.

.

Saturday, 30 January 2016

DURU la pili la Ligi Kuu Tanzania Bara linaanza leo wakati timu 12 zikiwemo za Yanga na Simba kushuka kwenye viwanja tofauti kusaka pointi tatu muhimu. Hata hivyo, Azam FC inayoshika nafasi ya pili katika msimamo wa ligi hiyo, leo ilitakiwa kucheza na Prisons ya Mbeya, haitashuka dimbani kwa sababu inashiriki mashindano ya timu nne nchini Zambia.
Yanga wenyewe wako kileleni wakiwa na pointi 39 sawa na Azam FC, lakini wanaongoza kwa uwiano wa tofauti ya magoli, leo watakuwa wageni wa Coastal Union katika mchezo utakaofanyika kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga.
Katika mchezo wa raundi ya awali, Yanga iliibuka na ushindi wa mabao 2-0 katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Yanga watataka kudhihirisha kuwa hawakubahatisha kuifunga Coastal katika mchezo wa kwanza, huku Wagosi hao wa Kaya nao watataka kudhihirisha wao sio wanyonge mbele ya mabingwa hao watetezi.
Vijana hao wa Jangwani wakishinda leo watakuwa wamejikusanyia pointi 42 na kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo na kuiacha Azam FC ikibaki na pointi zake 39 katika nafasi ya pili.
Kwa upande wa Simba, wenyewe katika mchezo wa kwanza dhidi ya African Sports uliochezwa Mkwakwani, iliibuka na ushindi kiduchi wa bao 1-0, hivyo na leo itataka kuendeleza ubabe dhidi ya vijana hao wa Tanga.
Simba yenye pointi 33, inazihitaji sana pointi tatu kutoka kwa African Sports ili angalau izidi kujisogeza katika nafasi ya tatu nyuma ya Azam katika mbio hizo za ubingwa wa ligi hiyo.
Kwa sasa Simba inafundishwa na Mganda Jackson Mayanja aliyechukua nafasi ya Muingereza Dylan Kerr aliyetimuliwa licha ya timu hiyo kuwa katika nafasi ya tatu ya msimamo wa ligi hiyo.
Mayanja alisema pamoja na ugumu wa mchezo huo, watajitahidi kuibuka na ushindi ili kuendelea kuzifukuza Yanga na Azam FC zilizoko kileleni. Coastal Union na African Sports ziko katika nafasi ya 14 na 15 baada ya kucheza mechi 15 na kuambulia pointi tisa na 10 badala ya kuwa na pointi 45 kutoka katika mechi hizo 15 za duru la kwanza.
Mechi zingine leo ni JKT Ruvu watakuwa wenyeji wa Majina ya Songea, huku Mtibwa Sugar wakiikaribisha Stand United, wakati Mwadui FC itaikaribisha Toto African wakati Kagera Sugar watacheza na Mbeya City na Mgambo JKT watakuwa wenyeji wa Ndanda FC.
Ligi hiyo itaendelea tena kesho kwa Mgambo kuikaribisha Ndanda FC kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga. Kwa upande wa ufungaji mabao, Amis Tambwe ndiye anayeongoza hadi duru la kwanza linapomalizika baada ya kupachika mabao 13 huku Hamisi Kiiza wa Simba akifuatia kwa mabao 10.

DURU la pili la Ligi Kuu Tanzania Bara linaanza leo wakati timu 12 zikiwemo za Yanga na Simba kushuka kwenye viwanja tofauti kusaka pointi tatu muhimu. Hata hivyo, Azam FC inayoshika nafasi ya pili katika msimamo wa ligi hiyo, leo ilitakiwa kucheza na Prisons ya Mbeya, haitashuka dimbani kwa sababu inashiriki mashindano ya timu nne nchini Zambia.
Yanga wenyewe wako kileleni wakiwa na pointi 39 sawa na Azam FC, lakini wanaongoza kwa uwiano wa tofauti ya magoli, leo watakuwa wageni wa Coastal Union katika mchezo utakaofanyika kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga.
Katika mchezo wa raundi ya awali, Yanga iliibuka na ushindi wa mabao 2-0 katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Yanga watataka kudhihirisha kuwa hawakubahatisha kuifunga Coastal katika mchezo wa kwanza, huku Wagosi hao wa Kaya nao watataka kudhihirisha wao sio wanyonge mbele ya mabingwa hao watetezi.
Vijana hao wa Jangwani wakishinda leo watakuwa wamejikusanyia pointi 42 na kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo na kuiacha Azam FC ikibaki na pointi zake 39 katika nafasi ya pili.
Kwa upande wa Simba, wenyewe katika mchezo wa kwanza dhidi ya African Sports uliochezwa Mkwakwani, iliibuka na ushindi kiduchi wa bao 1-0, hivyo na leo itataka kuendeleza ubabe dhidi ya vijana hao wa Tanga.
Simba yenye pointi 33, inazihitaji sana pointi tatu kutoka kwa African Sports ili angalau izidi kujisogeza katika nafasi ya tatu nyuma ya Azam katika mbio hizo za ubingwa wa ligi hiyo.
Kwa sasa Simba inafundishwa na Mganda Jackson Mayanja aliyechukua nafasi ya Muingereza Dylan Kerr aliyetimuliwa licha ya timu hiyo kuwa katika nafasi ya tatu ya msimamo wa ligi hiyo.
Mayanja alisema pamoja na ugumu wa mchezo huo, watajitahidi kuibuka na ushindi ili kuendelea kuzifukuza Yanga na Azam FC zilizoko kileleni. Coastal Union na African Sports ziko katika nafasi ya 14 na 15 baada ya kucheza mechi 15 na kuambulia pointi tisa na 10 badala ya kuwa na pointi 45 kutoka katika mechi hizo 15 za duru la kwanza.
Mechi zingine leo ni JKT Ruvu watakuwa wenyeji wa Majina ya Songea, huku Mtibwa Sugar wakiikaribisha Stand United, wakati Mwadui FC itaikaribisha Toto African wakati Kagera Sugar watacheza na Mbeya City na Mgambo JKT watakuwa wenyeji wa Ndanda FC.
Ligi hiyo itaendelea tena kesho kwa Mgambo kuikaribisha Ndanda FC kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga. Kwa upande wa ufungaji mabao, Amis Tambwe ndiye anayeongoza hadi duru la kwanza linapomalizika baada ya kupachika mabao 13 huku Hamisi Kiiza wa Simba akifuatia kwa mabao 10.

WIZARA ya Elimu, Sayansi Teknolojia na Ufundi imeeleza baadhi ya vigezo vitakavyotumika kupanga ada elekezi katika shule binafsi, kuwa ni pamoja na aina ya huduma zinazotolewa kwa wanafunzi, mishahara ya walimu.
Akizungumza jana bungeni wakati akijibu maswali ya wabunge waliojadili Hotuba ya Rais John Magufuli aliyotoa wakati kuzindua Bunge, Waziri wa Elimu, Sayansi Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako alisema kutokana na vigezo hivyo, ada elekezi hizo haziwezi kufanana.
Profesa Ndalichako aliwaambia wabunge kwamba tayari wanaye mtaalamu mshauri anayefanya kazi hiyo, ambaye baada ya kukamilisha kazi, watakubaliana kwa ajili ya kutoa ada elekezi zitakazotofautiana kulingana na viwango vya shule.
Kwa mujibu wa Profesa Ndalichako, mambo mengine yanayoangaliwa katika huduma zinazotolewa shuleni ni pamoja na chakula, aina ya miundombinu, viburudisho na mishahara ya walimu. Profesa Ndalichako aliwahakikishia wabunge kwamba wizara inafanyia kazi suala hilo.
Alisema suala hilo linahitaji kufanyiwa kazi kwa kina, kwa kuangalia vizuri makundi ya shule. “Unaweza kukuta huduma ambazo zinapatikana shuleni zinatofautiana sana. Kuna shule nyingine mpaka zina swimming pool (maeneo ya kuogelea), zimejengwa kwa terazo na nyingine zimejengwa kwa marumaru.
Sasa unapotoa ada elekezi lazima uzingatie kwamba mwanafunzi anasoma katika aina gani ya shule. “Zipo shule nyingine za binafsi ambazo hazina hata sakafu, kwa hiyo huwezi kuja na ada elekezi, ukasema tu kwamba ni shilingi kadhaa, lazima mambo haya yote uyaangalie.
“Hata chakula wanachokula wanafunzi kinatofautiana, baadhi ya shule wanapewa mpaka soseji, wanakula pilau na wengine wanakula ugali na maharage kila siku,” alisema. Profesa Ndalichako alisisitiza kwamba haiwezekani kuja na ada elekezi zinazofanana, kwa hiyo wizara yake lazima iangalie jambo hilo kwa umakini mkubwa.
“Kuna baadhi ya shule zinawaonea sana walimu, zinawalipa kidogo na nyingine zinawalipa vizuri. Nawaomba Watanzania tuwe na subira, wizara yangu inalifanyia kazi, lakini si jambo linalohitaji kufanyiwa kazi kwa haraka, tutakapokuwa tayari tutakuja kuwapa majibu,” alisema.

WIZARA ya Elimu, Sayansi Teknolojia na Ufundi imeeleza baadhi ya vigezo vitakavyotumika kupanga ada elekezi katika shule binafsi, kuwa ni pamoja na aina ya huduma zinazotolewa kwa wanafunzi, mishahara ya walimu.
Akizungumza jana bungeni wakati akijibu maswali ya wabunge waliojadili Hotuba ya Rais John Magufuli aliyotoa wakati kuzindua Bunge, Waziri wa Elimu, Sayansi Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako alisema kutokana na vigezo hivyo, ada elekezi hizo haziwezi kufanana.
Profesa Ndalichako aliwaambia wabunge kwamba tayari wanaye mtaalamu mshauri anayefanya kazi hiyo, ambaye baada ya kukamilisha kazi, watakubaliana kwa ajili ya kutoa ada elekezi zitakazotofautiana kulingana na viwango vya shule.
Kwa mujibu wa Profesa Ndalichako, mambo mengine yanayoangaliwa katika huduma zinazotolewa shuleni ni pamoja na chakula, aina ya miundombinu, viburudisho na mishahara ya walimu. Profesa Ndalichako aliwahakikishia wabunge kwamba wizara inafanyia kazi suala hilo.
Alisema suala hilo linahitaji kufanyiwa kazi kwa kina, kwa kuangalia vizuri makundi ya shule. “Unaweza kukuta huduma ambazo zinapatikana shuleni zinatofautiana sana. Kuna shule nyingine mpaka zina swimming pool (maeneo ya kuogelea), zimejengwa kwa terazo na nyingine zimejengwa kwa marumaru.
Sasa unapotoa ada elekezi lazima uzingatie kwamba mwanafunzi anasoma katika aina gani ya shule. “Zipo shule nyingine za binafsi ambazo hazina hata sakafu, kwa hiyo huwezi kuja na ada elekezi, ukasema tu kwamba ni shilingi kadhaa, lazima mambo haya yote uyaangalie.
“Hata chakula wanachokula wanafunzi kinatofautiana, baadhi ya shule wanapewa mpaka soseji, wanakula pilau na wengine wanakula ugali na maharage kila siku,” alisema. Profesa Ndalichako alisisitiza kwamba haiwezekani kuja na ada elekezi zinazofanana, kwa hiyo wizara yake lazima iangalie jambo hilo kwa umakini mkubwa.
“Kuna baadhi ya shule zinawaonea sana walimu, zinawalipa kidogo na nyingine zinawalipa vizuri. Nawaomba Watanzania tuwe na subira, wizara yangu inalifanyia kazi, lakini si jambo linalohitaji kufanyiwa kazi kwa haraka, tutakapokuwa tayari tutakuja kuwapa majibu,” alisema.

Saturday, 2 January 2016

http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/12/Samatta-JPN-5.jpgNeema imezidi kuwashukia wachezaji wa kimataifa wa Tanzania wanaokipiga kwenye klabu ya TP Mazembe ya Congo DR. Baada ya Mbwana Samatta kupata timu ya barani Ulaya hatimaye pacha wake Thomas Ulimwengu ‘Drogba wa Dodoma’ naye huenda akaungana na Samatta kwenda kuchea soka la kulipwa barani Ulaya.
Klabu ya TP mazembe imethibitisha kupokea offer rasmi kutoka timu ya AS Saint-Étienne inayoshiriki ligi kuu ya nchini Ufaransa maarufu kama Ligue 1.
TP Mazembe iko tayari kumwachia Ulimwengu kwenda kukipiga nchini Ufaransa kutokana na kuondoka kwa ‘pacha wake’ Mbwana Samatta ambaye yeye (Samatta) anaelekea nchini Ubelgiji kujiunga na klabu ya Genk ambayo inashiriki ligi kuu nchini humo inayofahamika kwa jina la Belgian Pro League.
Uongozi wa Mazembe umesema hauna tatizo juu ya suala hilo na uko tayari kumwachia Ulimwengu aondoke kwasababu hatakuwa katika wakati mzuri hasa kutokana na upweke unaotokana na kuondoka kwa Mbwana Samatta kwenye klabu hiyo.
Samatta na Ulimwengu wamekuwa karibu sana ndani na nje ya uwanja kwa muda wote ambao wamekuwa wakiitumikia klabu ya Mazembe, kuondoka kwa Samatta kwenye kikosi cha Mazembe huenda kukamfanya Ulimwengu awe mpweke (bored), ili hali hiyo isimkute Ulimwengu Mazembe wanaona ni vyema kumruhusu aondoke kwenda kwenye klabu mpya ambapo atakutana na changamoto mpya.
AS Saint-Étienne ipo nafasi ya sita kwenye msimamo wa Ligue 1 ikiwa imecheza mechi 19 na kukusanya pointi 29 hadi sasa. Imeshinda mechi tisa, imetoka sare michezo miwili na kupoteza mechi nane.
Hizo ni habari nzuri kwa Thomas Ulimwengu na kwa watanzania wote kwa ujumla, kufanikiwa kwa nyota hao kwenda kucheza soka barani Ulaya kutafungua fursa kwa wacheaji wengine wa kitanzania kwenda Ulaya lakini kutaisaidia timu ya taifa ya Tanzania kutokana na uzoefu watakaoupata kwenye timu zao za Ulaya ambapo tunaamini wao wamepiga hatua kwenye soka.

http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/12/Samatta-JPN-5.jpgNeema imezidi kuwashukia wachezaji wa kimataifa wa Tanzania wanaokipiga kwenye klabu ya TP Mazembe ya Congo DR. Baada ya Mbwana Samatta kupata timu ya barani Ulaya hatimaye pacha wake Thomas Ulimwengu ‘Drogba wa Dodoma’ naye huenda akaungana na Samatta kwenda kuchea soka la kulipwa barani Ulaya.
Klabu ya TP mazembe imethibitisha kupokea offer rasmi kutoka timu ya AS Saint-Étienne inayoshiriki ligi kuu ya nchini Ufaransa maarufu kama Ligue 1.
TP Mazembe iko tayari kumwachia Ulimwengu kwenda kukipiga nchini Ufaransa kutokana na kuondoka kwa ‘pacha wake’ Mbwana Samatta ambaye yeye (Samatta) anaelekea nchini Ubelgiji kujiunga na klabu ya Genk ambayo inashiriki ligi kuu nchini humo inayofahamika kwa jina la Belgian Pro League.
Uongozi wa Mazembe umesema hauna tatizo juu ya suala hilo na uko tayari kumwachia Ulimwengu aondoke kwasababu hatakuwa katika wakati mzuri hasa kutokana na upweke unaotokana na kuondoka kwa Mbwana Samatta kwenye klabu hiyo.
Samatta na Ulimwengu wamekuwa karibu sana ndani na nje ya uwanja kwa muda wote ambao wamekuwa wakiitumikia klabu ya Mazembe, kuondoka kwa Samatta kwenye kikosi cha Mazembe huenda kukamfanya Ulimwengu awe mpweke (bored), ili hali hiyo isimkute Ulimwengu Mazembe wanaona ni vyema kumruhusu aondoke kwenda kwenye klabu mpya ambapo atakutana na changamoto mpya.
AS Saint-Étienne ipo nafasi ya sita kwenye msimamo wa Ligue 1 ikiwa imecheza mechi 19 na kukusanya pointi 29 hadi sasa. Imeshinda mechi tisa, imetoka sare michezo miwili na kupoteza mechi nane.
Hizo ni habari nzuri kwa Thomas Ulimwengu na kwa watanzania wote kwa ujumla, kufanikiwa kwa nyota hao kwenda kucheza soka barani Ulaya kutafungua fursa kwa wacheaji wengine wa kitanzania kwenda Ulaya lakini kutaisaidia timu ya taifa ya Tanzania kutokana na uzoefu watakaoupata kwenye timu zao za Ulaya ambapo tunaamini wao wamepiga hatua kwenye soka.

Pazia la Mapinduzi Cup linafunguliwa rasmi leo mchana kwa michezo miwili, mchezo wa kwanza utaanza majira ya mchana kati ya mabingwa wa ligi kuu Tanzania bara Yanga SC dhidi ya Mafunzo ya Zanzibar.
Mchezo wa pili utachezwa saa 2:15 usiku kati ya Azam FC dhidi ya Mtibwa Sugar michezo yote itafanyika kwenye uwanja wa Amaan visiwani Zanzibar.
Kundi hili linajumuisha timu tatu kutoka Tanzania bara ambazo zote zinashiriki ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara na zinafanya vizuri kwenye ligi hiyo, timu hizo ni Azam FC, Yanga SC na Mtibwa Suga huku Mafunzo ya Zanzibar ikikamilisha idadi ya timu nne za kundi hilo.
Azam ndiyo vinara wa ligi kuu Tanzania bara wakiwa na pointi 35 wakifuatiwa na Yanga wenye pointi 33 katika nafasi ya pili wakati Mtibwa Sugar wao wakiwa nafasi ya nne kwa pointi zao 27 sawa na Simba lakini wekundu wa Msimbazi wakikaa nafasi ya tatu kwa tofauti ya magoli ya kufunga na kufungwa.
Mchezo unaopewa uzito wa juu ni mchezo wa usiku kati ya Azam FC vs Mtibwa Sugar kwasababu timu hizo zimekutana Jumatano iliyopita kwenye mchezo wa ligi uliopigwa kwenye uwanja wa Azam Complex na kuishuhudia Azam FC ikipata ushindi wa goli 1-0 kwa mbinde mbele ya Mtibwa mchezo uliokuwa mkali na wa kuvutia.
Msimu uliopita Mtibwa ilicheza fainali ya michuano hiyo dhidi ya Simba na kupoteza mchezo huo kwa mikwaju ya penati na Simba ikafanikiwa kutwaa taji hilo kwa mara nyingine tena.

Pazia la Mapinduzi Cup linafunguliwa rasmi leo mchana kwa michezo miwili, mchezo wa kwanza utaanza majira ya mchana kati ya mabingwa wa ligi kuu Tanzania bara Yanga SC dhidi ya Mafunzo ya Zanzibar.
Mchezo wa pili utachezwa saa 2:15 usiku kati ya Azam FC dhidi ya Mtibwa Sugar michezo yote itafanyika kwenye uwanja wa Amaan visiwani Zanzibar.
Kundi hili linajumuisha timu tatu kutoka Tanzania bara ambazo zote zinashiriki ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara na zinafanya vizuri kwenye ligi hiyo, timu hizo ni Azam FC, Yanga SC na Mtibwa Suga huku Mafunzo ya Zanzibar ikikamilisha idadi ya timu nne za kundi hilo.
Azam ndiyo vinara wa ligi kuu Tanzania bara wakiwa na pointi 35 wakifuatiwa na Yanga wenye pointi 33 katika nafasi ya pili wakati Mtibwa Sugar wao wakiwa nafasi ya nne kwa pointi zao 27 sawa na Simba lakini wekundu wa Msimbazi wakikaa nafasi ya tatu kwa tofauti ya magoli ya kufunga na kufungwa.
Mchezo unaopewa uzito wa juu ni mchezo wa usiku kati ya Azam FC vs Mtibwa Sugar kwasababu timu hizo zimekutana Jumatano iliyopita kwenye mchezo wa ligi uliopigwa kwenye uwanja wa Azam Complex na kuishuhudia Azam FC ikipata ushindi wa goli 1-0 kwa mbinde mbele ya Mtibwa mchezo uliokuwa mkali na wa kuvutia.
Msimu uliopita Mtibwa ilicheza fainali ya michuano hiyo dhidi ya Simba na kupoteza mchezo huo kwa mikwaju ya penati na Simba ikafanikiwa kutwaa taji hilo kwa mara nyingine tena.