Pazia la Mapinduzi Cup linafunguliwa rasmi leo mchana kwa michezo
miwili, mchezo wa kwanza utaanza majira ya mchana kati ya mabingwa wa
ligi kuu Tanzania bara Yanga SC dhidi ya Mafunzo ya Zanzibar.
Mchezo wa pili utachezwa saa 2:15 usiku kati ya Azam FC dhidi ya
Mtibwa Sugar michezo yote itafanyika kwenye uwanja wa Amaan visiwani
Zanzibar.
Kundi hili linajumuisha timu tatu kutoka Tanzania bara ambazo zote
zinashiriki ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara na zinafanya vizuri kwenye
ligi hiyo, timu hizo ni Azam FC, Yanga SC na Mtibwa Suga huku Mafunzo
ya Zanzibar ikikamilisha idadi ya timu nne za kundi hilo.
Azam ndiyo vinara wa ligi kuu Tanzania bara wakiwa na pointi 35
wakifuatiwa na Yanga wenye pointi 33 katika nafasi ya pili wakati Mtibwa
Sugar wao wakiwa nafasi ya nne kwa pointi zao 27 sawa na Simba lakini
wekundu wa Msimbazi wakikaa nafasi ya tatu kwa tofauti ya magoli ya
kufunga na kufungwa.
Mchezo unaopewa uzito wa juu ni mchezo wa usiku kati ya Azam FC vs
Mtibwa Sugar kwasababu timu hizo zimekutana Jumatano iliyopita kwenye
mchezo wa ligi uliopigwa kwenye uwanja wa Azam Complex na kuishuhudia
Azam FC ikipata ushindi wa goli 1-0 kwa mbinde mbele ya Mtibwa mchezo
uliokuwa mkali na wa kuvutia.
Msimu uliopita Mtibwa ilicheza fainali ya michuano hiyo dhidi ya
Simba na kupoteza mchezo huo kwa mikwaju ya penati na Simba ikafanikiwa
kutwaa taji hilo kwa mara nyingine tena.
Saturday, 2 January 2016
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment