.

.

Friday, 29 April 2016



 TOFAUTI YA KUOMBA MASTERS,
P HD KWA U LAYA NA MAREKANI, C ANADA
Ukiachilia kujumuisha mambo yote ya jumla
katika uombaji scholarship kama vile
recommendation letters, sample writing,
application nk, kuna utofauti uliopo ambao
utakusaidia kufanya maamuzi ya wapi uombe.
a) Application Fee:
Vyuo vya ulaya havina Application Fee. Hili ni
jambo muhimu sana, maana itakusaidia kuomba
vyuo vingi bure. Gharama ni za kutuma
documents kwa njia ya posta nk.
Kwa upande wa USA na Canada hii ni tofauti.
Kwa kila chuo uombacho, unatakiwa kulipa si
chini ya dola 50-100 kama fee. Hii kwa maisha
ya Kitanzania ni hela kubwa ukizingatia
unatakiwa uombe vyuo vingi ujiwekee uwezekano
wa kupata.
b) Admission Exams
TOEFL au IELTS
Kwa upande wa Ulaya, wao wana mtihani mmoja
wa English Proficiency. Unatakiwa kufanya aidha
mtihani wa TOEFL (Test of English as Foreign
Language) au IELTS (International English
Language Testing System). Huo mtihani wa
TOEFL ni wa kimarekani unafanyikia pale Chuo
cha Mwalimu Nyerere kule Kigamboni, ambapo
ada ya mtihani huo ni kama dola 185. Na mtihani
wa IELTS ni wa waingereza na hufanyikia pale
British Council ada yake ni kama laki nne hivi.
Unatakiwa kufanya mtihani mmmoja kati ya hiyo
miwili.
Kuna vyuo au nchi chache zinaruhusu applicants
kuomba vyuo bila kuonesha cheti cha Kiingereza
cha TOEFL au IELTS. Mfano, ukiomba vyuo vya
Norway wao kupitia Quota Scheme scholarship
applicants ambao wamesoma high school na
university kwa lugha ya kiingereza hawana haja
ya kuonesha/kufanya mitihani hiyo.
Ushauri wangu, usisubirie zali mpaka upate
exemption hiyo. Maana ni vyuo vichache/nchi
chache zenye kutoa exemption hiyo. Ukisubiria
zali hiyo utasubiria muda mrefu kama ukikosa
chuo husika. Ila ukifanya mtihani wa TOEFL au
IELTS utakuwa umejiongezea wigo wa kuomba
vyuo vingi, scholarships kibao ni LAZIMA uwe na
requirement hii.
Kwa upande wa USA, vyuo vyote na scholarships
zote ni lazima uoneshe cheti cha TOEFL au
IELTS. Ila sharti lingine kwa USA, kwa kila chuo
uombacho, ni lazima utumie original copy of test
results. Na ni wenye kumiliki mtihani wa TOEFL
yaani ETS ndio wenye mamlaka ya kutuma copy
ya matokeo yako ya mtihani kwenye chuo
uombacho. Na kwa kila chuo, copy ya cheti
kimoja lazima ulipie dola 15 kwa kila copy. Hivyo
ni gharama kwani ukiachilia kulipia application
fee let's say dola 70, utalipia tena dola 15 ya
TOEFL cheti kutumwa kwenye chuo. Kamwe
hawachukui copy ya matokeo toka kwako.
GRE na GMAT
Ulaya wao hawana hii mitihani ya GRE na GMAT.
Hii ni mitihani kama unataka kusoma USA only.
Mitihani hii ni kama ile matriculation enzi zile
kuingia chuoni. GRE (Graduate Record Exam) ni
kwa applicants ambao wanataka kusoma non-
management programs. Na kwa GMAT (Graduate
Management Admission Test) ni kwa wale
wanaotaka kusoma Management Programs.
Mitihani hii yote gharama yake ni kama dola 185
na inafanyikia pale kwa Mwalimu Nyerere, chuo
kikuu.
Ukiachilia gharama ya mtihani, kwa kila copy
moja utakayopata/utakayotuma kwenye chuo ni
dola 27. Kumbuka chuo chochote huku
hakichukui cheti/copy toka kwa applicant, all
results should be sent from official owners of the
exam, yaani ETS. Na hakuna chuo utakachopata
iwe ni kwa masters au PhD bila ya GRE au GMAT
exam.
Gharama unaiona: Kwa USA, kuna application fee
kati ya dola 50-100 kutegemeana na chuo, kuna
TOEFL, GRE, pamoja na gharama ya kila cheti/
copy utakayotuma kwenye chuo. Hivyo gharama
ya application ya chuo kimoja ni kama dola
100-120 kutegemeana na chuo, na bado unaweza
kukosa kwani mwombaji sio wewe peke yako.
Hivyo kiushauri, huwa ni vyema mtu kuomba vyuo
vingi vya ulaya sababu za gharama, na kama
ukiomba USA basi viwe vichache unless lengo
lako liwe ni lazima usome USA tu hivyo utaingia
gharama hizo.

Edited by Ommy Lee. 🏃🏼



 TOFAUTI YA KUOMBA MASTERS,
P HD KWA U LAYA NA MAREKANI, C ANADA
Ukiachilia kujumuisha mambo yote ya jumla
katika uombaji scholarship kama vile
recommendation letters, sample writing,
application nk, kuna utofauti uliopo ambao
utakusaidia kufanya maamuzi ya wapi uombe.
a) Application Fee:
Vyuo vya ulaya havina Application Fee. Hili ni
jambo muhimu sana, maana itakusaidia kuomba
vyuo vingi bure. Gharama ni za kutuma
documents kwa njia ya posta nk.
Kwa upande wa USA na Canada hii ni tofauti.
Kwa kila chuo uombacho, unatakiwa kulipa si
chini ya dola 50-100 kama fee. Hii kwa maisha
ya Kitanzania ni hela kubwa ukizingatia
unatakiwa uombe vyuo vingi ujiwekee uwezekano
wa kupata.
b) Admission Exams
TOEFL au IELTS
Kwa upande wa Ulaya, wao wana mtihani mmoja
wa English Proficiency. Unatakiwa kufanya aidha
mtihani wa TOEFL (Test of English as Foreign
Language) au IELTS (International English
Language Testing System). Huo mtihani wa
TOEFL ni wa kimarekani unafanyikia pale Chuo
cha Mwalimu Nyerere kule Kigamboni, ambapo
ada ya mtihani huo ni kama dola 185. Na mtihani
wa IELTS ni wa waingereza na hufanyikia pale
British Council ada yake ni kama laki nne hivi.
Unatakiwa kufanya mtihani mmmoja kati ya hiyo
miwili.
Kuna vyuo au nchi chache zinaruhusu applicants
kuomba vyuo bila kuonesha cheti cha Kiingereza
cha TOEFL au IELTS. Mfano, ukiomba vyuo vya
Norway wao kupitia Quota Scheme scholarship
applicants ambao wamesoma high school na
university kwa lugha ya kiingereza hawana haja
ya kuonesha/kufanya mitihani hiyo.
Ushauri wangu, usisubirie zali mpaka upate
exemption hiyo. Maana ni vyuo vichache/nchi
chache zenye kutoa exemption hiyo. Ukisubiria
zali hiyo utasubiria muda mrefu kama ukikosa
chuo husika. Ila ukifanya mtihani wa TOEFL au
IELTS utakuwa umejiongezea wigo wa kuomba
vyuo vingi, scholarships kibao ni LAZIMA uwe na
requirement hii.
Kwa upande wa USA, vyuo vyote na scholarships
zote ni lazima uoneshe cheti cha TOEFL au
IELTS. Ila sharti lingine kwa USA, kwa kila chuo
uombacho, ni lazima utumie original copy of test
results. Na ni wenye kumiliki mtihani wa TOEFL
yaani ETS ndio wenye mamlaka ya kutuma copy
ya matokeo yako ya mtihani kwenye chuo
uombacho. Na kwa kila chuo, copy ya cheti
kimoja lazima ulipie dola 15 kwa kila copy. Hivyo
ni gharama kwani ukiachilia kulipia application
fee let's say dola 70, utalipia tena dola 15 ya
TOEFL cheti kutumwa kwenye chuo. Kamwe
hawachukui copy ya matokeo toka kwako.
GRE na GMAT
Ulaya wao hawana hii mitihani ya GRE na GMAT.
Hii ni mitihani kama unataka kusoma USA only.
Mitihani hii ni kama ile matriculation enzi zile
kuingia chuoni. GRE (Graduate Record Exam) ni
kwa applicants ambao wanataka kusoma non-
management programs. Na kwa GMAT (Graduate
Management Admission Test) ni kwa wale
wanaotaka kusoma Management Programs.
Mitihani hii yote gharama yake ni kama dola 185
na inafanyikia pale kwa Mwalimu Nyerere, chuo
kikuu.
Ukiachilia gharama ya mtihani, kwa kila copy
moja utakayopata/utakayotuma kwenye chuo ni
dola 27. Kumbuka chuo chochote huku
hakichukui cheti/copy toka kwa applicant, all
results should be sent from official owners of the
exam, yaani ETS. Na hakuna chuo utakachopata
iwe ni kwa masters au PhD bila ya GRE au GMAT
exam.
Gharama unaiona: Kwa USA, kuna application fee
kati ya dola 50-100 kutegemeana na chuo, kuna
TOEFL, GRE, pamoja na gharama ya kila cheti/
copy utakayotuma kwenye chuo. Hivyo gharama
ya application ya chuo kimoja ni kama dola
100-120 kutegemeana na chuo, na bado unaweza
kukosa kwani mwombaji sio wewe peke yako.
Hivyo kiushauri, huwa ni vyema mtu kuomba vyuo
vingi vya ulaya sababu za gharama, na kama
ukiomba USA basi viwe vichache unless lengo
lako liwe ni lazima usome USA tu hivyo utaingia
gharama hizo.

Edited by Ommy Lee. 🏃🏼

Thursday, 21 April 2016

HAJI MANARA AMFANYIA KITU MBAYA JERRY MURO

Katika Hali Isiyokuwa Ya Kawaida Msemaji Wa Klabu Ya Simba Haji Manara Leo Ameamua Kumpiga Vibaya Sana Kwa Knock Out Msemaji Wa Klabu Ya Yanga Jerry Muro.

 Baada Ya Ubishani Mkubwa Wa Ni Timu Gani Kweli au Hakika Inastahili Kuitwa au Kujiita YA KIMATAIFA au WA KIMATAIFA Kutokana Na Rekodi ZaKUTUKUKA Ilizonazo Hiyo Timu.

Hiki Ndicho Msemaji Wa Simba Alichokisema...........Waungwana kila uchwao kwenye jiji hili na viunga vyake sambamba na maeneo mengi ya nchi, kuna neno wa ‘kimataifa’ hulisikia likiimbwa.

Waimbaji wakuu wa neno hilo ni mashabiki wa Yanga wakiongozwa na mpiga zumari wao aliyeacha kazi yake na kujigeuza muimbaji.

Kinyume chake hilo neno klabu ya Simba huitwa wa ‘mchangani’ au wa ‘matopeni’.

 Wengi wananilaumu kuwa kwa nini huwa sijibu neno lolote la ajabu kwa Yanga.

Jibu langu ni jepesi tu, lazima tujitofautishe msemaji wa klabu na mropokaji wa klabu.

Mimi hupenda kuzungumzia issues sio porojo au lugha za uchochoroni. Haiwezekani nikawa kiongozi kisha nikaongea lugha za mashabiki ‘maandazi’.

Kwa hiyo mtaniwia radhi wapenzi wa mpira kwa kutokuwa muimbaji wa ngonjera za uchochoroni.

Mara zote nitabaki msemaji wa klabu kubwa nchini na ntaongea facts kwa kadri zilivyo.

Wadau zisomeni sifa za kimataifa kwa klabu ya Simba nje ya nchi halafu zifananisheni na timu nyingine nchini.Walau kama zitafikia nusu tunawaruhusu watafute tusi jipya.

 Ombi langu kwenu isambazeni taarifa hii katak kilamtandao wa kijamii kisha waseme wao wanaojiita wa kimataifa.

1. Simba ndiyo timu ya kwanza nchini kupanda ndege na hii ilikuwa mwaka 1963 tena wakati huo taifa la Tanzania halikuwa limeundwa, ilikwenda Ethiopia kwa mwaliko wa rais wa taifa hilo Haile Selassie.

2. Simba ndiyo timu ya kwanza kuvaa jezi na hii ilikuwa 1938 ilipocheza na kombaini ya mabaharia wa meli zilizotia nanga kwenye bandari ya Dar es salaam.

3. Simba ndiyo timu ya kwanza kuvaa viatu nchini na hii ilikuwa1949 ilipocheza na kombaini ya jeshi la majini Navy ya Afrika Kusini.

4. Simba ndiyo timu ya kwanza kuwa na basi lake yenyewe na hili lilinuliwa mwaka1968.

5. Simba ndiyo timu ya kwanza kumiliki jengo lake lenyewe na hili lilizinduliwa 1971.

6. Simba ndiyo timu ya kwanza kuwa bingwa wa ligi kuu nchini1966.

7. Simba ndiyo timu ya kwanza kuwakilisha nchi na hii ilikuwa 1967.

8. Simba klabu ya kwanza nchini kwenda Ulaya na hii ilikuwa 1974 ilipokwenda Poland

9. Simba ndiyo timu ya kwanza kuwa mabingwa wa Afrika Mashariki na kati na hii ilikuwa 1974.

10.Simba ndio mabingwa wa kihistoria wa Afrika Mashariki na Kati, ndiyo timu iliyochukua ubingwa mara nyingi kuliko klabu yeyote Afrika Mashariki na Kati (Champs off all time.)

11.Simba ndiyo timu pekee nchini iliyowahi kufika nusu fainali ya klabu bingwa Afrika na hii ilikuwa1974.

12.Simba ndiyo timu pekee nchini na Afrika Mashariki kufika fainali ya kombe la Caf na hii ilikuwa1993.

13.Simba ndio timu inayoshikilia rekodi Afrika kama si duniani kwa kufungwa na Mufurila Wonderers ya Zambia magoli 4-0 na kwenda kuibamiza 5-0 kwao, mbele ya Rais wao Kenneth Kaunda.

Hii haijafanywa na klabu yeyote Afrika na nina mashaka duniani, hii ilikuwa 1979.

14.Simba ilicheza katik hatua ya makundi ya klabu bingwa Afrika 2003 kwa mafanikio makubwa kulinganisha na timu yoyote nchini.

15.Simba ndiyo timu pekee kuivua ubingwa klabu bingwaAfrika nadi Zamalek hii ilikuwa pia 2003.

16.Simba ndiyo klabu pekee nchini kuzifunga timu zote za mataifa ya kiarabu kuanzia· Waliowatoa mwaka jana Etoile du Sahel (Tunisia)·
Widad Casablanca (Morocco)·
 El Setif (Algeria)·
 El Harach (Algeria)
halaf tumezifunga timu zote kubwa za Misri Zamelek,Al Ahly, Arab Contractors, Ismailia, Mehala, Al kubra na timunyingine mnajua huwa inafanywaje ikigusa kule.
Pia imeshaitoa El Merekh ya Sudan 1994 katak klabu bingwa ya Afrika.

Simba pia imeshazifunga miamba ya Afrika Magharibi kuanzia Asec, Asante Kotoko, Hafia ya Guinea hata mabingwa wa kihistoria wa Zambia Nkana Red Devils.

17. Tukirudi juu Simba ndiyo timu ya kwanza kuvaa suti na hii ilikuwa 1974 ilipokwenda Poland.

18.Simba ndiyo klabu pekee nchini kujenga jengo lake yenyewe kwa nguvu za wanachama na mashabiki, wenzetu ni mkopo na msaada toka kwa mzee Karume100%, Simba ilipewa kiasi flan na mzee karume baada ya jengo kukamilika na hii ilikuwa mwanzoni mwamiaka ya 70.

19.Angalia idadi ya wachezaji wa Simba walioenda Ulaya kucheza soka la kulipwa.· Nico Njohole· Deo Njohole· Kassim Matitu· George Kulagwa

Huku ikiwa na makumi ya nyota wake kadhaa waliowahI kutapakaa sehemu mbalimbali duniani.

Nikutajie wachache.· Khalid Abeid· Haidar Abeid· Martin Kikwa· Athman Mambosasa· Zamoyoni Mogella· Hamis Gaga· Lilla Shomari· Iddi Pazi· Kiwelu Mussa· George Masatu· Hussein masha na wengine wengi.bila kumsahau nguli wa sasa mbwana samata.mutoto ya msimbazi.

Na hapa kumbukumbu zikae vizuri wazee wangu mimi, Sunday na Kassim Manara wakati wanaenda kucheza Ulaya hawakuwa wachezaji wa Yanga, walikuwa wakicheza Pan African.

20. Nimalizie kwa kuwaambia FIFA ilizitaja timu bora za karne kwa kila nchi kwa Tanzania Simba ilitajwa ndio timu bora ya karne na wenye mpira wao FIFA.

 Nenda kwenye rekodi za Caf ndio utajua nani wa kimataifa bainaya cc na wao.

Porojo za mjini ntakuwa nimezimaliza sasa na anayebisha abishe kwa data. Wakoloni wetu walitufundisha hivi…No reaserch no data no right to speak.
Tafsiri isiyo rasmi, hujafanya utafiti na huna takwimu funga bakuli lako.

Asanteni na nendeni mkawaambie.Haji S ManaraMsemaji wa klabu bora ya muda wote Tanzania (best club of all time)

Ukiona errors zipotezee jadili issues na nnaruhusu challenges kama zipoPorojo peleka kuleeeeeee.

Nimalizie Tu Kwa Kusema Msemaji Wa VYURA FC au Yanga Football Club Jerry Muro Anyamaze

Kwani Sasa Wanasimba Wameamua Kutembea Na Facts Hizi Ambapo Sasa Watakuwa Kama Wakimsikia Anaikashifu au Kuitukana Simba Sports Club Basi Na Wao Watamkabidhi Hizi Data Ili Kusudi Na Yeye Pia Atupatie Za Yanga Kama Zipo.

Shikamoo Msemaji Wa Simba Sports Club Haji Manara Hakika Leo Umemaliza Kila kitu

 Ningeshauri Sana Ewe Mwana Yanga Football Club Yoyote Utakayeiona Hii Na Kuisoma Basi Si Vibaya Ukaisambaza Kwa Wana Yanga FC Wenzio Popote Pale Walipo au Watakapokuwepo Ili KUMBUKUMBU Hii Muhimu Isije Ikawatoka AKILINI Mwenu. Kila Mwana Yanga Apate Copy Ya Hii Tafadhal

Kusambaza tu tunasambaza

HAJI MANARA AMFANYIA KITU MBAYA JERRY MURO

Katika Hali Isiyokuwa Ya Kawaida Msemaji Wa Klabu Ya Simba Haji Manara Leo Ameamua Kumpiga Vibaya Sana Kwa Knock Out Msemaji Wa Klabu Ya Yanga Jerry Muro.

 Baada Ya Ubishani Mkubwa Wa Ni Timu Gani Kweli au Hakika Inastahili Kuitwa au Kujiita YA KIMATAIFA au WA KIMATAIFA Kutokana Na Rekodi ZaKUTUKUKA Ilizonazo Hiyo Timu.

Hiki Ndicho Msemaji Wa Simba Alichokisema...........Waungwana kila uchwao kwenye jiji hili na viunga vyake sambamba na maeneo mengi ya nchi, kuna neno wa ‘kimataifa’ hulisikia likiimbwa.

Waimbaji wakuu wa neno hilo ni mashabiki wa Yanga wakiongozwa na mpiga zumari wao aliyeacha kazi yake na kujigeuza muimbaji.

Kinyume chake hilo neno klabu ya Simba huitwa wa ‘mchangani’ au wa ‘matopeni’.

 Wengi wananilaumu kuwa kwa nini huwa sijibu neno lolote la ajabu kwa Yanga.

Jibu langu ni jepesi tu, lazima tujitofautishe msemaji wa klabu na mropokaji wa klabu.

Mimi hupenda kuzungumzia issues sio porojo au lugha za uchochoroni. Haiwezekani nikawa kiongozi kisha nikaongea lugha za mashabiki ‘maandazi’.

Kwa hiyo mtaniwia radhi wapenzi wa mpira kwa kutokuwa muimbaji wa ngonjera za uchochoroni.

Mara zote nitabaki msemaji wa klabu kubwa nchini na ntaongea facts kwa kadri zilivyo.

Wadau zisomeni sifa za kimataifa kwa klabu ya Simba nje ya nchi halafu zifananisheni na timu nyingine nchini.Walau kama zitafikia nusu tunawaruhusu watafute tusi jipya.

 Ombi langu kwenu isambazeni taarifa hii katak kilamtandao wa kijamii kisha waseme wao wanaojiita wa kimataifa.

1. Simba ndiyo timu ya kwanza nchini kupanda ndege na hii ilikuwa mwaka 1963 tena wakati huo taifa la Tanzania halikuwa limeundwa, ilikwenda Ethiopia kwa mwaliko wa rais wa taifa hilo Haile Selassie.

2. Simba ndiyo timu ya kwanza kuvaa jezi na hii ilikuwa 1938 ilipocheza na kombaini ya mabaharia wa meli zilizotia nanga kwenye bandari ya Dar es salaam.

3. Simba ndiyo timu ya kwanza kuvaa viatu nchini na hii ilikuwa1949 ilipocheza na kombaini ya jeshi la majini Navy ya Afrika Kusini.

4. Simba ndiyo timu ya kwanza kuwa na basi lake yenyewe na hili lilinuliwa mwaka1968.

5. Simba ndiyo timu ya kwanza kumiliki jengo lake lenyewe na hili lilizinduliwa 1971.

6. Simba ndiyo timu ya kwanza kuwa bingwa wa ligi kuu nchini1966.

7. Simba ndiyo timu ya kwanza kuwakilisha nchi na hii ilikuwa 1967.

8. Simba klabu ya kwanza nchini kwenda Ulaya na hii ilikuwa 1974 ilipokwenda Poland

9. Simba ndiyo timu ya kwanza kuwa mabingwa wa Afrika Mashariki na kati na hii ilikuwa 1974.

10.Simba ndio mabingwa wa kihistoria wa Afrika Mashariki na Kati, ndiyo timu iliyochukua ubingwa mara nyingi kuliko klabu yeyote Afrika Mashariki na Kati (Champs off all time.)

11.Simba ndiyo timu pekee nchini iliyowahi kufika nusu fainali ya klabu bingwa Afrika na hii ilikuwa1974.

12.Simba ndiyo timu pekee nchini na Afrika Mashariki kufika fainali ya kombe la Caf na hii ilikuwa1993.

13.Simba ndio timu inayoshikilia rekodi Afrika kama si duniani kwa kufungwa na Mufurila Wonderers ya Zambia magoli 4-0 na kwenda kuibamiza 5-0 kwao, mbele ya Rais wao Kenneth Kaunda.

Hii haijafanywa na klabu yeyote Afrika na nina mashaka duniani, hii ilikuwa 1979.

14.Simba ilicheza katik hatua ya makundi ya klabu bingwa Afrika 2003 kwa mafanikio makubwa kulinganisha na timu yoyote nchini.

15.Simba ndiyo timu pekee kuivua ubingwa klabu bingwaAfrika nadi Zamalek hii ilikuwa pia 2003.

16.Simba ndiyo klabu pekee nchini kuzifunga timu zote za mataifa ya kiarabu kuanzia· Waliowatoa mwaka jana Etoile du Sahel (Tunisia)·
Widad Casablanca (Morocco)·
 El Setif (Algeria)·
 El Harach (Algeria)
halaf tumezifunga timu zote kubwa za Misri Zamelek,Al Ahly, Arab Contractors, Ismailia, Mehala, Al kubra na timunyingine mnajua huwa inafanywaje ikigusa kule.
Pia imeshaitoa El Merekh ya Sudan 1994 katak klabu bingwa ya Afrika.

Simba pia imeshazifunga miamba ya Afrika Magharibi kuanzia Asec, Asante Kotoko, Hafia ya Guinea hata mabingwa wa kihistoria wa Zambia Nkana Red Devils.

17. Tukirudi juu Simba ndiyo timu ya kwanza kuvaa suti na hii ilikuwa 1974 ilipokwenda Poland.

18.Simba ndiyo klabu pekee nchini kujenga jengo lake yenyewe kwa nguvu za wanachama na mashabiki, wenzetu ni mkopo na msaada toka kwa mzee Karume100%, Simba ilipewa kiasi flan na mzee karume baada ya jengo kukamilika na hii ilikuwa mwanzoni mwamiaka ya 70.

19.Angalia idadi ya wachezaji wa Simba walioenda Ulaya kucheza soka la kulipwa.· Nico Njohole· Deo Njohole· Kassim Matitu· George Kulagwa

Huku ikiwa na makumi ya nyota wake kadhaa waliowahI kutapakaa sehemu mbalimbali duniani.

Nikutajie wachache.· Khalid Abeid· Haidar Abeid· Martin Kikwa· Athman Mambosasa· Zamoyoni Mogella· Hamis Gaga· Lilla Shomari· Iddi Pazi· Kiwelu Mussa· George Masatu· Hussein masha na wengine wengi.bila kumsahau nguli wa sasa mbwana samata.mutoto ya msimbazi.

Na hapa kumbukumbu zikae vizuri wazee wangu mimi, Sunday na Kassim Manara wakati wanaenda kucheza Ulaya hawakuwa wachezaji wa Yanga, walikuwa wakicheza Pan African.

20. Nimalizie kwa kuwaambia FIFA ilizitaja timu bora za karne kwa kila nchi kwa Tanzania Simba ilitajwa ndio timu bora ya karne na wenye mpira wao FIFA.

 Nenda kwenye rekodi za Caf ndio utajua nani wa kimataifa bainaya cc na wao.

Porojo za mjini ntakuwa nimezimaliza sasa na anayebisha abishe kwa data. Wakoloni wetu walitufundisha hivi…No reaserch no data no right to speak.
Tafsiri isiyo rasmi, hujafanya utafiti na huna takwimu funga bakuli lako.

Asanteni na nendeni mkawaambie.Haji S ManaraMsemaji wa klabu bora ya muda wote Tanzania (best club of all time)

Ukiona errors zipotezee jadili issues na nnaruhusu challenges kama zipoPorojo peleka kuleeeeeee.

Nimalizie Tu Kwa Kusema Msemaji Wa VYURA FC au Yanga Football Club Jerry Muro Anyamaze

Kwani Sasa Wanasimba Wameamua Kutembea Na Facts Hizi Ambapo Sasa Watakuwa Kama Wakimsikia Anaikashifu au Kuitukana Simba Sports Club Basi Na Wao Watamkabidhi Hizi Data Ili Kusudi Na Yeye Pia Atupatie Za Yanga Kama Zipo.

Shikamoo Msemaji Wa Simba Sports Club Haji Manara Hakika Leo Umemaliza Kila kitu

 Ningeshauri Sana Ewe Mwana Yanga Football Club Yoyote Utakayeiona Hii Na Kuisoma Basi Si Vibaya Ukaisambaza Kwa Wana Yanga FC Wenzio Popote Pale Walipo au Watakapokuwepo Ili KUMBUKUMBU Hii Muhimu Isije Ikawatoka AKILINI Mwenu. Kila Mwana Yanga Apate Copy Ya Hii Tafadhal

Kusambaza tu tunasambaza

Saturday, 16 April 2016

Jürgen Klopp's press conference to preview Bournemouth game. Updates to follow:

Klopp: That was Thursday, today is Saturday and tomorrow it's Bournemouth. Of course it was wonderful. Game like that influences everything.

Klopp: "The atmosphere was like what I heard about. Driving through the streets was a great experience for all the lads."

Klopp on semi draw: "I don't think about Villarreal in this moment. We have sorted out organisation but there are 3 games before that."

Klopp: "It's not about dreaming of the final. How can we do that? We haven't played one minute of the semi-final yet."

Klopp on Can being out for 4 to 6 weeks: "It's a ligament in the ankle. It's not best news. We'll try everything to get him back."

Klopp: "Nobody told me about what would happen before the game with the fans. The players wanted to say a big thank-you."

Klopp: "Yes, we can reach those heights again. I just don't know when. You must believe things like this are possible."

Klopp: "It was all about the lads and the crowd. It was all about that special relationship."

Klopp: "We have to find other solutions. It's not about moaning about losing Emre."

Klopp on Lovren: "You have to use good moments. I don't have a bad word to say about Dejan Lovren."

Klopp: "The Sakho goal was only possible because of Sturridge's movement from the corner. He also played a key pass for Lovren's goal."

Klopp: "If someone here would like to talk about Bournemouth it would help me to focus on that game."

Klopp on Eddie Howe: "He's done a brilliant job. They had bad injuries to key players. I really like the way they handled that situation."

Klopp: "He's the most exciting manager in this league. He's still young. What he's done is really impressive."

Klopp: "We have to make changes for sure. Bournemouth have played a lot less games. But we'll go there to try to win with what we have."

Klopp: "We used the story of Istanbul. Maybe in years to come the next generation of #LFC players will use the Dortmund game."

YNWA.

Jürgen Klopp's press conference to preview Bournemouth game. Updates to follow:

Klopp: That was Thursday, today is Saturday and tomorrow it's Bournemouth. Of course it was wonderful. Game like that influences everything.

Klopp: "The atmosphere was like what I heard about. Driving through the streets was a great experience for all the lads."

Klopp on semi draw: "I don't think about Villarreal in this moment. We have sorted out organisation but there are 3 games before that."

Klopp: "It's not about dreaming of the final. How can we do that? We haven't played one minute of the semi-final yet."

Klopp on Can being out for 4 to 6 weeks: "It's a ligament in the ankle. It's not best news. We'll try everything to get him back."

Klopp: "Nobody told me about what would happen before the game with the fans. The players wanted to say a big thank-you."

Klopp: "Yes, we can reach those heights again. I just don't know when. You must believe things like this are possible."

Klopp: "It was all about the lads and the crowd. It was all about that special relationship."

Klopp: "We have to find other solutions. It's not about moaning about losing Emre."

Klopp on Lovren: "You have to use good moments. I don't have a bad word to say about Dejan Lovren."

Klopp: "The Sakho goal was only possible because of Sturridge's movement from the corner. He also played a key pass for Lovren's goal."

Klopp: "If someone here would like to talk about Bournemouth it would help me to focus on that game."

Klopp on Eddie Howe: "He's done a brilliant job. They had bad injuries to key players. I really like the way they handled that situation."

Klopp: "He's the most exciting manager in this league. He's still young. What he's done is really impressive."

Klopp: "We have to make changes for sure. Bournemouth have played a lot less games. But we'll go there to try to win with what we have."

Klopp: "We used the story of Istanbul. Maybe in years to come the next generation of #LFC players will use the Dortmund game."

YNWA.

Kutokwa na Uchafu Ukeni
Kwa kawaida mwanamke hutokwa na majimaji mepesi (vaginal fluids) yenye rangi nyeupe au ya njano. Inapotokea anatokwa na majimaji yenye ute mzito wenye rangi nyeupe au kahawia na yanatoa harufu kali na muwasho, hiyo huwa ni ishara ya ugonjwa uitwao wa kutokwa uchafu ukeni ujulikanao kwa kitaalamu kama ‘Vaginosis’.
Mwanamke mwenye tatizo hili hujisikia vibaya na anaweza akaacha kushiriki tendo la ndoa ama kwa kuhofia maumivu au kwa kuona aibu kwani mwanaume ni vigumu kuvumilia harufu hiyo au hata kuuona tu huo ute ute kwani humjengea hisia kwamba mwenza wake atakuwa na magonjwa ya zinaa au si mwaminifu kwa ujumla.
Kinachosababisha kutokwa na uchafu ukeni:
• Kuwa na wapenzi wengi
• Baadhi ya dawa za uzazi wa mpango
• Kusafisha uke kwa kutumia dawa zenye kemikali
• Uchafu
• Uvutaji sigara
• Pombe
• Maambukizi ya Bakteria au bakteria wabaya wanapozidi ukeni
Dalili:
• Kutokwa na uchafu usio wa kawaida
• Kutokwa na uchafu wenye harufu kali kama shombo ya samaki au kitu kilichooza
• Kuwashwa sehemu za siri na ndani ya uke
• Uke unaweza kubadilika na kuwa na rangi nyekundu
• Maumivu sehemu za siri wakati wa kukojoa
• Maumivu makali chini ya kitovu
• Kutokwa uchafu uliochanganyika na damu
Matibabu
Mara uonapo dalili hizo unashauriwa kwenda kumuona daktari haraka iwezekanavyo kwa vipimo zaidi na dawa zaweza kuwa ni za kunywa au za kupaka.
Pia unaweza kutumia dawa za asili zifuatazo:
1. Kitunguu Swaumu
Kitunguu swaumu ndiyo dawa ya asili nzuri kuliko zote kwa ajili ya maambukizi ya maambukizi ya bakteria kwa wanawake. Kitunguu swaumu ni antibiotiki ya asili na hufanya kazi ya kuua bakteria wasababishao huu uchafu ukeni bila shida yoyote.
Menya punje 3 au 5 za kitunguu swaumu na uzifunge vizuri ndani ya kitambaa laini na ingiza ndani ya uke wako kwa masaa 6 hivi kicha ukitoe. Pia menye punje 8 mpaka 10 za kitunguu swaumu na uzikate vipande vidogo vidogo (chop) na unywe na maji nusu lita asubuhi ukiamka tu na usiku unapoenda kulala kwa wiki mbili mpaka tatu.
2. Mtindi
Chukua mtindi ujazo wa kijiko kidogo cha chain a utumbukize ndani ya uke wako na uache huko usiku mzima. Mtindi una bakteria wazuri wanaohitajika ukeni kuweka sawa usawa wa PH (alikalini na asidi) na hivyo kuondoa maambukizi. Pia unashauriwa kula tu huu mtindi mara mbili kwa siku kuongeza kinga ya mwili wako kwa ujumla dhidi ya magonjwa mbalimbali
3. Siki ya tufaa
Chovya pamba ndani ya siki ya tufaa (apple cider vinegar) na uweke ndani ya uke kwa dakika 15 hadi 20 kila siku na bakteria wabaya wote watakufa.
4. Uwatu
Loweka kijiko kidogo cha mbegu za uwatu (fenugreek seeds) ndani ya maji glasi moja na uache kwa usiku mzima. Kesho yake asubuhi maji haya yaliyolowekwa mbegu za uwatu kabla ya kula au kunywa chochote. Uwatu husaidia kuweka sawa homoni za mwili na kuweka sawa mzunguko wa hedhi.
5. Maziwa na binzari
Changanya kijiko kimoja cha chai cha binzari (manjano) ya unga na kikombe kimoja cha maziwa ya moto na unywe mara mbili kila siku mpaka tatizo litakapoisha.
6. LEMONADE:
Lemonade inaandaliwa kwa kutumia limau na asali na mdalasini ya unga kidogo, nayo inaandaliwa hivi:
* Chukua asali nusu Lita
*Chukua limau kubwa 12, zikate katikati kila moja. Tumbukiza ndani ya sufuria na weka maji Lita 3, chemsha mpaka limau ziive (zisiive sana), ipua utowe zile nyama nyama za ndani za liamau moja baada ya nyingine, ganda la nje tupa na uchuje kupata juisi ambayo itakuwa na ujazo wa lita 2 na nusu hivi.
Kwenye sufuria nyingine kubwa changanya ile asali nusu Lita na hiyo juisi ya limau Lita 2 na nusu, ongeza maji Safi ya kawaida Lita 2 ili kupata lemonade ya ujazo wa lita 5. Ihifadhi katika friji
Kunywa robo Lita kutwa mara 2 kwa siku 10 hadi 11 hivi.
Unaweza kuongeza vijiko vikubwa vitatu vya mdalasini ya Unga ndani ya hii juisi ya LEMONADE
7. Jeli ya mshubiri (aloe vera jel):
Ingawa jeli fresh ya mshubiri haitibu moja kwa moja tatizo la kutokwa na uchafu ukeni inaweza kuwa msaada mkubwa katika kupunguza maumivu na muwasho ukeni. Chana kipande kidogo cha jani la mmea huu na ukamue kidogo kupata maji maji yake na upake vizuri taratibu ndani ya uke mara mbili kwa siku kwa majuma kadhaa hadi muwasho utakapoisha.
MAMBO MHIMU YA KUZINGATIA:
*Kunywa maji mengi kila siku kuanzia glasi 8 hadi 10
*Punguza vyakula vyenye wanga
*Acha kutumia sukari na badala yake tumia asali
*Acha vinywaji baridi, acha pia chai ya rangi na kahawa
*Acha matumizi ya pafyumu hasa maeneo ya huko
*Acha kutumia vidonge vya uzazi wa mpango, hii ni kwa sababu vidonge hivi vinasemwa huwa vinasababisha kushuka kwa kinga ya mwili na kukufanya mrahisi kupata maambukizi ya fangasi.
*Epuka mapenzi kinyume na maumbile
*Kuwa na mpenzi mmoja tu
*Pendelea kujiweka msafi muda wote
*Oga maji ya moto
Kwa maswali na ushauri zaidi: WhatsApp
+447399054714
Sami

Kutokwa na Uchafu Ukeni
Kwa kawaida mwanamke hutokwa na majimaji mepesi (vaginal fluids) yenye rangi nyeupe au ya njano. Inapotokea anatokwa na majimaji yenye ute mzito wenye rangi nyeupe au kahawia na yanatoa harufu kali na muwasho, hiyo huwa ni ishara ya ugonjwa uitwao wa kutokwa uchafu ukeni ujulikanao kwa kitaalamu kama ‘Vaginosis’.
Mwanamke mwenye tatizo hili hujisikia vibaya na anaweza akaacha kushiriki tendo la ndoa ama kwa kuhofia maumivu au kwa kuona aibu kwani mwanaume ni vigumu kuvumilia harufu hiyo au hata kuuona tu huo ute ute kwani humjengea hisia kwamba mwenza wake atakuwa na magonjwa ya zinaa au si mwaminifu kwa ujumla.
Kinachosababisha kutokwa na uchafu ukeni:
• Kuwa na wapenzi wengi
• Baadhi ya dawa za uzazi wa mpango
• Kusafisha uke kwa kutumia dawa zenye kemikali
• Uchafu
• Uvutaji sigara
• Pombe
• Maambukizi ya Bakteria au bakteria wabaya wanapozidi ukeni
Dalili:
• Kutokwa na uchafu usio wa kawaida
• Kutokwa na uchafu wenye harufu kali kama shombo ya samaki au kitu kilichooza
• Kuwashwa sehemu za siri na ndani ya uke
• Uke unaweza kubadilika na kuwa na rangi nyekundu
• Maumivu sehemu za siri wakati wa kukojoa
• Maumivu makali chini ya kitovu
• Kutokwa uchafu uliochanganyika na damu
Matibabu
Mara uonapo dalili hizo unashauriwa kwenda kumuona daktari haraka iwezekanavyo kwa vipimo zaidi na dawa zaweza kuwa ni za kunywa au za kupaka.
Pia unaweza kutumia dawa za asili zifuatazo:
1. Kitunguu Swaumu
Kitunguu swaumu ndiyo dawa ya asili nzuri kuliko zote kwa ajili ya maambukizi ya maambukizi ya bakteria kwa wanawake. Kitunguu swaumu ni antibiotiki ya asili na hufanya kazi ya kuua bakteria wasababishao huu uchafu ukeni bila shida yoyote.
Menya punje 3 au 5 za kitunguu swaumu na uzifunge vizuri ndani ya kitambaa laini na ingiza ndani ya uke wako kwa masaa 6 hivi kicha ukitoe. Pia menye punje 8 mpaka 10 za kitunguu swaumu na uzikate vipande vidogo vidogo (chop) na unywe na maji nusu lita asubuhi ukiamka tu na usiku unapoenda kulala kwa wiki mbili mpaka tatu.
2. Mtindi
Chukua mtindi ujazo wa kijiko kidogo cha chain a utumbukize ndani ya uke wako na uache huko usiku mzima. Mtindi una bakteria wazuri wanaohitajika ukeni kuweka sawa usawa wa PH (alikalini na asidi) na hivyo kuondoa maambukizi. Pia unashauriwa kula tu huu mtindi mara mbili kwa siku kuongeza kinga ya mwili wako kwa ujumla dhidi ya magonjwa mbalimbali
3. Siki ya tufaa
Chovya pamba ndani ya siki ya tufaa (apple cider vinegar) na uweke ndani ya uke kwa dakika 15 hadi 20 kila siku na bakteria wabaya wote watakufa.
4. Uwatu
Loweka kijiko kidogo cha mbegu za uwatu (fenugreek seeds) ndani ya maji glasi moja na uache kwa usiku mzima. Kesho yake asubuhi maji haya yaliyolowekwa mbegu za uwatu kabla ya kula au kunywa chochote. Uwatu husaidia kuweka sawa homoni za mwili na kuweka sawa mzunguko wa hedhi.
5. Maziwa na binzari
Changanya kijiko kimoja cha chai cha binzari (manjano) ya unga na kikombe kimoja cha maziwa ya moto na unywe mara mbili kila siku mpaka tatizo litakapoisha.
6. LEMONADE:
Lemonade inaandaliwa kwa kutumia limau na asali na mdalasini ya unga kidogo, nayo inaandaliwa hivi:
* Chukua asali nusu Lita
*Chukua limau kubwa 12, zikate katikati kila moja. Tumbukiza ndani ya sufuria na weka maji Lita 3, chemsha mpaka limau ziive (zisiive sana), ipua utowe zile nyama nyama za ndani za liamau moja baada ya nyingine, ganda la nje tupa na uchuje kupata juisi ambayo itakuwa na ujazo wa lita 2 na nusu hivi.
Kwenye sufuria nyingine kubwa changanya ile asali nusu Lita na hiyo juisi ya limau Lita 2 na nusu, ongeza maji Safi ya kawaida Lita 2 ili kupata lemonade ya ujazo wa lita 5. Ihifadhi katika friji
Kunywa robo Lita kutwa mara 2 kwa siku 10 hadi 11 hivi.
Unaweza kuongeza vijiko vikubwa vitatu vya mdalasini ya Unga ndani ya hii juisi ya LEMONADE
7. Jeli ya mshubiri (aloe vera jel):
Ingawa jeli fresh ya mshubiri haitibu moja kwa moja tatizo la kutokwa na uchafu ukeni inaweza kuwa msaada mkubwa katika kupunguza maumivu na muwasho ukeni. Chana kipande kidogo cha jani la mmea huu na ukamue kidogo kupata maji maji yake na upake vizuri taratibu ndani ya uke mara mbili kwa siku kwa majuma kadhaa hadi muwasho utakapoisha.
MAMBO MHIMU YA KUZINGATIA:
*Kunywa maji mengi kila siku kuanzia glasi 8 hadi 10
*Punguza vyakula vyenye wanga
*Acha kutumia sukari na badala yake tumia asali
*Acha vinywaji baridi, acha pia chai ya rangi na kahawa
*Acha matumizi ya pafyumu hasa maeneo ya huko
*Acha kutumia vidonge vya uzazi wa mpango, hii ni kwa sababu vidonge hivi vinasemwa huwa vinasababisha kushuka kwa kinga ya mwili na kukufanya mrahisi kupata maambukizi ya fangasi.
*Epuka mapenzi kinyume na maumbile
*Kuwa na mpenzi mmoja tu
*Pendelea kujiweka msafi muda wote
*Oga maji ya moto
Kwa maswali na ushauri zaidi: WhatsApp
+447399054714
Sami

Thursday, 14 April 2016

MASHABIKI AL AHLY WAONDOKA NA NEMBO YA SIMBA, WATAITUMIA KUMALIZA YANGA MISRI


Mashabiki wa Al Ahly wameondoka na nembo ya klabu ya Simba kwenda nayo Cairo kwa ajili ya kuonyesha shukurani yao kwa Simba.

Mashabiki hao waliokuwa wanaishi eneo la Kariakoo jijini Dar es Salaam, wanajiandaa kutengeneza bendera kubwa ya Simba ambayo wataitumia wakati wakishangilia timu yao itakapokuwa inapambana na Yanga katika mechi ya pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Katika mechi ya kwanza, timu hizo zilitoka sare ya bao 1-1 jijini Dar es Salaam. Mashabiki wa Simba walikuwa wakiwasaidia kushangilia wakiungana na mashabiki wao wa Ultras.


“Tukiwafunga tu, tutaitumia bendera ya Simba kuionyesha wakati tunashangilia. Tunafanya hivyo kuonyesha shukurani yetu kwao,” alisema mmoja wa mashabiki hao ambao kundi la mwisho liliondoka jana kurejea Cairo kuisubiri Yanga wiki ijayo.

MASHABIKI AL AHLY WAONDOKA NA NEMBO YA SIMBA, WATAITUMIA KUMALIZA YANGA MISRI


Mashabiki wa Al Ahly wameondoka na nembo ya klabu ya Simba kwenda nayo Cairo kwa ajili ya kuonyesha shukurani yao kwa Simba.

Mashabiki hao waliokuwa wanaishi eneo la Kariakoo jijini Dar es Salaam, wanajiandaa kutengeneza bendera kubwa ya Simba ambayo wataitumia wakati wakishangilia timu yao itakapokuwa inapambana na Yanga katika mechi ya pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Katika mechi ya kwanza, timu hizo zilitoka sare ya bao 1-1 jijini Dar es Salaam. Mashabiki wa Simba walikuwa wakiwasaidia kushangilia wakiungana na mashabiki wao wa Ultras.


“Tukiwafunga tu, tutaitumia bendera ya Simba kuionyesha wakati tunashangilia. Tunafanya hivyo kuonyesha shukurani yetu kwao,” alisema mmoja wa mashabiki hao ambao kundi la mwisho liliondoka jana kurejea Cairo kuisubiri Yanga wiki ijayo.

Tuesday, 12 April 2016

Umewahi kusikia kuhusu kanisa jipya linanoitwa 'The national church of Bey'?

Msanii Beyonce knowles wa Marekani ameacha maswali mengi baada ya kuanzisha kanisa lake na kuliita "The national church of Bey" means church of Beyonce.
Ambapo yeye ndio Mungu wa kanisa hilo na maelfu ya watu wanamuabudu kwa jina la "mother Bey"

Katika kànisa hilo kuna picha ya Beyonce akionekana na Vazi la yesu, na nyingine akiwa na vazi LA papa wa dhehebu LA RC.

Amekuwa akiitwa Mungu wa kike.. Na dini yake inaitwa "Beyism" ambapo pia wanatumia biblia yao inayoitwa Beyble, inamzungumzia Beyonce kama mwanamke mwenye uwezo wa ajabu kama Mungu na kuamua kumuita Goddess..

Dini hiyo ya Beyism ina waumini maelfu ambapo inaonesha baadhi ya wafuasi wa Mungu huyo Beyonce, watu maarufu kama Kanye west, Mariah carrey na wengine.


Umewahi kusikia kuhusu kanisa jipya linanoitwa 'The national church of Bey'?

Msanii Beyonce knowles wa Marekani ameacha maswali mengi baada ya kuanzisha kanisa lake na kuliita "The national church of Bey" means church of Beyonce.
Ambapo yeye ndio Mungu wa kanisa hilo na maelfu ya watu wanamuabudu kwa jina la "mother Bey"

Katika kànisa hilo kuna picha ya Beyonce akionekana na Vazi la yesu, na nyingine akiwa na vazi LA papa wa dhehebu LA RC.

Amekuwa akiitwa Mungu wa kike.. Na dini yake inaitwa "Beyism" ambapo pia wanatumia biblia yao inayoitwa Beyble, inamzungumzia Beyonce kama mwanamke mwenye uwezo wa ajabu kama Mungu na kuamua kumuita Goddess..

Dini hiyo ya Beyism ina waumini maelfu ambapo inaonesha baadhi ya wafuasi wa Mungu huyo Beyonce, watu maarufu kama Kanye west, Mariah carrey na wengine.


Malisa Godlisten

Alichokifanya Magufuli ni kudhibitisha madai ya muda mrefu ya vyama vya upinzani kuwa ni makosa kumteua mtu aliyekataliwa na wananchi kwa kushindwa "kudeliver".
Kutumbuliwa kwa Anne Kilango Malecela ni heshima kubwa kwa wananchi wa Same Mashariki waliomktaa kwenye sanduku la kura mwaka jana na kumchagua mama Kaboyoka (CHADEMA). Maana yake ni kwamba wanancahi wa Same Mashariki waliugundua udhaifu wa Mama Kilango kabla washauri wa Rais hawajauona.
Haiwezekani mtu aliyekataliwa na wananchi kwa kushindwa kuwajibika apewe mkoa au wilaya kuongoza. Wapinzani wamepiga kelele miaka mingi wakisema kumteua mtu aliyekataliwa na wananchi ni kuwatukana wananchi hao lakini serikali iliziba masikio.
JPM nae hakuamini hiyo falsafa kwa maneno. Akataka afanye experiment ajue kama madai hayo ni kweli au lah. Si unajua huyu ni "Mkemia" kwahiyo kila kitu anaprove.? Akaamua kuprove kwa kuwateua walewale waliokataliwa na wananchi. Sasa ameanza kupata majibu ya "experiment" yake.
Nategemea kabla hajatoka maabara (Ikulu) specimen zifuatazo zitakuwa "zimeshareact" kweny chemichals za "Pombe" na kuungua vibaya;
1. Godfrey Zambi – huyu alikataliwa na wananchi wa Mbozi, Wakamchagua Pascal Haonga (CHADEMA). Lakini JMP akamfanyia experiment na kumteua kuwa RC Lindi. Soon tutaona "reaction".
2. Dkt. Steven Kebwe – Huyu alikataliwa na wananchi wa Serengeti wakamchagua Mwal.Chacha Ryoba (CHADEMA), lakini JPM kuaamua kumfanyia experiment kwa kumpeleka Morogoro. Subiria "chemical reaction" soon.
3. Aggrey Mwanri – huyu alikataliwa na wananchi wa Siha na wakamchagua Dr.Godwin Mollel (CHADEMA). Lakini JPM kaamua kumtest kwa kumpa uRC Tabora. Hapa subiria "Acid-Base reaction".
4. Magesa Mulongo – huyu hakugombea popote lakini hana sifa ya uongozi. Kama umefanya nae kazi utaelewa nachosema. Ni mbabe, ana dharau, na majivuno. Alipigana na Katibu Tawala wa mkoa wa Mwanza kwenye kikao cha Kamati ya ulinzi na usalama lakini Katibu Tawala akafukuzwa kazi yeye akaachwa.
Alipopangiwa kuwa RC Mwanza alikataa nyumba aliyokua akikaa mtangulizi wake Everist Ndikilo kwa madai kuwa haina hadhi yake. Kwahiyo akaenda kupanga Capripoint kwa gharama ya Shilingi milini 7.8 kwa mwezi zilizokua zinalipwa na serikali. JPM alipoingia madarakani akaogopa kutumbuliwa akarudi kwny nyumba ile aliyoikataa na hapa ndio ukaanza ugomvi kati yake na Katibu Tawala.
Kila alipopita huyu jamaa ameacha migogoro. Arusha hawataki kumuona hata kumsikia. Huwa sielewi ilikuaje akapenya kwenye mchujo wa JPM. But haihitaji degree kujua kwamba yupo "maabara" anapimwa. Kapelekwa kwenda kuwa RC mkoa wa Mara, but very soon tegemea kusikia "Solid state reaction" kutoka Musoma.
Malisa GJ.!

Malisa Godlisten

Alichokifanya Magufuli ni kudhibitisha madai ya muda mrefu ya vyama vya upinzani kuwa ni makosa kumteua mtu aliyekataliwa na wananchi kwa kushindwa "kudeliver".
Kutumbuliwa kwa Anne Kilango Malecela ni heshima kubwa kwa wananchi wa Same Mashariki waliomktaa kwenye sanduku la kura mwaka jana na kumchagua mama Kaboyoka (CHADEMA). Maana yake ni kwamba wanancahi wa Same Mashariki waliugundua udhaifu wa Mama Kilango kabla washauri wa Rais hawajauona.
Haiwezekani mtu aliyekataliwa na wananchi kwa kushindwa kuwajibika apewe mkoa au wilaya kuongoza. Wapinzani wamepiga kelele miaka mingi wakisema kumteua mtu aliyekataliwa na wananchi ni kuwatukana wananchi hao lakini serikali iliziba masikio.
JPM nae hakuamini hiyo falsafa kwa maneno. Akataka afanye experiment ajue kama madai hayo ni kweli au lah. Si unajua huyu ni "Mkemia" kwahiyo kila kitu anaprove.? Akaamua kuprove kwa kuwateua walewale waliokataliwa na wananchi. Sasa ameanza kupata majibu ya "experiment" yake.
Nategemea kabla hajatoka maabara (Ikulu) specimen zifuatazo zitakuwa "zimeshareact" kweny chemichals za "Pombe" na kuungua vibaya;
1. Godfrey Zambi – huyu alikataliwa na wananchi wa Mbozi, Wakamchagua Pascal Haonga (CHADEMA). Lakini JMP akamfanyia experiment na kumteua kuwa RC Lindi. Soon tutaona "reaction".
2. Dkt. Steven Kebwe – Huyu alikataliwa na wananchi wa Serengeti wakamchagua Mwal.Chacha Ryoba (CHADEMA), lakini JPM kuaamua kumfanyia experiment kwa kumpeleka Morogoro. Subiria "chemical reaction" soon.
3. Aggrey Mwanri – huyu alikataliwa na wananchi wa Siha na wakamchagua Dr.Godwin Mollel (CHADEMA). Lakini JPM kaamua kumtest kwa kumpa uRC Tabora. Hapa subiria "Acid-Base reaction".
4. Magesa Mulongo – huyu hakugombea popote lakini hana sifa ya uongozi. Kama umefanya nae kazi utaelewa nachosema. Ni mbabe, ana dharau, na majivuno. Alipigana na Katibu Tawala wa mkoa wa Mwanza kwenye kikao cha Kamati ya ulinzi na usalama lakini Katibu Tawala akafukuzwa kazi yeye akaachwa.
Alipopangiwa kuwa RC Mwanza alikataa nyumba aliyokua akikaa mtangulizi wake Everist Ndikilo kwa madai kuwa haina hadhi yake. Kwahiyo akaenda kupanga Capripoint kwa gharama ya Shilingi milini 7.8 kwa mwezi zilizokua zinalipwa na serikali. JPM alipoingia madarakani akaogopa kutumbuliwa akarudi kwny nyumba ile aliyoikataa na hapa ndio ukaanza ugomvi kati yake na Katibu Tawala.
Kila alipopita huyu jamaa ameacha migogoro. Arusha hawataki kumuona hata kumsikia. Huwa sielewi ilikuaje akapenya kwenye mchujo wa JPM. But haihitaji degree kujua kwamba yupo "maabara" anapimwa. Kapelekwa kwenda kuwa RC mkoa wa Mara, but very soon tegemea kusikia "Solid state reaction" kutoka Musoma.
Malisa GJ.!

Sunday, 10 April 2016

Sunday, April 10, 2016
MAYANJA: SINA MATATIZO NA MCHEZAJI YEYOTE SIMBA

Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
KOCHA wa Simba, Jackson Mayanja  amesema hana matatizo na mchezaji hata mmoja na Simba, na hajawahi kugombana na yeyote kati yao.
Na kiungo huyo wa zamani wa kimataifa wa Uganda, amesema kwamba haiwezi kutokea siku akagombana na mchezaji, ila anasikitika sasa kumeibuka kama kampeni ya kumchafulia jina lake kutokana na mafanikio aliyoyapa katika klabu hiyo.
Akizungumza na BIN ZUBEIRY SPORTS – ONLINE jioni ya leo, Mayanja amesema kwamba amesikitishwa na sakata jipya lililoibuka kuhusu mshambuliaji Mganda mwenzake, Hamisi Kiiza.
“Nashangaa kuambiwa nimemfukuza Kiiza, mimi sijafanya hivyo, Kiiza alikuwa anawasiliana na Meneja tu (Abbas Ally) na tatizo lao lilikuwa katika kuvaa sare za timu wakati wa kwenda uwanjani na kupanda basi la timu,”amesema Mayanja.
Kocha huyo wa zamani wa Kagera Sugar, amesema kwamba Meneja Abbas ametoa agizo la kuzuia wachezaji kwenda na gari zao binafsi kambini na pia wachezaji wote kutakiwa kuvaa sare wakati wa misafara ya kitimu.
“Sasa inapotokea mchezaji akakiuka maagizo ya Meneja, ni yeye ndiye anayeshughulikia, siyo mimi, mimi nawasubiri wachezaji uwanjani na Kiiza japokuwa alichelewa kurejea kutoka Uganda, wote yeye na Juuko (Murshid) niliwapokea mazoezini na nimeendelea kuwa nao,”amesema Mayanja.
Kiungo huyo wa zamani wa SC Villa na KCCA za Uganda amesema kwamba, matatizo yaliyojitokeza kati ya Meneja Abbas na Kiiza yamekwisha na mchezaji huyo yupo kambini Ndege Beach, Dar es Salaam kwa maandalizi ya mchezo wa kesho dhidi ya Coastal Union Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Mayanja amesema hata matukio ya awali kuhusu wachezaji Hassan Isihaka na Abdi Banda pia yanapotoshwa, lakini ukweli ni kwamba hakuwahi kugombana na wachezaji hao.
“Ndiyo maana Isihaka baadaye alikuja kuniomba msamaha na leo amemaliza adhabu yake na tupo naye tena kwenye timu, lakini Banda hakuwahi kuja kuniomba msamaha hadi sasa na hajaja tena mazoezini,”amesema.
Aidha, Mayanja amesema hali ya kambi ya Simba ni shwari kabisa kuelekea mchezo wa kesho wa Robo Fainali ya Kombe ka TFF dhidi ya Coastal Union na matarajio kesho ni ushindi.

Sunday, April 10, 2016
MAYANJA: SINA MATATIZO NA MCHEZAJI YEYOTE SIMBA

Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
KOCHA wa Simba, Jackson Mayanja  amesema hana matatizo na mchezaji hata mmoja na Simba, na hajawahi kugombana na yeyote kati yao.
Na kiungo huyo wa zamani wa kimataifa wa Uganda, amesema kwamba haiwezi kutokea siku akagombana na mchezaji, ila anasikitika sasa kumeibuka kama kampeni ya kumchafulia jina lake kutokana na mafanikio aliyoyapa katika klabu hiyo.
Akizungumza na BIN ZUBEIRY SPORTS – ONLINE jioni ya leo, Mayanja amesema kwamba amesikitishwa na sakata jipya lililoibuka kuhusu mshambuliaji Mganda mwenzake, Hamisi Kiiza.
“Nashangaa kuambiwa nimemfukuza Kiiza, mimi sijafanya hivyo, Kiiza alikuwa anawasiliana na Meneja tu (Abbas Ally) na tatizo lao lilikuwa katika kuvaa sare za timu wakati wa kwenda uwanjani na kupanda basi la timu,”amesema Mayanja.
Kocha huyo wa zamani wa Kagera Sugar, amesema kwamba Meneja Abbas ametoa agizo la kuzuia wachezaji kwenda na gari zao binafsi kambini na pia wachezaji wote kutakiwa kuvaa sare wakati wa misafara ya kitimu.
“Sasa inapotokea mchezaji akakiuka maagizo ya Meneja, ni yeye ndiye anayeshughulikia, siyo mimi, mimi nawasubiri wachezaji uwanjani na Kiiza japokuwa alichelewa kurejea kutoka Uganda, wote yeye na Juuko (Murshid) niliwapokea mazoezini na nimeendelea kuwa nao,”amesema Mayanja.
Kiungo huyo wa zamani wa SC Villa na KCCA za Uganda amesema kwamba, matatizo yaliyojitokeza kati ya Meneja Abbas na Kiiza yamekwisha na mchezaji huyo yupo kambini Ndege Beach, Dar es Salaam kwa maandalizi ya mchezo wa kesho dhidi ya Coastal Union Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Mayanja amesema hata matukio ya awali kuhusu wachezaji Hassan Isihaka na Abdi Banda pia yanapotoshwa, lakini ukweli ni kwamba hakuwahi kugombana na wachezaji hao.
“Ndiyo maana Isihaka baadaye alikuja kuniomba msamaha na leo amemaliza adhabu yake na tupo naye tena kwenye timu, lakini Banda hakuwahi kuja kuniomba msamaha hadi sasa na hajaja tena mazoezini,”amesema.
Aidha, Mayanja amesema hali ya kambi ya Simba ni shwari kabisa kuelekea mchezo wa kesho wa Robo Fainali ya Kombe ka TFF dhidi ya Coastal Union na matarajio kesho ni ushindi.

HOTUBA YA MAALIM SEIF SHARIF HAMAD KWENYE MKUTANO NA WAANDISHI WA HABARI – PARK HYATT ZANZIBAR,
TAREHE 10 APRILI, 2016

Ndugu zangu Waandishi wa Habari,
Ndugu Waalikwa,

Naanza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa kutujaalia uhai na uzima tukaweza kukutana hapa leo. Namshukuru Mwenyezi Mungu pia kwa kuijaalia nchi yetu kwa kiasi kikubwa kubaki katika hali ya amani na utulivu licha ya jitihada kubwa zilizofanywa na zinazoendelea kufanywa na baadhi ya watu za kuivuruga amani yetu. Naendelea kumuomba Mola wetu aendelee kuibariki nchi yetu na watu wake, aijaalie kuwa nchi ya amani na atujaalie hekima na busara katika kuendesha mambo yetu.

Nichukue fursa hii pia kukushukuruni nyinyi waandishi wa habari kwa kuitikia wito wetu na kuja kutusikiliza. Shukrani maalum zije kwenu wale ambao mmesafiri kutoka Dar es Salaam na kuja Zanzibar makhsusi kwa ajili ya mkutano huu. Tunathamini sana mashirikiano yenu nyote tukitambua nafasi na mchango mkubwa wa vyombo vya habari katika maendeleo ya nchi yoyote ile.

Mtakumbuka kwamba siku saba zilizopita tulizungumza nanyi ambapo tuliwasilisha kwenu maazimio 13 ya Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la Chama Cha Wananchi (CUF) kuhusiana na msimamo wa Chama chetu dhidi ya ubakaji wa demokrasia Zanzibar uliofanyika tarehe 20 Machi, 2016 na ambao ulipewa jina la uchaguzi wa marudio.

Leo hii tumekuiteni ili kutimiza agizo nililopewa na Baraza Kuu lililonitaka nizungumze na wananchi wa Zanzibar ili kuwaeleza kwa kina mwelekeo wa hali ya kisiasa ya Zanzibar na hatua zinazochukuliwa na CUF kuhakikisha maamuzi halali ya kidemokrasia ya Wazanzibari waliyoyafanya tarehe 25 Oktoba, 2015 yanaheshimiwa.

UCHAFUZI WA TAREHE 20 MACHI, 2016
Nilieleza kwa urefu katika mkutano wangu na waandishi wa habari wa tarehe 11 Januari, 2016 nilioufanya Dar es Salaam juu ya nini kilitokea baina ya tarehe 25 Oktoba 2015 hadi tarehe 28 Oktoba, 2015, siku ambayo Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar, Jecha Salim Jecha, alitoa tangazo batili na haramu la kufuta uchaguzi huru na wa haki uliofanyika tarehe 25 Oktoba, 2015. Nilieleza pia hoja za kikatiba na kisheria za kwa nini tangazo lile ni haramu na batili na hoja zile hadi leo watawala wameshindwa kuzijibu. Kwa hoja hizo hizo, nikaeleza kwamba hakuna vifungu vya Katiba wala Sheria ya Uchaguzi ya Zanzibar Nam. 11 ya 1984 vinavyozungumzia kitu kinachoitwa uchaguzi wa marudio ukiondoa pale inapotokea wagombea wanapopata idadi sawa ya kura.

Sikusudii kurudia yale ambayo nilishayaeleza siku ile maana hayo sasa yanaeleweka na kila mtu ndani na nje ya nchi.

Leo hii nataka niwapongeze kwa mara nyengine tena wananchi jasiri na shupavu wa Zanzibar kwa kuitumia tarehe 20 Machi, 2016 kukifedhehesha Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa mara ya pili ndani ya miezi sita mbele ya macho ya Watanzania na mbele ya macho ya jumuiya ya kimataifa. Wananchi wazalendo wa Zanzibar wanaoipenda nchi yao waliwakataa watawala waovu wa CCM na sera zao mbovu zinazoidhalilisha Zanzibar yao kupitia sanduku la kura tarehe 25 Oktoba, 2015. Watawala waovu wa CCM wakaamua kutumia mabavu na uvunjwaji wa katiba na sheria kuyapindua maamuzi ya Wazanzibari, kwa sababu tu maamuzi hayo yalikuwa ni ya kuwakataa watawala hao.

Kwa miezi mitano kuanzia Oktoba 2015 hadi Machi 2016, watawala waovu wa CCM wakawaingiza wananchi watulivu na wanaopenda amani wa Zanzibar katika idhilali na hilaki kubwa kwa kuwazuilia haki zao za msingi za binadamu ili wasiweze kuonesha hisia zao dhidi ya watawala. Kwa namna ya pekee na ya ustaraabu wa hali ya juu na wa kupigiwa mfano, wananchi wa Zanzibar wakaisubiri tarehe 20 Machi, 2016 na wakapeleka ujumbe wao kwa watawala hao na kwa dunia nzima kwa njia za amani za kuususia uchafuzi ulioitishwa siku hiyo. Hali halisi iliyoonekana na kila aliyetaka kuona ni kwamba zaidi ya asilimia 80 ya Wazanzibari hawakwenda kupiga kura siku hiyo ili kuonesha hisia zao na kuthibitisha tena maamuzi yao ya tarehe 25 Oktoba, 2015.

Kituo cha televisheni cha ITV kilichokuwa kikirusha matangazo ya moja kwa moja kutoka katika mikoa mitano ya Unguja na Pemba kilionesha vile vilivyoitwa vituo vya kupigia kura vikiwa havina watu kabisa au vikiwa na watu wachache sana. Walipowahoji wale walioitwa maofisa uchaguzi na walioitwa mawakala kila mmoja alikuwa akija na majibu yake na takwimu zake zinazopingana na za mwenzake. Vituo vya televisheni vya kimataifa hasa kile cha Al-Jazeera na CCTV ya China vilionesha na kuripoti vituo vikiwa vitupu. Hata televisheni ya watawala ya ZBC ilikuwa ikipata kigugumizi kuonesha hali ilivyokuwa katika vile vilivyoitwa vituo vya kupigia kura hadi kuamua kukatisha matangazo ya moja kwa moja. Magazeti ya Tanzania na ya nje ya nchi yaliripoti na kuchapisha picha zilizoonesha kususiwa kwa uchafuzi huo ulioitishwa na watawala wakidhani wanajihalalishia haramu yao. Mitandao ya kijamii nayo ilijaa maelezo na vielelezo kutoka watu na taasisi za kimataifa zinazoheshimika vikionesha hali halisi ilivyokuwa na ujasiri wa Wazanzibari wa kuususia uchafuzi huo. Na hatimaye nchi 16 zikatoa taarifa yao tarehe 21 Machi, 2016 wakieleza kwamba uchaguzi huo haukuwa wa kuheshimika kwa sababu haukuwa shirikishi na wala haukuwakilisha matakwa ya wapiga kura wa Zanzibar.

Nitumie fursa hii kwa mara nyengine tena kuwapongeza wananchi wote wa Zanzibar kwa ujasiri, uzalendo na ari kubwa walioionesha kwa kuitikia kwa kiasi kikubwa wito wa chama chao cha CUF wa kuwataka wasishiriki katika uhuni na ubakaji wa demokrasia uliopewa jina la uchaguzi wa marudio wa tarehe 20 Machi, 2016, na hivyo kuudhihirishia ulimwengu kwamba Chama Cha Mapinduzi (CCM) hakina ridhaa ya wananchi wa Zanzibar.

Naungana na Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la CUF kuwapongeza waliokuwa wagombea wenzangu wa CUF kwa nafasi za Uwakilishi na Udiwani kwa kusimama na wananchi wa Zanzibar na kutoshiriki katika uchaguzi huo haramu na batili wa marudio, jambo ambalo limethibitisha kwamba hawapo kwa ajili ya kutaka nafasi na vyeo binafsi bali wanachotaka ni kuleta mabadiliko ya kweli kwa maslahi ya watu wote wa Zanzibar.

Pongezi zangu za dhati kabisa zinakwenda kwa wagombea Urais, Uwakilishi na Udiwani wa vyama vyengine vya upinzani ambavyo ni NRA, DEMOKRASIA MAKINI, SAU, UMD, JAHAZI ASILIA, CHAUMMA, UPDP, DP, na ACT-WAZALENDO, na vile vinavyoshirikiana kupitia UKAWA ambavyo ni CHADEMA, NCCR na NLD kwa kuungana pamoja na Wazanzibari kutetea demokrasia yao.

CCM WANAPENDA NAMBA LAKINI HAWAJUI HESABU
Jambo moja ambalo CCM wamejifedhehesha wenyewe ni lile la kutangaza kile walichokiita matokeo ya uchafuzi wao bila ya kuzingatia kwamba takwimu zina sifa moja, huwa hazisemi uongo. Vijana wana msemo wao siku hizi; wanasema CCM wanapenda namba lakini hawajui hesabu. Matokeo ya tarehe 20 Machi, 2016 waliyoyatangaza ni kwamba eti jumla ya watu waliopiga kura walikuwa 341,865 na kwamba Dk. Ali Mohamed Shein eti alipata kura 299,982 sawa na asilimia 91.4.

Takwimu za uchaguzi mkuu wa tarehe 25 Oktoba, 2015 zilionesha kwamba jumla ya wananchi waliojitokeza kupiga kura walikuwa ni 402,354 na Dk. Ali Mohamed Shein alipata kura 182,011 sawa na asilimia 46.28.

Wakati huo huo kwa uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzaia, wapiga kura kwa upande wa Zanzibar walikuwa 417,882 ambapo mgombea wa CCM, Dk. John Pombe Magufuli alipata kura 194,317 sawa na asilimia 46.5.

Kwa hivyo, kwa kutumia takwimu hizi, mtu anapochukua takwimu hizi na kulinganisha wapiga kura 402,354 waliojitokeza tarehe 25 Oktoba, 2015 na wale wanaodai eti walijitokeza tarehe 20 Machi kwamba ni 341,865 watawala wa CCM walichotaka kutuaminisha ni kwamba tofauti ya waliokuwa hawakujitokeza kupiga kura ilikuwa ni 60,489 tu. Suala la kujiuliza ni kwamba iwapo hilo ni kweli kwa nini vituo vionekane vitupu kabisa tarehe 20 Machi, 2016?

Lakini kwa upande mwengine, mtu anapokosa hata tahayuri na kudai Dk. Ali Mohamed Shein amepata kura 299,982 anachotaka kutwambia ni kwamba ndani ya miezi mitano ya idhilali na mateso aliyowapatisha Wazanzibari ameweza kuongeza kura 117,971.

Kufedheheka kwa CCM kunakuja zaidi kwamba walisahau kwamba waliyakubali matokeo ya uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa tarehe 25 Oktoba 2015 kwa upande wa Zanzibar ambapo kama tulivyokwisha onesha waliopiga kura walikuwa wengi zaidi wakiwa ni 417,882 (na hilo ungetegemea lingeinufaisha CCM) na bado mgombea wa CCM akapata kura 194,317 sawa na asilimia 46.5. Kwa kutumia idadi waliyotangaza ya kura 299,982 walizompa Dk. Shein wanataka kutwambia kwamba yeye amepata kura 105,665 zaidi kuliko Dr. Magufuli kwa Zanzibar.

Kama takwimu zao zingekuwa sahihi ina maana pia wapiga kura waliomuunga mkono mgombea wa CUF ambao hawakwenda kupiga kura ni 60,489 tu (sawa na asilimia 15 tu). Hivi nani utamdanganya kwamba Maalim Seif Sharif Hamad anaungwa mkono na asilimia 15 tu ya wapiga kura wa Zanzibar? Nani utamdanganya kwamba ndani ya miezi mitano, CCM imeongeza kura 105,665 zaidi ya alizopata mgombea wake Dk. Magufuli kwa upande wa Zanzibar?

Kutokana na ubabe na kiburi cha utawala walicho nacho CCM, wameishia kujifedhehesha kwa takwimu zao za kupika wenyewe. Ndiyo vijana wakasema, CCM wanapenda namba lakini hawajui hesabu.

NINI MWELEKEO WA CUF NA WAZANZIBARI BAADA YA UBAKAJI HUU WA DEMOKRASIA?
Wazanzibari walio wengi wamekuwa wakituuliza nini mwelekeo wa CUF baada ya ubakaji huu wa demokrasia? Wanatuuliza viongozi wao na hasa mimi tunatokaje katika hali hii ambayo imedumu miaka nenda miaka rudi kila pale Zanzibar inapofanya uchaguzi?

Kabla sijalieleza hilo, nataka niweke wazi leo kwamba tulipofanya uamuzi wa kuususia uchaguzi haramu na batili wa tarehe 20 Machi, 2016 tuliamua kusimama juu ya uamuzi unaoheshimu misingi ya kikatiba ambayo watu wa Zanzibar tumeamua ndiyo inapaswa iongoze na iendeshe nchi yetu. Tulijua kwamba uamuzi huo utakuwa na athari kwa CUF na kwa Zanzibar lakini tulijua na tuliamini pia kwamba athari hiyo haiwezi kuwa kubwa zaidi kuliko gharama ya kuikanyaga Katiba na Sheria za nchi yetu na gharama za kupiga teke demokrasia, haki za binadamu na utawala wa sheria.

Tulipima na tukatafakari kwa kina na kuona ni kheri kumeza machungu ya athari binafsi kwetu lakini tusimame kidete na kifua mbele katika kutetea maamuzi ya watu wa Zanzibar waliyoyafanya tarehe 25 Oktoba, 2015, na pia kulinda misingi ya Katiba na Sheria za nchi yetu na misingi ya demokrasia na haki za watu. Tuliona hayo ni kheri kwa huko twendako badala ya kushiriki katika haramu ya ubakaji wa demokrasia na matumizi ya nguvu za kijeshi kulazimisha watawala wasio na ridhaa ya watu. Tulifanya maamuzi yale pia kwa lengo la kuepusha shari katika nchi yetu. Leo Wazanzibari na dunia nzima ni mashahidi kwamba uamuzi ule ulikuwa sahihi na wa busara. Maana mateso na vitisho walivyokumbana navyo Wazanzibari wakati tumewaachia uchaguzi ule watawala waovu peke yao vilikuwa vya kiasi kile kilichoshuhudiwa. Je, tungeliamua kushiriki na kusimama kulinda na kutetea ushindi wetu hali ingekuwaje? Bila shaka nchi ingetumbukia katika machafuko ambayo watawala waovu walikuwa tayari yatokee kuliko kuridhia maamuzi halali ya wananchi wa Zanzibar.

Maamuzi yale yamethibitika pia kwamba ni sahihi kwa jinsi watu wa Zanzibar walivyoudharau na kuupuuza uchaguzi haramu na batili wa tarehe 20 Machi, 2016. Watawala waovu wa CCM waliwadharau watu wa Zanzibar na watu wa Zanzibar wakaamua kuwadharau wao tarehe 20 Machi 2016.

Kwa upande mwengine, uamuzi tuliouchukua na kuusimamia pia ni uamuzi uliosimama juu ya misingi ya heshima na misingi ya utu wa watu, ambayo yalikuwa ndiyo malengo sahihi ya Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, Hayati Mzee Abeid Amani Karume, malengo sahihi ya Chama cha Afro Shirazi na malengo sahihi ya Mapinduzi ya Januari 12, 1964.

Kwa hakika, uamuzi wa kuupuuza na kuudharau uchafuzi wa tarehe 20 Machi, 2016 ni ushindi mwengine wa Zanzibar katika historia yake ya kisiasa.

Nimalizie sasa kwa kujibu hoja ya ni upi mwelekeo wa CUF na wa Wazanzibari baada ya ubakaji huu wa wazi wa demokrasia na haki za watu wa Zanzibar?

Kwanza, nirudie na kusisitiza msimamo wetu kwamba hatukubaliani na ubakaji wa demokrasia na haki za watu wa Zanzibar uliofanywa na watawala waovu wakisaidiwa na vyombo vya dola. Kwa msingi huo, Wazanzibari wataendelea kuipinga serikali isiyo na ridhaa ya watu kwa kutumia njia za amani, za kidemokrsia na zinazoendana na misingi ya Katiba na Sheria za nchi yetu.

Jana kumetangazwa kile kilichoitwa ni Baraza la Mawaziri. Msimamo wetu uko pale pale. Kama tusivyomtambua aliyelitangaza Baraza hilo, vivyo hivyo hatulitambui Baraza lake la Mawaziri.

Kwa hakika, kwa sababu msingi wa watawala waliojinyakulia madaraka ni kupitia uvunjwaji wa Katiba, kila kinachofuata kimekuwa kikiendeleza uvunjwaji wa Katiba. Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 kupitia Marekebisho ya 10 ya mwaka 2010, Ibara ya 9 (1) inalazimisha Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwa na muundo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa. Ibara za 39, 39A na 42 za Katiba zimeeleza namna Serikali hiyo ya Umoja wa Kitaifa itakavyoundwa. Masharti yote hayo yanaendelea kuvunjwa na mtawala aliyeamua kuyapiga teke maamuzi ya Wazanzibari na kujiweka madarakani kwa nguvu. Kwa hivyo, Serikali yake haiwezi kuwa Serikali inayokwenda na Katiba. Kwa ufupi, si Serikali halali kwa mujibu wa Katiba.

Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la CUF katika kikao chake cha tarehe 2 – 3 Aprili, 2016 lilipitisha maazimio yafuatayo miongoni mwa maazimio yake:

“Azimio Nam. 9:
Haliyatambui matokeo ya uchaguzi huo haramu na batili, na kwa msingi huo halimtambui Dk. Ali Mohamed Shein kuwa Rais wa Zanzibar, haliwatambui waliotangazwa kuwa Wawakilishi na wala haliwatambui waliotangazwa kuwa Madiwani. Baraza Kuu linaungana na wananchi wa Zanzibar waliokataa kuwapa uhalali watu hao na kwa hivyo halitoitambua Serikali, Manispaa na Halmashauri za Wilaya zitakazoundwa na watu hao. CUF haitoshirikiana na Serikali itakayoundwa kwa sababu ni kinyume na Katiba ya Zanzibar, kinyume na Sheria ya Uchaguzi na haikutokana na ridhaa ya watu. Kwa vyovyote vile, Serikali itakayoundwa haitakidhi matakwa ya Katiba ya Zanzibar na hivyo CUF haitoshiriki kwenye uvunjaji wa Katiba ambayo inaeleza kwa uwazi kabisa namna ya kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar.

“Azimio Nam. 10:
Linawataka wananchi wote wa Zanzibar kutumia njia za amani, za kikatiba na kisheria ambazo zimewahi kutumika katika nchi nyingine duniani kuwakataa watawala waovu na wasio na ridhaa ya watu waliojiweka madarakani kwa kutumia nguvu na ubakaji wa demokrasia kwa kutoipa ushirikiano Serikali itakayoundwa na watawala hao.”

Baada ya maazimio hayo ya Baraza Kuu, kinachofuata sasa ni utekelezaji wake. Hivi sasa tunapanga mikakati madhubuti ya utekelezaji wa maazimio hayo kwa kutumia njia za amani, za kidemokrasia na za kikatiba ili kutufikisha kwenye malengo yetu ya kuona maamuzi ya watu wa Zanzibar yanaheshimiwa.
Nina hakika kabisa kuwa mikakati tunayoipanga itazaa hatua ambazo zitaibana Serikali haramu na hatimaye itasalimu amri kwa wananchi wa Zanzibar ambayo kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar ndiyo wenye mamlaka ya kuiweka madarakani Serikali wanayoitaka. Katika dunia ya leo, hatuwezi kuongozwa na watawala ambao hawakupewa mamlaka na watu wenyewe.

Pili, naipongeza na kuishukuru jumuiya ya kimataifa na washirika wa maendeleo kwa msimamo waliochukua wa kukataa kubariki ubakaji huo wa demokrasia na haki za watu wa Zanzibar na kukataa kushiriki katika uapishwaji wa mtu asiye na ridhaa ya wapiga kura wa Zanzibar. Napongeza hatua ambazo wameanza kuzichukua dhidi ya Serikali za CCM ambazo ndizo zilizosimamia ubakaji huo wa demokrasia na haki za watu. Natoa wito kwao kuchukua hatua kali zaidi dhidi ya watawala hawa waovu zikiwemo kuwawekea vikwazo vya kusafiri, kufuatilia akaunti zao za fedha nje ya nchi na hatua za kuchunguza matendo yao ya uhalifu dhidi ya binadamu. Wananchi waliodhulumiwa haki zao wanaziunga mkono hatua hizo wakiamini kwamba CCM ni lazima iwajibishwe kwa matendo yake maovu dhidi yao.

Nitumie fursa hii kwa mara nyengine tena kuwataka wananchi wa Zanzibar kudumisha amani ya nchi yetu na umoja wa watu wetu. Nikiwa kiongozi wao ninayewapenda na ambaye nimejitolea kuwatumikia katika umri wangu wote siwezi kuwaongoza kuelekea kwenye fujo na ghasia au vitendo vitakavyopelekea kuiharibu nchi yetu na kuathiri watu wetu. Nina imani kabisa kwamba njia tunayoifuata ni njia ya haki; na haki siku zote itashinda.

Mwaka 2009, mimi na mwenzangu, Dk. Amani Abeid Karume, tuliwaongoza Wazanzibari katika Maridhiano yaliyoashiria mwanzo wa ujenzi wa mahusiano mapya baina ya watu wema wa Zanzibar kwa kuzika siasa za ubaguzi, utengano, chuki, hasama na fujo na badala yake kusimamisha siasa za maelewano, umoja, upendo, mshikamano na udugu katika jamii yetu. Tulitegemea kuanzia pale tungeendelea mbele kwa kuchukua hatua za kuyaimarisha maridhiano yetu na kuyazamisha zaidi kwenye nyoyo za Wazanzibari. Binafsi nasikitishwa na kuhuzunishwa sana kuona watawala waovu wasiowatakia mema watu wa nchi hii wameturudisha tulikotoka kwa maslahi yao binafsi. Natoa wito kwa Wazanzibari wenzangu kuwa tukatae kurudishwa kwenye siasa zile za ubaguzi, utengano, chuki, hasama na fujo na kila mmoja afanye lile liliomo katika uwezo wake kuendeleza maelewano, umoja, upendo, mshikamano na udugu katika jamii yetu.

Wazanzibari tumeamua kuisimamisha tena Zanzibar yetu na Zanzibar itasimama tena Inshallah. Hilo sina wasiwasi nalo kama kiongozi wa Wazanzibari waliyenipa ridhaa yao.

HATIMAYE TUTASHINDA.
WANANCHI JASIRI NA SHUPAVU WA ZANZIBAR WATASHINDA.

Ahsanteni sana.

HOTUBA YA MAALIM SEIF SHARIF HAMAD KWENYE MKUTANO NA WAANDISHI WA HABARI – PARK HYATT ZANZIBAR,
TAREHE 10 APRILI, 2016

Ndugu zangu Waandishi wa Habari,
Ndugu Waalikwa,

Naanza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa kutujaalia uhai na uzima tukaweza kukutana hapa leo. Namshukuru Mwenyezi Mungu pia kwa kuijaalia nchi yetu kwa kiasi kikubwa kubaki katika hali ya amani na utulivu licha ya jitihada kubwa zilizofanywa na zinazoendelea kufanywa na baadhi ya watu za kuivuruga amani yetu. Naendelea kumuomba Mola wetu aendelee kuibariki nchi yetu na watu wake, aijaalie kuwa nchi ya amani na atujaalie hekima na busara katika kuendesha mambo yetu.

Nichukue fursa hii pia kukushukuruni nyinyi waandishi wa habari kwa kuitikia wito wetu na kuja kutusikiliza. Shukrani maalum zije kwenu wale ambao mmesafiri kutoka Dar es Salaam na kuja Zanzibar makhsusi kwa ajili ya mkutano huu. Tunathamini sana mashirikiano yenu nyote tukitambua nafasi na mchango mkubwa wa vyombo vya habari katika maendeleo ya nchi yoyote ile.

Mtakumbuka kwamba siku saba zilizopita tulizungumza nanyi ambapo tuliwasilisha kwenu maazimio 13 ya Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la Chama Cha Wananchi (CUF) kuhusiana na msimamo wa Chama chetu dhidi ya ubakaji wa demokrasia Zanzibar uliofanyika tarehe 20 Machi, 2016 na ambao ulipewa jina la uchaguzi wa marudio.

Leo hii tumekuiteni ili kutimiza agizo nililopewa na Baraza Kuu lililonitaka nizungumze na wananchi wa Zanzibar ili kuwaeleza kwa kina mwelekeo wa hali ya kisiasa ya Zanzibar na hatua zinazochukuliwa na CUF kuhakikisha maamuzi halali ya kidemokrasia ya Wazanzibari waliyoyafanya tarehe 25 Oktoba, 2015 yanaheshimiwa.

UCHAFUZI WA TAREHE 20 MACHI, 2016
Nilieleza kwa urefu katika mkutano wangu na waandishi wa habari wa tarehe 11 Januari, 2016 nilioufanya Dar es Salaam juu ya nini kilitokea baina ya tarehe 25 Oktoba 2015 hadi tarehe 28 Oktoba, 2015, siku ambayo Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar, Jecha Salim Jecha, alitoa tangazo batili na haramu la kufuta uchaguzi huru na wa haki uliofanyika tarehe 25 Oktoba, 2015. Nilieleza pia hoja za kikatiba na kisheria za kwa nini tangazo lile ni haramu na batili na hoja zile hadi leo watawala wameshindwa kuzijibu. Kwa hoja hizo hizo, nikaeleza kwamba hakuna vifungu vya Katiba wala Sheria ya Uchaguzi ya Zanzibar Nam. 11 ya 1984 vinavyozungumzia kitu kinachoitwa uchaguzi wa marudio ukiondoa pale inapotokea wagombea wanapopata idadi sawa ya kura.

Sikusudii kurudia yale ambayo nilishayaeleza siku ile maana hayo sasa yanaeleweka na kila mtu ndani na nje ya nchi.

Leo hii nataka niwapongeze kwa mara nyengine tena wananchi jasiri na shupavu wa Zanzibar kwa kuitumia tarehe 20 Machi, 2016 kukifedhehesha Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa mara ya pili ndani ya miezi sita mbele ya macho ya Watanzania na mbele ya macho ya jumuiya ya kimataifa. Wananchi wazalendo wa Zanzibar wanaoipenda nchi yao waliwakataa watawala waovu wa CCM na sera zao mbovu zinazoidhalilisha Zanzibar yao kupitia sanduku la kura tarehe 25 Oktoba, 2015. Watawala waovu wa CCM wakaamua kutumia mabavu na uvunjwaji wa katiba na sheria kuyapindua maamuzi ya Wazanzibari, kwa sababu tu maamuzi hayo yalikuwa ni ya kuwakataa watawala hao.

Kwa miezi mitano kuanzia Oktoba 2015 hadi Machi 2016, watawala waovu wa CCM wakawaingiza wananchi watulivu na wanaopenda amani wa Zanzibar katika idhilali na hilaki kubwa kwa kuwazuilia haki zao za msingi za binadamu ili wasiweze kuonesha hisia zao dhidi ya watawala. Kwa namna ya pekee na ya ustaraabu wa hali ya juu na wa kupigiwa mfano, wananchi wa Zanzibar wakaisubiri tarehe 20 Machi, 2016 na wakapeleka ujumbe wao kwa watawala hao na kwa dunia nzima kwa njia za amani za kuususia uchafuzi ulioitishwa siku hiyo. Hali halisi iliyoonekana na kila aliyetaka kuona ni kwamba zaidi ya asilimia 80 ya Wazanzibari hawakwenda kupiga kura siku hiyo ili kuonesha hisia zao na kuthibitisha tena maamuzi yao ya tarehe 25 Oktoba, 2015.

Kituo cha televisheni cha ITV kilichokuwa kikirusha matangazo ya moja kwa moja kutoka katika mikoa mitano ya Unguja na Pemba kilionesha vile vilivyoitwa vituo vya kupigia kura vikiwa havina watu kabisa au vikiwa na watu wachache sana. Walipowahoji wale walioitwa maofisa uchaguzi na walioitwa mawakala kila mmoja alikuwa akija na majibu yake na takwimu zake zinazopingana na za mwenzake. Vituo vya televisheni vya kimataifa hasa kile cha Al-Jazeera na CCTV ya China vilionesha na kuripoti vituo vikiwa vitupu. Hata televisheni ya watawala ya ZBC ilikuwa ikipata kigugumizi kuonesha hali ilivyokuwa katika vile vilivyoitwa vituo vya kupigia kura hadi kuamua kukatisha matangazo ya moja kwa moja. Magazeti ya Tanzania na ya nje ya nchi yaliripoti na kuchapisha picha zilizoonesha kususiwa kwa uchafuzi huo ulioitishwa na watawala wakidhani wanajihalalishia haramu yao. Mitandao ya kijamii nayo ilijaa maelezo na vielelezo kutoka watu na taasisi za kimataifa zinazoheshimika vikionesha hali halisi ilivyokuwa na ujasiri wa Wazanzibari wa kuususia uchafuzi huo. Na hatimaye nchi 16 zikatoa taarifa yao tarehe 21 Machi, 2016 wakieleza kwamba uchaguzi huo haukuwa wa kuheshimika kwa sababu haukuwa shirikishi na wala haukuwakilisha matakwa ya wapiga kura wa Zanzibar.

Nitumie fursa hii kwa mara nyengine tena kuwapongeza wananchi wote wa Zanzibar kwa ujasiri, uzalendo na ari kubwa walioionesha kwa kuitikia kwa kiasi kikubwa wito wa chama chao cha CUF wa kuwataka wasishiriki katika uhuni na ubakaji wa demokrasia uliopewa jina la uchaguzi wa marudio wa tarehe 20 Machi, 2016, na hivyo kuudhihirishia ulimwengu kwamba Chama Cha Mapinduzi (CCM) hakina ridhaa ya wananchi wa Zanzibar.

Naungana na Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la CUF kuwapongeza waliokuwa wagombea wenzangu wa CUF kwa nafasi za Uwakilishi na Udiwani kwa kusimama na wananchi wa Zanzibar na kutoshiriki katika uchaguzi huo haramu na batili wa marudio, jambo ambalo limethibitisha kwamba hawapo kwa ajili ya kutaka nafasi na vyeo binafsi bali wanachotaka ni kuleta mabadiliko ya kweli kwa maslahi ya watu wote wa Zanzibar.

Pongezi zangu za dhati kabisa zinakwenda kwa wagombea Urais, Uwakilishi na Udiwani wa vyama vyengine vya upinzani ambavyo ni NRA, DEMOKRASIA MAKINI, SAU, UMD, JAHAZI ASILIA, CHAUMMA, UPDP, DP, na ACT-WAZALENDO, na vile vinavyoshirikiana kupitia UKAWA ambavyo ni CHADEMA, NCCR na NLD kwa kuungana pamoja na Wazanzibari kutetea demokrasia yao.

CCM WANAPENDA NAMBA LAKINI HAWAJUI HESABU
Jambo moja ambalo CCM wamejifedhehesha wenyewe ni lile la kutangaza kile walichokiita matokeo ya uchafuzi wao bila ya kuzingatia kwamba takwimu zina sifa moja, huwa hazisemi uongo. Vijana wana msemo wao siku hizi; wanasema CCM wanapenda namba lakini hawajui hesabu. Matokeo ya tarehe 20 Machi, 2016 waliyoyatangaza ni kwamba eti jumla ya watu waliopiga kura walikuwa 341,865 na kwamba Dk. Ali Mohamed Shein eti alipata kura 299,982 sawa na asilimia 91.4.

Takwimu za uchaguzi mkuu wa tarehe 25 Oktoba, 2015 zilionesha kwamba jumla ya wananchi waliojitokeza kupiga kura walikuwa ni 402,354 na Dk. Ali Mohamed Shein alipata kura 182,011 sawa na asilimia 46.28.

Wakati huo huo kwa uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzaia, wapiga kura kwa upande wa Zanzibar walikuwa 417,882 ambapo mgombea wa CCM, Dk. John Pombe Magufuli alipata kura 194,317 sawa na asilimia 46.5.

Kwa hivyo, kwa kutumia takwimu hizi, mtu anapochukua takwimu hizi na kulinganisha wapiga kura 402,354 waliojitokeza tarehe 25 Oktoba, 2015 na wale wanaodai eti walijitokeza tarehe 20 Machi kwamba ni 341,865 watawala wa CCM walichotaka kutuaminisha ni kwamba tofauti ya waliokuwa hawakujitokeza kupiga kura ilikuwa ni 60,489 tu. Suala la kujiuliza ni kwamba iwapo hilo ni kweli kwa nini vituo vionekane vitupu kabisa tarehe 20 Machi, 2016?

Lakini kwa upande mwengine, mtu anapokosa hata tahayuri na kudai Dk. Ali Mohamed Shein amepata kura 299,982 anachotaka kutwambia ni kwamba ndani ya miezi mitano ya idhilali na mateso aliyowapatisha Wazanzibari ameweza kuongeza kura 117,971.

Kufedheheka kwa CCM kunakuja zaidi kwamba walisahau kwamba waliyakubali matokeo ya uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa tarehe 25 Oktoba 2015 kwa upande wa Zanzibar ambapo kama tulivyokwisha onesha waliopiga kura walikuwa wengi zaidi wakiwa ni 417,882 (na hilo ungetegemea lingeinufaisha CCM) na bado mgombea wa CCM akapata kura 194,317 sawa na asilimia 46.5. Kwa kutumia idadi waliyotangaza ya kura 299,982 walizompa Dk. Shein wanataka kutwambia kwamba yeye amepata kura 105,665 zaidi kuliko Dr. Magufuli kwa Zanzibar.

Kama takwimu zao zingekuwa sahihi ina maana pia wapiga kura waliomuunga mkono mgombea wa CUF ambao hawakwenda kupiga kura ni 60,489 tu (sawa na asilimia 15 tu). Hivi nani utamdanganya kwamba Maalim Seif Sharif Hamad anaungwa mkono na asilimia 15 tu ya wapiga kura wa Zanzibar? Nani utamdanganya kwamba ndani ya miezi mitano, CCM imeongeza kura 105,665 zaidi ya alizopata mgombea wake Dk. Magufuli kwa upande wa Zanzibar?

Kutokana na ubabe na kiburi cha utawala walicho nacho CCM, wameishia kujifedhehesha kwa takwimu zao za kupika wenyewe. Ndiyo vijana wakasema, CCM wanapenda namba lakini hawajui hesabu.

NINI MWELEKEO WA CUF NA WAZANZIBARI BAADA YA UBAKAJI HUU WA DEMOKRASIA?
Wazanzibari walio wengi wamekuwa wakituuliza nini mwelekeo wa CUF baada ya ubakaji huu wa demokrasia? Wanatuuliza viongozi wao na hasa mimi tunatokaje katika hali hii ambayo imedumu miaka nenda miaka rudi kila pale Zanzibar inapofanya uchaguzi?

Kabla sijalieleza hilo, nataka niweke wazi leo kwamba tulipofanya uamuzi wa kuususia uchaguzi haramu na batili wa tarehe 20 Machi, 2016 tuliamua kusimama juu ya uamuzi unaoheshimu misingi ya kikatiba ambayo watu wa Zanzibar tumeamua ndiyo inapaswa iongoze na iendeshe nchi yetu. Tulijua kwamba uamuzi huo utakuwa na athari kwa CUF na kwa Zanzibar lakini tulijua na tuliamini pia kwamba athari hiyo haiwezi kuwa kubwa zaidi kuliko gharama ya kuikanyaga Katiba na Sheria za nchi yetu na gharama za kupiga teke demokrasia, haki za binadamu na utawala wa sheria.

Tulipima na tukatafakari kwa kina na kuona ni kheri kumeza machungu ya athari binafsi kwetu lakini tusimame kidete na kifua mbele katika kutetea maamuzi ya watu wa Zanzibar waliyoyafanya tarehe 25 Oktoba, 2015, na pia kulinda misingi ya Katiba na Sheria za nchi yetu na misingi ya demokrasia na haki za watu. Tuliona hayo ni kheri kwa huko twendako badala ya kushiriki katika haramu ya ubakaji wa demokrasia na matumizi ya nguvu za kijeshi kulazimisha watawala wasio na ridhaa ya watu. Tulifanya maamuzi yale pia kwa lengo la kuepusha shari katika nchi yetu. Leo Wazanzibari na dunia nzima ni mashahidi kwamba uamuzi ule ulikuwa sahihi na wa busara. Maana mateso na vitisho walivyokumbana navyo Wazanzibari wakati tumewaachia uchaguzi ule watawala waovu peke yao vilikuwa vya kiasi kile kilichoshuhudiwa. Je, tungeliamua kushiriki na kusimama kulinda na kutetea ushindi wetu hali ingekuwaje? Bila shaka nchi ingetumbukia katika machafuko ambayo watawala waovu walikuwa tayari yatokee kuliko kuridhia maamuzi halali ya wananchi wa Zanzibar.

Maamuzi yale yamethibitika pia kwamba ni sahihi kwa jinsi watu wa Zanzibar walivyoudharau na kuupuuza uchaguzi haramu na batili wa tarehe 20 Machi, 2016. Watawala waovu wa CCM waliwadharau watu wa Zanzibar na watu wa Zanzibar wakaamua kuwadharau wao tarehe 20 Machi 2016.

Kwa upande mwengine, uamuzi tuliouchukua na kuusimamia pia ni uamuzi uliosimama juu ya misingi ya heshima na misingi ya utu wa watu, ambayo yalikuwa ndiyo malengo sahihi ya Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, Hayati Mzee Abeid Amani Karume, malengo sahihi ya Chama cha Afro Shirazi na malengo sahihi ya Mapinduzi ya Januari 12, 1964.

Kwa hakika, uamuzi wa kuupuuza na kuudharau uchafuzi wa tarehe 20 Machi, 2016 ni ushindi mwengine wa Zanzibar katika historia yake ya kisiasa.

Nimalizie sasa kwa kujibu hoja ya ni upi mwelekeo wa CUF na wa Wazanzibari baada ya ubakaji huu wa wazi wa demokrasia na haki za watu wa Zanzibar?

Kwanza, nirudie na kusisitiza msimamo wetu kwamba hatukubaliani na ubakaji wa demokrasia na haki za watu wa Zanzibar uliofanywa na watawala waovu wakisaidiwa na vyombo vya dola. Kwa msingi huo, Wazanzibari wataendelea kuipinga serikali isiyo na ridhaa ya watu kwa kutumia njia za amani, za kidemokrsia na zinazoendana na misingi ya Katiba na Sheria za nchi yetu.

Jana kumetangazwa kile kilichoitwa ni Baraza la Mawaziri. Msimamo wetu uko pale pale. Kama tusivyomtambua aliyelitangaza Baraza hilo, vivyo hivyo hatulitambui Baraza lake la Mawaziri.

Kwa hakika, kwa sababu msingi wa watawala waliojinyakulia madaraka ni kupitia uvunjwaji wa Katiba, kila kinachofuata kimekuwa kikiendeleza uvunjwaji wa Katiba. Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 kupitia Marekebisho ya 10 ya mwaka 2010, Ibara ya 9 (1) inalazimisha Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwa na muundo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa. Ibara za 39, 39A na 42 za Katiba zimeeleza namna Serikali hiyo ya Umoja wa Kitaifa itakavyoundwa. Masharti yote hayo yanaendelea kuvunjwa na mtawala aliyeamua kuyapiga teke maamuzi ya Wazanzibari na kujiweka madarakani kwa nguvu. Kwa hivyo, Serikali yake haiwezi kuwa Serikali inayokwenda na Katiba. Kwa ufupi, si Serikali halali kwa mujibu wa Katiba.

Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la CUF katika kikao chake cha tarehe 2 – 3 Aprili, 2016 lilipitisha maazimio yafuatayo miongoni mwa maazimio yake:

“Azimio Nam. 9:
Haliyatambui matokeo ya uchaguzi huo haramu na batili, na kwa msingi huo halimtambui Dk. Ali Mohamed Shein kuwa Rais wa Zanzibar, haliwatambui waliotangazwa kuwa Wawakilishi na wala haliwatambui waliotangazwa kuwa Madiwani. Baraza Kuu linaungana na wananchi wa Zanzibar waliokataa kuwapa uhalali watu hao na kwa hivyo halitoitambua Serikali, Manispaa na Halmashauri za Wilaya zitakazoundwa na watu hao. CUF haitoshirikiana na Serikali itakayoundwa kwa sababu ni kinyume na Katiba ya Zanzibar, kinyume na Sheria ya Uchaguzi na haikutokana na ridhaa ya watu. Kwa vyovyote vile, Serikali itakayoundwa haitakidhi matakwa ya Katiba ya Zanzibar na hivyo CUF haitoshiriki kwenye uvunjaji wa Katiba ambayo inaeleza kwa uwazi kabisa namna ya kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar.

“Azimio Nam. 10:
Linawataka wananchi wote wa Zanzibar kutumia njia za amani, za kikatiba na kisheria ambazo zimewahi kutumika katika nchi nyingine duniani kuwakataa watawala waovu na wasio na ridhaa ya watu waliojiweka madarakani kwa kutumia nguvu na ubakaji wa demokrasia kwa kutoipa ushirikiano Serikali itakayoundwa na watawala hao.”

Baada ya maazimio hayo ya Baraza Kuu, kinachofuata sasa ni utekelezaji wake. Hivi sasa tunapanga mikakati madhubuti ya utekelezaji wa maazimio hayo kwa kutumia njia za amani, za kidemokrasia na za kikatiba ili kutufikisha kwenye malengo yetu ya kuona maamuzi ya watu wa Zanzibar yanaheshimiwa.
Nina hakika kabisa kuwa mikakati tunayoipanga itazaa hatua ambazo zitaibana Serikali haramu na hatimaye itasalimu amri kwa wananchi wa Zanzibar ambayo kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar ndiyo wenye mamlaka ya kuiweka madarakani Serikali wanayoitaka. Katika dunia ya leo, hatuwezi kuongozwa na watawala ambao hawakupewa mamlaka na watu wenyewe.

Pili, naipongeza na kuishukuru jumuiya ya kimataifa na washirika wa maendeleo kwa msimamo waliochukua wa kukataa kubariki ubakaji huo wa demokrasia na haki za watu wa Zanzibar na kukataa kushiriki katika uapishwaji wa mtu asiye na ridhaa ya wapiga kura wa Zanzibar. Napongeza hatua ambazo wameanza kuzichukua dhidi ya Serikali za CCM ambazo ndizo zilizosimamia ubakaji huo wa demokrasia na haki za watu. Natoa wito kwao kuchukua hatua kali zaidi dhidi ya watawala hawa waovu zikiwemo kuwawekea vikwazo vya kusafiri, kufuatilia akaunti zao za fedha nje ya nchi na hatua za kuchunguza matendo yao ya uhalifu dhidi ya binadamu. Wananchi waliodhulumiwa haki zao wanaziunga mkono hatua hizo wakiamini kwamba CCM ni lazima iwajibishwe kwa matendo yake maovu dhidi yao.

Nitumie fursa hii kwa mara nyengine tena kuwataka wananchi wa Zanzibar kudumisha amani ya nchi yetu na umoja wa watu wetu. Nikiwa kiongozi wao ninayewapenda na ambaye nimejitolea kuwatumikia katika umri wangu wote siwezi kuwaongoza kuelekea kwenye fujo na ghasia au vitendo vitakavyopelekea kuiharibu nchi yetu na kuathiri watu wetu. Nina imani kabisa kwamba njia tunayoifuata ni njia ya haki; na haki siku zote itashinda.

Mwaka 2009, mimi na mwenzangu, Dk. Amani Abeid Karume, tuliwaongoza Wazanzibari katika Maridhiano yaliyoashiria mwanzo wa ujenzi wa mahusiano mapya baina ya watu wema wa Zanzibar kwa kuzika siasa za ubaguzi, utengano, chuki, hasama na fujo na badala yake kusimamisha siasa za maelewano, umoja, upendo, mshikamano na udugu katika jamii yetu. Tulitegemea kuanzia pale tungeendelea mbele kwa kuchukua hatua za kuyaimarisha maridhiano yetu na kuyazamisha zaidi kwenye nyoyo za Wazanzibari. Binafsi nasikitishwa na kuhuzunishwa sana kuona watawala waovu wasiowatakia mema watu wa nchi hii wameturudisha tulikotoka kwa maslahi yao binafsi. Natoa wito kwa Wazanzibari wenzangu kuwa tukatae kurudishwa kwenye siasa zile za ubaguzi, utengano, chuki, hasama na fujo na kila mmoja afanye lile liliomo katika uwezo wake kuendeleza maelewano, umoja, upendo, mshikamano na udugu katika jamii yetu.

Wazanzibari tumeamua kuisimamisha tena Zanzibar yetu na Zanzibar itasimama tena Inshallah. Hilo sina wasiwasi nalo kama kiongozi wa Wazanzibari waliyenipa ridhaa yao.

HATIMAYE TUTASHINDA.
WANANCHI JASIRI NA SHUPAVU WA ZANZIBAR WATASHINDA.

Ahsanteni sana.

Saturday, 9 April 2016

Ndiyo maneno ya yanga dk chache kabla ya kuanza pambano lao dhidi ya al-ahly! Huku kwetu wameshajitenga huko kwenu vp?

Ndiyo maneno ya yanga dk chache kabla ya kuanza pambano lao dhidi ya al-ahly! Huku kwetu wameshajitenga huko kwenu vp?

Ni Mbwana Sammata ucku wa kuamkia leo tarehe 9-4-2015 aliipatia timu yake goli la 3 katika ushindi wa 4-0, goli ambalo alilifunga dak sawa na jezzy yake dk ya 77' akitokea benchi na ilikuwa ndo first tourch! Congratration mbwana ally sammata.

Ni Mbwana Sammata ucku wa kuamkia leo tarehe 9-4-2015 aliipatia timu yake goli la 3 katika ushindi wa 4-0, goli ambalo alilifunga dak sawa na jezzy yake dk ya 77' akitokea benchi na ilikuwa ndo first tourch! Congratration mbwana ally sammata.

Dondoo muhimu kuelekea mechi za Leo ...
#Yanga vs #Al_Ahly ...
Leo club ya Yanga itaikaribisha Al Ahly katika uwanja wa taifa kwa ajili ya mechi ya  kwanza Ligi ya Mabingwa .... Yanga na Al Ahly weshakutana mala 4 mpaka sasa na Al ahly imeweza kumtoa mala zote , Yanga anaonekana kuwa na matokeo mazuri akiwa ndani ya uwanja wa taifa kwani mala ya mwisho kukutana Yanga alishinda 1-0 huku mchezo wa marudiano   Misri  Yanga alifungwa 1-0 kisha akaja kutolewa kwenye mikwaju ya Penat (4-3 )

Kocha wa Al Ahly Maltine Jol  amesema watachukua dakika 15, kusoma kasi ya wapinzani wao baada ya hapo wataanza kucheza soka lao la kushambulia kwa kutumia viungo wengi zaidi ili kuweza kujilinda na kupata matokeo mazuri wakiwa ugenini.

 Kocha wa #Yanga Pluijm amesema, maandalizi yao yamekwenda vizuri na vijana wake wote wapo tayari kwa mchezo dhidi ya Al Ahly, na wamemuahidi ushindi kutokana na kukusudia kufika mbali mwaka huu kwenye michuano hiyo.

“Tulicheza nao mwaka 2014, wenyewe waliona kazi yetu ingawa walitutoa kwa panelti, lakini mwaka huu tunakutana nao tukiwa kivingine zaidi tumeimarika sana hasa safu yetu ya ushambuliaji tunawakaribisha Tanzania lakini wasitarajie kurudi na pointi Misri,”amesema Pluijm.

  Kila la Kheri Yanga f.c

Leo ndio siku ukisikia Maisha bila unafiki huwa hayaendi ...   Totenham vs Manchester united na West ham vs Arsenal ..  Mechi hizi   zinawafanya mashabiki wa Arsenal na man utd wapatane kwa muda mfupi

Man utd anataka arsenal Amfunge west ham na arsenal anaombea man utd amfunge totenhm ...

Ushindi wa Leo kwa Arsenal utamuweka katika mazingira mazuri ya kupigania Ubingwa wa ligi na vile vile matokeo ya wet ham yatamuweka mazingira mazuri ya kuingia Top 4 .. Mechi yao ya kwanza ndani ya Emirates studium Arsenal alifungwa bao 2-0 , mabao ya cheikhou kouyate ,Maoro zarate yaliweza kuacha majonzi Emiretes .

Mechi zingine za Leo ni pamoja na

Swansea City watamkaribisha Chelsea Liberty studium , mechi yao ya kwanza walitoka sare ya 2-2  ..

Manchester City atamkaribisha West Bromwich etihad studim. ...hii mechi ni muhimu kwa City ushindi wa Leo utamuweka katika mazingira mazuri ya kubaki top 4 ..

Ni hayo tu kwa Leo ..

Dondoo muhimu kuelekea mechi za Leo ...
#Yanga vs #Al_Ahly ...
Leo club ya Yanga itaikaribisha Al Ahly katika uwanja wa taifa kwa ajili ya mechi ya  kwanza Ligi ya Mabingwa .... Yanga na Al Ahly weshakutana mala 4 mpaka sasa na Al ahly imeweza kumtoa mala zote , Yanga anaonekana kuwa na matokeo mazuri akiwa ndani ya uwanja wa taifa kwani mala ya mwisho kukutana Yanga alishinda 1-0 huku mchezo wa marudiano   Misri  Yanga alifungwa 1-0 kisha akaja kutolewa kwenye mikwaju ya Penat (4-3 )

Kocha wa Al Ahly Maltine Jol  amesema watachukua dakika 15, kusoma kasi ya wapinzani wao baada ya hapo wataanza kucheza soka lao la kushambulia kwa kutumia viungo wengi zaidi ili kuweza kujilinda na kupata matokeo mazuri wakiwa ugenini.

 Kocha wa #Yanga Pluijm amesema, maandalizi yao yamekwenda vizuri na vijana wake wote wapo tayari kwa mchezo dhidi ya Al Ahly, na wamemuahidi ushindi kutokana na kukusudia kufika mbali mwaka huu kwenye michuano hiyo.

“Tulicheza nao mwaka 2014, wenyewe waliona kazi yetu ingawa walitutoa kwa panelti, lakini mwaka huu tunakutana nao tukiwa kivingine zaidi tumeimarika sana hasa safu yetu ya ushambuliaji tunawakaribisha Tanzania lakini wasitarajie kurudi na pointi Misri,”amesema Pluijm.

  Kila la Kheri Yanga f.c

Leo ndio siku ukisikia Maisha bila unafiki huwa hayaendi ...   Totenham vs Manchester united na West ham vs Arsenal ..  Mechi hizi   zinawafanya mashabiki wa Arsenal na man utd wapatane kwa muda mfupi

Man utd anataka arsenal Amfunge west ham na arsenal anaombea man utd amfunge totenhm ...

Ushindi wa Leo kwa Arsenal utamuweka katika mazingira mazuri ya kupigania Ubingwa wa ligi na vile vile matokeo ya wet ham yatamuweka mazingira mazuri ya kuingia Top 4 .. Mechi yao ya kwanza ndani ya Emirates studium Arsenal alifungwa bao 2-0 , mabao ya cheikhou kouyate ,Maoro zarate yaliweza kuacha majonzi Emiretes .

Mechi zingine za Leo ni pamoja na

Swansea City watamkaribisha Chelsea Liberty studium , mechi yao ya kwanza walitoka sare ya 2-2  ..

Manchester City atamkaribisha West Bromwich etihad studim. ...hii mechi ni muhimu kwa City ushindi wa Leo utamuweka katika mazingira mazuri ya kubaki top 4 ..

Ni hayo tu kwa Leo ..

Aliyoniambia Mwalimu kuhusu Maalim

Na Ahmed Rajab

KAMA ilivyo kwa Julius Kambarage Nyerere ndivyo ilivyo kwa Seif Sharif Hamad. Wote ni maarufu kimataifa kwa jina moja tu. Mmoja Mwalimu, mwengine Maalim. Majina mawili yenye maana moja. Majina hayo hutamkwa tofauti kutegemea mtu yuko wapi na amekulia katika mazingira gani.

Wote wawili, Mwalimu na Maalim, walikuwa na kazi ya ualimu kabla hawajawa wanasiasa waliobobea.

Nilianza kumjuwa Maalim kabla hajawa mwalimu tulipokuwa wanafunzi katika skuli ya King George VI Memorial Grammar Secondary School, (siku hizi Skuli ya Sekondari ya Lumumba) iliyoko Saateni, Unguja. Alikuwa mbele yangu kwa miaka miwili.

Hakuwa mzungumzaji wangu. Kwa hakika, hakuwa akichanganyika sana na wanafunzi wengine. Miaka hiyo nikimuona tu skuli, akiwa mmoja wa wanafunzi kutoka Pemba waliokuwa wakiishi katika bweni ya Beit el Ras, nje kidogo ya mji. Wakiletwa skuli kila asubuhi na kurejeshwa mchana kwa magari ya bweni.

Seif wa siku hizo alikuwa mrefu, mwembamba, aliyepinda kidogo na aliyekuwa akivaa sare ya skuli, shati jeupe na suruali ya kaki. Mara nyingine akija skuli akiwa amepiga kanzu na kofia. Mwalimu Mkuu wa skuli, G.G. Davies, akiruhusu kanzu na kofia kuwa ni sare mbadala.

Nadhani sikio moja la Seif likimpa taabu kwani alikuwa heshi kutia pamba sikioni. Jengine ninalolikumbuka ni kwamba alikuwa akitafakari sana. Daima uso wake ulikuwa chini akiwa mwenye mawazo. Akifikiri nini? Sijui. Na alikuwa na macho, ambayo Waingereza wangeliyaita “meditative eyes”, yaani macho ya tafakuri au ya mazingatio.

Waliosoma naye klasi moja wanasema Seif hakuwa mtu wa maneno mengi, wa mizaha isiyo na maana. Alikuwa mtulivu, mpole na mkimya. Wanasema ilikuwa taabu kuzijuwa fikira zake kwa vile alikuwa si mbobokaji. Akipendelea kuchunguza mambo tu na kuwasikiliza wengine kwa makini. Hata katika mijadala ya skuli alikuwa si mtetezi ingawa alikuwa hakosi kuhudhuria mijadala hiyo.

Seif alionyesha mapema dalili za uongozi. Alipokuwa darasa la kumi alikuwa kepteni wa bweni lao akiwasimamia hata wakubwa zake kwa umri.

Kwenye bweni lao akijulikana kwa kupenda kusoma. Baada ya saa nne za usiku jenereta lilipokuwa linazimwa, Seif alikuwa akiwasha taa ya kandili au karabai na akiendelea kusoma. Nadhani hiyo ndio sababu iliyomfanya baadhi ya wakati aonekane kama mtu aliyekosa usingizi.

Alipoingia Kidato cha Tano alikuwa ama kiranja au naibu wa kiranja wa skuli.

Tangu enzi hizo vijana wa Kipemba walikuwa wakinung’unika kwa namna kisiwa chao kilivyokuwa kikionewa na watawala licha ya kwamba Zanzibar ikipata sehemu kubwa ya mapato yake kutoka mauzo ya karafuu za Pemba na, kwa hivyo, kisiwa cha Unguja kikinufaika zaidi.

Kulikuwa na jengine lililokuwa likiwaudhi: sisi wa Unguja tukipenda kuwafanyia stihizai.

Tukiwatumbukiza katika kapu moja na tukiwafanyia tashititi na kuwacheka, kwa mfano, kwa lafudhi zao au kwamba eti wakipenda sana vitu vitamu kiasi cha kuwafanya wawe wanakula haluwa kwa chai ya maziwa.

Nadhani idhilali hizo ndizo zilizozidi kuwafanya wawe kitu kimoja na zilizowafanya waamue kuwa na chama chao cha wanafunzi wazawa wa Pemba. Badala ya kujiunga na All Zanzibar Students’ Union (AZSU), chama cha wanafunzi wa Zanzibar nzima, wao waliunda chama walichokiita rasmi Pemba Students’ Union (PSU, Chama cha Wanafunzi wa Pemba). Wengine wakikiita Pemba-Born Students’ Union, yaani Chama cha Wanafunzi Waliozaliwa Pemba.

Chama cha PSU kilikuwa na kamati ya watu watano na Seif ndiye aliyekuwa kiongozi wao.

Wanafunzi hao wa Kipemba wakishikamana bila ya kujali vyama vyao vya siasa. Seif alikuwa mfuasi wa Afro-Shirazi Party (ASP). Mwanafunzi mwengine wa Kipemba, Enosh Timothy Bilal, niliyekuwa nikikaa naye deski moja skuli na aliyekuwa akiishi Beit el Ras, naye pia alikuwa mfuasi mkubwa wa ASP.

Nakumbuka kuna wakati vijana hawa kutoka Pemba walianzisha vuguvugu lao lisilo rasmi waliloliita “Pemba Yekka”. Waliliigiza jina la chama cha Kabaka Yekka cha Uganda, chama ambacho kilikuwa kikimuunga mkono Kabaka Mutesa, mfalme wa Wabaganda.

Kwa lugha ya Kiganda “yekka” maana yake ni “tu”, kwa hivyo “Kabaka Yekka” ilikuwa na maana ya “Kabaka Tu”.

Wabaganda wakiyatumia matamshi hayo kusalimiana. Mmoja akisema “Kabaka”, mwengine akiitika “Yekka” na halafu kila mmojawao akionyesha juu kidole chake cha shahada.

Wafuasi wa Pemba Yekka hawakuwa wakisalimiana kwa kaulimbiu hiyo iliyokuwa na maana ya “Pemba Tu”.

Nilipoondoka Zanzibar 1964 kwenda Uingereza kwa masomo Seif alikuwa ameshahitimu Kidato cha Sita na alilazimishwa kusomesha skuli za sekondari. Kwanza aliajiriwa Lumumba alikosomesha Kiingereza, Fasihi na Historia.

Nasikia Maalim Seif alikuwa mwalimu mzuri. Aliendelea kusomesha hadi 1972, pale serikali ya Rais Aboud Jumbe ilipompatia nafasi ya kuingia Chuo Kikuu cha Dar es Salaam alikohitimu na kutunukiwa shahada ya B.A. (Hons) miaka mitatu baadaye.

Tangu 1964 sikumshuhudia tena Seif hadi mwezi wa mfungo wa Ramadhani katika miaka ya kati ya 1970 nilipokutana naye Mombasa. Ilisadifu kwamba akija kufuturu Mji wa Kale katika nyumba niliyoshukia ya Maalim Saleh Abdallah Jahadhmy “mwandani”, mwalimu wetu wa zamani aliyekuwa na asili ya Lamu.

Tulikuwa tukifuturu watu wanne; mwengine akiwa kijana wa Kikenya. Wakati wa futari Maalim Jahadhmy alikuwa akiulizauliza habari za siasa. Wakati wote, kama kawaida yake, Seif alikuwa akisikiliza tu. Hakujifanya mjuaji ingawa nina hakika akiyajuwa mengi. Mimi ndiye niliyejidai kujuwa na nikimjibu Jahadhmy.

Maalim aliweza kuchupa na kutua kwenye medani ya siasa za kitaifa alipoteuliwa na Jumbe awe waziri wa elimu wa Zanzibar 1977.

Jumbe, mwalimu wetu wa zamani katika skuli ya King George, akimpenda Maalim na alimsaidia kwa kumpa fursa ya kusoma masomo ya juu na kwa kumuingiza katika siasa za kitaifa. Unaweza kusema kwamba ndiye aliyemjenga.

Mwalimu Nyerere, ambaye mwanzoni akimpenda Maalim, akijigamba kwamba ni yeye aliyemjenga.

Niliwahi kuandika katika ukurasa huu nilipomkuta Mwalimu akibugia njugu na bia chumbani kwake katika hoteli ya Intercontinental jijini Nairobi kabla ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kumpata mgombea wake wa urais katika uchaguzi wa 1995. Mwalimu aliniuliza watu wakisemaje kuhusu mchuano huo.

Nikamjibu: “Wanasema una mtu wako.”

“Nani?”

“Salim (Salim Ahmed Salim)”

“Kwa nini?”

“Kwa sababu mtoto wako.”

Kumwambia hivyo aliruka na akanambia kwa mkazo: “Lakini wote watoto wangu. Kwani hata Seif, nani unadhani kamjenga?”

Nikamwambia: “Wewe” kwa sababu nikijuwa kwamba ndivyo alivyotaka nimwambie.

“Tena!” Mwalimu alisema kwa hamasa na kana kwamba akijipongeza akiwa anapiga soga barazani na vijana wa mjini.

Ilikuwa wazi alipoyasema hayo kwamba aliona fahari kubwa kujihusisha na Maalim kwani aliutambua uwezo wake, kipaji chake na utendajikazi wake. Ndio maana alimkabidhi nyadhifa kubwa kubwa ndani ya CCM. Hata wakati wa sokomoko la kisiasa Zanzibar katika enzi ya Rais mstaafu Salmin Amour, Nyerere aliwahi kutamka kwamba ufumbuzi wa mgogoro wa Zanzibar lazima umhusishe Maalim.

Na kuna ule mkutano wa siri Butiama ambao mpaka leo hatujui kilipita nini baina ya Maalim na Mwalimu.

Tunachokijuwa ni kwamba Maalim hakuzuzuka kwa kupendwa na Mwalimu. Alithubutu kusimama imara akitetea msimamo wake kuhusu Zanzibar, hatua ambayo ilisababisha akamatwe na kuwekwa ndani gerezani.

Katika ushirikiano wa Maalim na Mwalimu kuna kadhia moja iliyomtia doa Maalim, doa litalomganda maisha. Hii ni kadhia ya jinsi Mwalimu na CCM walivyompindua Jumbe.

Kuna wanaomtuhumu Maalim kwamba alimwendea kinyume Jumbe na kumfanyia hiyana. Juu ya hayo, tusisahau tu kwamba historia ina mifano mingi ya watu waliowahini wenzao kwa malengo adhimu.

Maalim amejaribu sana kujitetea lakini utetezi wake bado haukuwaridhisha wanaomtuhumu.

Kwa upande mwingine, msimamo wa Maalim kuhusu suala la usawa wa Tanganyika na Zanzibar ulimfanya awe mwiba uliokuwa ukimchoma Mwalimu. Aliushikilia msimamo huo hata alipokuwa waziri kiongozi wa Zanzibar (1984-1988). Mwishowe Mwalimu alibidi ampikie jungu la kumfukuzisha kutoka CCM.

Moja ya sababu zilizomfukuzisha Maalim kutoka CCM ni idadi ndogo sana ya kura alizopata Rais Idrissa Abdul Wakil huko Pemba katika uchaguzi wa chama kimoja uliofanywa 1985.

Lawama ilimwangukia Maalim kuwa eti alimtilia fitna Abdul Wakil Pemba na ndio maana huko aliondokea patupu.

Baada ya kufukuzwa CCM na kabla ya vyama vya siasa kuhalalishwa nchini 1992, Maalim Seif alikuwa akiliongoza vuguvugu la KAMAHURU pamoja na akina Shaaban Mloo, Maulidi Makame, Ali Haji Pandu na Hamad Rashid.

Kilikuwa kipindi kigumu kwake. Wakati huo katika miaka ya 1980 tayari kulikuwako na vuguvugu la Wazanzibari nje ya nchi lililoasisiwa kwenye mkutano uliofanywa mjini Malmo, Sweden, chini ya uenyekiti wa Abdulrahman Babu, aliyekuwa kiongozi wa chama cha zamani cha Umma Party.

Vuguvugu hilo likiitwa Harakati za Kuleta Mabadiliko ya Kidemokrasia (kwa ufupi HAMAKI na kwa Kiingereza likiitwa Zanzibar Democratic Alternative). Waliokuwa kwenye vuguvugu hilo walikuwa Wazanzibari wa itikadi tofauti za kisiasa. Miongoni mwao alikuwa Dk. Yusuf Saleh Salim aliyekuwa na mahusiano mazuri na viongozi wa KAMAHURU.

Alipokuwa akiongoza KAMAHURU ndipo ukomavu wa kisiasa wa Maalim ulipoanza kudhihirika na dunia ilipoanza kutambua kwamba Zanzibar ina kiongozi wa kipaji cha juu. Naweza kusema kwamba miongoni mwa magwiji wa kisiasa waliovutiwa naye alikuwa Babu.

Watu wawili hao walikuwa na itikadi tofauti lakini kwa maslahi ya Zanzibar fikira zao zilioana. Ninayajuwa hayo kwa sababu mimi ndiye niliyewakutanisha ana kwa ana kwa mara ya kwanza. Ilikuwa 1988 nilipowaalika kwa chakula cha usiku nyumbani kwangu, siku hizo nikiwa katika mtaa wa Stoke Newington, London.

Babu baadaye alijiunga na NCCR-Mageuzi lakini akitambua kwamba kiongozi atayeweza kuleta mageuzi ya kimaendeleo Zanzibar ni Maalim. Alikuwa na sababu zilizomfanya ajiunge na NCCR-Mageuzi lakini hazikuwa za kutokuwa na imani na Maalim.

Maalim Seif hajakamilika na wala hawezi kukamilika kwani ni mwanadamu. Hata hivyo, ninaamini ukiwachukuwa wanasiasa wote wa Zanzibar ya leo ukawaweka kwenye mezani uwapime kwa vigezo vyote vya umahiri wa kisiasa, Maalim atawapiku wenzake.

Yeye pamoja na Rais Mstaafu Dk. Amani Karume ni viongozi wenye sifa tofauti, kwa mfano, na zile walizokuwa nazo akina Sheikh Ali Muhsin Barwani (aliyekuwa kiongozi wa Zanzibar Nationalist Party au Hizbu) na Sheikh Abeid Amani Karume (aliyekuwa kiongozi wa ASP). Hao walikuwa viongozi wa kihistoria.

Watu wengi husahau kwamba kwa upande wa Sheikh Ali jambo la mwanzo alilolifanya baada ya kuingia siasa ni kujiuzulu kutoka Jumuiya ya Waarabu akiuweka mbele Uzanzibari wake. Sheikh Karume, kwa upande wake, akionekana na wengi wa Wazanzibari waliokuwa wakijifaharisha na “Uafrika” kuwa ni mkombozi wao.

Babu, niliyekuwa mimi nikimfuata, kidogo ananipa taabu. Ninaweza nikamuweka katika shubaka la viongozi wa kihistoria lakini nadhani nitakuwa sahihi zaidi nikimpachika kwenye shubaka la peke yake akiwa mkunga wa historia.

Hawa viongozi wa leo, Maalim Seif na Dk. Karume, wamethibitisha kwamba wao ni viongozi wenye ujasiri na bisara (vision) kubwa. Tunaweza kuyamithilisha Maridhiano yao ya 2010 kuwa, kwa kiwango fulani, kama yale ya Afrika ya Kusini.

Amani Karume alikuwa kama FW de Klerk kwa kuwa na ujasiri wa kuwashawishi wenzake wafuate mkondo wa kihistoria baada ya kutanabahi kwamba Zanzibar imekuwa ikielekea pabaya na watu wake wamechoka na uhasama.

Maalim, kiongozi aliyekuwa upande wa haki na aliyedhulumiwa, amekuwa kama Nelson Mandela. Kwa bahati mbaya, Maalim hadi leo bado anadhulumiwa. Ni dalili ya ujasiri wake kuwa ameweza kuwafanya wafuasi wake wawe watulivu na wayakubali Maridhiano.

Wa mwanzo kumbandika Maalim sifa ya “Umandela” walikuwa wafungwa aliowakuta gerezani Unguja alipokuwa katiwa ndani kuanzia Mei 11, 1989. Julai na Septemba 6 ya mwaka huo aliniandikia barua mbili akiwa jela akinieleza maisha yake yalivyokuwa huko kifungoni. Miezi sita baadaye aliniletea waraka alioandika wenye kurasa 32 akizichambua siasa za kimataifa, za barani Afrika na za Tanzania.

Baruapepe: ahmed@ahmedrajab.com

CHANZO: RAIA MWEMA, Toleo 452, Aprili 6, 2016

Aliyoniambia Mwalimu kuhusu Maalim

Na Ahmed Rajab

KAMA ilivyo kwa Julius Kambarage Nyerere ndivyo ilivyo kwa Seif Sharif Hamad. Wote ni maarufu kimataifa kwa jina moja tu. Mmoja Mwalimu, mwengine Maalim. Majina mawili yenye maana moja. Majina hayo hutamkwa tofauti kutegemea mtu yuko wapi na amekulia katika mazingira gani.

Wote wawili, Mwalimu na Maalim, walikuwa na kazi ya ualimu kabla hawajawa wanasiasa waliobobea.

Nilianza kumjuwa Maalim kabla hajawa mwalimu tulipokuwa wanafunzi katika skuli ya King George VI Memorial Grammar Secondary School, (siku hizi Skuli ya Sekondari ya Lumumba) iliyoko Saateni, Unguja. Alikuwa mbele yangu kwa miaka miwili.

Hakuwa mzungumzaji wangu. Kwa hakika, hakuwa akichanganyika sana na wanafunzi wengine. Miaka hiyo nikimuona tu skuli, akiwa mmoja wa wanafunzi kutoka Pemba waliokuwa wakiishi katika bweni ya Beit el Ras, nje kidogo ya mji. Wakiletwa skuli kila asubuhi na kurejeshwa mchana kwa magari ya bweni.

Seif wa siku hizo alikuwa mrefu, mwembamba, aliyepinda kidogo na aliyekuwa akivaa sare ya skuli, shati jeupe na suruali ya kaki. Mara nyingine akija skuli akiwa amepiga kanzu na kofia. Mwalimu Mkuu wa skuli, G.G. Davies, akiruhusu kanzu na kofia kuwa ni sare mbadala.

Nadhani sikio moja la Seif likimpa taabu kwani alikuwa heshi kutia pamba sikioni. Jengine ninalolikumbuka ni kwamba alikuwa akitafakari sana. Daima uso wake ulikuwa chini akiwa mwenye mawazo. Akifikiri nini? Sijui. Na alikuwa na macho, ambayo Waingereza wangeliyaita “meditative eyes”, yaani macho ya tafakuri au ya mazingatio.

Waliosoma naye klasi moja wanasema Seif hakuwa mtu wa maneno mengi, wa mizaha isiyo na maana. Alikuwa mtulivu, mpole na mkimya. Wanasema ilikuwa taabu kuzijuwa fikira zake kwa vile alikuwa si mbobokaji. Akipendelea kuchunguza mambo tu na kuwasikiliza wengine kwa makini. Hata katika mijadala ya skuli alikuwa si mtetezi ingawa alikuwa hakosi kuhudhuria mijadala hiyo.

Seif alionyesha mapema dalili za uongozi. Alipokuwa darasa la kumi alikuwa kepteni wa bweni lao akiwasimamia hata wakubwa zake kwa umri.

Kwenye bweni lao akijulikana kwa kupenda kusoma. Baada ya saa nne za usiku jenereta lilipokuwa linazimwa, Seif alikuwa akiwasha taa ya kandili au karabai na akiendelea kusoma. Nadhani hiyo ndio sababu iliyomfanya baadhi ya wakati aonekane kama mtu aliyekosa usingizi.

Alipoingia Kidato cha Tano alikuwa ama kiranja au naibu wa kiranja wa skuli.

Tangu enzi hizo vijana wa Kipemba walikuwa wakinung’unika kwa namna kisiwa chao kilivyokuwa kikionewa na watawala licha ya kwamba Zanzibar ikipata sehemu kubwa ya mapato yake kutoka mauzo ya karafuu za Pemba na, kwa hivyo, kisiwa cha Unguja kikinufaika zaidi.

Kulikuwa na jengine lililokuwa likiwaudhi: sisi wa Unguja tukipenda kuwafanyia stihizai.

Tukiwatumbukiza katika kapu moja na tukiwafanyia tashititi na kuwacheka, kwa mfano, kwa lafudhi zao au kwamba eti wakipenda sana vitu vitamu kiasi cha kuwafanya wawe wanakula haluwa kwa chai ya maziwa.

Nadhani idhilali hizo ndizo zilizozidi kuwafanya wawe kitu kimoja na zilizowafanya waamue kuwa na chama chao cha wanafunzi wazawa wa Pemba. Badala ya kujiunga na All Zanzibar Students’ Union (AZSU), chama cha wanafunzi wa Zanzibar nzima, wao waliunda chama walichokiita rasmi Pemba Students’ Union (PSU, Chama cha Wanafunzi wa Pemba). Wengine wakikiita Pemba-Born Students’ Union, yaani Chama cha Wanafunzi Waliozaliwa Pemba.

Chama cha PSU kilikuwa na kamati ya watu watano na Seif ndiye aliyekuwa kiongozi wao.

Wanafunzi hao wa Kipemba wakishikamana bila ya kujali vyama vyao vya siasa. Seif alikuwa mfuasi wa Afro-Shirazi Party (ASP). Mwanafunzi mwengine wa Kipemba, Enosh Timothy Bilal, niliyekuwa nikikaa naye deski moja skuli na aliyekuwa akiishi Beit el Ras, naye pia alikuwa mfuasi mkubwa wa ASP.

Nakumbuka kuna wakati vijana hawa kutoka Pemba walianzisha vuguvugu lao lisilo rasmi waliloliita “Pemba Yekka”. Waliliigiza jina la chama cha Kabaka Yekka cha Uganda, chama ambacho kilikuwa kikimuunga mkono Kabaka Mutesa, mfalme wa Wabaganda.

Kwa lugha ya Kiganda “yekka” maana yake ni “tu”, kwa hivyo “Kabaka Yekka” ilikuwa na maana ya “Kabaka Tu”.

Wabaganda wakiyatumia matamshi hayo kusalimiana. Mmoja akisema “Kabaka”, mwengine akiitika “Yekka” na halafu kila mmojawao akionyesha juu kidole chake cha shahada.

Wafuasi wa Pemba Yekka hawakuwa wakisalimiana kwa kaulimbiu hiyo iliyokuwa na maana ya “Pemba Tu”.

Nilipoondoka Zanzibar 1964 kwenda Uingereza kwa masomo Seif alikuwa ameshahitimu Kidato cha Sita na alilazimishwa kusomesha skuli za sekondari. Kwanza aliajiriwa Lumumba alikosomesha Kiingereza, Fasihi na Historia.

Nasikia Maalim Seif alikuwa mwalimu mzuri. Aliendelea kusomesha hadi 1972, pale serikali ya Rais Aboud Jumbe ilipompatia nafasi ya kuingia Chuo Kikuu cha Dar es Salaam alikohitimu na kutunukiwa shahada ya B.A. (Hons) miaka mitatu baadaye.

Tangu 1964 sikumshuhudia tena Seif hadi mwezi wa mfungo wa Ramadhani katika miaka ya kati ya 1970 nilipokutana naye Mombasa. Ilisadifu kwamba akija kufuturu Mji wa Kale katika nyumba niliyoshukia ya Maalim Saleh Abdallah Jahadhmy “mwandani”, mwalimu wetu wa zamani aliyekuwa na asili ya Lamu.

Tulikuwa tukifuturu watu wanne; mwengine akiwa kijana wa Kikenya. Wakati wa futari Maalim Jahadhmy alikuwa akiulizauliza habari za siasa. Wakati wote, kama kawaida yake, Seif alikuwa akisikiliza tu. Hakujifanya mjuaji ingawa nina hakika akiyajuwa mengi. Mimi ndiye niliyejidai kujuwa na nikimjibu Jahadhmy.

Maalim aliweza kuchupa na kutua kwenye medani ya siasa za kitaifa alipoteuliwa na Jumbe awe waziri wa elimu wa Zanzibar 1977.

Jumbe, mwalimu wetu wa zamani katika skuli ya King George, akimpenda Maalim na alimsaidia kwa kumpa fursa ya kusoma masomo ya juu na kwa kumuingiza katika siasa za kitaifa. Unaweza kusema kwamba ndiye aliyemjenga.

Mwalimu Nyerere, ambaye mwanzoni akimpenda Maalim, akijigamba kwamba ni yeye aliyemjenga.

Niliwahi kuandika katika ukurasa huu nilipomkuta Mwalimu akibugia njugu na bia chumbani kwake katika hoteli ya Intercontinental jijini Nairobi kabla ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kumpata mgombea wake wa urais katika uchaguzi wa 1995. Mwalimu aliniuliza watu wakisemaje kuhusu mchuano huo.

Nikamjibu: “Wanasema una mtu wako.”

“Nani?”

“Salim (Salim Ahmed Salim)”

“Kwa nini?”

“Kwa sababu mtoto wako.”

Kumwambia hivyo aliruka na akanambia kwa mkazo: “Lakini wote watoto wangu. Kwani hata Seif, nani unadhani kamjenga?”

Nikamwambia: “Wewe” kwa sababu nikijuwa kwamba ndivyo alivyotaka nimwambie.

“Tena!” Mwalimu alisema kwa hamasa na kana kwamba akijipongeza akiwa anapiga soga barazani na vijana wa mjini.

Ilikuwa wazi alipoyasema hayo kwamba aliona fahari kubwa kujihusisha na Maalim kwani aliutambua uwezo wake, kipaji chake na utendajikazi wake. Ndio maana alimkabidhi nyadhifa kubwa kubwa ndani ya CCM. Hata wakati wa sokomoko la kisiasa Zanzibar katika enzi ya Rais mstaafu Salmin Amour, Nyerere aliwahi kutamka kwamba ufumbuzi wa mgogoro wa Zanzibar lazima umhusishe Maalim.

Na kuna ule mkutano wa siri Butiama ambao mpaka leo hatujui kilipita nini baina ya Maalim na Mwalimu.

Tunachokijuwa ni kwamba Maalim hakuzuzuka kwa kupendwa na Mwalimu. Alithubutu kusimama imara akitetea msimamo wake kuhusu Zanzibar, hatua ambayo ilisababisha akamatwe na kuwekwa ndani gerezani.

Katika ushirikiano wa Maalim na Mwalimu kuna kadhia moja iliyomtia doa Maalim, doa litalomganda maisha. Hii ni kadhia ya jinsi Mwalimu na CCM walivyompindua Jumbe.

Kuna wanaomtuhumu Maalim kwamba alimwendea kinyume Jumbe na kumfanyia hiyana. Juu ya hayo, tusisahau tu kwamba historia ina mifano mingi ya watu waliowahini wenzao kwa malengo adhimu.

Maalim amejaribu sana kujitetea lakini utetezi wake bado haukuwaridhisha wanaomtuhumu.

Kwa upande mwingine, msimamo wa Maalim kuhusu suala la usawa wa Tanganyika na Zanzibar ulimfanya awe mwiba uliokuwa ukimchoma Mwalimu. Aliushikilia msimamo huo hata alipokuwa waziri kiongozi wa Zanzibar (1984-1988). Mwishowe Mwalimu alibidi ampikie jungu la kumfukuzisha kutoka CCM.

Moja ya sababu zilizomfukuzisha Maalim kutoka CCM ni idadi ndogo sana ya kura alizopata Rais Idrissa Abdul Wakil huko Pemba katika uchaguzi wa chama kimoja uliofanywa 1985.

Lawama ilimwangukia Maalim kuwa eti alimtilia fitna Abdul Wakil Pemba na ndio maana huko aliondokea patupu.

Baada ya kufukuzwa CCM na kabla ya vyama vya siasa kuhalalishwa nchini 1992, Maalim Seif alikuwa akiliongoza vuguvugu la KAMAHURU pamoja na akina Shaaban Mloo, Maulidi Makame, Ali Haji Pandu na Hamad Rashid.

Kilikuwa kipindi kigumu kwake. Wakati huo katika miaka ya 1980 tayari kulikuwako na vuguvugu la Wazanzibari nje ya nchi lililoasisiwa kwenye mkutano uliofanywa mjini Malmo, Sweden, chini ya uenyekiti wa Abdulrahman Babu, aliyekuwa kiongozi wa chama cha zamani cha Umma Party.

Vuguvugu hilo likiitwa Harakati za Kuleta Mabadiliko ya Kidemokrasia (kwa ufupi HAMAKI na kwa Kiingereza likiitwa Zanzibar Democratic Alternative). Waliokuwa kwenye vuguvugu hilo walikuwa Wazanzibari wa itikadi tofauti za kisiasa. Miongoni mwao alikuwa Dk. Yusuf Saleh Salim aliyekuwa na mahusiano mazuri na viongozi wa KAMAHURU.

Alipokuwa akiongoza KAMAHURU ndipo ukomavu wa kisiasa wa Maalim ulipoanza kudhihirika na dunia ilipoanza kutambua kwamba Zanzibar ina kiongozi wa kipaji cha juu. Naweza kusema kwamba miongoni mwa magwiji wa kisiasa waliovutiwa naye alikuwa Babu.

Watu wawili hao walikuwa na itikadi tofauti lakini kwa maslahi ya Zanzibar fikira zao zilioana. Ninayajuwa hayo kwa sababu mimi ndiye niliyewakutanisha ana kwa ana kwa mara ya kwanza. Ilikuwa 1988 nilipowaalika kwa chakula cha usiku nyumbani kwangu, siku hizo nikiwa katika mtaa wa Stoke Newington, London.

Babu baadaye alijiunga na NCCR-Mageuzi lakini akitambua kwamba kiongozi atayeweza kuleta mageuzi ya kimaendeleo Zanzibar ni Maalim. Alikuwa na sababu zilizomfanya ajiunge na NCCR-Mageuzi lakini hazikuwa za kutokuwa na imani na Maalim.

Maalim Seif hajakamilika na wala hawezi kukamilika kwani ni mwanadamu. Hata hivyo, ninaamini ukiwachukuwa wanasiasa wote wa Zanzibar ya leo ukawaweka kwenye mezani uwapime kwa vigezo vyote vya umahiri wa kisiasa, Maalim atawapiku wenzake.

Yeye pamoja na Rais Mstaafu Dk. Amani Karume ni viongozi wenye sifa tofauti, kwa mfano, na zile walizokuwa nazo akina Sheikh Ali Muhsin Barwani (aliyekuwa kiongozi wa Zanzibar Nationalist Party au Hizbu) na Sheikh Abeid Amani Karume (aliyekuwa kiongozi wa ASP). Hao walikuwa viongozi wa kihistoria.

Watu wengi husahau kwamba kwa upande wa Sheikh Ali jambo la mwanzo alilolifanya baada ya kuingia siasa ni kujiuzulu kutoka Jumuiya ya Waarabu akiuweka mbele Uzanzibari wake. Sheikh Karume, kwa upande wake, akionekana na wengi wa Wazanzibari waliokuwa wakijifaharisha na “Uafrika” kuwa ni mkombozi wao.

Babu, niliyekuwa mimi nikimfuata, kidogo ananipa taabu. Ninaweza nikamuweka katika shubaka la viongozi wa kihistoria lakini nadhani nitakuwa sahihi zaidi nikimpachika kwenye shubaka la peke yake akiwa mkunga wa historia.

Hawa viongozi wa leo, Maalim Seif na Dk. Karume, wamethibitisha kwamba wao ni viongozi wenye ujasiri na bisara (vision) kubwa. Tunaweza kuyamithilisha Maridhiano yao ya 2010 kuwa, kwa kiwango fulani, kama yale ya Afrika ya Kusini.

Amani Karume alikuwa kama FW de Klerk kwa kuwa na ujasiri wa kuwashawishi wenzake wafuate mkondo wa kihistoria baada ya kutanabahi kwamba Zanzibar imekuwa ikielekea pabaya na watu wake wamechoka na uhasama.

Maalim, kiongozi aliyekuwa upande wa haki na aliyedhulumiwa, amekuwa kama Nelson Mandela. Kwa bahati mbaya, Maalim hadi leo bado anadhulumiwa. Ni dalili ya ujasiri wake kuwa ameweza kuwafanya wafuasi wake wawe watulivu na wayakubali Maridhiano.

Wa mwanzo kumbandika Maalim sifa ya “Umandela” walikuwa wafungwa aliowakuta gerezani Unguja alipokuwa katiwa ndani kuanzia Mei 11, 1989. Julai na Septemba 6 ya mwaka huo aliniandikia barua mbili akiwa jela akinieleza maisha yake yalivyokuwa huko kifungoni. Miezi sita baadaye aliniletea waraka alioandika wenye kurasa 32 akizichambua siasa za kimataifa, za barani Afrika na za Tanzania.

Baruapepe: ahmed@ahmedrajab.com

CHANZO: RAIA MWEMA, Toleo 452, Aprili 6, 2016