.

.

Sunday, 1 November 2015

Coutinho vs ChelseaJose Mourinho ameendelea kupata wakati mgumu tena katika kibarua chake mara baada ya kushuhudia timu yake ya Chelsea leo ikipokea kipigo kitakatifu cha mabao 3-1 kutoka kwa Majogoo wa Liverpool, mchezo uliopigwa katika dimba la Stamford Bridge, maskani kwa Chelsea.
Chelsea ndio walikuwa wa kwanza kupata bao mapema kabisa katika kipindi cha kwanza mara baada ya kiungo Mbrazil Ramires kuunganisha kwa kichwa krosi iliyochongwa na Cesar Azpilicueta mnamo dakika ya 4 na kuipa Chelsea bao la kuongoza.
Ndoto za Chelsea zilizimwa mnamo dakika ya 45 na Mbrazil Coutinho baada ya kuuchinja mpira kwa uzuri na kumwacha kipa wa Chelsea Begovic akiwa hana la kufanya.
Coutinho tena alishindilia msumari wa pili kwa Chelsea baada ya kupiga shuti kali na kutinga moja kwa moja wavuni mnao dakika ya 74.
Ndoto za Chelsea zilizimwa kabisa mnamo dakika ya 83 na Christian Benteke ambaye aliingia kuchukua nafasi ya James Milner na kuipa Liverpool goli la tatu lililopeleka machungu makubwa kwa Chelsea huku presha ikizidi kumuendea Mourinho baada ya timu hiyo kuwa na matokea mabovu tangu mwanzo wa msimu huu, wakiwa nafasi ya 15 mpaka sasa.
 
Liverpool forward Philippe Coutinho (right) whips this strike past the challenge of John Terry (left) to equalise for the away sideContinho akifunga goli la kusawazisha.Coutinho heaped more misery on Jose Mourinho's men with this strike late in the second-half to give Liverpool a 2-1 lead 
Continho akifunga goli la pili
Chelsea's backline was once again undone by this shot from Christian Benteke, who fired in Liverpool's third at Stamford BridgeHuyo ndo Christian Benteke akimalizia msumari wenye sumu kali wa mwisho.

0 comments:

Post a Comment