.

.

Sunday, 1 November 2015





Simba imetoa kipigo cha mbwa mwizi jana baada ya kuichapa timu ya Majimaji ya Songea ‘wanalizombe’ kwa goli 6-0 kwenye mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara uliochezwa kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam
Vijana wa Msimbazi walianza kupata goli lao mapema kutoka kwa mchezaji wao chipukizi Ibrahim Ajib aliyetupia goli tatu pekeyake (hat-trick).


Kocha wa Simba Dylan Kerr akishangilia na wachezaji wake
Kwenye mchezo huo Simkba SC ilianza mchezo kwa kasi kwa kuishambulia mara kwa mara timu ya Majimaji na kupelekea kupata magoli ya mawili ya haraka katika dakika 15 za mwanzo, dakika ya nane na dakika ya 14 yote yakifungwa na Ajib.
Dakika za 15 za katikati ya kipindi cha kwanza mchezo ulitulia na Majimaji wakaonesha uhai kidogo na kufanikiwa kutengeneza nafasi kadhaa lakini safu ya ushambuliaji inayoongozwa na Stamili Mbonde ilishindwa kutumia vyema nafasi hizo kuipa goli Majimaji.
 Simba 61

0 comments:

Post a Comment