.

.

Wednesday, 3 June 2015

Zurich, Uswisi. Rais wa Shirikisho la Soka Duniani (Fifa), Sepp Blatter ametangaza kuwa atajiuzulu nafasi yake hiyo kutokana na kashfa ya rushwa iliyolikumba shirikisho hilo.
Akitangaza uamuzi huo, Blatter (79) alisema baada ya kuitisha mkutano wa dharula wa Fifa: ”Muda mfupi ujao kunatakiwa kuchaguliwe rais mpya.”
Blatter alichaguliwa wiki iliyopita kuliongoza shirikisho hilo, licha ya wajumbe saba wa juu wa Fifa kukamatwa na maafisa usalama wa Marekani siku mbili kabla ya uchaguzi huo.
Blatter alisema: “Uamuzi huu hauungwi mkono na kila mtu.”
Awali Fifa ilikanusha madai kwamba katibu wao mkuu, Jerome Valcke alihusika katika kashfa ya ufisadi ambapo hongo ya mamilioni ya dola ilitolewa.
Fifa inasema hamna afisa wake yeyote wa ngazi ya juu aliyehusika kwa njia yoyote katika kashfa hiyo.
Inasemekana malipo hayo ya rushwa yalitolewa na serikali ya Afrika Kusini kwa maafisa wa soka wa huko Marekani ili waunge mkono

Awali Fifa ilikanusha madai kwamba katibu wao mkuu, Jerome Valcke alihusika katika kashfa ya ufisadi ambapo hongo ya mamilioni ya dola ilitolewa.
Fifa inasema hamna afisa wake yeyote wa ngazi ya juu aliyehusika kwa njia yoyote katika kashfa hiyo.
Inasemekana malipo hayo ya rushwa yalitolewa na serikali ya Afrika Kusini kwa maafisa wa soka wa huko Marekani ili waunge mkono wenzao Waafrika waliong’ambo katika nchi za visiwa vya Caribbean.
Waendesha mashtaka wa Marekani wanasema hongo hiyo ilinuiwa kusaidia kununua kura kuiwezesha Afrika Kusini kuwa mwenyeji wa Kombe la Dunia lililofanyika mwaka 2010.

0 comments:

Post a Comment