.

.

Wednesday, 17 August 2016

YANGA na Azam leo zinakutana kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam katika mechi ya Ngao ya Jamii kuashiria uzinduzi wa Ligi Kuu inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi mwishoni mwa wiki hii.
Timu hizo kwa muda mrefu zimekuwa zikipokezana kijiti kwenye anga za soka la kitaifa na kimataifa ambapo mwaka huu.
Azam ilishiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika na kutolewa mapema na Yanga iliyokuwa ikishiriki Ligi ya Mabingwa kabla ya kuangukia kwenye Kombe la Shirikisho ipo hatua ya makundi ya michuano hiyo licha ya kutokuwa na nafasi ya kusonga mbele.
Mara ya mwisho timu hizo zilikutana kwenye fainali ya Kombe la Shirikisho la TFF katika Uwanja wa Taifa ambapo Yanga ilishinda mabao 3-1. Aidha Yanga iliendelea kuitambia Azam tena katika mechi ya ngao ya Jamii msimu uliopita ambapo iliichapa kwa mikwaju ya penalti 8-7 baada ya kutoka sare ya bila kufungana kwa dakika 120 .
Katika mechi ya leo, Yanga itashuka dimbani ikitoka kupata ushindi wa bao 1-0 katika mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Mo Bejaia Jumamosi iliyopita baada ya kucheza mechi nne mfululizo kwenye michuano hiyo bila ushindi.
Lakini pia, ikiwa na rekodi ya kupoteza michezo kadhaa iliyopita ya michuano hiyo dhidi ya TP Mazembe 1-0, Medeama ugenini (3-1) na nyumbani (1-1), Mo Bejaia ugenini (1-0).
Yanga sasa inasubiri kukamilisha ratiba dhidi ya Mazembe katika mechi ya mwisho ya makundi baada ya kutokuwa na nafasi ya kufuzu nusu fainali ya michuano hiyo kutokana na ushindi wa mabao 3-2 wa Medeama dhidi ya Mazembe mwishoni mwa wiki iliyopita.
Kocha Mkuu wa Yanga Hans Pluijm alisema jana kuwa wamesahau yaliyopita na matarajio yao ni kushinda mchezo wa leo ili kuwa na mwanzo mzuri wa maandalizi ya Ligi Kuu Tanzania bara wakiwa mabingwa watetezi.
“Hakuna timu yoyote inayotutisha na kila siku tumekuwa tukifanya mazoezi na kujiimarisha, lengo letu ni kuendeleza rekodi ya kushinda mataji,” alisema.
Huenda Yanga ikawakosa wachezaji wake muhimu kama kipa Ally Mustafa ‘Barthez’ anayesumbuliwa na maumivu ya kifundo cha mguu, mabeki Juma Abdul, Andrew Vincent ‘Dante’ wanaosumbuliwa na maumivu ya miguu, Kevin Yondani anayeumwa jicho na kiungo Obrey Chirwa anayeumwa goti.
Aidha, mchezo wa leo utakuwa ni mtihani mkubwa wa kwanza kwa Kocha Mkuu wa Azam Mhispania Zeben Hernandez ambaye aliahidi kurejesha imani ya mashabiki wa Azam FC kwani anatarajia kutumia mfumo wa pasi nyingi ambao unatumiwa na timu ya Ligi Kuu Hispania ‘La Liga’ Barcelona.
Timu hiyo imefanya maandalizi ya muda mrefu na kucheza mechi kadhaa za kirafiki ikiwa ni sehemu ya maandalizi yao ya ligi. Ilicheza dhidi ya URA ya Uganda (1-1), dhidi ya Friends Rangers (2-1), Ashanti United (2-0), Mshikamano (1-0), Kombaini ya Wilaya ya Mjini (1-0), Taifa Jang’ombe (1-0), na sare mbili ilipocheza na JKT Ruvu (1-1) na Ruvu Shooting (1-1).
Akizungumzia mchezo huo Hernandez, aliweka wazi kuwa ana uhakika mkubwa wa kuifunga Yanga kwenye mchezo wa leo kwani tayari amepata kikosi chake cha kwanza baada ya michezo hiyo ya kirafiki.
“Siwezi kuzungumzia sana mechi ya Yanga kwa sababu naamini ya kuwa jitihada zangu na taaluma ninayowapa wachezaji wangu naamini itatoa matunda, lakini natambua ya kuwa Yanga ni timu ya zamani ipo na inacheza vizuri, kikubwa naamini nitashinda mchezo huo kulingana na kile ninachowapa wachezaji wangu,” alisema.
Azam FC huenda ikawakosa wachezaji wake Aggrey Morris na Paschal Wawa ambao ni majeruhi wa muda mrefu, ingawa wameshaanza mazoezi mepesi. Lakini pia, wanajivunia usajili wa beki mpya Bruce Kangwa anayetokea Highlanders ya Zimbabwe.

YANGA na Azam leo zinakutana kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam katika mechi ya Ngao ya Jamii kuashiria uzinduzi wa Ligi Kuu inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi mwishoni mwa wiki hii.
Timu hizo kwa muda mrefu zimekuwa zikipokezana kijiti kwenye anga za soka la kitaifa na kimataifa ambapo mwaka huu.
Azam ilishiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika na kutolewa mapema na Yanga iliyokuwa ikishiriki Ligi ya Mabingwa kabla ya kuangukia kwenye Kombe la Shirikisho ipo hatua ya makundi ya michuano hiyo licha ya kutokuwa na nafasi ya kusonga mbele.
Mara ya mwisho timu hizo zilikutana kwenye fainali ya Kombe la Shirikisho la TFF katika Uwanja wa Taifa ambapo Yanga ilishinda mabao 3-1. Aidha Yanga iliendelea kuitambia Azam tena katika mechi ya ngao ya Jamii msimu uliopita ambapo iliichapa kwa mikwaju ya penalti 8-7 baada ya kutoka sare ya bila kufungana kwa dakika 120 .
Katika mechi ya leo, Yanga itashuka dimbani ikitoka kupata ushindi wa bao 1-0 katika mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Mo Bejaia Jumamosi iliyopita baada ya kucheza mechi nne mfululizo kwenye michuano hiyo bila ushindi.
Lakini pia, ikiwa na rekodi ya kupoteza michezo kadhaa iliyopita ya michuano hiyo dhidi ya TP Mazembe 1-0, Medeama ugenini (3-1) na nyumbani (1-1), Mo Bejaia ugenini (1-0).
Yanga sasa inasubiri kukamilisha ratiba dhidi ya Mazembe katika mechi ya mwisho ya makundi baada ya kutokuwa na nafasi ya kufuzu nusu fainali ya michuano hiyo kutokana na ushindi wa mabao 3-2 wa Medeama dhidi ya Mazembe mwishoni mwa wiki iliyopita.
Kocha Mkuu wa Yanga Hans Pluijm alisema jana kuwa wamesahau yaliyopita na matarajio yao ni kushinda mchezo wa leo ili kuwa na mwanzo mzuri wa maandalizi ya Ligi Kuu Tanzania bara wakiwa mabingwa watetezi.
“Hakuna timu yoyote inayotutisha na kila siku tumekuwa tukifanya mazoezi na kujiimarisha, lengo letu ni kuendeleza rekodi ya kushinda mataji,” alisema.
Huenda Yanga ikawakosa wachezaji wake muhimu kama kipa Ally Mustafa ‘Barthez’ anayesumbuliwa na maumivu ya kifundo cha mguu, mabeki Juma Abdul, Andrew Vincent ‘Dante’ wanaosumbuliwa na maumivu ya miguu, Kevin Yondani anayeumwa jicho na kiungo Obrey Chirwa anayeumwa goti.
Aidha, mchezo wa leo utakuwa ni mtihani mkubwa wa kwanza kwa Kocha Mkuu wa Azam Mhispania Zeben Hernandez ambaye aliahidi kurejesha imani ya mashabiki wa Azam FC kwani anatarajia kutumia mfumo wa pasi nyingi ambao unatumiwa na timu ya Ligi Kuu Hispania ‘La Liga’ Barcelona.
Timu hiyo imefanya maandalizi ya muda mrefu na kucheza mechi kadhaa za kirafiki ikiwa ni sehemu ya maandalizi yao ya ligi. Ilicheza dhidi ya URA ya Uganda (1-1), dhidi ya Friends Rangers (2-1), Ashanti United (2-0), Mshikamano (1-0), Kombaini ya Wilaya ya Mjini (1-0), Taifa Jang’ombe (1-0), na sare mbili ilipocheza na JKT Ruvu (1-1) na Ruvu Shooting (1-1).
Akizungumzia mchezo huo Hernandez, aliweka wazi kuwa ana uhakika mkubwa wa kuifunga Yanga kwenye mchezo wa leo kwani tayari amepata kikosi chake cha kwanza baada ya michezo hiyo ya kirafiki.
“Siwezi kuzungumzia sana mechi ya Yanga kwa sababu naamini ya kuwa jitihada zangu na taaluma ninayowapa wachezaji wangu naamini itatoa matunda, lakini natambua ya kuwa Yanga ni timu ya zamani ipo na inacheza vizuri, kikubwa naamini nitashinda mchezo huo kulingana na kile ninachowapa wachezaji wangu,” alisema.
Azam FC huenda ikawakosa wachezaji wake Aggrey Morris na Paschal Wawa ambao ni majeruhi wa muda mrefu, ingawa wameshaanza mazoezi mepesi. Lakini pia, wanajivunia usajili wa beki mpya Bruce Kangwa anayetokea Highlanders ya Zimbabwe.

Monday, 15 August 2016

MANJI AAMUA KUKAA PEMBENI YANGA

Habari za uhakika ambazo tumezipata kutoka katika chanzo cha uhakika ndani ya Yanga zinaonyesha kuwa mwenyekiti wa Yanga Bw Yusuf manji ameamua kujiuzulu nafasi yake ya uenyekiti wa yanga pamoja na kusitisha kusudio lake la kuichukua na kuendesha kibiashara timu ya Yanga na nembo yake .
Hili ni anguko kuu kwa yanga endapo Bw Yusuf manji atajionda Yanga kutokana na ukweli kuwa tayari mahasimu wao wa jadi Simba wanakamilisha taratibu za kumkabidhi timu Bw mohamed Dewji MO.
Uamuzi wa manji kujiondoa yanga unatajwa kuchangiwa na shutuma zinazotolewa na baadhi ya viongozi wa serikali, na wengine kutoka ndani ya yanga ambao wanatumiwa na baadhi ya wafanyabiashara kwa maslahi yao binafsi na sio ya yanga.
Manji anaonekana kuchoshwa na tabia za baadhi ya watu kumtukana na kumkebehi kwa hatua yake ya kuichukua timu ya Yanga na sasa ameamua kukaa pembeni kulinda heshima yake .
Hata hivyo viongozi wa Secretary ya yanga siku nzima ya leo wameonekana kuchanganyikiwa uku baadhi wakiwa wanapigana vikumbo kuingia na kutoka quality plaza zilizopo ofisi za Bw manji hatua inayoashiri kuna jambo kubwa linatokea.

MANJI AAMUA KUKAA PEMBENI YANGA

Habari za uhakika ambazo tumezipata kutoka katika chanzo cha uhakika ndani ya Yanga zinaonyesha kuwa mwenyekiti wa Yanga Bw Yusuf manji ameamua kujiuzulu nafasi yake ya uenyekiti wa yanga pamoja na kusitisha kusudio lake la kuichukua na kuendesha kibiashara timu ya Yanga na nembo yake .
Hili ni anguko kuu kwa yanga endapo Bw Yusuf manji atajionda Yanga kutokana na ukweli kuwa tayari mahasimu wao wa jadi Simba wanakamilisha taratibu za kumkabidhi timu Bw mohamed Dewji MO.
Uamuzi wa manji kujiondoa yanga unatajwa kuchangiwa na shutuma zinazotolewa na baadhi ya viongozi wa serikali, na wengine kutoka ndani ya yanga ambao wanatumiwa na baadhi ya wafanyabiashara kwa maslahi yao binafsi na sio ya yanga.
Manji anaonekana kuchoshwa na tabia za baadhi ya watu kumtukana na kumkebehi kwa hatua yake ya kuichukua timu ya Yanga na sasa ameamua kukaa pembeni kulinda heshima yake .
Hata hivyo viongozi wa Secretary ya yanga siku nzima ya leo wameonekana kuchanganyikiwa uku baadhi wakiwa wanapigana vikumbo kuingia na kutoka quality plaza zilizopo ofisi za Bw manji hatua inayoashiri kuna jambo kubwa linatokea.

Friday, 12 August 2016

RAIS John Magufuli ameutaka uongozi wa Mkoa wa Mwanza, kuhakikisha kuwa watu waliopora mali za Chama cha Ushirika cha Nyanza (NCU), wanapatikana na kuzirudisha mali hizo mara moja, huku akiitaja Kampuni ya Simon Group yenye umiliki katika kampuni za UDA na mabasi ya haraka Dar es Salaam (UDA-RT).
Amesema NCU kwa sasa inashindwa kujiendesha kutokana na watu wachache kujitwalia mali za NCU kwa kuzinunua kwa bei ya hasara, kiasi cha kuifanya NCU kutokuwa na uwezo wa kununua mazao ya wakulima.
“RC (mkuu wa mkoa) umezungumza kwamba katika miaka yote aliyepewa alikuwa anunue kwa bilioni moja pointi amelipa milioni 30 tu na nasikia ni Simon Group. Mimi ni msemakweli na wala sitaki kuzunguka sijui nikasemee wapi,” alisema Rais Magufuli akiitaja kampuni hiyo inayomilikiwa na mfanyabiashara Simon Kisena.
Rais Magufuli aliyasema hayo jana jijini hapa wakati akiwahutubia maelfu ya wakazi wa Mwanza kwenye Viwanja vya Furahisha vilivyopo Manispaa ya Ilemela.
Awali Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella alimshukuru Rais Magufuli licha ya kuwa na ratiba ngumu ya kikazi, lakini ameonesha mapenzi makubwa kwa wakazi wa Mkoa wa Mwanza na kufanya ziara ya kikazi ya siku mbili.
Alisema mkoa umeanza na juhudi ya kufufua zao la pamba sanjari na kuanza kurudisha mali za NCU, ambazo ziliporwa na baadhi ya watu, alimuomba Rais Magufuli kuisaidia Serikali ya Mkoa ili kuhakikisha watu wote waliopora mali za NCU wanazirudisha kwa wakulima na wafikishwe mahakamani.
Lakini Rais Magufuli katika hotuba yake, alisema NCU kwa sasa inashindwa kujiendesha kutokana na watu wachache kujitwalia mali zake kwa kuzinunua kwa bei ya hasara, kiasi cha kuifanya kutokuwa na uwezo wa kununua mazao ya wakulima.
“Hata kama walichukua miaka 20 iliyopita, vyombo vya dola vichukue hatua na mali hizo zirudishwe kwa umma. Waziri wa Ushirika, ni heri ukose kula, mimi nitakuchagua kwenye viti maalumu, lakini mali za Nyanza zirudi,” alisema Rais Magufuli.
Aliwataka mafisadi wakae chonjo kuwa tayari kufikishwa mahakamani kwa sababu Bunge tayari limeishaipitisha sheria hiyo, ambayo itaanza utekelezaji wake mara moja.
Alisema sheria hiyo itakuwa ni mkombozi wa Watanzania ambao hivi sasa wamechoka na rushwa, ambapo alikiri kuwa kwa sasa rushwa ipo kila mahali nchini.
“Nawashukuru sana wabunge (hasa wa CCM) kwa kupitisha sheria hiyo ya mafisadi,” alisema Rais Magufuli.
Kuhusu uvuvi haramu kwa kutumia zana zisizokubalika kisheria, Rais Magufuli alishangaa kuona vyombo vilivyopewa jukumu la kudhibiti hali hiyo vikizembea wakati uharamia huo ukiendelea.
“Kama kuna mtu alichoma makokoro ni mimi na samaki waliongezeka. Wanapita kuna Polisi, Uhamiaji, TRA, lazima tulinde rasilimali yetu ili Watanzania waweze kufaidika. Hizo zana zinapitishwa kwenye mipaka, shikeni na hilo gari mtaifishe moja kwa moja kwa sababu hayapiti angani,” alieleza.
Katika hotuba yake, Rais Magufuli alisisitiza kuwa uchaguzi umekwisha na kwamba hakuna aliyeshinda wala kushindwa, bali Watanzania wote wameshinda. Alisisitiza kuwa atatekeleza ahadi zote alizoahidi wakati wa Uchaguzi Mkuu ikiwamo kulifanya Jiji la Mwanza kuwa jiji la biashara.
Akizungumzia hatua ambazo amekwishazichukua hadi sasa katika uongozi wake, alisema amebana matumizi ya serikali kwa kufuta safari zisizo za lazima nje ya nchi, kutumbua watumishi hewa, kutoa elimu bure, na mwezi ujao ndege mbili mpya zitatua nchini kutoka Canada zinaponunuliwa.
Akizungumzia upanuzi wa barabara ya Airport, Rais Magufuli aliyeongozana na mkewe, Janet, alimtaka Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk Edwin Ngonyani, Mtendaji Mkuu wa Tanroads, Patrick Mfugale kuhakikisha kuwa ujenzi wa barabara hiyo hadi Airport, badala ya kuishia Pasiansi, inajengwa haraka iwezekanavyo.
“Upanuzi wa barabara hii usiishie Pasiansi, uende hadi Airport na iwe ni barabara yenye njia nne ili kusudi watalii wanapofika hapa watambue kuwa wameingia jijini Mwanza,” alisema na kuongeza kuwa serikali itatoa fedha za upanuzi wa barabara hiyo hadi Airport na kuahidi kutoa kiasi cha fedha kitakachohitajika ukamilishaji ujenzi wake.
Aidha, alikerwa na ukusanyaji duni wa mapato yanayokusanywa kutoka kwenye vitega uchumi vya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuwataka viongozi wote wa chama kuhakikisha kuwa wanakusanya mapato halali yanayolingana na vitega uchumi walivyo navyo.
Kwa upande wake, Naibu Waziri Ngonyani aliwashukuru wakazi wa Mwanza kwa kazi kubwa waliyofanya ya kumchagua Dk Magufuli kuwa Rais wa Tanzania.

RAIS John Magufuli ameutaka uongozi wa Mkoa wa Mwanza, kuhakikisha kuwa watu waliopora mali za Chama cha Ushirika cha Nyanza (NCU), wanapatikana na kuzirudisha mali hizo mara moja, huku akiitaja Kampuni ya Simon Group yenye umiliki katika kampuni za UDA na mabasi ya haraka Dar es Salaam (UDA-RT).
Amesema NCU kwa sasa inashindwa kujiendesha kutokana na watu wachache kujitwalia mali za NCU kwa kuzinunua kwa bei ya hasara, kiasi cha kuifanya NCU kutokuwa na uwezo wa kununua mazao ya wakulima.
“RC (mkuu wa mkoa) umezungumza kwamba katika miaka yote aliyepewa alikuwa anunue kwa bilioni moja pointi amelipa milioni 30 tu na nasikia ni Simon Group. Mimi ni msemakweli na wala sitaki kuzunguka sijui nikasemee wapi,” alisema Rais Magufuli akiitaja kampuni hiyo inayomilikiwa na mfanyabiashara Simon Kisena.
Rais Magufuli aliyasema hayo jana jijini hapa wakati akiwahutubia maelfu ya wakazi wa Mwanza kwenye Viwanja vya Furahisha vilivyopo Manispaa ya Ilemela.
Awali Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella alimshukuru Rais Magufuli licha ya kuwa na ratiba ngumu ya kikazi, lakini ameonesha mapenzi makubwa kwa wakazi wa Mkoa wa Mwanza na kufanya ziara ya kikazi ya siku mbili.
Alisema mkoa umeanza na juhudi ya kufufua zao la pamba sanjari na kuanza kurudisha mali za NCU, ambazo ziliporwa na baadhi ya watu, alimuomba Rais Magufuli kuisaidia Serikali ya Mkoa ili kuhakikisha watu wote waliopora mali za NCU wanazirudisha kwa wakulima na wafikishwe mahakamani.
Lakini Rais Magufuli katika hotuba yake, alisema NCU kwa sasa inashindwa kujiendesha kutokana na watu wachache kujitwalia mali zake kwa kuzinunua kwa bei ya hasara, kiasi cha kuifanya kutokuwa na uwezo wa kununua mazao ya wakulima.
“Hata kama walichukua miaka 20 iliyopita, vyombo vya dola vichukue hatua na mali hizo zirudishwe kwa umma. Waziri wa Ushirika, ni heri ukose kula, mimi nitakuchagua kwenye viti maalumu, lakini mali za Nyanza zirudi,” alisema Rais Magufuli.
Aliwataka mafisadi wakae chonjo kuwa tayari kufikishwa mahakamani kwa sababu Bunge tayari limeishaipitisha sheria hiyo, ambayo itaanza utekelezaji wake mara moja.
Alisema sheria hiyo itakuwa ni mkombozi wa Watanzania ambao hivi sasa wamechoka na rushwa, ambapo alikiri kuwa kwa sasa rushwa ipo kila mahali nchini.
“Nawashukuru sana wabunge (hasa wa CCM) kwa kupitisha sheria hiyo ya mafisadi,” alisema Rais Magufuli.
Kuhusu uvuvi haramu kwa kutumia zana zisizokubalika kisheria, Rais Magufuli alishangaa kuona vyombo vilivyopewa jukumu la kudhibiti hali hiyo vikizembea wakati uharamia huo ukiendelea.
“Kama kuna mtu alichoma makokoro ni mimi na samaki waliongezeka. Wanapita kuna Polisi, Uhamiaji, TRA, lazima tulinde rasilimali yetu ili Watanzania waweze kufaidika. Hizo zana zinapitishwa kwenye mipaka, shikeni na hilo gari mtaifishe moja kwa moja kwa sababu hayapiti angani,” alieleza.
Katika hotuba yake, Rais Magufuli alisisitiza kuwa uchaguzi umekwisha na kwamba hakuna aliyeshinda wala kushindwa, bali Watanzania wote wameshinda. Alisisitiza kuwa atatekeleza ahadi zote alizoahidi wakati wa Uchaguzi Mkuu ikiwamo kulifanya Jiji la Mwanza kuwa jiji la biashara.
Akizungumzia hatua ambazo amekwishazichukua hadi sasa katika uongozi wake, alisema amebana matumizi ya serikali kwa kufuta safari zisizo za lazima nje ya nchi, kutumbua watumishi hewa, kutoa elimu bure, na mwezi ujao ndege mbili mpya zitatua nchini kutoka Canada zinaponunuliwa.
Akizungumzia upanuzi wa barabara ya Airport, Rais Magufuli aliyeongozana na mkewe, Janet, alimtaka Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk Edwin Ngonyani, Mtendaji Mkuu wa Tanroads, Patrick Mfugale kuhakikisha kuwa ujenzi wa barabara hiyo hadi Airport, badala ya kuishia Pasiansi, inajengwa haraka iwezekanavyo.
“Upanuzi wa barabara hii usiishie Pasiansi, uende hadi Airport na iwe ni barabara yenye njia nne ili kusudi watalii wanapofika hapa watambue kuwa wameingia jijini Mwanza,” alisema na kuongeza kuwa serikali itatoa fedha za upanuzi wa barabara hiyo hadi Airport na kuahidi kutoa kiasi cha fedha kitakachohitajika ukamilishaji ujenzi wake.
Aidha, alikerwa na ukusanyaji duni wa mapato yanayokusanywa kutoka kwenye vitega uchumi vya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuwataka viongozi wote wa chama kuhakikisha kuwa wanakusanya mapato halali yanayolingana na vitega uchumi walivyo navyo.
Kwa upande wake, Naibu Waziri Ngonyani aliwashukuru wakazi wa Mwanza kwa kazi kubwa waliyofanya ya kumchagua Dk Magufuli kuwa Rais wa Tanzania.