda), Al-Shandy (Sudan),LLB AFC (Burundi) na Heegan FC
(Somalia).
Kundi C lina timu za Azam FC (Tanzania), Malakia (Sudan Kusini), Adama City (Ethiopia) na KCCA (Uganda).
Vikosi Yanga ilianza na:- Ally Mustafa Barthez, Amiss Tambwe, Nadir
Haroub, Mbuyi Twitte, Simon Msuva, Juma Abdul, Deus Kaseke, Haruna
Niyozima, Kelvin Yondan, Mwinyi Haji na Donald Ngoma
Gor Mahia: Boniface Oluoch, Karim Nizigiyimana, Mussa Mohammed, Haron
Shakava, Abouba Sibomana, Innocent Wafura, Diikir Glay, Kharid Aucho,
Godfrey Walusimbi, Michael Olunga na Meddie Kagere, Michuano hiyo
itaendelea tena leo kwa Azam FC kucheza na Katika mchezo wa awali kwenye
mashindano hayo, APR ya Rwanda iliibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya
Al Shandy ya Sudan.
Katika Uwanja wa Karume, KMKM ya Zanzibar iliibuka na ushindi wa bao
1-0 katika mchezo mwingine wa michuano hiyo dhidi ya Telecom ya Djibout.
Sunday, 19 July 2015
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment