.

.

Wednesday, 16 September 2015

MGOMBEA wa urais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kupitia Chadema, Edward Lowassa, amesema haitoshi kwa watu kuendelea kufurika katika mikutano yake pasipo kutia nia ya kumpigia kura ili aweze kuwa Rais wa Serikali ya Awamu ya Tano.
Lowassa anayeungwa mkono na vyama vingine vitatu vya CUF, NCCR- Mageuzi na NLD, alisema umati wa watu wanaojitokeza kumsikiliza kila mahali ikiwemo Morogoro Mjini hakutoshi iwapo hawataweza kumpigia kura nyingi za kuingia madarakani Oktoba 25, mwaka huu.
Lowassa aliyekuwa Waziri Mkuu wa kwanza katika Serikali ya Awamu ya Nne na kulazimika kuachia madaraka mapema mwaka 2008, alihutubia takribani kwa dakika kumi na baadaye kuwakaribisha na kuwatambulisha wagombea wa ubunge wa Jimbo la Morogoro Mjini na madiwani wa Kata mbalimbali ili kuwaombea kura kwa wananchi.
Alianza ziara yake kwa kuwahutubia wananchi wa kata ya Dumila, Turiani na kuwasili mjini Morogoro jioni ya saa kumi akiambatana na aliyekuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Tatu, Frederick Sumaye ambaye kama Lowassa, amejiengua CCM baada ya kukataliwa kuwania urais kwa tiketi ya chama hicho tawala.
Akihubutia katika mkutano huo uliofanyika katika uwanja wa Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege, Manispaa ya Morogoro, alisema mahudhurio hayo na kumshangilia huko kwa wingi kuonekane pia katika sanduku la kura.
Pia alitumia muda huo kuelezea azma yake endapo wananchi watamchagua kuwa Rais wa Tanzania, ataangalia namna ya kufufua viwanda vya Morogoro na ikiwezekana kuanzisha vipya ili kuwezesha upatikanaji wa ajira na kuuza bidhaa ghafi nje badala ya kuuza malighafi kama ilivyo kwa sasa.
Alisema, si dhambi viwanda kuendeshwa na serikali kwa kuwa jambo hilo linafanyika hata katika nchi nyingine za Ulaya na kutolea mfano Ufaransa ambako baadhi ya viwanda na mabenki yanamilikiwa na serikali.
Hivyo aliwataka wananchi kuwapigia kura wagombea wa Chadema kwa nafasi ya udiwani, ubunge ili aweza kupata timu atakayofanya nayo kazi endapo atachaguliwa kuwa rais.
Pamoja na hayo, alisema serikali yake atakayoiunda itakuwa rafiki wa mama lishe, bodaboda na wamachinga na kwamba ataanzisha benki itakayoshughulikia makundi hayo.
Pia alisema serikali yake itasimamia uboreshaji wa elimu, maslahi ya walimu na kutoa elimu bure kuanzia darasa la kwanza hadi chuo kikuu na kwamba endapo ataingia madarakani wanafunzi wote watasomba bure bila kulipa michango.

MGOMBEA wa urais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kupitia Chadema, Edward Lowassa, amesema haitoshi kwa watu kuendelea kufurika katika mikutano yake pasipo kutia nia ya kumpigia kura ili aweze kuwa Rais wa Serikali ya Awamu ya Tano.
Lowassa anayeungwa mkono na vyama vingine vitatu vya CUF, NCCR- Mageuzi na NLD, alisema umati wa watu wanaojitokeza kumsikiliza kila mahali ikiwemo Morogoro Mjini hakutoshi iwapo hawataweza kumpigia kura nyingi za kuingia madarakani Oktoba 25, mwaka huu.
Lowassa aliyekuwa Waziri Mkuu wa kwanza katika Serikali ya Awamu ya Nne na kulazimika kuachia madaraka mapema mwaka 2008, alihutubia takribani kwa dakika kumi na baadaye kuwakaribisha na kuwatambulisha wagombea wa ubunge wa Jimbo la Morogoro Mjini na madiwani wa Kata mbalimbali ili kuwaombea kura kwa wananchi.
Alianza ziara yake kwa kuwahutubia wananchi wa kata ya Dumila, Turiani na kuwasili mjini Morogoro jioni ya saa kumi akiambatana na aliyekuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Tatu, Frederick Sumaye ambaye kama Lowassa, amejiengua CCM baada ya kukataliwa kuwania urais kwa tiketi ya chama hicho tawala.
Akihubutia katika mkutano huo uliofanyika katika uwanja wa Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege, Manispaa ya Morogoro, alisema mahudhurio hayo na kumshangilia huko kwa wingi kuonekane pia katika sanduku la kura.
Pia alitumia muda huo kuelezea azma yake endapo wananchi watamchagua kuwa Rais wa Tanzania, ataangalia namna ya kufufua viwanda vya Morogoro na ikiwezekana kuanzisha vipya ili kuwezesha upatikanaji wa ajira na kuuza bidhaa ghafi nje badala ya kuuza malighafi kama ilivyo kwa sasa.
Alisema, si dhambi viwanda kuendeshwa na serikali kwa kuwa jambo hilo linafanyika hata katika nchi nyingine za Ulaya na kutolea mfano Ufaransa ambako baadhi ya viwanda na mabenki yanamilikiwa na serikali.
Hivyo aliwataka wananchi kuwapigia kura wagombea wa Chadema kwa nafasi ya udiwani, ubunge ili aweza kupata timu atakayofanya nayo kazi endapo atachaguliwa kuwa rais.
Pamoja na hayo, alisema serikali yake atakayoiunda itakuwa rafiki wa mama lishe, bodaboda na wamachinga na kwamba ataanzisha benki itakayoshughulikia makundi hayo.
Pia alisema serikali yake itasimamia uboreshaji wa elimu, maslahi ya walimu na kutoa elimu bure kuanzia darasa la kwanza hadi chuo kikuu na kwamba endapo ataingia madarakani wanafunzi wote watasomba bure bila kulipa michango.

Saturday, 5 September 2015

Mgombea Urais wa CC, Dk John Magufuli akihutubia wananchi wa Morogoro.MGOMBEA urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk John Magufuli ameahidi kunyang’any’a mashamba ambayo yamehodhiwa na watu bila kutumiwa kwa ufugaji wala kilimo, na kuyagawa kwa wakulima na wafugaji wasio na maeneo ya kilimo. Alisema hayo alipozungumza na wananchi wa wilaya za Ulanga na Kilombero mkoani Morogoro jana.
Dk Magufuli alisema akiwa rais, kuna mambo mengi anaweza kufanya, kukabiliana na migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji na mojawapo ni kutoa ardhi zaidi kwaajili ya wakulima na wafugaji, ili kuondoa uhaba wa ardhi, unaosababisha ugomvi wa maeneo ya kulishia mifugo na kulima.
Alisema kuna watu wanamiliki maelfu ya eka za ardhi bila kulima na kwamba atanyang’any’a mashamba hayo ambayo yamehodhiwa na watu hao bila kutumiwa kwa ufugaji wala kilimo. Akihutubia maelfu ya wananchi, pia Dk Magufuli alisema kuwa anajivunia uzoefu wa marais wastaafu wa Awamu ya Pili mpaka Awamu ya Nne na wa Zanzibar, kwamba ndio atakaowafuata kwa ushauri akikwama popote.
Alisema hiyo ni moja ya tofauti kubwa kati yake na wagombea wengine wa urais. “Nitaingia Ikulu nikiwa na washauri wazuri, nikikwama mahali nitakwenda kwa Rais Jakaya Kikwete, nikikwama nitaenda kwa mzee Benjamin Mkapa, nikikwama tena nakwenda kwa mzee Ali Hasan Mwinyi.
“Wako wengi, upo ushauri nitauchukua kutoka kwa mzee Salmin Amour (Rais Mstaafu wa Zanzibar), Dk Ali Mohamed Shein na kwa Amani Abeid Karume,” alisema. Kutokana na fursa hiyo ya kiuongozi aliyonayo ndani ya Chama Cha Mapinduzi, Dk Magufuli aliomba Watanzania wote bila kujali vyama vya siasa, makabila wala dini kumpa kura kwa wingi kwa kuwa atakuwa na washauri wazuri wenye uzoefu.
Alisema wagombea wengine, akiwemo wa Chadema anayeungwa mkono na vyama vinavyounda Ukawa, Edward Lowassa, hawataweza kupata ushauri wa washauri hao kama ilivyo rahisi kwake.
Kutokana na uhakika huo wa washauri wazoefu, Dk Magufuli alisema ndio maana baadhi ya wagombea hao wanaweza kuja na ahadi za uongo, ikiwemo ya kuondoa nyumba za tembe na za nyasi.
Aliwataka wananchi kuwapima wagombea hao katika ahadi zao, kwa kuwa baadhi walikuwepo ndani ya Serikali kwa muda mrefu, lakini walishindwa kuondoa nyumba hizo katika majimbo walikotokea.
Dk Magufuli alisema yeye hataahidi kuondoa nyumba hizo, bali anaahidi kushusha bei ya vifaa vya ujenzi hasa saruji, mabati na misumari, ili wananchi wanaofanya kazi wajenge nyumba bora.
Katika kuongeza idadi ya Watanzania wanaofanya kazi ili kufikia lengo hilo, Dk Magufuli alisema katika kila mtaa na kijiji, serikali yake itatoa Sh milioni 50 kwa ajili ya kuanzisha na kukuza biashara ndogo za wanawake na vijana.
Alisema atataka kila anayefanya kazi apate kipato kizuri kitakachomsaidia kukabiliana na mahitaji ya maisha yake, ikiwemo kujenga nyumba bora kutokana na kushushwa kwa bei za bidhaa za ujenzi. Kwa wakulima, alisema atahakikisha pembejeo sahihi zinatolewa kwa wakati na mazao yatakayovunwa, itakuwa marufuku kwa Serikali kukopa mazao yao.

Mgombea Urais wa CC, Dk John Magufuli akihutubia wananchi wa Morogoro.MGOMBEA urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk John Magufuli ameahidi kunyang’any’a mashamba ambayo yamehodhiwa na watu bila kutumiwa kwa ufugaji wala kilimo, na kuyagawa kwa wakulima na wafugaji wasio na maeneo ya kilimo. Alisema hayo alipozungumza na wananchi wa wilaya za Ulanga na Kilombero mkoani Morogoro jana.
Dk Magufuli alisema akiwa rais, kuna mambo mengi anaweza kufanya, kukabiliana na migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji na mojawapo ni kutoa ardhi zaidi kwaajili ya wakulima na wafugaji, ili kuondoa uhaba wa ardhi, unaosababisha ugomvi wa maeneo ya kulishia mifugo na kulima.
Alisema kuna watu wanamiliki maelfu ya eka za ardhi bila kulima na kwamba atanyang’any’a mashamba hayo ambayo yamehodhiwa na watu hao bila kutumiwa kwa ufugaji wala kilimo. Akihutubia maelfu ya wananchi, pia Dk Magufuli alisema kuwa anajivunia uzoefu wa marais wastaafu wa Awamu ya Pili mpaka Awamu ya Nne na wa Zanzibar, kwamba ndio atakaowafuata kwa ushauri akikwama popote.
Alisema hiyo ni moja ya tofauti kubwa kati yake na wagombea wengine wa urais. “Nitaingia Ikulu nikiwa na washauri wazuri, nikikwama mahali nitakwenda kwa Rais Jakaya Kikwete, nikikwama nitaenda kwa mzee Benjamin Mkapa, nikikwama tena nakwenda kwa mzee Ali Hasan Mwinyi.
“Wako wengi, upo ushauri nitauchukua kutoka kwa mzee Salmin Amour (Rais Mstaafu wa Zanzibar), Dk Ali Mohamed Shein na kwa Amani Abeid Karume,” alisema. Kutokana na fursa hiyo ya kiuongozi aliyonayo ndani ya Chama Cha Mapinduzi, Dk Magufuli aliomba Watanzania wote bila kujali vyama vya siasa, makabila wala dini kumpa kura kwa wingi kwa kuwa atakuwa na washauri wazuri wenye uzoefu.
Alisema wagombea wengine, akiwemo wa Chadema anayeungwa mkono na vyama vinavyounda Ukawa, Edward Lowassa, hawataweza kupata ushauri wa washauri hao kama ilivyo rahisi kwake.
Kutokana na uhakika huo wa washauri wazoefu, Dk Magufuli alisema ndio maana baadhi ya wagombea hao wanaweza kuja na ahadi za uongo, ikiwemo ya kuondoa nyumba za tembe na za nyasi.
Aliwataka wananchi kuwapima wagombea hao katika ahadi zao, kwa kuwa baadhi walikuwepo ndani ya Serikali kwa muda mrefu, lakini walishindwa kuondoa nyumba hizo katika majimbo walikotokea.
Dk Magufuli alisema yeye hataahidi kuondoa nyumba hizo, bali anaahidi kushusha bei ya vifaa vya ujenzi hasa saruji, mabati na misumari, ili wananchi wanaofanya kazi wajenge nyumba bora.
Katika kuongeza idadi ya Watanzania wanaofanya kazi ili kufikia lengo hilo, Dk Magufuli alisema katika kila mtaa na kijiji, serikali yake itatoa Sh milioni 50 kwa ajili ya kuanzisha na kukuza biashara ndogo za wanawake na vijana.
Alisema atataka kila anayefanya kazi apate kipato kizuri kitakachomsaidia kukabiliana na mahitaji ya maisha yake, ikiwemo kujenga nyumba bora kutokana na kushushwa kwa bei za bidhaa za ujenzi. Kwa wakulima, alisema atahakikisha pembejeo sahihi zinatolewa kwa wakati na mazao yatakayovunwa, itakuwa marufuku kwa Serikali kukopa mazao yao.

Wednesday, 2 September 2015

BAADA ya kutoweka hadharani tangu Julai 28, mwaka huu, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbrod Slaa amejitokeza hadharani na kuelezea kilichomsibu, akiweka wazi kwamba amestaafu siasa baada ya chama hicho kumpokea aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa ambaye amesisitiza hawezi kukwepa kashfa ya Richmond.
Dk Slaa aliwaambia waandishi wa habari katika mkutano uliodumu kwa takribani saa mbili katika Hoteli ya Serena, Dar es Salaam jana kuwa Lowassa si kiongozi anayefaa kuwa rais wa nchi kutokana na kuhusika na vitendo vya rushwa na kwamba ni mhusika namba moja katika kashfa ya Richmond, iliyomwondoa madarakani Februari 2008. Tangu Julai 28, wakati Lowassa alipoanza kuonekana katika vikao vya Chadema, Dk Slaa amekuwa haonekani katika vikao vya chama hicho ikiwemo Mkutano Mkuu uliomtangaza Lowassa kuwa mgombea urais wa chama hicho na umoja wa wapinzani (Ukawa) katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka huu.
Mbali ya Mkutano Mkuu, Dk Slaa hakuonekana katika matukio muhimu kama yale ya Lowassa kufika Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuchukua fomu ya kugombea urais na wakati wa kuirejesha, na pia katika mkutano wa uzinduzi wa kampeni kwenye Viwanja vya Jangwani, Agosti 29, mwaka huu.
Katika mkutano wa jana, Dk Slaa alieleza kwa kirefu kilichotokea na kumfanya kupotea katika harakati za Chadema huku akiweka wazi kuwa ujio wa Lowassa ulimfanya ajiuzulu nafasi ya Ukatibu Mkuu, tofauti na madai ya Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe kwamba alikuwa likizo. “Nimejitokeza leo, mimi sikuwa likizo.
Mengi yamesemwa na viongozi wangu, lakini ukweli ni kwamba sikupewa likizo na yeyote, nasisitiza sina barua yoyote ya likizo. “Kilichotokea ni kwamba niliamua kuachana na siasa tangu tarehe 28/7 majira ya saa 3 usiku, baada ya kuona yanayofanyika ndani ya chama changu na sikukubaliana nayo,” alisema Dk Slaa na kuongeza: “Wapo watu wanaosema Dk Slaa alishiriki kutoka mwanzo katika ujio wa Lowassa.
Nilishiriki kweli, lakini niliweka msingi tangu dakika ya kwanza kutaka kujua Lowassa anakuja Chadema kama mali au anakuja kama mzigo? Msimamo wangu huu haukupatiwa majibu na hadi sasa viongozi wa Chadema hawana majibu katika hili.”
Akisimulia mkasa mzima, padri huyo wa zamani wa Kanisa Katoliki alisema baada ya Lowassa kukatwa kwenye mchakato wa kumpata mgombea urais kupitia CCM mjini Dodoma, alipigiwa simu na Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima aliyemwita kuwa mshenga wa Lowassa, akimuarifu hatua hiyo ya kukatwa Lowassa ni mtaji kwa Chadema.
Alisema katika maelekezo yake, Askofu Gwajima alimuelekeza Dk Slaa awasiliane na Mwenyekiti wa Chadema, Mbowe kuhusu mpango huo na kumrejeshea majibu ya kile walichoafikiana na kwamba alitekeleza ombi hilo kwa kuwasiliana na Mbowe na baadaye walimkaribisha Askofu Gwajima ili kuzungumza kwa kina.
“Tangu wakati huo niliweka msimamo wangu. Unajua kwa kawaida ni vizuri kumsikia mtu ana nini na si kutomsikiliza kabisa. Chadema ni chama cha siasa haikatazwi kumpokea mtu. “Niliweka msimamo kwanza atangaze kutoka ndani ya CCM, baada ya kutangaza hilo atangaze pia ni chama gani anakwenda, halafu tatu atumie nafasi hiyo kujisafisha na tuhuma zake anazoshutumiwa.
Niliweka msimamo huo kwa kuamini kuwa Chadema ni chama kilichojijenga katika misingi ya uadilifu na iwapo asingefanya hivyo ni hatari,” alifafanua Dk Slaa aliyegombea urais kwa chama hicho mwaka 2010. Alisema kinyume cha msimamo aliouweka, Lowassa hakutangaza kujitoa CCM na kutangaza anakwenda chama gani kwa wakati huo, lakini pia hakujisafisha hadi alipokuwa katika kikao cha utambulisho Chadema ndipo alipozungumzia suala la Richmond baada ya kuulizwa na waandishi wa habari tena katika hali ya udikteta.
Alisema mbali ya msimamo huo, aliweka msimamo mwingine wa kutaka kujua, Lowassa anakwenda Chadema akiwa ni mali au mzigo, katika kile alichosema ilikuwa ni kutaka kutathmini kama ujio huo wa Lowassa kwa Chadema ungekuwa na manufaa au hasara. “Ujue kwenye biashara au siasa, anayejiunga leo ni lazima mfahamu, je, anakuja kama mali au kama mzigo?
Watu hapa wanasema nilipatwa na hasira kwa vile alipewa nafasi ya kugombea urais, suala si urais, hadi siku hiyo nilikuwa sijachukua fomu ya urais, kama ningekuwa nataka urais ningetangaza au kuchukua fomu kwani jina langu lilishapitishwa na vikao tangu Februari. “Hapa ukweli ni kwamba Slaa alikuwa anataka mgombea mwenye uwezo, sifa na anayeweza kuivusha Chadema kuiondoa CCM.
Hata mwaka 2010 sikujitokeza mimi kugombea urais, bali niliombwa. Urais si wangu, mimi binafsi ni kwa ajili ya watu,” alieleza akifafanua madai hayo ya kuwa alikasirika kwa kutoteuliwa kuwania urais. Alisema kutokana na swali hilo, alijibiwa kwamba Lowassa angekwenda Chadema na wabunge 50 waliokuwa wakimaliza muda wao, wenyeviti wa CCM wa mikoa 22, wenyeviti wa CCM wa wilaya 88, na hivyo aliamini kama ingekuwa hivyo nchi ingeweza kutetemeka.
“Niliweka sharti majina yatajwe, nilifanya vile kwa kuwa Katibu Mkuu makini wa chama hawezi kupokea tu watu, bila kujua ni akina nani na wanagombea wapi maana tulikuwa tayari na mfumo wa kuwaandaa wagombea ndani ya chama, hata hivyo majina hayo sikuyapata. Alisema ilipofika Julai 25, kilifanyika kikao ambacho aliagizwa kuitisha kikao cha Halmashauri Kuu na alipohoji nini kinaenda kuzungumzwa, hakupewa jibu.
Alisema Julai 25, alipigiwa simu na Mbowe ambapo katika mazungumzo yao kwa mara ya kwanza walitofautiana, ingawa alikubali kufika katika kikao alichowakuta Mbowe, Askofu Gwajima na Mwanasheria wao, Tundu Lissu. “Kikao kile kilianza saa 3 asubuhi hadi saa 9 jioni, na tulibishana sana, maana swali langu lilibakia kuwa lile lile, je Lowassa anakuja Chadema kama mali au kama mzigo?
Baada ya pale walisema twende nyumbani kwa Lowassa, lakini nilikataa kwani Lowassa ni mwanachama wa CCM hivyo mimi nisingeweza kwenda. “Tulirejea tena katika kikao kuanzia saa 9 jioni hadi saa 12.30, tukapumzika, lakini hatukuelewana. Wakaunda kamati ndogo ya kuzungumza na mimi na kunishauri, lakini nilikataa. Pale pale niliandika barua ya kujiuzulu nikampa Mwenyekiti wa kikao, Profesa Safari (Abdalah) lakini aliichana pale pale.
“Sikuridhika na hatua hiyo niliandika barua nyingine na kumkabidhi Makamu Mwenyekiti wa Zanzibar ambaye alinijibu kwamba Dk Slaa unajisumbua bure haya mambo yamepangwa. Hata hivyo, kesho yake niliandika barua rasmi ya kujizulu,” alieleza kiongozi huyo aliyeheshimika kwa misimamo yake ndani ya Chadema.
Akizungumzia nini kilifuata baada ya Lowassa kupokelewa Chadema; alisema alikwenda kama mzigo na si mali kwani yeye na wafuasi wake ni watu ambao ama walikataliwa na wananchi katika kura za maoni, au ni ambao wamekuwa wakituhumiwa katika masuala ya ufisadi na hawawezi kukubalika ndani ya jamii.
“Awali niliweka msimamo kwamba wale watakaokuja na Lowassa ni vizuri waje kabla ya kufanyika kura ya maoni, hilo halikuzingatiwa. Dk Mahanga (Makongoro, aliyekuwa Mbunge wa Ukonga na Naibu Waziri wa Kazi na Ajira) huyo ni mali au ni mzigo? Huyo amekataliwa na wananchi hivyo alikuwa anatafuta kichaka cha kujificha. “Hivi Sumaye (Frederick, Waziri Mkuu mstaafu) huyo ni mtu safi kweli. Watu wote wanamfahamu kwamba ni fisadi.
Nilimwita fisadi ndani ya Bunge wakati ule alipopokonya shamba la Magereza Kibaigwa. “Huyu Sumaye ndiye ambaye alisema CCM ikimteua Lowassa atahama chama. Watu wote mnajua Sumaye alikuwa anaitwa nani wakati ule… (kicheko). Leo makapi yametoka CCM yamekwenda Chadema.
Wenyeviti waliondoka ni mizigo, wote tunamjua Msindai (Mgana, aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida na Mwenyekiti wa Wenyeviti wa CCM). “Mimi namfahamu Msindai, alikuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali kabla yangu pale Bungeni alichokifanya ipo siku nitamuweka hadharani.
Mtu ambaye siwezi kumsema ni Mgeja (Khamis, aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Shinyanga)… huyo siwezi kumsema maana simfahamu,” alieleza Dk Slaa. “Kuna mtu anaitwa Chizi, hivi Chizi ni nani? Nilipofuatilia ili kumjua vizuri nikaambiwa eti alikuwa anapanga mipango ya wizi wa kura ndani ya CCM.
Yaani Chadema inampokea mtu kwa vile tu alikuwa mwizi wa kura? Kama tunataka Chadema kuiba kura kuna umuhimu gani wa kuiondoa CCM madarakani? Unaiondoa CCM kwa programu safi serious (makini) na watu serious (makini).”
Kuhusu Richmond, Dk Slaa alisema bado anaamini kuwa Lowassa hawezi kukwepa kashfa hiyo na alionesha na kusoma vielelezo na barua mbalimbali, alizosema zinadhihirisha Lowassa kuwa mpangaji mkuu wa mpango wa ufisadi wa Richmond na kwamba kupokelewa na Chadema, kumekifanya chama hicho kupoteza nguvu ya hoja ya kupambana na ufisadi, hoja aliyosema ilikuwa silaha pekee kwa Chadema.
Dk Slaa alimtaka Waziri Mkuu huyo wa zamani, kujitokeza na kueleza namna alivyohusika na sakata la Richmond, kwa kutaja Richmond ilikuwa kampuni ya nani, na ni wakubwa gani walioshinikiza kutolewa kwa zabuni hiyo ya kufua umeme wa dharura kama alivyodai na kuahidi kutoa taarifa zaidi ya umma kwa suala hilo.

BAADA ya kutoweka hadharani tangu Julai 28, mwaka huu, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbrod Slaa amejitokeza hadharani na kuelezea kilichomsibu, akiweka wazi kwamba amestaafu siasa baada ya chama hicho kumpokea aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa ambaye amesisitiza hawezi kukwepa kashfa ya Richmond.
Dk Slaa aliwaambia waandishi wa habari katika mkutano uliodumu kwa takribani saa mbili katika Hoteli ya Serena, Dar es Salaam jana kuwa Lowassa si kiongozi anayefaa kuwa rais wa nchi kutokana na kuhusika na vitendo vya rushwa na kwamba ni mhusika namba moja katika kashfa ya Richmond, iliyomwondoa madarakani Februari 2008. Tangu Julai 28, wakati Lowassa alipoanza kuonekana katika vikao vya Chadema, Dk Slaa amekuwa haonekani katika vikao vya chama hicho ikiwemo Mkutano Mkuu uliomtangaza Lowassa kuwa mgombea urais wa chama hicho na umoja wa wapinzani (Ukawa) katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka huu.
Mbali ya Mkutano Mkuu, Dk Slaa hakuonekana katika matukio muhimu kama yale ya Lowassa kufika Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuchukua fomu ya kugombea urais na wakati wa kuirejesha, na pia katika mkutano wa uzinduzi wa kampeni kwenye Viwanja vya Jangwani, Agosti 29, mwaka huu.
Katika mkutano wa jana, Dk Slaa alieleza kwa kirefu kilichotokea na kumfanya kupotea katika harakati za Chadema huku akiweka wazi kuwa ujio wa Lowassa ulimfanya ajiuzulu nafasi ya Ukatibu Mkuu, tofauti na madai ya Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe kwamba alikuwa likizo. “Nimejitokeza leo, mimi sikuwa likizo.
Mengi yamesemwa na viongozi wangu, lakini ukweli ni kwamba sikupewa likizo na yeyote, nasisitiza sina barua yoyote ya likizo. “Kilichotokea ni kwamba niliamua kuachana na siasa tangu tarehe 28/7 majira ya saa 3 usiku, baada ya kuona yanayofanyika ndani ya chama changu na sikukubaliana nayo,” alisema Dk Slaa na kuongeza: “Wapo watu wanaosema Dk Slaa alishiriki kutoka mwanzo katika ujio wa Lowassa.
Nilishiriki kweli, lakini niliweka msingi tangu dakika ya kwanza kutaka kujua Lowassa anakuja Chadema kama mali au anakuja kama mzigo? Msimamo wangu huu haukupatiwa majibu na hadi sasa viongozi wa Chadema hawana majibu katika hili.”
Akisimulia mkasa mzima, padri huyo wa zamani wa Kanisa Katoliki alisema baada ya Lowassa kukatwa kwenye mchakato wa kumpata mgombea urais kupitia CCM mjini Dodoma, alipigiwa simu na Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima aliyemwita kuwa mshenga wa Lowassa, akimuarifu hatua hiyo ya kukatwa Lowassa ni mtaji kwa Chadema.
Alisema katika maelekezo yake, Askofu Gwajima alimuelekeza Dk Slaa awasiliane na Mwenyekiti wa Chadema, Mbowe kuhusu mpango huo na kumrejeshea majibu ya kile walichoafikiana na kwamba alitekeleza ombi hilo kwa kuwasiliana na Mbowe na baadaye walimkaribisha Askofu Gwajima ili kuzungumza kwa kina.
“Tangu wakati huo niliweka msimamo wangu. Unajua kwa kawaida ni vizuri kumsikia mtu ana nini na si kutomsikiliza kabisa. Chadema ni chama cha siasa haikatazwi kumpokea mtu. “Niliweka msimamo kwanza atangaze kutoka ndani ya CCM, baada ya kutangaza hilo atangaze pia ni chama gani anakwenda, halafu tatu atumie nafasi hiyo kujisafisha na tuhuma zake anazoshutumiwa.
Niliweka msimamo huo kwa kuamini kuwa Chadema ni chama kilichojijenga katika misingi ya uadilifu na iwapo asingefanya hivyo ni hatari,” alifafanua Dk Slaa aliyegombea urais kwa chama hicho mwaka 2010. Alisema kinyume cha msimamo aliouweka, Lowassa hakutangaza kujitoa CCM na kutangaza anakwenda chama gani kwa wakati huo, lakini pia hakujisafisha hadi alipokuwa katika kikao cha utambulisho Chadema ndipo alipozungumzia suala la Richmond baada ya kuulizwa na waandishi wa habari tena katika hali ya udikteta.
Alisema mbali ya msimamo huo, aliweka msimamo mwingine wa kutaka kujua, Lowassa anakwenda Chadema akiwa ni mali au mzigo, katika kile alichosema ilikuwa ni kutaka kutathmini kama ujio huo wa Lowassa kwa Chadema ungekuwa na manufaa au hasara. “Ujue kwenye biashara au siasa, anayejiunga leo ni lazima mfahamu, je, anakuja kama mali au kama mzigo?
Watu hapa wanasema nilipatwa na hasira kwa vile alipewa nafasi ya kugombea urais, suala si urais, hadi siku hiyo nilikuwa sijachukua fomu ya urais, kama ningekuwa nataka urais ningetangaza au kuchukua fomu kwani jina langu lilishapitishwa na vikao tangu Februari. “Hapa ukweli ni kwamba Slaa alikuwa anataka mgombea mwenye uwezo, sifa na anayeweza kuivusha Chadema kuiondoa CCM.
Hata mwaka 2010 sikujitokeza mimi kugombea urais, bali niliombwa. Urais si wangu, mimi binafsi ni kwa ajili ya watu,” alieleza akifafanua madai hayo ya kuwa alikasirika kwa kutoteuliwa kuwania urais. Alisema kutokana na swali hilo, alijibiwa kwamba Lowassa angekwenda Chadema na wabunge 50 waliokuwa wakimaliza muda wao, wenyeviti wa CCM wa mikoa 22, wenyeviti wa CCM wa wilaya 88, na hivyo aliamini kama ingekuwa hivyo nchi ingeweza kutetemeka.
“Niliweka sharti majina yatajwe, nilifanya vile kwa kuwa Katibu Mkuu makini wa chama hawezi kupokea tu watu, bila kujua ni akina nani na wanagombea wapi maana tulikuwa tayari na mfumo wa kuwaandaa wagombea ndani ya chama, hata hivyo majina hayo sikuyapata. Alisema ilipofika Julai 25, kilifanyika kikao ambacho aliagizwa kuitisha kikao cha Halmashauri Kuu na alipohoji nini kinaenda kuzungumzwa, hakupewa jibu.
Alisema Julai 25, alipigiwa simu na Mbowe ambapo katika mazungumzo yao kwa mara ya kwanza walitofautiana, ingawa alikubali kufika katika kikao alichowakuta Mbowe, Askofu Gwajima na Mwanasheria wao, Tundu Lissu. “Kikao kile kilianza saa 3 asubuhi hadi saa 9 jioni, na tulibishana sana, maana swali langu lilibakia kuwa lile lile, je Lowassa anakuja Chadema kama mali au kama mzigo?
Baada ya pale walisema twende nyumbani kwa Lowassa, lakini nilikataa kwani Lowassa ni mwanachama wa CCM hivyo mimi nisingeweza kwenda. “Tulirejea tena katika kikao kuanzia saa 9 jioni hadi saa 12.30, tukapumzika, lakini hatukuelewana. Wakaunda kamati ndogo ya kuzungumza na mimi na kunishauri, lakini nilikataa. Pale pale niliandika barua ya kujiuzulu nikampa Mwenyekiti wa kikao, Profesa Safari (Abdalah) lakini aliichana pale pale.
“Sikuridhika na hatua hiyo niliandika barua nyingine na kumkabidhi Makamu Mwenyekiti wa Zanzibar ambaye alinijibu kwamba Dk Slaa unajisumbua bure haya mambo yamepangwa. Hata hivyo, kesho yake niliandika barua rasmi ya kujizulu,” alieleza kiongozi huyo aliyeheshimika kwa misimamo yake ndani ya Chadema.
Akizungumzia nini kilifuata baada ya Lowassa kupokelewa Chadema; alisema alikwenda kama mzigo na si mali kwani yeye na wafuasi wake ni watu ambao ama walikataliwa na wananchi katika kura za maoni, au ni ambao wamekuwa wakituhumiwa katika masuala ya ufisadi na hawawezi kukubalika ndani ya jamii.
“Awali niliweka msimamo kwamba wale watakaokuja na Lowassa ni vizuri waje kabla ya kufanyika kura ya maoni, hilo halikuzingatiwa. Dk Mahanga (Makongoro, aliyekuwa Mbunge wa Ukonga na Naibu Waziri wa Kazi na Ajira) huyo ni mali au ni mzigo? Huyo amekataliwa na wananchi hivyo alikuwa anatafuta kichaka cha kujificha. “Hivi Sumaye (Frederick, Waziri Mkuu mstaafu) huyo ni mtu safi kweli. Watu wote wanamfahamu kwamba ni fisadi.
Nilimwita fisadi ndani ya Bunge wakati ule alipopokonya shamba la Magereza Kibaigwa. “Huyu Sumaye ndiye ambaye alisema CCM ikimteua Lowassa atahama chama. Watu wote mnajua Sumaye alikuwa anaitwa nani wakati ule… (kicheko). Leo makapi yametoka CCM yamekwenda Chadema.
Wenyeviti waliondoka ni mizigo, wote tunamjua Msindai (Mgana, aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida na Mwenyekiti wa Wenyeviti wa CCM). “Mimi namfahamu Msindai, alikuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali kabla yangu pale Bungeni alichokifanya ipo siku nitamuweka hadharani.
Mtu ambaye siwezi kumsema ni Mgeja (Khamis, aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Shinyanga)… huyo siwezi kumsema maana simfahamu,” alieleza Dk Slaa. “Kuna mtu anaitwa Chizi, hivi Chizi ni nani? Nilipofuatilia ili kumjua vizuri nikaambiwa eti alikuwa anapanga mipango ya wizi wa kura ndani ya CCM.
Yaani Chadema inampokea mtu kwa vile tu alikuwa mwizi wa kura? Kama tunataka Chadema kuiba kura kuna umuhimu gani wa kuiondoa CCM madarakani? Unaiondoa CCM kwa programu safi serious (makini) na watu serious (makini).”
Kuhusu Richmond, Dk Slaa alisema bado anaamini kuwa Lowassa hawezi kukwepa kashfa hiyo na alionesha na kusoma vielelezo na barua mbalimbali, alizosema zinadhihirisha Lowassa kuwa mpangaji mkuu wa mpango wa ufisadi wa Richmond na kwamba kupokelewa na Chadema, kumekifanya chama hicho kupoteza nguvu ya hoja ya kupambana na ufisadi, hoja aliyosema ilikuwa silaha pekee kwa Chadema.
Dk Slaa alimtaka Waziri Mkuu huyo wa zamani, kujitokeza na kueleza namna alivyohusika na sakata la Richmond, kwa kutaja Richmond ilikuwa kampuni ya nani, na ni wakubwa gani walioshinikiza kutolewa kwa zabuni hiyo ya kufua umeme wa dharura kama alivyodai na kuahidi kutoa taarifa zaidi ya umma kwa suala hilo.

MGOMBEA urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk John Magufuli amesema Serikali atakayoiongoza baada ya kuchaguliwa, itapandisha mishahara ya watumishi wote wa umma ilingane na ile ya Wakala wa Taifa wa Barabara (Tanroads), ambayo aliianzisha na kuwapa wafanyakazi wake mishahara minono.
Hata hivyo, Dk Magufuli alisema baada ya kuongeza mishahara hiyo, wafanyakazi lazima wachape kazi na kuonya kuwa wasipofanya hivyo atapambana nao. Aidha, amesema Serikali atakayoiongoza, itapunguza bei ya vifaa vya ujenzi, hasa saruji na mabati.
Alisema hayo jana katika mikutano midogo aliyofanya njiani alikokuwa akisimamishwa na wananchi wakati alipokuwa akitoka Songea, kupitia Namtumbo na Tunduru kwenda Masasi mkoani Mtwara.
Dk Magufuli alisema mkoani Mtwara tayari ujenzi umeanza wa kiwanda cha saruji ambacho ndio kikubwa kuliko vyote Afrika Mashariki na Kati na kikikamilika, kitazalisha saruji nyingi na kupunguza bei ya bidhaa hiyo muhimu ya ujenzi.
Alisema kusudio la kushusha bei ya vifaa hivyo ni kusaidia wananchi wajenge nyumba nzuri na bora za makazi kwa ajili ya kuboresha maisha yao. Kuhusu kuboresha kipato cha wananchi ili wafanikishe azma ya kutumia punguzo la bei za bidhaa za ujenzi na kujenga nyumba bora, Dk Magufuli alisema umeme umeanza kufika katika maeneo hayo na Serikali yake itahakikisha vijijini kunajengwa viwanda vidogo vitakavyotoa ajira vijijini.
Mbali na ajira, pia aliahidi kutoa Sh milioni 50 kwa kila kijiji na kila mtaa, kwa ajili ya kuanzisha na kuendeleza miradi midogo midogo ya kujipatia kipato kwa ajili ya wanawake na vijana.

MGOMBEA urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk John Magufuli amesema Serikali atakayoiongoza baada ya kuchaguliwa, itapandisha mishahara ya watumishi wote wa umma ilingane na ile ya Wakala wa Taifa wa Barabara (Tanroads), ambayo aliianzisha na kuwapa wafanyakazi wake mishahara minono.
Hata hivyo, Dk Magufuli alisema baada ya kuongeza mishahara hiyo, wafanyakazi lazima wachape kazi na kuonya kuwa wasipofanya hivyo atapambana nao. Aidha, amesema Serikali atakayoiongoza, itapunguza bei ya vifaa vya ujenzi, hasa saruji na mabati.
Alisema hayo jana katika mikutano midogo aliyofanya njiani alikokuwa akisimamishwa na wananchi wakati alipokuwa akitoka Songea, kupitia Namtumbo na Tunduru kwenda Masasi mkoani Mtwara.
Dk Magufuli alisema mkoani Mtwara tayari ujenzi umeanza wa kiwanda cha saruji ambacho ndio kikubwa kuliko vyote Afrika Mashariki na Kati na kikikamilika, kitazalisha saruji nyingi na kupunguza bei ya bidhaa hiyo muhimu ya ujenzi.
Alisema kusudio la kushusha bei ya vifaa hivyo ni kusaidia wananchi wajenge nyumba nzuri na bora za makazi kwa ajili ya kuboresha maisha yao. Kuhusu kuboresha kipato cha wananchi ili wafanikishe azma ya kutumia punguzo la bei za bidhaa za ujenzi na kujenga nyumba bora, Dk Magufuli alisema umeme umeanza kufika katika maeneo hayo na Serikali yake itahakikisha vijijini kunajengwa viwanda vidogo vitakavyotoa ajira vijijini.
Mbali na ajira, pia aliahidi kutoa Sh milioni 50 kwa kila kijiji na kila mtaa, kwa ajili ya kuanzisha na kuendeleza miradi midogo midogo ya kujipatia kipato kwa ajili ya wanawake na vijana.