Ama kweli Mbeya City msimu huu imepania, kwani imetangaza kula sahani moja na Yanga katika maandalizi yao ya Ligi Kuu Tanzania Bara. Unajua ikoje? Uongozi wa timu hiyo umesema unajua Yanga na Azam zimejifua vilivyo kupitia Kagame, lakini hiyo haiwapi shida kwani nao watatumia wiki zilizosalia kufanya yao mapema ili wafunike katika ligi.
Uongozi huo umesema moja ya mikakati yao ni
kucheza mechi kadhaa za kimataifa na klabu toka nje ya nchi za Zesco ya
Zambia na Bata Bullets ya Malawi ambazo zitacheza pia na Yanga hivi
karibuni jijini Mbeya.
Kabla ya kucheza mechi hizo za kirafiki za
kimataifa, Mbeya City itaanza na Yanga, Agosti 18, jijini Mbeya ambako
Wanajangwani wataweka kambi kwa ajili ya kujiandaa na mechi ya Ngao ya
Jamii dhidi ya Azam.
Katibu Mkuu wa timu hiyo, Emmanuel Kimbe alisema
wapo kwenye mazungumzo na timu hizo ambazo pia zitacheza mechi za
kirafiki na Yanga na kwamba wana asilimia kubwa ya kufanikisha mpango
huo.
“Tunajua changamoto ambazo tutakabiliana nazo kwa
Yanga na Azam, katika ligi maana hizo zimepata muda wa kujipima uwezo
kwenye Kagame ndio maana tunataka kujifua kupitia timu zenye uwezo,”
alisema.
Kimbe alisema pia katika mechi hizo zitawasaidia
kujua uwezo wa wachezaji wao na kutambua kombeneshani, hivyo wanajifanya
mazoezi kuhakikisha kile wanachokitarajia kinatimia.
0 comments:
Post a Comment