.

.

Wednesday, 18 November 2015

Usiku wa November 17 watanzania wengi na wapenzi wa soka walikuwa wakisubiri kuona mchezo wa pili wa marudiano wa kuwania kufuzu Kombe la Dunia 2018 Urusi kati ya timu ya taifa ya Algeria dhidi ya timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars, mchezo ambao ulichezwa Blida Algeria katika uwanja wa Mustapha Tchaker.
Taifa Stars ambayo ilionesha kiwango kizuri katika uwanja wa nyumbani Dar Es Salaam licha ya kulazimishwa sare ya goli 2-2, wameshindwa kutamba katika mchezo wa pili na kukubali kipigo cha goli 7-0, ilichukua dakika 45 za kwanza Taifa Stars  kuanza kuruhusu magoli matatu ya mwanzo, magoli ambayo yalianza kukatisha tamaa wa Tanzania.http://i1.wp.com/millardayo.com/wp-content/uploads/2015/11/Algeria.jpg
Wakati Taifa Stars wanatafakari namna ambavyo watasawazisha magoli Mudathir Yahaya alioneshwa kadi nyekundu dakika ya 41, kipindi cha pili kocha wa Tanzania Boniface Mkwasa alifanya mabadiliko ya kumuingiza Aishi Manula na kumtoa golikipa Aly Mustapha na Farid Mussa nafasi yake ikachuliwa na Salum Telela, mabadiliko ambayo hayakuzaa matunda.
Magoli ya Algeria yalifungwa na Yacine Brahimi dakika ya 1, Faouzi Ghoulam dakika ya 23 na dakika ya 59 akapachika goli jingine kwa mkwaju wa penati, Riyad Mahrez dakika ya 43 na Islam Slimani kafunga kwa mkwaju wa penati dakika ya 49 na 75, Carl Medjani dakika ya 72 . Kwa matokeo hayo Taifa Stars imetolewa kwa jumla ya magoli 9-2 baada ya mchezo wa awali kumalizika kwa sare ya goli 2-2.

Usiku wa November 17 watanzania wengi na wapenzi wa soka walikuwa wakisubiri kuona mchezo wa pili wa marudiano wa kuwania kufuzu Kombe la Dunia 2018 Urusi kati ya timu ya taifa ya Algeria dhidi ya timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars, mchezo ambao ulichezwa Blida Algeria katika uwanja wa Mustapha Tchaker.
Taifa Stars ambayo ilionesha kiwango kizuri katika uwanja wa nyumbani Dar Es Salaam licha ya kulazimishwa sare ya goli 2-2, wameshindwa kutamba katika mchezo wa pili na kukubali kipigo cha goli 7-0, ilichukua dakika 45 za kwanza Taifa Stars  kuanza kuruhusu magoli matatu ya mwanzo, magoli ambayo yalianza kukatisha tamaa wa Tanzania.http://i1.wp.com/millardayo.com/wp-content/uploads/2015/11/Algeria.jpg
Wakati Taifa Stars wanatafakari namna ambavyo watasawazisha magoli Mudathir Yahaya alioneshwa kadi nyekundu dakika ya 41, kipindi cha pili kocha wa Tanzania Boniface Mkwasa alifanya mabadiliko ya kumuingiza Aishi Manula na kumtoa golikipa Aly Mustapha na Farid Mussa nafasi yake ikachuliwa na Salum Telela, mabadiliko ambayo hayakuzaa matunda.
Magoli ya Algeria yalifungwa na Yacine Brahimi dakika ya 1, Faouzi Ghoulam dakika ya 23 na dakika ya 59 akapachika goli jingine kwa mkwaju wa penati, Riyad Mahrez dakika ya 43 na Islam Slimani kafunga kwa mkwaju wa penati dakika ya 49 na 75, Carl Medjani dakika ya 72 . Kwa matokeo hayo Taifa Stars imetolewa kwa jumla ya magoli 9-2 baada ya mchezo wa awali kumalizika kwa sare ya goli 2-2.

Tuesday, 17 November 2015

NAHODHA wa timu ya soka ya taifa, Taifa Stars, Nadir Haroub amesema leo watafia uwanjani mjini Algiers katika mechi ya kuwania kufuzu michuano ya Kombe la Dunia Urusi 2018 watakaporudiana na wenyeji Algeria.
Stars inaingia uwanjani leo ikiwa na kumbukumbu ya kutoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya vigogo hivyo vya Afrika katika mechi ya kwanza iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita.
Katika mechi hiyo, Stars ilikuwa mbele kwa mabao 2-0 mpaka dakika ya 71 ndipo Algeria wakapata mabao ya harakaharaka na kuondoa furaha miongoni mwa watanzania waliofurika uwanjani siku hiyo.
Matokeo hayo yanaifanya Stars ihitaji ushindi katika mechi ya leo au sare ya kuanzia mabao 3-3 ili kujihakikishia kukata tiketi ya kucheza hatua ya makundi ya michuano hiyo, ambayo ni ya mwisho kabla ya kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia.
Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya mtandao jana, Haroub alisema anaamini timu yake inaweza kuibuka na ushindi ugenini leo. “Soka imebadilika sana siku hizi, ile ya miaka ile sio ya leo lolote linaweza kutokea kesho (leo) na tukasonga mbele, mbona hao Algeria tulienda nao sawa tu mechi ya kwanza makosa madogo tu yamefanyika wakasazisha lakini tunao uwezo wa kuwafunga,” alisema.
Mashabiki wa timu ya taifa, Taifa Stars, bado wana taharuki ya matokeo ya sare ya 2-2 dhidi ya Algeria, lakini nahodha wa Stars, Haroub ametamka kishujaa kuwa kazi haijaisha na anaamini timu hiyo itafanya makubwa kutokana na safu kali ya ushambuliaji waliyonayo.
“Mimi naamini kabisa timu yetu ipo vizuri kila sehemu nawaambieni washambuliaji wangu kwamba watatubeba katika mechi hiyo bila shaka yoyote,” alisema. Safu ya ushambuliaji ya Stars inaongozwa na wachezaji Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wanaocheza soka ya kulipwa TP Mazembe ya Congo DR.
Haroub ambaye pia ni nahodha wa mabingwa wa soka Bara, Yanga, alisema Stars itawashangaza wengi leo kama ilivyokuwa kwenye mechi iliyopita. “Mechi iliyopita hakuna aliyetarajia tungepata bao hata moja lakini matokeo yake tulifunga mabao mawili mpaka waarabu (Algeria) wenyewe walichanganyikiwa, hivyo hata huku inawezekana tu kushinda,” alisema.
Awali, kabla ya safari ya Algiers juzi, kocha mkuu wa timu hiyo Charles Mkwasa alisema anatarajia timu yake kupata matokeo mazuri. Mkwasa alikiri kufanya makosa ya kiufundi wakati wa mabadiliko katika mechi hiyo lakini akasema hiyo ni hali ya mpira hutokea mara nyingi.
Katika mechi hiyo ,Mkwasa aliwatoa Mudathir Yahya na Elias Maguli na nafasi zao kuchukuliwa na Said Ndemla na Mrisho Ngassa, mabadiliko ambayo hayakuwa na faida kwa timu, jambo lililofanya wapinzani wao kusawazisha mabao hayo mawili ndani ya dakika nne.
“Makosa hutokea kwenye mpira, ni jambo la kawaida nasi safari hii tumekutana na makosa hayo, benchi la ufundi imeyaona itayafanyia kazi yasijirudie katika mechi ya marudiano,” alisema Mkwasa.

NAHODHA wa timu ya soka ya taifa, Taifa Stars, Nadir Haroub amesema leo watafia uwanjani mjini Algiers katika mechi ya kuwania kufuzu michuano ya Kombe la Dunia Urusi 2018 watakaporudiana na wenyeji Algeria.
Stars inaingia uwanjani leo ikiwa na kumbukumbu ya kutoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya vigogo hivyo vya Afrika katika mechi ya kwanza iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita.
Katika mechi hiyo, Stars ilikuwa mbele kwa mabao 2-0 mpaka dakika ya 71 ndipo Algeria wakapata mabao ya harakaharaka na kuondoa furaha miongoni mwa watanzania waliofurika uwanjani siku hiyo.
Matokeo hayo yanaifanya Stars ihitaji ushindi katika mechi ya leo au sare ya kuanzia mabao 3-3 ili kujihakikishia kukata tiketi ya kucheza hatua ya makundi ya michuano hiyo, ambayo ni ya mwisho kabla ya kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia.
Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya mtandao jana, Haroub alisema anaamini timu yake inaweza kuibuka na ushindi ugenini leo. “Soka imebadilika sana siku hizi, ile ya miaka ile sio ya leo lolote linaweza kutokea kesho (leo) na tukasonga mbele, mbona hao Algeria tulienda nao sawa tu mechi ya kwanza makosa madogo tu yamefanyika wakasazisha lakini tunao uwezo wa kuwafunga,” alisema.
Mashabiki wa timu ya taifa, Taifa Stars, bado wana taharuki ya matokeo ya sare ya 2-2 dhidi ya Algeria, lakini nahodha wa Stars, Haroub ametamka kishujaa kuwa kazi haijaisha na anaamini timu hiyo itafanya makubwa kutokana na safu kali ya ushambuliaji waliyonayo.
“Mimi naamini kabisa timu yetu ipo vizuri kila sehemu nawaambieni washambuliaji wangu kwamba watatubeba katika mechi hiyo bila shaka yoyote,” alisema. Safu ya ushambuliaji ya Stars inaongozwa na wachezaji Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wanaocheza soka ya kulipwa TP Mazembe ya Congo DR.
Haroub ambaye pia ni nahodha wa mabingwa wa soka Bara, Yanga, alisema Stars itawashangaza wengi leo kama ilivyokuwa kwenye mechi iliyopita. “Mechi iliyopita hakuna aliyetarajia tungepata bao hata moja lakini matokeo yake tulifunga mabao mawili mpaka waarabu (Algeria) wenyewe walichanganyikiwa, hivyo hata huku inawezekana tu kushinda,” alisema.
Awali, kabla ya safari ya Algiers juzi, kocha mkuu wa timu hiyo Charles Mkwasa alisema anatarajia timu yake kupata matokeo mazuri. Mkwasa alikiri kufanya makosa ya kiufundi wakati wa mabadiliko katika mechi hiyo lakini akasema hiyo ni hali ya mpira hutokea mara nyingi.
Katika mechi hiyo ,Mkwasa aliwatoa Mudathir Yahya na Elias Maguli na nafasi zao kuchukuliwa na Said Ndemla na Mrisho Ngassa, mabadiliko ambayo hayakuwa na faida kwa timu, jambo lililofanya wapinzani wao kusawazisha mabao hayo mawili ndani ya dakika nne.
“Makosa hutokea kwenye mpira, ni jambo la kawaida nasi safari hii tumekutana na makosa hayo, benchi la ufundi imeyaona itayafanyia kazi yasijirudie katika mechi ya marudiano,” alisema Mkwasa.

Sunday, 1 November 2015





Simba imetoa kipigo cha mbwa mwizi jana baada ya kuichapa timu ya Majimaji ya Songea ‘wanalizombe’ kwa goli 6-0 kwenye mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara uliochezwa kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam
Vijana wa Msimbazi walianza kupata goli lao mapema kutoka kwa mchezaji wao chipukizi Ibrahim Ajib aliyetupia goli tatu pekeyake (hat-trick).


Kocha wa Simba Dylan Kerr akishangilia na wachezaji wake
Kwenye mchezo huo Simkba SC ilianza mchezo kwa kasi kwa kuishambulia mara kwa mara timu ya Majimaji na kupelekea kupata magoli ya mawili ya haraka katika dakika 15 za mwanzo, dakika ya nane na dakika ya 14 yote yakifungwa na Ajib.
Dakika za 15 za katikati ya kipindi cha kwanza mchezo ulitulia na Majimaji wakaonesha uhai kidogo na kufanikiwa kutengeneza nafasi kadhaa lakini safu ya ushambuliaji inayoongozwa na Stamili Mbonde ilishindwa kutumia vyema nafasi hizo kuipa goli Majimaji.
 Simba 61





Simba imetoa kipigo cha mbwa mwizi jana baada ya kuichapa timu ya Majimaji ya Songea ‘wanalizombe’ kwa goli 6-0 kwenye mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara uliochezwa kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam
Vijana wa Msimbazi walianza kupata goli lao mapema kutoka kwa mchezaji wao chipukizi Ibrahim Ajib aliyetupia goli tatu pekeyake (hat-trick).


Kocha wa Simba Dylan Kerr akishangilia na wachezaji wake
Kwenye mchezo huo Simkba SC ilianza mchezo kwa kasi kwa kuishambulia mara kwa mara timu ya Majimaji na kupelekea kupata magoli ya mawili ya haraka katika dakika 15 za mwanzo, dakika ya nane na dakika ya 14 yote yakifungwa na Ajib.
Dakika za 15 za katikati ya kipindi cha kwanza mchezo ulitulia na Majimaji wakaonesha uhai kidogo na kufanikiwa kutengeneza nafasi kadhaa lakini safu ya ushambuliaji inayoongozwa na Stamili Mbonde ilishindwa kutumia vyema nafasi hizo kuipa goli Majimaji.
 Simba 61

Coutinho vs ChelseaJose Mourinho ameendelea kupata wakati mgumu tena katika kibarua chake mara baada ya kushuhudia timu yake ya Chelsea leo ikipokea kipigo kitakatifu cha mabao 3-1 kutoka kwa Majogoo wa Liverpool, mchezo uliopigwa katika dimba la Stamford Bridge, maskani kwa Chelsea.
Chelsea ndio walikuwa wa kwanza kupata bao mapema kabisa katika kipindi cha kwanza mara baada ya kiungo Mbrazil Ramires kuunganisha kwa kichwa krosi iliyochongwa na Cesar Azpilicueta mnamo dakika ya 4 na kuipa Chelsea bao la kuongoza.
Ndoto za Chelsea zilizimwa mnamo dakika ya 45 na Mbrazil Coutinho baada ya kuuchinja mpira kwa uzuri na kumwacha kipa wa Chelsea Begovic akiwa hana la kufanya.
Coutinho tena alishindilia msumari wa pili kwa Chelsea baada ya kupiga shuti kali na kutinga moja kwa moja wavuni mnao dakika ya 74.
Ndoto za Chelsea zilizimwa kabisa mnamo dakika ya 83 na Christian Benteke ambaye aliingia kuchukua nafasi ya James Milner na kuipa Liverpool goli la tatu lililopeleka machungu makubwa kwa Chelsea huku presha ikizidi kumuendea Mourinho baada ya timu hiyo kuwa na matokea mabovu tangu mwanzo wa msimu huu, wakiwa nafasi ya 15 mpaka sasa.
 
Liverpool forward Philippe Coutinho (right) whips this strike past the challenge of John Terry (left) to equalise for the away sideContinho akifunga goli la kusawazisha.Coutinho heaped more misery on Jose Mourinho's men with this strike late in the second-half to give Liverpool a 2-1 lead 
Continho akifunga goli la pili
Chelsea's backline was once again undone by this shot from Christian Benteke, who fired in Liverpool's third at Stamford BridgeHuyo ndo Christian Benteke akimalizia msumari wenye sumu kali wa mwisho.

Coutinho vs ChelseaJose Mourinho ameendelea kupata wakati mgumu tena katika kibarua chake mara baada ya kushuhudia timu yake ya Chelsea leo ikipokea kipigo kitakatifu cha mabao 3-1 kutoka kwa Majogoo wa Liverpool, mchezo uliopigwa katika dimba la Stamford Bridge, maskani kwa Chelsea.
Chelsea ndio walikuwa wa kwanza kupata bao mapema kabisa katika kipindi cha kwanza mara baada ya kiungo Mbrazil Ramires kuunganisha kwa kichwa krosi iliyochongwa na Cesar Azpilicueta mnamo dakika ya 4 na kuipa Chelsea bao la kuongoza.
Ndoto za Chelsea zilizimwa mnamo dakika ya 45 na Mbrazil Coutinho baada ya kuuchinja mpira kwa uzuri na kumwacha kipa wa Chelsea Begovic akiwa hana la kufanya.
Coutinho tena alishindilia msumari wa pili kwa Chelsea baada ya kupiga shuti kali na kutinga moja kwa moja wavuni mnao dakika ya 74.
Ndoto za Chelsea zilizimwa kabisa mnamo dakika ya 83 na Christian Benteke ambaye aliingia kuchukua nafasi ya James Milner na kuipa Liverpool goli la tatu lililopeleka machungu makubwa kwa Chelsea huku presha ikizidi kumuendea Mourinho baada ya timu hiyo kuwa na matokea mabovu tangu mwanzo wa msimu huu, wakiwa nafasi ya 15 mpaka sasa.
 
Liverpool forward Philippe Coutinho (right) whips this strike past the challenge of John Terry (left) to equalise for the away sideContinho akifunga goli la kusawazisha.Coutinho heaped more misery on Jose Mourinho's men with this strike late in the second-half to give Liverpool a 2-1 lead 
Continho akifunga goli la pili
Chelsea's backline was once again undone by this shot from Christian Benteke, who fired in Liverpool's third at Stamford BridgeHuyo ndo Christian Benteke akimalizia msumari wenye sumu kali wa mwisho.