.

.

Wednesday, 9 December 2015

Rais Dk John Magufuli.RAIS John Magufuli amegeuka gumzo kimataifa, kutokana na kasi ya mabadiliko ya kweli ya uongozi wake katika kipindi kifupi, hasa kudhibiti matumizi na kueleza fedha katika huduma za jamii.
Aidha, uongozi wake umeelezwa kuwa wa mfano, kwani miongoni mwa mambo anayoyafanya, yanagusa ulimwengu na anatekeleza yote bila kufanya safari yoyote ya nje ya nchi kama wanavyofanya viongozi wengine.
Tangu aingie madakarani mwezi mmoja na siku chache zilizopita, Dk Magufuli amedhibiti mabilioni ya fedha na kuwezesha fedha hizo kuboresha huduma za afya, ikiwamo kuongeza upatikanaji wa dawa za kupunguza makali ya Ukimwi (ARV’s), shule na miundombinu ya barabara.
Gazeti la The Sunday Independent linalochapishwa na chombo cha habari chenye nguvu nchini Afrika Kusini, liliandika katika tahariri yake hivi karibuni katika kichwa cha habari kisemacho, “Afrika ifuate mfano wa Tanzania.” Tahariri hiyo iliyochapishwa Jumapili iliyopita, ilisisitiza kuwa utekelezaji wa maazimio ya Mkutano wa Sita wa Mawaziri wa Baraza la Ushirikiano kati ya Afrika na China (FOCAC), unahitaji Rais kama Magufuli ambaye ameonesha kwa dhati nidhamu katika matumizi ya serikali.
Gazeti hilo limekuwa miongoni mwa vyombo vya habari vinavyosifu utendaji wa Dk Magufuli, ambaye anafanya kazi bila Baraza la Mawaziri kwa zaidi ya siku 30 tangu aapishwe. Baadhi ya waandishi wa habari kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika, walilieleza gazeti dada la gazeti hili, Daily News katika siku za mwisho wa mkutano wa FOCAC kwamba wameguswa kwa utendaji wa Dk Magufuli na kuwataka viongozi wengine wa Afrika kuiga.
Mwandishi wa gazeti la Daily Graphic la Ghana, Emmanuel Adu- Gyamerah alisema kazi anayofanya Dk Magufuli, ikiwamo kubadili sherehe za Uhuru ambazo mataifa mengi huzifanya kwa gharama kubwa, ni jambo ambalo viongozi wengi wa Afrika wameshindwa, lakini yeye amefanya kwa muda mfupi tangu aingie madarakani. “Hii hatua ya kupunguza matumizi inapaswa kufanywa na Waghana pia,” alisema Adu-Gyamerah.
Dk Magufuli alibadili namna ya kusherehekea sikukuu ya Uhuru na kuagiza Watanzania wote wafanye usafi katika maeneo yao ya kazi na makazi ili kupambana na magonjwa ya mlipuko, ikiwamo kipindupindu na kutunza mazingira. Baadhi ya wananchi wa Rwanda, walieleza kuwa hatua aliyochukua Dk Magufuli kuhusu sherehe za uhuru ni “ya Kinyarwanda” kwa kuwa kwao serikali ilifanya Jumamosi ya kwanza ya kila mwezi kuwa siku rasmi ya usafi nchi nzima.
Mtangazaji wa Televisheni ya China (CCTV) wa Kenya, alisema kufuta safari za nje ni moja ya hatua muhimu na alisema Wakenya wamekuwa wakizungumzia safari za Rais wao, Uhuru Kenyatta anazofaa nje ya nchi.
“Natamani hatua kama hizi zifanyike pia nchini mwangu,” alisema mtangazaji huyo huku akiionesha Daily News ujumbe wa twita unaoonesha sifa kemkem kwa Dk Magufuli. Gazeti la Sunday’s Paper of New Zimbabwe liliandika hivi, “Tanzania’s Magufuli: A new African” (Magufuli wa Tanzania: Mwafrika Mpya”, ikieleza kuwa Dk Magufuli ameleta mapinduzi na njia mpya katika kutawala.
Gazeti hilo lilieleza kuwa, uongozi wa Dk Magufuli umelenga kushughulika na wavivu na wala rushwa na kuandika, “Mpaka sasa mambo ni mazuri; hongera Magufuli.” Gazeti la mtandaoni la Nigeria, naij.com, lilieleza kuwa hatua ya kupunguza matumizi ni ya kuchukuliwa na serikali ya Nigeria vile vile. Naij.com ilimnukuu mhariri wake, Abang Mercy akitwiti hivi karibuni na kuandika ujumbe huu, “Tangu achaguliwe, Rais wa Tanzania, John Magufuli ametekeleza mabadiliko makubwa; na ndivyo ninavyotarajia kwa Rais Buhari (Rais wa Nigeria).”
Gazeti hilo la mtandaoni lilimfananisha Dk Magufuli na Baba wa Taifa wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere, mwasisi na mtu asiyekwepeka katika historia ya Tanzania. Gazeti la Daily Nation la Kenya limeripoti kuwa hatua ya Dk Magufuli kuzuia safari za nje, inapaswa kuchukuliwa pia nchini humo, hasa kutokana na wananchi kuonesha kutokupendezwa na safari za Rais Kenyatta nje ya nchi.
Aidha, suala la kupunguza matumizi kwa kuzuia kuchapisha kadi za sikukuu za Krismasi na Mwaka Mpya kwa taasisi na mashirika ya umma, limepongezwa pia na kumtaka Kenyatta kuiga mfano huo.

Rais Dk John Magufuli.RAIS John Magufuli amegeuka gumzo kimataifa, kutokana na kasi ya mabadiliko ya kweli ya uongozi wake katika kipindi kifupi, hasa kudhibiti matumizi na kueleza fedha katika huduma za jamii.
Aidha, uongozi wake umeelezwa kuwa wa mfano, kwani miongoni mwa mambo anayoyafanya, yanagusa ulimwengu na anatekeleza yote bila kufanya safari yoyote ya nje ya nchi kama wanavyofanya viongozi wengine.
Tangu aingie madakarani mwezi mmoja na siku chache zilizopita, Dk Magufuli amedhibiti mabilioni ya fedha na kuwezesha fedha hizo kuboresha huduma za afya, ikiwamo kuongeza upatikanaji wa dawa za kupunguza makali ya Ukimwi (ARV’s), shule na miundombinu ya barabara.
Gazeti la The Sunday Independent linalochapishwa na chombo cha habari chenye nguvu nchini Afrika Kusini, liliandika katika tahariri yake hivi karibuni katika kichwa cha habari kisemacho, “Afrika ifuate mfano wa Tanzania.” Tahariri hiyo iliyochapishwa Jumapili iliyopita, ilisisitiza kuwa utekelezaji wa maazimio ya Mkutano wa Sita wa Mawaziri wa Baraza la Ushirikiano kati ya Afrika na China (FOCAC), unahitaji Rais kama Magufuli ambaye ameonesha kwa dhati nidhamu katika matumizi ya serikali.
Gazeti hilo limekuwa miongoni mwa vyombo vya habari vinavyosifu utendaji wa Dk Magufuli, ambaye anafanya kazi bila Baraza la Mawaziri kwa zaidi ya siku 30 tangu aapishwe. Baadhi ya waandishi wa habari kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika, walilieleza gazeti dada la gazeti hili, Daily News katika siku za mwisho wa mkutano wa FOCAC kwamba wameguswa kwa utendaji wa Dk Magufuli na kuwataka viongozi wengine wa Afrika kuiga.
Mwandishi wa gazeti la Daily Graphic la Ghana, Emmanuel Adu- Gyamerah alisema kazi anayofanya Dk Magufuli, ikiwamo kubadili sherehe za Uhuru ambazo mataifa mengi huzifanya kwa gharama kubwa, ni jambo ambalo viongozi wengi wa Afrika wameshindwa, lakini yeye amefanya kwa muda mfupi tangu aingie madarakani. “Hii hatua ya kupunguza matumizi inapaswa kufanywa na Waghana pia,” alisema Adu-Gyamerah.
Dk Magufuli alibadili namna ya kusherehekea sikukuu ya Uhuru na kuagiza Watanzania wote wafanye usafi katika maeneo yao ya kazi na makazi ili kupambana na magonjwa ya mlipuko, ikiwamo kipindupindu na kutunza mazingira. Baadhi ya wananchi wa Rwanda, walieleza kuwa hatua aliyochukua Dk Magufuli kuhusu sherehe za uhuru ni “ya Kinyarwanda” kwa kuwa kwao serikali ilifanya Jumamosi ya kwanza ya kila mwezi kuwa siku rasmi ya usafi nchi nzima.
Mtangazaji wa Televisheni ya China (CCTV) wa Kenya, alisema kufuta safari za nje ni moja ya hatua muhimu na alisema Wakenya wamekuwa wakizungumzia safari za Rais wao, Uhuru Kenyatta anazofaa nje ya nchi.
“Natamani hatua kama hizi zifanyike pia nchini mwangu,” alisema mtangazaji huyo huku akiionesha Daily News ujumbe wa twita unaoonesha sifa kemkem kwa Dk Magufuli. Gazeti la Sunday’s Paper of New Zimbabwe liliandika hivi, “Tanzania’s Magufuli: A new African” (Magufuli wa Tanzania: Mwafrika Mpya”, ikieleza kuwa Dk Magufuli ameleta mapinduzi na njia mpya katika kutawala.
Gazeti hilo lilieleza kuwa, uongozi wa Dk Magufuli umelenga kushughulika na wavivu na wala rushwa na kuandika, “Mpaka sasa mambo ni mazuri; hongera Magufuli.” Gazeti la mtandaoni la Nigeria, naij.com, lilieleza kuwa hatua ya kupunguza matumizi ni ya kuchukuliwa na serikali ya Nigeria vile vile. Naij.com ilimnukuu mhariri wake, Abang Mercy akitwiti hivi karibuni na kuandika ujumbe huu, “Tangu achaguliwe, Rais wa Tanzania, John Magufuli ametekeleza mabadiliko makubwa; na ndivyo ninavyotarajia kwa Rais Buhari (Rais wa Nigeria).”
Gazeti hilo la mtandaoni lilimfananisha Dk Magufuli na Baba wa Taifa wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere, mwasisi na mtu asiyekwepeka katika historia ya Tanzania. Gazeti la Daily Nation la Kenya limeripoti kuwa hatua ya Dk Magufuli kuzuia safari za nje, inapaswa kuchukuliwa pia nchini humo, hasa kutokana na wananchi kuonesha kutokupendezwa na safari za Rais Kenyatta nje ya nchi.
Aidha, suala la kupunguza matumizi kwa kuzuia kuchapisha kadi za sikukuu za Krismasi na Mwaka Mpya kwa taasisi na mashirika ya umma, limepongezwa pia na kumtaka Kenyatta kuiga mfano huo.

Rais Magufuli akizoa takataka baada ya kumaliza kufanya usafi karibu na lango kuu la kuingilia Ikulu jijini Dar es Salaam.
Kama umefurahishwa na kitendo hiki, tupia neno lolote kumpongeza.

Rais Magufuli akizoa takataka baada ya kumaliza kufanya usafi karibu na lango kuu la kuingilia Ikulu jijini Dar es Salaam.
Kama umefurahishwa na kitendo hiki, tupia neno lolote kumpongeza.

Sunday, 6 December 2015

KOCHA wa Simba Dylan Kerr, amesema amefurahishwa na usajili wa mshambuliaji wa kimataifa wa Kenya, Paul Kiongera.
Kiongera ni mmoja wa wachezaji walioongezwa kwenye dirisha dogo la usajili na Simba baada ya timu hiyo kuonesha upungufu katika baadhi ya nafasi kwenye mechi tisa za mzunguko wa kwanza.
Akizungumza na gazeti hili, Kerr alisema anamhitaji mshambuliaji huyo ili aweze kumwelekeza namna na kucheza kwa kushirikiana na Hamisi Kiiza kwenye ushambuliaji. “Nimefurahi sana kwamba tayari amejiunga na sisi na sasa ni jukumu langu kuwaunganisha na wenzake,” alisema Kerr.
Alisema ujio wa mchezaji huyo ni fursa nzuri katika maandalizi kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Azam FC Jumamosi.
Alisema amekuwa akiweka mkazo mkubwa kwenye safu ya ushambuliaji kwa sababu kwake hiyo ndiyo sehemu muhimu ambayo inaweza kuwapa ubingwa msimu huu kama watafunga idadi kubwa ya mabao.
Alisema kuongezeka kwa Kiongera na Brian Majwega, ana uhakika atakuwa amemaliza tatizo la mabao lililojitokeza katika mechi za awali za ligi hiyo. Kocha huyo alisisitiza kuwa ujio wa wachezaji hao utabadilisha kikosi chake katika ushambuliaji na kuwa na safu inayotisha katika kufunga.
Kiongera alirudishwa KCB na Simba baada ya kupata majeraha makubwa ya goti msimu uliopita na timu hiyo kumpeleka India kwa ajili ya matibabu na baada ya hapo ilimruhusu acheze kwa mkopo kwa makubaliano ya kumrudisha atakapopona.K

KOCHA wa Simba Dylan Kerr, amesema amefurahishwa na usajili wa mshambuliaji wa kimataifa wa Kenya, Paul Kiongera.
Kiongera ni mmoja wa wachezaji walioongezwa kwenye dirisha dogo la usajili na Simba baada ya timu hiyo kuonesha upungufu katika baadhi ya nafasi kwenye mechi tisa za mzunguko wa kwanza.
Akizungumza na gazeti hili, Kerr alisema anamhitaji mshambuliaji huyo ili aweze kumwelekeza namna na kucheza kwa kushirikiana na Hamisi Kiiza kwenye ushambuliaji. “Nimefurahi sana kwamba tayari amejiunga na sisi na sasa ni jukumu langu kuwaunganisha na wenzake,” alisema Kerr.
Alisema ujio wa mchezaji huyo ni fursa nzuri katika maandalizi kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Azam FC Jumamosi.
Alisema amekuwa akiweka mkazo mkubwa kwenye safu ya ushambuliaji kwa sababu kwake hiyo ndiyo sehemu muhimu ambayo inaweza kuwapa ubingwa msimu huu kama watafunga idadi kubwa ya mabao.
Alisema kuongezeka kwa Kiongera na Brian Majwega, ana uhakika atakuwa amemaliza tatizo la mabao lililojitokeza katika mechi za awali za ligi hiyo. Kocha huyo alisisitiza kuwa ujio wa wachezaji hao utabadilisha kikosi chake katika ushambuliaji na kuwa na safu inayotisha katika kufunga.
Kiongera alirudishwa KCB na Simba baada ya kupata majeraha makubwa ya goti msimu uliopita na timu hiyo kumpeleka India kwa ajili ya matibabu na baada ya hapo ilimruhusu acheze kwa mkopo kwa makubaliano ya kumrudisha atakapopona.K

RC amsihi Yussuf Manji akubali kuachia Coco BeachMKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadiki amemuomba mmiliki wa Kampuni ya Q Consult inayomilikiwa na mfanyabiashara Yussuf Manji kutumia busara kukubali kuuachia ufukwe wa Coco jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Sadiki alisema Mahakama Kuu ya Tanzania, Kitengo cha Ardhi katika uamuzi wake imeiamuru Manispaa ya Kinondoni, kutekeleza mkataba wake na kampuni ya Q Consult kwa ajili ya kampuni hiyo kuendeleza ufukwe huo hata hivyo Manispaa ya Kinondoni imekata rufaa.
“Kampuni ya Q Consult kwa busara tu iachane na kesi, ikubali kurudisha ufukwe huo chini ya mamlaka ya Kinondoni ili iweze kuuendeleza ufukwe huo kwa manufaa ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam na sio kwa manufaa ya mtu mmoja kama anavyotaka mtu huyo,” alisema Sadiki.
Alisema wananchi wafahamu kuwa ufukwe huo wa Coco haujauzwa, kama watu wanavyodai na kwamba kesi hiyo iko mahakamani, ambapo Ofisi ya Manispaa ya Kinondoni kupitia Mwanasheria Mkuu wa Serikali wamekata rufaa.
Akielezea sakata hilo, Sadiki alisema kampuni ya Q Consult inayomilikiwa na Manji mwaka 2007 iliingia mkataba na Manispaa ya Kinondoni kuendeleza ufukwe huo.
Alisema, hata hivyo, baadaye Manispaa ya hiyo ilivunja mkataba huo baada ya Kampuni ya Q Consult kushindwa kutimiza masharti, jambo ambalo liliifanya kampuni hiyo kwenda mahakamani.
Mahakama Kuu ya Tanzania Kitengo cha Ardhi iliamuru Manispaa ya Kinondoni, kutekeleza mkataba wake na kampuni hiyo kwa ajili ya kuendeleza ufukwe huo.
“Kama nilivyosema kupitia mwanasheria mkuu wa Serikali tumekata rufaa katika uamuzi huo kwasababu tunaamini haukuwa sahihi, hata hivyo mwekezaji huyo namshauri tu anaweza kufanya maamuzi akaachana na kesi hiyo na kuamua kurudisha ufukwe huo uendelee kutumiwa na Watanzania wote,” alisema Sadiki.
Kwa kampuni hiyo kushinda kesi hiyo, inamaanisha kuwa mwekezaji huyo endapo ataendeleza eneo hilo, wananchi hawatakuwa na fursa hiyo tena, kama wanavyoutumia sasa.
Sadiki alisema tayari serikali imefanya mazungumzo na moja na benki hapa nchini kwa ajili ya kupata mkopo, ambao utasaidia kuendeleza eneo hilo ili liendelee kubaki chini ya Manispaa ya Kinondoni na kutumiwa na watu wote.






















RC amsihi Yussuf Manji akubali kuachia Coco BeachMKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadiki amemuomba mmiliki wa Kampuni ya Q Consult inayomilikiwa na mfanyabiashara Yussuf Manji kutumia busara kukubali kuuachia ufukwe wa Coco jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Sadiki alisema Mahakama Kuu ya Tanzania, Kitengo cha Ardhi katika uamuzi wake imeiamuru Manispaa ya Kinondoni, kutekeleza mkataba wake na kampuni ya Q Consult kwa ajili ya kampuni hiyo kuendeleza ufukwe huo hata hivyo Manispaa ya Kinondoni imekata rufaa.
“Kampuni ya Q Consult kwa busara tu iachane na kesi, ikubali kurudisha ufukwe huo chini ya mamlaka ya Kinondoni ili iweze kuuendeleza ufukwe huo kwa manufaa ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam na sio kwa manufaa ya mtu mmoja kama anavyotaka mtu huyo,” alisema Sadiki.
Alisema wananchi wafahamu kuwa ufukwe huo wa Coco haujauzwa, kama watu wanavyodai na kwamba kesi hiyo iko mahakamani, ambapo Ofisi ya Manispaa ya Kinondoni kupitia Mwanasheria Mkuu wa Serikali wamekata rufaa.
Akielezea sakata hilo, Sadiki alisema kampuni ya Q Consult inayomilikiwa na Manji mwaka 2007 iliingia mkataba na Manispaa ya Kinondoni kuendeleza ufukwe huo.
Alisema, hata hivyo, baadaye Manispaa ya hiyo ilivunja mkataba huo baada ya Kampuni ya Q Consult kushindwa kutimiza masharti, jambo ambalo liliifanya kampuni hiyo kwenda mahakamani.
Mahakama Kuu ya Tanzania Kitengo cha Ardhi iliamuru Manispaa ya Kinondoni, kutekeleza mkataba wake na kampuni hiyo kwa ajili ya kuendeleza ufukwe huo.
“Kama nilivyosema kupitia mwanasheria mkuu wa Serikali tumekata rufaa katika uamuzi huo kwasababu tunaamini haukuwa sahihi, hata hivyo mwekezaji huyo namshauri tu anaweza kufanya maamuzi akaachana na kesi hiyo na kuamua kurudisha ufukwe huo uendelee kutumiwa na Watanzania wote,” alisema Sadiki.
Kwa kampuni hiyo kushinda kesi hiyo, inamaanisha kuwa mwekezaji huyo endapo ataendeleza eneo hilo, wananchi hawatakuwa na fursa hiyo tena, kama wanavyoutumia sasa.
Sadiki alisema tayari serikali imefanya mazungumzo na moja na benki hapa nchini kwa ajili ya kupata mkopo, ambao utasaidia kuendeleza eneo hilo ili liendelee kubaki chini ya Manispaa ya Kinondoni na kutumiwa na watu wote.






















Wednesday, 18 November 2015

Usiku wa November 17 watanzania wengi na wapenzi wa soka walikuwa wakisubiri kuona mchezo wa pili wa marudiano wa kuwania kufuzu Kombe la Dunia 2018 Urusi kati ya timu ya taifa ya Algeria dhidi ya timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars, mchezo ambao ulichezwa Blida Algeria katika uwanja wa Mustapha Tchaker.
Taifa Stars ambayo ilionesha kiwango kizuri katika uwanja wa nyumbani Dar Es Salaam licha ya kulazimishwa sare ya goli 2-2, wameshindwa kutamba katika mchezo wa pili na kukubali kipigo cha goli 7-0, ilichukua dakika 45 za kwanza Taifa Stars  kuanza kuruhusu magoli matatu ya mwanzo, magoli ambayo yalianza kukatisha tamaa wa Tanzania.http://i1.wp.com/millardayo.com/wp-content/uploads/2015/11/Algeria.jpg
Wakati Taifa Stars wanatafakari namna ambavyo watasawazisha magoli Mudathir Yahaya alioneshwa kadi nyekundu dakika ya 41, kipindi cha pili kocha wa Tanzania Boniface Mkwasa alifanya mabadiliko ya kumuingiza Aishi Manula na kumtoa golikipa Aly Mustapha na Farid Mussa nafasi yake ikachuliwa na Salum Telela, mabadiliko ambayo hayakuzaa matunda.
Magoli ya Algeria yalifungwa na Yacine Brahimi dakika ya 1, Faouzi Ghoulam dakika ya 23 na dakika ya 59 akapachika goli jingine kwa mkwaju wa penati, Riyad Mahrez dakika ya 43 na Islam Slimani kafunga kwa mkwaju wa penati dakika ya 49 na 75, Carl Medjani dakika ya 72 . Kwa matokeo hayo Taifa Stars imetolewa kwa jumla ya magoli 9-2 baada ya mchezo wa awali kumalizika kwa sare ya goli 2-2.

Usiku wa November 17 watanzania wengi na wapenzi wa soka walikuwa wakisubiri kuona mchezo wa pili wa marudiano wa kuwania kufuzu Kombe la Dunia 2018 Urusi kati ya timu ya taifa ya Algeria dhidi ya timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars, mchezo ambao ulichezwa Blida Algeria katika uwanja wa Mustapha Tchaker.
Taifa Stars ambayo ilionesha kiwango kizuri katika uwanja wa nyumbani Dar Es Salaam licha ya kulazimishwa sare ya goli 2-2, wameshindwa kutamba katika mchezo wa pili na kukubali kipigo cha goli 7-0, ilichukua dakika 45 za kwanza Taifa Stars  kuanza kuruhusu magoli matatu ya mwanzo, magoli ambayo yalianza kukatisha tamaa wa Tanzania.http://i1.wp.com/millardayo.com/wp-content/uploads/2015/11/Algeria.jpg
Wakati Taifa Stars wanatafakari namna ambavyo watasawazisha magoli Mudathir Yahaya alioneshwa kadi nyekundu dakika ya 41, kipindi cha pili kocha wa Tanzania Boniface Mkwasa alifanya mabadiliko ya kumuingiza Aishi Manula na kumtoa golikipa Aly Mustapha na Farid Mussa nafasi yake ikachuliwa na Salum Telela, mabadiliko ambayo hayakuzaa matunda.
Magoli ya Algeria yalifungwa na Yacine Brahimi dakika ya 1, Faouzi Ghoulam dakika ya 23 na dakika ya 59 akapachika goli jingine kwa mkwaju wa penati, Riyad Mahrez dakika ya 43 na Islam Slimani kafunga kwa mkwaju wa penati dakika ya 49 na 75, Carl Medjani dakika ya 72 . Kwa matokeo hayo Taifa Stars imetolewa kwa jumla ya magoli 9-2 baada ya mchezo wa awali kumalizika kwa sare ya goli 2-2.

Tuesday, 17 November 2015

NAHODHA wa timu ya soka ya taifa, Taifa Stars, Nadir Haroub amesema leo watafia uwanjani mjini Algiers katika mechi ya kuwania kufuzu michuano ya Kombe la Dunia Urusi 2018 watakaporudiana na wenyeji Algeria.
Stars inaingia uwanjani leo ikiwa na kumbukumbu ya kutoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya vigogo hivyo vya Afrika katika mechi ya kwanza iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita.
Katika mechi hiyo, Stars ilikuwa mbele kwa mabao 2-0 mpaka dakika ya 71 ndipo Algeria wakapata mabao ya harakaharaka na kuondoa furaha miongoni mwa watanzania waliofurika uwanjani siku hiyo.
Matokeo hayo yanaifanya Stars ihitaji ushindi katika mechi ya leo au sare ya kuanzia mabao 3-3 ili kujihakikishia kukata tiketi ya kucheza hatua ya makundi ya michuano hiyo, ambayo ni ya mwisho kabla ya kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia.
Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya mtandao jana, Haroub alisema anaamini timu yake inaweza kuibuka na ushindi ugenini leo. “Soka imebadilika sana siku hizi, ile ya miaka ile sio ya leo lolote linaweza kutokea kesho (leo) na tukasonga mbele, mbona hao Algeria tulienda nao sawa tu mechi ya kwanza makosa madogo tu yamefanyika wakasazisha lakini tunao uwezo wa kuwafunga,” alisema.
Mashabiki wa timu ya taifa, Taifa Stars, bado wana taharuki ya matokeo ya sare ya 2-2 dhidi ya Algeria, lakini nahodha wa Stars, Haroub ametamka kishujaa kuwa kazi haijaisha na anaamini timu hiyo itafanya makubwa kutokana na safu kali ya ushambuliaji waliyonayo.
“Mimi naamini kabisa timu yetu ipo vizuri kila sehemu nawaambieni washambuliaji wangu kwamba watatubeba katika mechi hiyo bila shaka yoyote,” alisema. Safu ya ushambuliaji ya Stars inaongozwa na wachezaji Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wanaocheza soka ya kulipwa TP Mazembe ya Congo DR.
Haroub ambaye pia ni nahodha wa mabingwa wa soka Bara, Yanga, alisema Stars itawashangaza wengi leo kama ilivyokuwa kwenye mechi iliyopita. “Mechi iliyopita hakuna aliyetarajia tungepata bao hata moja lakini matokeo yake tulifunga mabao mawili mpaka waarabu (Algeria) wenyewe walichanganyikiwa, hivyo hata huku inawezekana tu kushinda,” alisema.
Awali, kabla ya safari ya Algiers juzi, kocha mkuu wa timu hiyo Charles Mkwasa alisema anatarajia timu yake kupata matokeo mazuri. Mkwasa alikiri kufanya makosa ya kiufundi wakati wa mabadiliko katika mechi hiyo lakini akasema hiyo ni hali ya mpira hutokea mara nyingi.
Katika mechi hiyo ,Mkwasa aliwatoa Mudathir Yahya na Elias Maguli na nafasi zao kuchukuliwa na Said Ndemla na Mrisho Ngassa, mabadiliko ambayo hayakuwa na faida kwa timu, jambo lililofanya wapinzani wao kusawazisha mabao hayo mawili ndani ya dakika nne.
“Makosa hutokea kwenye mpira, ni jambo la kawaida nasi safari hii tumekutana na makosa hayo, benchi la ufundi imeyaona itayafanyia kazi yasijirudie katika mechi ya marudiano,” alisema Mkwasa.

NAHODHA wa timu ya soka ya taifa, Taifa Stars, Nadir Haroub amesema leo watafia uwanjani mjini Algiers katika mechi ya kuwania kufuzu michuano ya Kombe la Dunia Urusi 2018 watakaporudiana na wenyeji Algeria.
Stars inaingia uwanjani leo ikiwa na kumbukumbu ya kutoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya vigogo hivyo vya Afrika katika mechi ya kwanza iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita.
Katika mechi hiyo, Stars ilikuwa mbele kwa mabao 2-0 mpaka dakika ya 71 ndipo Algeria wakapata mabao ya harakaharaka na kuondoa furaha miongoni mwa watanzania waliofurika uwanjani siku hiyo.
Matokeo hayo yanaifanya Stars ihitaji ushindi katika mechi ya leo au sare ya kuanzia mabao 3-3 ili kujihakikishia kukata tiketi ya kucheza hatua ya makundi ya michuano hiyo, ambayo ni ya mwisho kabla ya kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia.
Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya mtandao jana, Haroub alisema anaamini timu yake inaweza kuibuka na ushindi ugenini leo. “Soka imebadilika sana siku hizi, ile ya miaka ile sio ya leo lolote linaweza kutokea kesho (leo) na tukasonga mbele, mbona hao Algeria tulienda nao sawa tu mechi ya kwanza makosa madogo tu yamefanyika wakasazisha lakini tunao uwezo wa kuwafunga,” alisema.
Mashabiki wa timu ya taifa, Taifa Stars, bado wana taharuki ya matokeo ya sare ya 2-2 dhidi ya Algeria, lakini nahodha wa Stars, Haroub ametamka kishujaa kuwa kazi haijaisha na anaamini timu hiyo itafanya makubwa kutokana na safu kali ya ushambuliaji waliyonayo.
“Mimi naamini kabisa timu yetu ipo vizuri kila sehemu nawaambieni washambuliaji wangu kwamba watatubeba katika mechi hiyo bila shaka yoyote,” alisema. Safu ya ushambuliaji ya Stars inaongozwa na wachezaji Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wanaocheza soka ya kulipwa TP Mazembe ya Congo DR.
Haroub ambaye pia ni nahodha wa mabingwa wa soka Bara, Yanga, alisema Stars itawashangaza wengi leo kama ilivyokuwa kwenye mechi iliyopita. “Mechi iliyopita hakuna aliyetarajia tungepata bao hata moja lakini matokeo yake tulifunga mabao mawili mpaka waarabu (Algeria) wenyewe walichanganyikiwa, hivyo hata huku inawezekana tu kushinda,” alisema.
Awali, kabla ya safari ya Algiers juzi, kocha mkuu wa timu hiyo Charles Mkwasa alisema anatarajia timu yake kupata matokeo mazuri. Mkwasa alikiri kufanya makosa ya kiufundi wakati wa mabadiliko katika mechi hiyo lakini akasema hiyo ni hali ya mpira hutokea mara nyingi.
Katika mechi hiyo ,Mkwasa aliwatoa Mudathir Yahya na Elias Maguli na nafasi zao kuchukuliwa na Said Ndemla na Mrisho Ngassa, mabadiliko ambayo hayakuwa na faida kwa timu, jambo lililofanya wapinzani wao kusawazisha mabao hayo mawili ndani ya dakika nne.
“Makosa hutokea kwenye mpira, ni jambo la kawaida nasi safari hii tumekutana na makosa hayo, benchi la ufundi imeyaona itayafanyia kazi yasijirudie katika mechi ya marudiano,” alisema Mkwasa.

Sunday, 1 November 2015





Simba imetoa kipigo cha mbwa mwizi jana baada ya kuichapa timu ya Majimaji ya Songea ‘wanalizombe’ kwa goli 6-0 kwenye mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara uliochezwa kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam
Vijana wa Msimbazi walianza kupata goli lao mapema kutoka kwa mchezaji wao chipukizi Ibrahim Ajib aliyetupia goli tatu pekeyake (hat-trick).


Kocha wa Simba Dylan Kerr akishangilia na wachezaji wake
Kwenye mchezo huo Simkba SC ilianza mchezo kwa kasi kwa kuishambulia mara kwa mara timu ya Majimaji na kupelekea kupata magoli ya mawili ya haraka katika dakika 15 za mwanzo, dakika ya nane na dakika ya 14 yote yakifungwa na Ajib.
Dakika za 15 za katikati ya kipindi cha kwanza mchezo ulitulia na Majimaji wakaonesha uhai kidogo na kufanikiwa kutengeneza nafasi kadhaa lakini safu ya ushambuliaji inayoongozwa na Stamili Mbonde ilishindwa kutumia vyema nafasi hizo kuipa goli Majimaji.
 Simba 61





Simba imetoa kipigo cha mbwa mwizi jana baada ya kuichapa timu ya Majimaji ya Songea ‘wanalizombe’ kwa goli 6-0 kwenye mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara uliochezwa kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam
Vijana wa Msimbazi walianza kupata goli lao mapema kutoka kwa mchezaji wao chipukizi Ibrahim Ajib aliyetupia goli tatu pekeyake (hat-trick).


Kocha wa Simba Dylan Kerr akishangilia na wachezaji wake
Kwenye mchezo huo Simkba SC ilianza mchezo kwa kasi kwa kuishambulia mara kwa mara timu ya Majimaji na kupelekea kupata magoli ya mawili ya haraka katika dakika 15 za mwanzo, dakika ya nane na dakika ya 14 yote yakifungwa na Ajib.
Dakika za 15 za katikati ya kipindi cha kwanza mchezo ulitulia na Majimaji wakaonesha uhai kidogo na kufanikiwa kutengeneza nafasi kadhaa lakini safu ya ushambuliaji inayoongozwa na Stamili Mbonde ilishindwa kutumia vyema nafasi hizo kuipa goli Majimaji.
 Simba 61

Coutinho vs ChelseaJose Mourinho ameendelea kupata wakati mgumu tena katika kibarua chake mara baada ya kushuhudia timu yake ya Chelsea leo ikipokea kipigo kitakatifu cha mabao 3-1 kutoka kwa Majogoo wa Liverpool, mchezo uliopigwa katika dimba la Stamford Bridge, maskani kwa Chelsea.
Chelsea ndio walikuwa wa kwanza kupata bao mapema kabisa katika kipindi cha kwanza mara baada ya kiungo Mbrazil Ramires kuunganisha kwa kichwa krosi iliyochongwa na Cesar Azpilicueta mnamo dakika ya 4 na kuipa Chelsea bao la kuongoza.
Ndoto za Chelsea zilizimwa mnamo dakika ya 45 na Mbrazil Coutinho baada ya kuuchinja mpira kwa uzuri na kumwacha kipa wa Chelsea Begovic akiwa hana la kufanya.
Coutinho tena alishindilia msumari wa pili kwa Chelsea baada ya kupiga shuti kali na kutinga moja kwa moja wavuni mnao dakika ya 74.
Ndoto za Chelsea zilizimwa kabisa mnamo dakika ya 83 na Christian Benteke ambaye aliingia kuchukua nafasi ya James Milner na kuipa Liverpool goli la tatu lililopeleka machungu makubwa kwa Chelsea huku presha ikizidi kumuendea Mourinho baada ya timu hiyo kuwa na matokea mabovu tangu mwanzo wa msimu huu, wakiwa nafasi ya 15 mpaka sasa.
 
Liverpool forward Philippe Coutinho (right) whips this strike past the challenge of John Terry (left) to equalise for the away sideContinho akifunga goli la kusawazisha.Coutinho heaped more misery on Jose Mourinho's men with this strike late in the second-half to give Liverpool a 2-1 lead 
Continho akifunga goli la pili
Chelsea's backline was once again undone by this shot from Christian Benteke, who fired in Liverpool's third at Stamford BridgeHuyo ndo Christian Benteke akimalizia msumari wenye sumu kali wa mwisho.

Coutinho vs ChelseaJose Mourinho ameendelea kupata wakati mgumu tena katika kibarua chake mara baada ya kushuhudia timu yake ya Chelsea leo ikipokea kipigo kitakatifu cha mabao 3-1 kutoka kwa Majogoo wa Liverpool, mchezo uliopigwa katika dimba la Stamford Bridge, maskani kwa Chelsea.
Chelsea ndio walikuwa wa kwanza kupata bao mapema kabisa katika kipindi cha kwanza mara baada ya kiungo Mbrazil Ramires kuunganisha kwa kichwa krosi iliyochongwa na Cesar Azpilicueta mnamo dakika ya 4 na kuipa Chelsea bao la kuongoza.
Ndoto za Chelsea zilizimwa mnamo dakika ya 45 na Mbrazil Coutinho baada ya kuuchinja mpira kwa uzuri na kumwacha kipa wa Chelsea Begovic akiwa hana la kufanya.
Coutinho tena alishindilia msumari wa pili kwa Chelsea baada ya kupiga shuti kali na kutinga moja kwa moja wavuni mnao dakika ya 74.
Ndoto za Chelsea zilizimwa kabisa mnamo dakika ya 83 na Christian Benteke ambaye aliingia kuchukua nafasi ya James Milner na kuipa Liverpool goli la tatu lililopeleka machungu makubwa kwa Chelsea huku presha ikizidi kumuendea Mourinho baada ya timu hiyo kuwa na matokea mabovu tangu mwanzo wa msimu huu, wakiwa nafasi ya 15 mpaka sasa.
 
Liverpool forward Philippe Coutinho (right) whips this strike past the challenge of John Terry (left) to equalise for the away sideContinho akifunga goli la kusawazisha.Coutinho heaped more misery on Jose Mourinho's men with this strike late in the second-half to give Liverpool a 2-1 lead 
Continho akifunga goli la pili
Chelsea's backline was once again undone by this shot from Christian Benteke, who fired in Liverpool's third at Stamford BridgeHuyo ndo Christian Benteke akimalizia msumari wenye sumu kali wa mwisho.

Saturday, 31 October 2015

Mshambuliaji wa Simba, Hamisi Kiiza.KIVUMBI cha Ligi Kuu Tanzania Bara, kinaendelea tena leo kwenye viwanja vitano tofauti, huku miamba ya soka Yanga na Simba ikirejea tena kusaka pointi tatu. Yanga ambayo kabla ya mechi ya Jumatano iliyotoka sare ya mabao 2-2 na Mwadui FC Uwanja wa Kambarage Shinyanga ilikuwa na pointi 19 sawa na Azam FC ikiongoza ligi hiyo, ilijikuta ikipata matokeo hayo ambayo yaliwapa majonzi mashabiki wao.
Majonzi hayo yaliongezeka zaidi Alhamisi baada ya Azam kuibuka na ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya JKT Ruvu Uwanja wa Karume, Dar es Salaam, hivyo Azam kuipiku Yanga kileleni mwa msimamo ikiwa na pointi 22 ikiiacha Yanga nafasi ya pili na pointi zake 20.
Kutokana na hali hiyo, leo Yanga itashuka Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi Tabora kuivaa Kagera Sugar, ikiwa na dhamira moja ya kurejea kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo. Kama Yanga ikishinda leo itafikisha pointi 23 na itaombea Azam FC ambayo kesho itacheza na Toto Africans Uwanja wa Azam Chamazi ipate matokeo mabovu.
Yanga inapewa nafasi ya kushinda leo kutokana na mwenendo mbaya wa wenyeji wao Kagera Sugar, ambao tangu kuanza msimu huu wameshinda mchezo mmoja na kupoteza mitano kati ya tisa waliyocheza.
Leo utakuwa mtihani wa pili kwa Kocha Mkuu wa Kagera Sugar, Mohammed Adolf Rishard, tangu akabidhiwe timu akirithi mikoba ya Mbwana Makatta aliyeachia ngazi kutokana na matokeo mabaya. Ni wazi Kocha Mkuu wa Yanga, Hans Pluijm naye ataingia uwanjani kuhakikisha vijana wake wanaibuka na ushindi ili kuwapa furaha mashabiki wao.
Hata hivyo pamoja na mwanzo mbaya wa Kagera Sugar, lakini timu hiyo inaweza kuzinduka na kufanya maajabu kwa kuifunga Yanga, kwani inakikosi bora cha wachezaji waliodumu kwa muda mrefu na timu hiyo akiwemo nahodha wake George Kavila na Paul Ngwai.
Yanga itaingia kwenye mchezo huo ikizidi kujivunia safu yake ya ushambuliaji inayoongozwa na Mzimbabwe, Donald Ngoma mwenye mabao saba na Amissi Tambwe ambao wamekuwa wakipambana kuhakikisha timu yao inafanya vizuri kwa kufunga mabao mengi.
Kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam, Simba inawakaribisha Majimaji ya Songea huku kocha wake Dylan Kerr, akijivunia ushindi wa bao 1-0, walioupata kwenye mchezo uliopita dhidi ya Coastal Union ya Tanga na timu hiyo kufikisha pointi 18 na kupanda hadi nafasi ya nne.
Mshambuliaji Hamisi Kiiza amekuwa tegemeo kwa kocha Kerr, katika upande wa mabao baada ya kufunga bao lake la sita Jumatano iliyopita ukiwa ni mchezo wake wa kwanza tangu kurejea uwanjani baada ya kukosa mechi tatu kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya nyama za paja.
Pamoja na kuonesha kiwango cha chini kwenye mchezo uliopita, lakini Simba wanapewa nafasi ya kushinda mchezo wa leo kutokana na udhaifu wa wapinzani wao Majimaji waliopo nafasi ya 10 wakiwa na pointi 11.
Rekodi zinaonesha Majimaji imekuwa hatari msimu huu inapocheza nyumbani uwanja wa Majimaji Songea, lakini mambo huwa tofauti inapokuwa ugenini na takwimu zinaonesha imepoteza mchezo mmoja nyumbani na kushinda mitatu, huku ikifungwa michezo mitatu na miwili ikitoka sare.
Mechi nyingine za leo, Mtibwa Sugar inayoshika nafasi ya tatu kwenye msimamo, itakuwa nyumbani Uwanja wa Manungu kucheza na Mwadui FC ya Shinyanga na Prisons itakuwa nyumbani Uwanja wa Sokoine kuchuana na Ndanda FC ya Mtwara na Coastal Union itakuwa Uwanja wa Mkwakwani ikicheza na Mbeya City.

Mshambuliaji wa Simba, Hamisi Kiiza.KIVUMBI cha Ligi Kuu Tanzania Bara, kinaendelea tena leo kwenye viwanja vitano tofauti, huku miamba ya soka Yanga na Simba ikirejea tena kusaka pointi tatu. Yanga ambayo kabla ya mechi ya Jumatano iliyotoka sare ya mabao 2-2 na Mwadui FC Uwanja wa Kambarage Shinyanga ilikuwa na pointi 19 sawa na Azam FC ikiongoza ligi hiyo, ilijikuta ikipata matokeo hayo ambayo yaliwapa majonzi mashabiki wao.
Majonzi hayo yaliongezeka zaidi Alhamisi baada ya Azam kuibuka na ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya JKT Ruvu Uwanja wa Karume, Dar es Salaam, hivyo Azam kuipiku Yanga kileleni mwa msimamo ikiwa na pointi 22 ikiiacha Yanga nafasi ya pili na pointi zake 20.
Kutokana na hali hiyo, leo Yanga itashuka Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi Tabora kuivaa Kagera Sugar, ikiwa na dhamira moja ya kurejea kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo. Kama Yanga ikishinda leo itafikisha pointi 23 na itaombea Azam FC ambayo kesho itacheza na Toto Africans Uwanja wa Azam Chamazi ipate matokeo mabovu.
Yanga inapewa nafasi ya kushinda leo kutokana na mwenendo mbaya wa wenyeji wao Kagera Sugar, ambao tangu kuanza msimu huu wameshinda mchezo mmoja na kupoteza mitano kati ya tisa waliyocheza.
Leo utakuwa mtihani wa pili kwa Kocha Mkuu wa Kagera Sugar, Mohammed Adolf Rishard, tangu akabidhiwe timu akirithi mikoba ya Mbwana Makatta aliyeachia ngazi kutokana na matokeo mabaya. Ni wazi Kocha Mkuu wa Yanga, Hans Pluijm naye ataingia uwanjani kuhakikisha vijana wake wanaibuka na ushindi ili kuwapa furaha mashabiki wao.
Hata hivyo pamoja na mwanzo mbaya wa Kagera Sugar, lakini timu hiyo inaweza kuzinduka na kufanya maajabu kwa kuifunga Yanga, kwani inakikosi bora cha wachezaji waliodumu kwa muda mrefu na timu hiyo akiwemo nahodha wake George Kavila na Paul Ngwai.
Yanga itaingia kwenye mchezo huo ikizidi kujivunia safu yake ya ushambuliaji inayoongozwa na Mzimbabwe, Donald Ngoma mwenye mabao saba na Amissi Tambwe ambao wamekuwa wakipambana kuhakikisha timu yao inafanya vizuri kwa kufunga mabao mengi.
Kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam, Simba inawakaribisha Majimaji ya Songea huku kocha wake Dylan Kerr, akijivunia ushindi wa bao 1-0, walioupata kwenye mchezo uliopita dhidi ya Coastal Union ya Tanga na timu hiyo kufikisha pointi 18 na kupanda hadi nafasi ya nne.
Mshambuliaji Hamisi Kiiza amekuwa tegemeo kwa kocha Kerr, katika upande wa mabao baada ya kufunga bao lake la sita Jumatano iliyopita ukiwa ni mchezo wake wa kwanza tangu kurejea uwanjani baada ya kukosa mechi tatu kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya nyama za paja.
Pamoja na kuonesha kiwango cha chini kwenye mchezo uliopita, lakini Simba wanapewa nafasi ya kushinda mchezo wa leo kutokana na udhaifu wa wapinzani wao Majimaji waliopo nafasi ya 10 wakiwa na pointi 11.
Rekodi zinaonesha Majimaji imekuwa hatari msimu huu inapocheza nyumbani uwanja wa Majimaji Songea, lakini mambo huwa tofauti inapokuwa ugenini na takwimu zinaonesha imepoteza mchezo mmoja nyumbani na kushinda mitatu, huku ikifungwa michezo mitatu na miwili ikitoka sare.
Mechi nyingine za leo, Mtibwa Sugar inayoshika nafasi ya tatu kwenye msimamo, itakuwa nyumbani Uwanja wa Manungu kucheza na Mwadui FC ya Shinyanga na Prisons itakuwa nyumbani Uwanja wa Sokoine kuchuana na Ndanda FC ya Mtwara na Coastal Union itakuwa Uwanja wa Mkwakwani ikicheza na Mbeya City.

Kiongozi wa timu ya waangalizi wa Jumuiya ya EAC katika Uchaguzi Mkuu wa Tanzania, Moody Awori akizungumza na wajumbe wa Jumuiya hiyo mjini Dar es Salaam.WAANGALIZI kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), wameelezea kushangazwa na amani na utulivu uliokuwepo wakati wa kupiga kura. Kiongozi wa Timu ya Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu kutoka EAC, Moody Awori, ambaye pia ni Makamu wa Rais mstaafu wa Kenya amemueleza hayo Rais Jakaya Kikwete alipofika Ikulu jana mchana.
“Sisi kutoka Kenya tulishangaa, unakwenda kwenye kituo watu wako kimya, tunakupongeza pamoja na Chama Cha Mapinduzi (CCM),” alisema Awori. Aliongeza kuwa, “Tunatarajia kuwa uongozi mpya unaoingia madarakani, utafuata nyayo zako.”
Awori alimueleza Rais kuwa katika shughuli zao za uangalizi, walitembelea vituo zaidi ya 12 kwa siku jijini Dar es Salaam na kote hali ilikuwa shwari. Alieleza kuwa wamejifunza kitu kikubwa katika uchaguzi huo.
Watanzania kwa jadi yao ni watu wa amani na utulivu, lakini pia kabla ya uchaguzi, Rais Kikwete aliweka wazi kuwa Serikali yake ina wajibu wa kulinda watu na mali zao na kuhakikisha watu wote wanashiriki katika kupata haki yao ya kupiga kura kwa amani, uhuru na utulivu bila kubughudhiwa na hilo ndiyo jambo kubwa na la msingi kwa Serikali yake.
Awali jana asubuhi, Rais Kikwete alihudhuria hafla ya kukabidhiwa vyeti kwa washindi wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, Rais mteule Dk John Magufuli na Makamu wa Rais mteule, Mama Samia Suluhu Hassan.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa vyama na Serikali na viongozi wa waangalizi wa uchaguzi hapa nchini, viongozi wa dini na watu mbalimbali. Baadaye Rais Kikwete aliongoza mapokezi ya Rais mteule katika Ofisi ndogo za CCM Lumumba, ambako wanachama, mashabiki na wapenzi wa CCM walifika kumpokea na kumsalimia mgombea wao, ambaye ameibuka mshindi wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

Kiongozi wa timu ya waangalizi wa Jumuiya ya EAC katika Uchaguzi Mkuu wa Tanzania, Moody Awori akizungumza na wajumbe wa Jumuiya hiyo mjini Dar es Salaam.WAANGALIZI kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), wameelezea kushangazwa na amani na utulivu uliokuwepo wakati wa kupiga kura. Kiongozi wa Timu ya Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu kutoka EAC, Moody Awori, ambaye pia ni Makamu wa Rais mstaafu wa Kenya amemueleza hayo Rais Jakaya Kikwete alipofika Ikulu jana mchana.
“Sisi kutoka Kenya tulishangaa, unakwenda kwenye kituo watu wako kimya, tunakupongeza pamoja na Chama Cha Mapinduzi (CCM),” alisema Awori. Aliongeza kuwa, “Tunatarajia kuwa uongozi mpya unaoingia madarakani, utafuata nyayo zako.”
Awori alimueleza Rais kuwa katika shughuli zao za uangalizi, walitembelea vituo zaidi ya 12 kwa siku jijini Dar es Salaam na kote hali ilikuwa shwari. Alieleza kuwa wamejifunza kitu kikubwa katika uchaguzi huo.
Watanzania kwa jadi yao ni watu wa amani na utulivu, lakini pia kabla ya uchaguzi, Rais Kikwete aliweka wazi kuwa Serikali yake ina wajibu wa kulinda watu na mali zao na kuhakikisha watu wote wanashiriki katika kupata haki yao ya kupiga kura kwa amani, uhuru na utulivu bila kubughudhiwa na hilo ndiyo jambo kubwa na la msingi kwa Serikali yake.
Awali jana asubuhi, Rais Kikwete alihudhuria hafla ya kukabidhiwa vyeti kwa washindi wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, Rais mteule Dk John Magufuli na Makamu wa Rais mteule, Mama Samia Suluhu Hassan.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa vyama na Serikali na viongozi wa waangalizi wa uchaguzi hapa nchini, viongozi wa dini na watu mbalimbali. Baadaye Rais Kikwete aliongoza mapokezi ya Rais mteule katika Ofisi ndogo za CCM Lumumba, ambako wanachama, mashabiki na wapenzi wa CCM walifika kumpokea na kumsalimia mgombea wao, ambaye ameibuka mshindi wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

Friday, 30 October 2015

KOCHA wa Yanga Hans van der Pluijm, ameitupia lawama safu yake ya ulinzi kwa kusema ilikosa umakini na kusababisha wapinzani wao Mwadui FC kusawazisha bao la pili dakika za mwisho.
Yanga juzi ilikuwa ugenini Uwanja wa Kambarage Shinyanga kupambana na Mwadui FC, na kulazimishwa sare ya 2-2, matokeo ambayo yameiweka rehani nafasi yake ya kuongoza ligi hiyo.
Akizungumza na gazeti hili Pluijm, alisema safu yake ya ulinzi iliwanyima pointi tatu kwenye mchezo huo kitu ambacho kinaweza kuwagharimu kutokana na ushindani mkali uliopo kati yao na wapinzani wao Azam FC.
“Hatukucheza kwenye kiwango chetu cha kawaida, lakini tulistahili ushindi kutokana na namna ambavyo wachezaji wangu walivyocheza kwa kujitolea na kupata mabao yale mawili.
“Hata hivyo safu yetu ya ulinzi ilituangusha kwa kuruhusu bao la kusawazisha la dakika za mwisho,” alisema Pluijm. Mholanzi huyo alisema matokeo hayo siyo mabaya, lakini wanalazimika kupambana kwenye mchezo wao unaokuja dhidi ya Kagera Sugar ili kurudisha wimbi lao la ushindi na kuendelea kujiwekea mazingira mazuri ya ubingwa msimu huu.
Alisema katika mchezo huo wapinzani wao Mwadui, walionekana kucheza kwa kutumia nguvu nyingi na kuwakamia, kitu ambacho kiliwasumbua wachezaji wake kushindwa kuonesha kiwango chao cha kawaida ambacho wamekuwa wakikionesha kwenye michezo iliyopita.
“Mchezo ulikuwa mgumu kwa sababu tulicheza na timu ambayo ilipania kutuvurugia mipango yetu kwa kucheza vurugu, lakini nimefurahi kupata sare hiyo kwa sababu vijana wangu walilazimika kubadilika na kuendana na hali ya mchezo ilivyokuwa,” alisema Pluijm.
Katika mchezo huo mabao ya Yanga yote mawili yalifungwa na Mzimbabwe Donald Ngoma, huku yale ya Mwadui yakifungwa na Poul Nonga na Bakari Kigodeko na kuifanya timu hiyo ya Jangwani kufikisha pointi 20 katika mechi nane ilizocheza msimu huu.

KOCHA wa Yanga Hans van der Pluijm, ameitupia lawama safu yake ya ulinzi kwa kusema ilikosa umakini na kusababisha wapinzani wao Mwadui FC kusawazisha bao la pili dakika za mwisho.
Yanga juzi ilikuwa ugenini Uwanja wa Kambarage Shinyanga kupambana na Mwadui FC, na kulazimishwa sare ya 2-2, matokeo ambayo yameiweka rehani nafasi yake ya kuongoza ligi hiyo.
Akizungumza na gazeti hili Pluijm, alisema safu yake ya ulinzi iliwanyima pointi tatu kwenye mchezo huo kitu ambacho kinaweza kuwagharimu kutokana na ushindani mkali uliopo kati yao na wapinzani wao Azam FC.
“Hatukucheza kwenye kiwango chetu cha kawaida, lakini tulistahili ushindi kutokana na namna ambavyo wachezaji wangu walivyocheza kwa kujitolea na kupata mabao yale mawili.
“Hata hivyo safu yetu ya ulinzi ilituangusha kwa kuruhusu bao la kusawazisha la dakika za mwisho,” alisema Pluijm. Mholanzi huyo alisema matokeo hayo siyo mabaya, lakini wanalazimika kupambana kwenye mchezo wao unaokuja dhidi ya Kagera Sugar ili kurudisha wimbi lao la ushindi na kuendelea kujiwekea mazingira mazuri ya ubingwa msimu huu.
Alisema katika mchezo huo wapinzani wao Mwadui, walionekana kucheza kwa kutumia nguvu nyingi na kuwakamia, kitu ambacho kiliwasumbua wachezaji wake kushindwa kuonesha kiwango chao cha kawaida ambacho wamekuwa wakikionesha kwenye michezo iliyopita.
“Mchezo ulikuwa mgumu kwa sababu tulicheza na timu ambayo ilipania kutuvurugia mipango yetu kwa kucheza vurugu, lakini nimefurahi kupata sare hiyo kwa sababu vijana wangu walilazimika kubadilika na kuendana na hali ya mchezo ilivyokuwa,” alisema Pluijm.
Katika mchezo huo mabao ya Yanga yote mawili yalifungwa na Mzimbabwe Donald Ngoma, huku yale ya Mwadui yakifungwa na Poul Nonga na Bakari Kigodeko na kuifanya timu hiyo ya Jangwani kufikisha pointi 20 katika mechi nane ilizocheza msimu huu.

DAKTARI wa Kemia, John Pombe Joseph Magufuli ndiye Rais wa Tano wa Tanzania.
Jana ambapo alitimiza miaka 56 ya kuzaliwa kwake, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ilimtangaza kuwa mshindi wa Uchaguzi Mkuu wa Urais mwaka 2015, uliofanyika Jumapili iliyopita.
Mbunge huyo wa Chato kwa miaka 20, aliyezaliwa Oktoba 29, 1959, ametangazwa mshindi baada ya kupata kura 8,882,935, sawa na asilimia 58.46 ya kura halali zilizopigwa Jumapili, hivyo kumrithi Rais Jakaya Kikwete katika Ikulu ya Magogoni ambayo tayari imeshakaliwa na Watanzania wengine wanne.
Mbali ya Rais Kikwete, marais wengine waliowahi kuiongoza Tanzania ni Mwalimu Julius Nyerere, Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa, ambao wameshika madaraka hayo ya juu ya nchi tangu Uhuru wa mwaka 1961.
Akitangaza matokeo hayo jana kwenye Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNCC), Dar es Salaam, Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu Damian Lubuva alisema Dk Magufuli ameshinda nafasi hiyo baada ya kujikusanyia kura 8,882,935 ambayo sawa na asilimia 58.46 ya kura halali zilizopigwa.
“Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977 Ibara ya 41 (6) mgombea yeyote wa kiti cha urais atatangazwa kuwa amechaguliwa kuwa rais, iwapo tu amepata kura nyingi zaidi kuliko mgombea mwingine yeyote. Na Ibara ya 47 (ii) inasema mgombea urais akichaguliwa kuwa mshindi, basi mgombea mwenza atatangazwa kuwa Makamu wa Rais,” alisema Jaji Lubuva.
“Kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi Kifungu wa 35 (e) na 35 (f) na Kifungu cha 81 (b) vya Sheria ya Uchaguzi Sura ya 343, namtangaza John Magufuli kuwa mshindi wa uchaguzi wa Rais wa mwaka 2015 na pia namtangaza Samia Suluhu Hassan kuwa Makamu wa Rais.” Kwa msingi huo, Mgombea Mwenza wa CCM, Samia Suluhu Hassan atakuwa Makamu wa Rais, akiwa ni mwanamke wa kwanza kushika wadhifa huo Tanzania tangu nchi ilipoundwa.
Dk Magufuli alifuatiwa na mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) aliyeungwa mkono na vyama vinne vya upinzani (Ukawa), Edward Lowassa aliyepata kura 6,072,848, sawa na asilimia 39.97 ya kura halali zilizopigwa.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Uchaguzi, Kailima Kombwey, katika uchaguzi wa mwaka huu, wapiga kura 23,161,440 walijiandikisha na waliopiga kura ni 15,589,639, ambayo ni asilimia 67.31 ya waliojiandikisha.
Kombwey alisema kura halali ni 15,193,862 ambayo ni asilimia 97.46 na kura zilizokataliwa ni 402,248 ambayo ni asilimia 2.58. Katika uchaguzi huo, ambao wagombea wa urais walikuwa wanane, mwanamke pekee, Anna Mgwhira wa chama kipya cha ACT-Wazalendo alishika nafasi ya tatu kwa kupata kura 98,763 sawa na asilimia 0.65.
Wagombea wengine kura walizopata na asilimia kwenye mabano ni Chief Lutalosa Yemba wa ADC kura 66,049 (asilimia 0.43), Hashim Rungwe wa Chaumma kura 49,256 (asilimia 0.32), Janken Kasambala wa NRA kura 8,028 (asilimia 0.05), Macmillan Lyimo wa TLP kura 8,198 (asilimia 0.05), Fahmi Dovutwa wa UPDP kura 7,785 (0.05%).
Katika uchaguzi uliofanyika mwaka 2010, mgombea wa CCM, Jakaya Kikwete alishinda uchaguzi huo akiwa amepata asilimia 61.17 baada ya kupata kura zaidi ya milioni 5.27 na kufuatiwa na mgombea wa Chadema, Dk Willbrod Slaa aliyepata kura ya zaidi ya milioni 2.27.
Nafasi ya tatu ilikwenda kwa Profesa Ibrahim Lipumba wa CUF aliyepata kura 697,014, Peter Mziray alipata kura 96,932, Rungwe aliyegombea kwa tiketi ya NCCRMageuzi alipata kura 26,321, Mutamwega Mughwaya wa TLP alipata kura 17,434 na Dovutwa alipata kura 13,123. Ujumlishwaji wa matokeo ulishuhudiwa na mawakala wa vyama mbalimbali, waangalizi, Polisi pamoja na wananchi wa kawaida, pamoja na kuhakiki matokeo hayo.
Hata hivyo, vyama viwili kati ya vinane vilivyoshiriki uchaguzi havikusaini matokeo hayo ambavyo ni Chadema na Chaumma. Chadema katika majumuisho, wakala wake Goodluck ole Medeye, waziri wa zamani katika Serikali ya Awamu ya Nne aliyemfuata swahiba wake Lowassa katika Chadema, ambaye alikuwepo wakati wa kutangaza matokeo ya majimbo, hakuwepo wakati wa kujumuisha na kusaini matokeo huku wakala wa Chaumma akigoma kusaini.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Kailima Kombwey alisema pamoja na mawakala hao kugoma kusaini hakuzuii, Tume kutangaza matokeo ya uchaguzi. Kwa mujibu wa Kombwey, Rais mteule Dk Magufuli atakabidhiwa cheti cha ushindi leo kwenye Viwanja vya Diamond Jubilee, Dar es Salaam pamoja na Makamu wa Rais, Samia.
Dakika chache kabla ya Dk Magufuli kutangazwa na NEC baada ya kumaliza kujumuisha matokeo, ambayo yalianza kutangazwa kwa umma kuanzia Jumatatu asubuhi, Rais Kikwete aliweka picha ya Magufuli katika akaunti yake ya Twitter na kuandika, “Amiri Jeshi Mkuu mpya wa Tanzania, chaguo la Watanzania, Rais John Pombe Magufuli.”
Aidha, mgombea wa ACT – Wazalendo, Anna Mghwira alimpigia simu Dk Magufuli muda mfupi baada ya kutangazwa mshindi na kumpongeza, huku Dk Magufuli akimshukuru na kumwita mkomavu wa siasa na mwanademokrasia wa mfano.
Kwa mujibu wa Rais Kikwete, baada ya kupiga kura kijijini kwake Msoga wilayani Bagamoyo, ataondoka madarakani kwa mujibu wa Katiba Alhamisi ya Novemba 5, mwaka huu, siku ambayo Dk Magufuli atakula kiapo kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam kuiongoza Tanzania kwa miaka mitano ijayo.
Dk Magufuli ambaye ni Waziri wa Ujenzi, atakuwa Rais wa kwanza wa Tanzania ambaye ni mwanasayansi, na pia mwalimu wa tatu kukaa Ikulu ya Magogoni, akitanguliwa na walimu wenzake Mwalimu Nyerere na Alhaj Mwinyi.
Amewahi kufundisha katika Shule ya Sekondari ya Sengerema mkoani Mwanza akifundisha masomo ya Kemia na Hisabati, na baadaye kufanya kazi katika Chama cha Ushirika cha Nyanza jijini Mwanza akiwa Mkemia.
Alijitosa katika siasa ambako alichaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Biharamulo Mashariki mkoani Kagera (wakati huo sasa Chato mkoani Geita) mwaka 1995. Amekuwa mbunge wa jimbo hilo hadi Juni mwaka huu, alipojitosa katika mchakato wa kuwania urais. Aliteuliwa na Rais Mkapa kuwa Naibu Waziri wa Ujenzi kuanzia mwaka 2000 hadi mwaka 2005. Baadaye alikuwa Waziri kamili wa wizara hiyo.
Chini ya Rais Kikwete, amewahi kuwa Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kabla ya kumrejesha Ujenzi. Dk Magufuli anasifika kwa uchapakazi na weledi katika kazi zote, alizokabidhiwa akiwa serikalini na wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu kaulimbiu yake ilikuwa “Hapa Kazi Tu”.
Kaulimbiu hiyo ilimbeba na kumpambanua na wagombea wengine saba, huku akiahidi kuwa Tanzania itakuwa nchi ya viwanda chini ya uongozi wake. Katika uchaguzi uliokuwa na ushindani mkubwa pengine kuliko chaguzi nyingine nne za mfumo wa vyama vingi ulioanzishwa mwaka 1992, Dk Magufuli aliendesha kampeni zake, akijipambanua kuwa ni mtu atakayeleta mabadiliko ya kweli katika utendaji wa serikali.
Aliwaahidi Watanzania kwamba atasimamia mabadiliko hayo katika kila sekta, akisisitiza zaidi maendeleo ya viwanda hasa katika kuiwezesha Tanzania kuingia kuwa nchi ya uchumi wa kati.
Akifunga kampeni zake jijini Mwanza kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Dk Magufuli alisema amepokea ushauri kutoka kwa wananchi kwa njia mbalimbali, kutoka facebook, tweeter, mabango, vikao mbalimbali na hata ujumbe mfupi wa simu ambapo alisema imeonekana kero kubwa ni maji.
Kero nyingine alizoahidi kushughulikia ni ya nishati ya umeme, kulinda Muungano, kuendeleza ulinzi na usalama wa nchi na wananchi wake, kuimarisha kilimo, uvuvi na ufugaji kwa kuboresha bei ya mazao ya kazi hizo na kuimarisha viwanda, viongeze thamani ya mazao hayo.
Aliahidi kuhakikisha kila Mtanzania mwenye uwezo wa kufanya kazi anapata kazi yenye kipato kizuri, kutoa mikopo ya Sh milioni 50 kila kijiji na mtaa ya kuanzisha na kuendeleza biashara, kuhakikisha elimu inatolewa bure kuanzia awali mpaka kidato cha nne na kuwashughulikia mafisadi kwa kuanzisha Mahakama ya Rushwa.
Mshindani wake wa karibu, Waziri Mkuu wa zamani, Lowassa ambaye alikuwa ndani ya CCM kabla ya kujitoa Agosti mwaka huu, aliingia Chadema na kubeba kaulimbiu ya mabadiliko, huku akiwaahidi Watanzania kuwa ataendesha serikali kwa mchakamchaka na kubadili hali ya maisha kwa Watanzania kwa muda mfupi.

DAKTARI wa Kemia, John Pombe Joseph Magufuli ndiye Rais wa Tano wa Tanzania.
Jana ambapo alitimiza miaka 56 ya kuzaliwa kwake, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ilimtangaza kuwa mshindi wa Uchaguzi Mkuu wa Urais mwaka 2015, uliofanyika Jumapili iliyopita.
Mbunge huyo wa Chato kwa miaka 20, aliyezaliwa Oktoba 29, 1959, ametangazwa mshindi baada ya kupata kura 8,882,935, sawa na asilimia 58.46 ya kura halali zilizopigwa Jumapili, hivyo kumrithi Rais Jakaya Kikwete katika Ikulu ya Magogoni ambayo tayari imeshakaliwa na Watanzania wengine wanne.
Mbali ya Rais Kikwete, marais wengine waliowahi kuiongoza Tanzania ni Mwalimu Julius Nyerere, Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa, ambao wameshika madaraka hayo ya juu ya nchi tangu Uhuru wa mwaka 1961.
Akitangaza matokeo hayo jana kwenye Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNCC), Dar es Salaam, Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu Damian Lubuva alisema Dk Magufuli ameshinda nafasi hiyo baada ya kujikusanyia kura 8,882,935 ambayo sawa na asilimia 58.46 ya kura halali zilizopigwa.
“Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977 Ibara ya 41 (6) mgombea yeyote wa kiti cha urais atatangazwa kuwa amechaguliwa kuwa rais, iwapo tu amepata kura nyingi zaidi kuliko mgombea mwingine yeyote. Na Ibara ya 47 (ii) inasema mgombea urais akichaguliwa kuwa mshindi, basi mgombea mwenza atatangazwa kuwa Makamu wa Rais,” alisema Jaji Lubuva.
“Kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi Kifungu wa 35 (e) na 35 (f) na Kifungu cha 81 (b) vya Sheria ya Uchaguzi Sura ya 343, namtangaza John Magufuli kuwa mshindi wa uchaguzi wa Rais wa mwaka 2015 na pia namtangaza Samia Suluhu Hassan kuwa Makamu wa Rais.” Kwa msingi huo, Mgombea Mwenza wa CCM, Samia Suluhu Hassan atakuwa Makamu wa Rais, akiwa ni mwanamke wa kwanza kushika wadhifa huo Tanzania tangu nchi ilipoundwa.
Dk Magufuli alifuatiwa na mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) aliyeungwa mkono na vyama vinne vya upinzani (Ukawa), Edward Lowassa aliyepata kura 6,072,848, sawa na asilimia 39.97 ya kura halali zilizopigwa.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Uchaguzi, Kailima Kombwey, katika uchaguzi wa mwaka huu, wapiga kura 23,161,440 walijiandikisha na waliopiga kura ni 15,589,639, ambayo ni asilimia 67.31 ya waliojiandikisha.
Kombwey alisema kura halali ni 15,193,862 ambayo ni asilimia 97.46 na kura zilizokataliwa ni 402,248 ambayo ni asilimia 2.58. Katika uchaguzi huo, ambao wagombea wa urais walikuwa wanane, mwanamke pekee, Anna Mgwhira wa chama kipya cha ACT-Wazalendo alishika nafasi ya tatu kwa kupata kura 98,763 sawa na asilimia 0.65.
Wagombea wengine kura walizopata na asilimia kwenye mabano ni Chief Lutalosa Yemba wa ADC kura 66,049 (asilimia 0.43), Hashim Rungwe wa Chaumma kura 49,256 (asilimia 0.32), Janken Kasambala wa NRA kura 8,028 (asilimia 0.05), Macmillan Lyimo wa TLP kura 8,198 (asilimia 0.05), Fahmi Dovutwa wa UPDP kura 7,785 (0.05%).
Katika uchaguzi uliofanyika mwaka 2010, mgombea wa CCM, Jakaya Kikwete alishinda uchaguzi huo akiwa amepata asilimia 61.17 baada ya kupata kura zaidi ya milioni 5.27 na kufuatiwa na mgombea wa Chadema, Dk Willbrod Slaa aliyepata kura ya zaidi ya milioni 2.27.
Nafasi ya tatu ilikwenda kwa Profesa Ibrahim Lipumba wa CUF aliyepata kura 697,014, Peter Mziray alipata kura 96,932, Rungwe aliyegombea kwa tiketi ya NCCRMageuzi alipata kura 26,321, Mutamwega Mughwaya wa TLP alipata kura 17,434 na Dovutwa alipata kura 13,123. Ujumlishwaji wa matokeo ulishuhudiwa na mawakala wa vyama mbalimbali, waangalizi, Polisi pamoja na wananchi wa kawaida, pamoja na kuhakiki matokeo hayo.
Hata hivyo, vyama viwili kati ya vinane vilivyoshiriki uchaguzi havikusaini matokeo hayo ambavyo ni Chadema na Chaumma. Chadema katika majumuisho, wakala wake Goodluck ole Medeye, waziri wa zamani katika Serikali ya Awamu ya Nne aliyemfuata swahiba wake Lowassa katika Chadema, ambaye alikuwepo wakati wa kutangaza matokeo ya majimbo, hakuwepo wakati wa kujumuisha na kusaini matokeo huku wakala wa Chaumma akigoma kusaini.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Kailima Kombwey alisema pamoja na mawakala hao kugoma kusaini hakuzuii, Tume kutangaza matokeo ya uchaguzi. Kwa mujibu wa Kombwey, Rais mteule Dk Magufuli atakabidhiwa cheti cha ushindi leo kwenye Viwanja vya Diamond Jubilee, Dar es Salaam pamoja na Makamu wa Rais, Samia.
Dakika chache kabla ya Dk Magufuli kutangazwa na NEC baada ya kumaliza kujumuisha matokeo, ambayo yalianza kutangazwa kwa umma kuanzia Jumatatu asubuhi, Rais Kikwete aliweka picha ya Magufuli katika akaunti yake ya Twitter na kuandika, “Amiri Jeshi Mkuu mpya wa Tanzania, chaguo la Watanzania, Rais John Pombe Magufuli.”
Aidha, mgombea wa ACT – Wazalendo, Anna Mghwira alimpigia simu Dk Magufuli muda mfupi baada ya kutangazwa mshindi na kumpongeza, huku Dk Magufuli akimshukuru na kumwita mkomavu wa siasa na mwanademokrasia wa mfano.
Kwa mujibu wa Rais Kikwete, baada ya kupiga kura kijijini kwake Msoga wilayani Bagamoyo, ataondoka madarakani kwa mujibu wa Katiba Alhamisi ya Novemba 5, mwaka huu, siku ambayo Dk Magufuli atakula kiapo kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam kuiongoza Tanzania kwa miaka mitano ijayo.
Dk Magufuli ambaye ni Waziri wa Ujenzi, atakuwa Rais wa kwanza wa Tanzania ambaye ni mwanasayansi, na pia mwalimu wa tatu kukaa Ikulu ya Magogoni, akitanguliwa na walimu wenzake Mwalimu Nyerere na Alhaj Mwinyi.
Amewahi kufundisha katika Shule ya Sekondari ya Sengerema mkoani Mwanza akifundisha masomo ya Kemia na Hisabati, na baadaye kufanya kazi katika Chama cha Ushirika cha Nyanza jijini Mwanza akiwa Mkemia.
Alijitosa katika siasa ambako alichaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Biharamulo Mashariki mkoani Kagera (wakati huo sasa Chato mkoani Geita) mwaka 1995. Amekuwa mbunge wa jimbo hilo hadi Juni mwaka huu, alipojitosa katika mchakato wa kuwania urais. Aliteuliwa na Rais Mkapa kuwa Naibu Waziri wa Ujenzi kuanzia mwaka 2000 hadi mwaka 2005. Baadaye alikuwa Waziri kamili wa wizara hiyo.
Chini ya Rais Kikwete, amewahi kuwa Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kabla ya kumrejesha Ujenzi. Dk Magufuli anasifika kwa uchapakazi na weledi katika kazi zote, alizokabidhiwa akiwa serikalini na wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu kaulimbiu yake ilikuwa “Hapa Kazi Tu”.
Kaulimbiu hiyo ilimbeba na kumpambanua na wagombea wengine saba, huku akiahidi kuwa Tanzania itakuwa nchi ya viwanda chini ya uongozi wake. Katika uchaguzi uliokuwa na ushindani mkubwa pengine kuliko chaguzi nyingine nne za mfumo wa vyama vingi ulioanzishwa mwaka 1992, Dk Magufuli aliendesha kampeni zake, akijipambanua kuwa ni mtu atakayeleta mabadiliko ya kweli katika utendaji wa serikali.
Aliwaahidi Watanzania kwamba atasimamia mabadiliko hayo katika kila sekta, akisisitiza zaidi maendeleo ya viwanda hasa katika kuiwezesha Tanzania kuingia kuwa nchi ya uchumi wa kati.
Akifunga kampeni zake jijini Mwanza kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Dk Magufuli alisema amepokea ushauri kutoka kwa wananchi kwa njia mbalimbali, kutoka facebook, tweeter, mabango, vikao mbalimbali na hata ujumbe mfupi wa simu ambapo alisema imeonekana kero kubwa ni maji.
Kero nyingine alizoahidi kushughulikia ni ya nishati ya umeme, kulinda Muungano, kuendeleza ulinzi na usalama wa nchi na wananchi wake, kuimarisha kilimo, uvuvi na ufugaji kwa kuboresha bei ya mazao ya kazi hizo na kuimarisha viwanda, viongeze thamani ya mazao hayo.
Aliahidi kuhakikisha kila Mtanzania mwenye uwezo wa kufanya kazi anapata kazi yenye kipato kizuri, kutoa mikopo ya Sh milioni 50 kila kijiji na mtaa ya kuanzisha na kuendeleza biashara, kuhakikisha elimu inatolewa bure kuanzia awali mpaka kidato cha nne na kuwashughulikia mafisadi kwa kuanzisha Mahakama ya Rushwa.
Mshindani wake wa karibu, Waziri Mkuu wa zamani, Lowassa ambaye alikuwa ndani ya CCM kabla ya kujitoa Agosti mwaka huu, aliingia Chadema na kubeba kaulimbiu ya mabadiliko, huku akiwaahidi Watanzania kuwa ataendesha serikali kwa mchakamchaka na kubadili hali ya maisha kwa Watanzania kwa muda mfupi.

TANZANIA imeandika historia mpya, ambapo jana imempata Rais Mteule wa Awamu ya Tano, Dk John Pombe Magufuli, ambaye alikuwa mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Uchaguzi Mkuu uliohitimishwa Jumapili ya Oktoba 25, mwaka huu.
Dk Magufuli ambaye katika kampeni ya kuwania urais alikuwa na kauli mbiu ya Hapa Kazi Tu, si mgeni katika safu za uongozi wa Tanzania kwa kuwa amekuwa serikalini kwa miaka 20, akishika majukumu mbalimbali ambayo yalitumiwa na Watanzania kumpima.
Moja ya sifa yake kubwa tangu alipotangaza nia ya kugombea urais kupitia chama hicho mwishoni mwa Mei mwaka huu, ni uadilifu katika utendaji kazi wake katika majukumu tofauti aliyokabidhiwa Rais huyo mteule wa Awamu ya Tano, anatajwa kuwa katika majukumu yote ya kitaifa aliyowahi kukabidhiwa, alionesha sifa ya juu ya uaminifu na uadilifu, ambao umeelezwa kwa namna mbili tofauti.
Ujenzi barabara Kwanza ni uongozi wake wa miradi mikubwa ya fedha nyingi, ambayo kwa muda wote wa uongozi wake hakuwahi kukumbwa na kashfa. Kwa mfano mwaka huu tu, alikuwa akiongoza Wizara ya Ujenzi, iliyokuwa na bajeti ya Sh trilioni 1.2 na Mfuko wa Barabara uliokabidhiwa zaidi ya Sh bilioni 866.
Katika miaka 15 aliyoongoza Wizara hiyo ya Ujenzi, katika ngazi hiyo alisimamia miradi ya zaidi ya Sh trilioni 9.5, lakini hakula hata senti tano, badala yake alijenga mtandao mrefu wa barabara za lami nchi nzima. Usimamizi Namna ya pili ya kuzungumzia uadilifu wake ni usimamizi wake wa watendaji na wadau wa sekta ya ujenzi, ambao amekuwa akiwapa kazi za mabilioni ya shilingi na kuisimamia kwa karibu katika kuwatumikia Watanzania.
Dk Magufuli amekuwa akisimamia makandarasi zaidi ya 8,500, wahandisi zaidi ya 15,000 na wakadiriaji majengo zaidi ya 1,300, ambao wamekuwa wakinufaika na kazi za Serikali za mabilioni ya shilingi.
Kama angetumia vibaya nafasi hiyo na angetaka kumuomba au kushinikiza kila mmoja wao ampe Sh milioni moja tu kwa mwaka, angeweza kujikusanyia pato binafsi lisilo halali la zaidi ya Sh bilioni 100 kila mwaka. Pamoja na kuwa karibu na kishawishi hicho, lakini Dk Magufuli hakushiriki kuhujumu hata senti moja na hana historia wala hakuwahi kutajwa popote kutumia vibaya nafasi yake hiyo katika sekta yenye maslahi makubwa ya kifedha.
Ukali kwa wazembe Badala ya kuomba michango ya kujinufaisha kutoka kwa wadau hao wa ujenzi, Dk Magufuli alijikuta akifukuza kazi makandarasi zaidi ya 3,000 wa ndani na nje ya nchi, bila kujali utajiri wao, pale makandarasi hao walipozembea kazi au kufanya kazi chini ya kiwango.
Namna ya tatu inayotumika kuelezea uadilifu wa Dk Magufuli, imeelezwa mara kadhaa na Jaji Joseph Warioba, ambapo alisema mwaka 1996 alipoteuliwa na Rais Benjamin Mkapa kuongoza Tume ya Kero za Rushwa, alikuta sekta ya ujenzi ikinuka rushwa kubwa. Lakini, anafafanua kuwa baada ya Dk Magufuli kuanza kufanya kazi katika sekta hiyo, kelele ya rushwa katika sekta hiyo imetoweka. Uchapakazi Mbali na uadilifu, Dk Magufuli pia anatajwa kuwa mchapakazi.
Hata Rais wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi mara kadhaa amempa jina la ‘simba wa kazi’, huku Rais Jakaya Kikwete anayemaliza muda wake, akimpa jina la ‘tingatinga’ ambalo huwa halishindwi kazi katika mazingira yoyote ya ujenzi, huku wananchi wengine wakimuita ‘jembe’. Matokeo ya uchapakazi wake, yanaonekana katika sekta ya ujenzi, alikofanya kazi kwa miaka 15 tu, ambapo amefanikiwa kusimamia ujenzi wa barabara za lami zenye urefu wa zaidi ya kilometa 17,700.
Kazi hiyo imeweka historia ambayo hata wakoloni, Wajerumani na Waingereza, waliotawala Tanganyika wakati huo tangu mwaka 1884/1885 mpaka wakati wa Uhuru mwaka 1961, zaidi ya miaka 75 walijenga mtandao wa barabara za lami wenye urefu wa kilometa 1,360 tu. Wasifu wake Dk Magufuli alizaliwa Oktoba 29, 1959 Chato (sasa Mkoa wa Geita), hivyo jana alipotangazwa kuwa Rais Mteule wa Awamu ya Tano, ilikuwa siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwake, ambapo alitimiza miaka 56.
Dk Magufuli ana Shahada ya Uzamivu ya Kemia (2006 – 2009) kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Mwaka 1991 – 1994 alisoma Shahada ya Uzamili (Kemia) katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, na baadaye Chuo Kikuu cha Salford nchini Uingereza. Mwaka 1985 – 1988 alisoma Shahada ya Kwanza ya Elimu katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam akichukua masomo ya Kemia na Hisabati. Mwaka 1981 – 1982 alisoma Diploma katika Chuo cha Mkwawa akichukua masomo ya Kemia na Hisabati.
Kati ya mwaka 1979 – 1981 alipata elimu ya juu ya sekondari katika Shule ya Juu ya Sekondari Mkwawa, Iringa. Mwaka 1977 – 1978 alisoma elimu ya sekondari katika Shule ya Sekondari Lake, Mwanza. Mwaka 1975 – 1977 alisema Shule ya Msingi Katoke, Biharamulo mkoani Kagera. Mwaka 1967 – 1974 alisoma Shule ya Msingi, Chato. Machi 1984 – Juni 1984 alihudhuria mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Mpwapwa mkoani Dodoma.
Januari 1984 – Machi 1984 alikuwa JKT Makuyuni, Arusha. Julai 1983 – Desemba 1983 alikuwa JKT Makutupora, Dodoma. Uzoefu wa kazi Kuanzia mwaka 2010 alikuwa Waziri wa Ujenzi na Mbunge wa Chato. Mwaka 2008 – 2010 Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Mbunge wa Biharamulo Mashariki (Chato). Mwaka 2005 – 2008 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; na Mbunge wa Biharamulo Mashariki (Chato).
Mwaka 2000 – 2005 Waziri wa Ujenzi, na Mbunge wa Biharamulo Mashariki. Mwaka 1995 – 2000 Naibu Waziri wa Ujenzi; na Mbunge wa Biharamulo Mashariki. Mwaka 1989 – 1995 Mkemia Chama cha Ushirika cha Nyanza Co-operative Union (Ltd) Mwanza. Mwaka 1982 – 1983 Mwalimu Shule ya Sekondari Sengerema (akifundisha masomo ya Kemia na Hisabati). Amepata tuzo mbalimbali za ndani na nje ya nchi.
Ameshiriki na kuongoza mikutano mingi ya kitaifa na kimataifa. Ameandika vitabu na majarida mbalimbali. Ameoa na ana watoto kadhaa. Mchakato wa urais Dk Magufuli alitangaza rasmi nia yake ya kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwishoni mwa Mei mwaka huu, baada ya CCM kutangaza rasmi ratiba ya mchakato wa urais kwa wanachama wake. Aliingia kwenye harakati za kuwania nafasi ya urais kimya kimya, tofauti na makada wengine wa CCM ambao walihutubia Taifa.
Lakini, kimya chake kiliufanya mchuano wa uchaguzi wa nafasi hiyo ndani ya CCM, uliokuwa na wagombea 42 kuwa mkali zaidi. Baada ya hapo, waliorejesha fomu walikuwa wagombea 38 na kati ya hao baada ya kujadiliwa na vikao vya juu vya Chama, ikiwemo Kamati Kuu, wagombea watano - Dk Magufuli, Bernard Membe, Dk Asha Rose Migiro, Balozi Amina Salum Ally na January Makamba, ndio waliofanikiwa kupelekwa katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM.
Baada ya Nec, ambako wagombea hao walijadiliwa na kupigiwa kura, Dk Magufuli, Balozi Amina na Dk Migiro ndio waliofanikiwa kuingia tatu bora, ambapo walifikishwa katika Mkutano Mkuu na kuomba kura na baada ya kupigiwa kura na wajumbe wa mkutano huo, akapatikana Dk Magufuli kupeperusha bendera ya CCM. Ahadi zake Dk Magufuli katika mikutano yake ya kampeni, alikuwa akiahidi kushusha bei ya vifaa vya ujenzi hasa saruji, mabati na misumari, ili wananchi aliosema atapigania kila mmoja awe na kazi ya kumpa kipato, wajenge nyumba bora.
Katika kuongeza idadi ya Watanzania wanaofanya kazi ili kufikia lengo hilo, Dk Magufuli alisema katika kila mtaa na kijiji, Serikali yake itatoa Sh milioni 50 kwa ajili ya kuanzisha na kukuza biashara ndogo za wanawake na vijana. Mbali na kutoa mikopo hiyo izunguke katika ngazi ya kijiji na mtaa, Dk Magufuli pia alisema Serikali yake itazuia kila aina ya usumbufu, unaofanywa kwa wafanyabiashara hao, ikiwemo kukamatwa kwa bodaboda na mama ntilie.
Kwa wakulima, alisema atahakikisha pembejeo sahihi zinatolewa kwa wakati na mazao yatakayovunwa, itakuwa marufuku kwa Serikali kukopa mazao yao kwa kuwa atahakikisha mbali na wakulima kupata bei nzuri ya mazao yao, watakapoiuzia Serikali itakuwa bidhaa kwa fedha taslimu. Aidha, aliahidi kuondoa ushuru unaosumbua wafanyabiashara wadogo na wakulima, ili wafanye biashara kwa uhuru wajipatie kipato halali.
Dk Magufuli pia alisema baada ya kusambaza umeme, atahakikisha viwanda vidogo, vya kati na vikubwa vinajengwa vijijini ili kusindika mazao ya kilimo shambani ili kutoka shambani bidhaa za mazao hayo ziuzwe katika masoko ya ndani na nje ya nchi. Kuhusu migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji, Dk Magufuli aliahidi kukabiliana na migogoro hiyo, ikiwa ni pamoja na kutoa ardhi zaidi kwaajili ya wakulima na wafugaji, ili kuondoa uhaba wa ardhi uliosababisha ugomvi wa maeneo ya kulishia mifugo na kulima.
Lakini pia aliahidi kunyang’anya mashamba ambayo yamehodhiwa na watu bila kutumiwa, na kuyagawa kwa wakulima na wafugaji wasio na maeneo ya kilimo. Katika elimu, alikuwa akiahidi kuhakikisha kuanzia mwakani, wanafunzi kutoka darasa la awali mpaka kidato cha nne, wanasoma bila kulipa ada, ili kuondolea wazazi usumbufu wa watoto wao kurudishwa nyumbani kwa kukosa ada.
Kwa wanafunzi wa elimu ya juu, aliwahakikishia kuwa hakutakuwa na usumbufu wa kupata mikopo na kuwataka wanahusika na kazi hiyo, kuwa tayari kwa kuwa atataka kila mwenye sifa ya kusoma elimu ya juu, apate mkopo. Katika sekta ya afya, aliahidi kujenga zahanati kwa kila kijiji na mtaa, kituo cha afya kwa kila kata na hospitali ya rufaa katika kila mkoa, na ameahidi kukomesha kero ya kukosekana dawa katika hospitali za Serikali.
Katika kero ya maji, alikuwa akisema kama amefanikiwa kujenga zaidi ya kilometa 17,700 za barabara ya lami, hatashindwa kujenga mabwawa na mtandao wa mabomba kwenda kwa wananchi ili kukomesha kero hiyo.
Pia aliahidi kujenga barabara mbalimbali za lami za kuunganisha wilaya na za mijini, huku akiahidi kuongeza mishahara ya wafanyakazi, ifanane na ya Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), taasisi aliyoianzisha na kuitetea, ambayo leo watu wengi wanatamani kuitumikia kutokana na maslahi mazuri na mafanikio yake.

TANZANIA imeandika historia mpya, ambapo jana imempata Rais Mteule wa Awamu ya Tano, Dk John Pombe Magufuli, ambaye alikuwa mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Uchaguzi Mkuu uliohitimishwa Jumapili ya Oktoba 25, mwaka huu.
Dk Magufuli ambaye katika kampeni ya kuwania urais alikuwa na kauli mbiu ya Hapa Kazi Tu, si mgeni katika safu za uongozi wa Tanzania kwa kuwa amekuwa serikalini kwa miaka 20, akishika majukumu mbalimbali ambayo yalitumiwa na Watanzania kumpima.
Moja ya sifa yake kubwa tangu alipotangaza nia ya kugombea urais kupitia chama hicho mwishoni mwa Mei mwaka huu, ni uadilifu katika utendaji kazi wake katika majukumu tofauti aliyokabidhiwa Rais huyo mteule wa Awamu ya Tano, anatajwa kuwa katika majukumu yote ya kitaifa aliyowahi kukabidhiwa, alionesha sifa ya juu ya uaminifu na uadilifu, ambao umeelezwa kwa namna mbili tofauti.
Ujenzi barabara Kwanza ni uongozi wake wa miradi mikubwa ya fedha nyingi, ambayo kwa muda wote wa uongozi wake hakuwahi kukumbwa na kashfa. Kwa mfano mwaka huu tu, alikuwa akiongoza Wizara ya Ujenzi, iliyokuwa na bajeti ya Sh trilioni 1.2 na Mfuko wa Barabara uliokabidhiwa zaidi ya Sh bilioni 866.
Katika miaka 15 aliyoongoza Wizara hiyo ya Ujenzi, katika ngazi hiyo alisimamia miradi ya zaidi ya Sh trilioni 9.5, lakini hakula hata senti tano, badala yake alijenga mtandao mrefu wa barabara za lami nchi nzima. Usimamizi Namna ya pili ya kuzungumzia uadilifu wake ni usimamizi wake wa watendaji na wadau wa sekta ya ujenzi, ambao amekuwa akiwapa kazi za mabilioni ya shilingi na kuisimamia kwa karibu katika kuwatumikia Watanzania.
Dk Magufuli amekuwa akisimamia makandarasi zaidi ya 8,500, wahandisi zaidi ya 15,000 na wakadiriaji majengo zaidi ya 1,300, ambao wamekuwa wakinufaika na kazi za Serikali za mabilioni ya shilingi.
Kama angetumia vibaya nafasi hiyo na angetaka kumuomba au kushinikiza kila mmoja wao ampe Sh milioni moja tu kwa mwaka, angeweza kujikusanyia pato binafsi lisilo halali la zaidi ya Sh bilioni 100 kila mwaka. Pamoja na kuwa karibu na kishawishi hicho, lakini Dk Magufuli hakushiriki kuhujumu hata senti moja na hana historia wala hakuwahi kutajwa popote kutumia vibaya nafasi yake hiyo katika sekta yenye maslahi makubwa ya kifedha.
Ukali kwa wazembe Badala ya kuomba michango ya kujinufaisha kutoka kwa wadau hao wa ujenzi, Dk Magufuli alijikuta akifukuza kazi makandarasi zaidi ya 3,000 wa ndani na nje ya nchi, bila kujali utajiri wao, pale makandarasi hao walipozembea kazi au kufanya kazi chini ya kiwango.
Namna ya tatu inayotumika kuelezea uadilifu wa Dk Magufuli, imeelezwa mara kadhaa na Jaji Joseph Warioba, ambapo alisema mwaka 1996 alipoteuliwa na Rais Benjamin Mkapa kuongoza Tume ya Kero za Rushwa, alikuta sekta ya ujenzi ikinuka rushwa kubwa. Lakini, anafafanua kuwa baada ya Dk Magufuli kuanza kufanya kazi katika sekta hiyo, kelele ya rushwa katika sekta hiyo imetoweka. Uchapakazi Mbali na uadilifu, Dk Magufuli pia anatajwa kuwa mchapakazi.
Hata Rais wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi mara kadhaa amempa jina la ‘simba wa kazi’, huku Rais Jakaya Kikwete anayemaliza muda wake, akimpa jina la ‘tingatinga’ ambalo huwa halishindwi kazi katika mazingira yoyote ya ujenzi, huku wananchi wengine wakimuita ‘jembe’. Matokeo ya uchapakazi wake, yanaonekana katika sekta ya ujenzi, alikofanya kazi kwa miaka 15 tu, ambapo amefanikiwa kusimamia ujenzi wa barabara za lami zenye urefu wa zaidi ya kilometa 17,700.
Kazi hiyo imeweka historia ambayo hata wakoloni, Wajerumani na Waingereza, waliotawala Tanganyika wakati huo tangu mwaka 1884/1885 mpaka wakati wa Uhuru mwaka 1961, zaidi ya miaka 75 walijenga mtandao wa barabara za lami wenye urefu wa kilometa 1,360 tu. Wasifu wake Dk Magufuli alizaliwa Oktoba 29, 1959 Chato (sasa Mkoa wa Geita), hivyo jana alipotangazwa kuwa Rais Mteule wa Awamu ya Tano, ilikuwa siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwake, ambapo alitimiza miaka 56.
Dk Magufuli ana Shahada ya Uzamivu ya Kemia (2006 – 2009) kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Mwaka 1991 – 1994 alisoma Shahada ya Uzamili (Kemia) katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, na baadaye Chuo Kikuu cha Salford nchini Uingereza. Mwaka 1985 – 1988 alisoma Shahada ya Kwanza ya Elimu katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam akichukua masomo ya Kemia na Hisabati. Mwaka 1981 – 1982 alisoma Diploma katika Chuo cha Mkwawa akichukua masomo ya Kemia na Hisabati.
Kati ya mwaka 1979 – 1981 alipata elimu ya juu ya sekondari katika Shule ya Juu ya Sekondari Mkwawa, Iringa. Mwaka 1977 – 1978 alisoma elimu ya sekondari katika Shule ya Sekondari Lake, Mwanza. Mwaka 1975 – 1977 alisema Shule ya Msingi Katoke, Biharamulo mkoani Kagera. Mwaka 1967 – 1974 alisoma Shule ya Msingi, Chato. Machi 1984 – Juni 1984 alihudhuria mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Mpwapwa mkoani Dodoma.
Januari 1984 – Machi 1984 alikuwa JKT Makuyuni, Arusha. Julai 1983 – Desemba 1983 alikuwa JKT Makutupora, Dodoma. Uzoefu wa kazi Kuanzia mwaka 2010 alikuwa Waziri wa Ujenzi na Mbunge wa Chato. Mwaka 2008 – 2010 Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Mbunge wa Biharamulo Mashariki (Chato). Mwaka 2005 – 2008 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; na Mbunge wa Biharamulo Mashariki (Chato).
Mwaka 2000 – 2005 Waziri wa Ujenzi, na Mbunge wa Biharamulo Mashariki. Mwaka 1995 – 2000 Naibu Waziri wa Ujenzi; na Mbunge wa Biharamulo Mashariki. Mwaka 1989 – 1995 Mkemia Chama cha Ushirika cha Nyanza Co-operative Union (Ltd) Mwanza. Mwaka 1982 – 1983 Mwalimu Shule ya Sekondari Sengerema (akifundisha masomo ya Kemia na Hisabati). Amepata tuzo mbalimbali za ndani na nje ya nchi.
Ameshiriki na kuongoza mikutano mingi ya kitaifa na kimataifa. Ameandika vitabu na majarida mbalimbali. Ameoa na ana watoto kadhaa. Mchakato wa urais Dk Magufuli alitangaza rasmi nia yake ya kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwishoni mwa Mei mwaka huu, baada ya CCM kutangaza rasmi ratiba ya mchakato wa urais kwa wanachama wake. Aliingia kwenye harakati za kuwania nafasi ya urais kimya kimya, tofauti na makada wengine wa CCM ambao walihutubia Taifa.
Lakini, kimya chake kiliufanya mchuano wa uchaguzi wa nafasi hiyo ndani ya CCM, uliokuwa na wagombea 42 kuwa mkali zaidi. Baada ya hapo, waliorejesha fomu walikuwa wagombea 38 na kati ya hao baada ya kujadiliwa na vikao vya juu vya Chama, ikiwemo Kamati Kuu, wagombea watano - Dk Magufuli, Bernard Membe, Dk Asha Rose Migiro, Balozi Amina Salum Ally na January Makamba, ndio waliofanikiwa kupelekwa katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM.
Baada ya Nec, ambako wagombea hao walijadiliwa na kupigiwa kura, Dk Magufuli, Balozi Amina na Dk Migiro ndio waliofanikiwa kuingia tatu bora, ambapo walifikishwa katika Mkutano Mkuu na kuomba kura na baada ya kupigiwa kura na wajumbe wa mkutano huo, akapatikana Dk Magufuli kupeperusha bendera ya CCM. Ahadi zake Dk Magufuli katika mikutano yake ya kampeni, alikuwa akiahidi kushusha bei ya vifaa vya ujenzi hasa saruji, mabati na misumari, ili wananchi aliosema atapigania kila mmoja awe na kazi ya kumpa kipato, wajenge nyumba bora.
Katika kuongeza idadi ya Watanzania wanaofanya kazi ili kufikia lengo hilo, Dk Magufuli alisema katika kila mtaa na kijiji, Serikali yake itatoa Sh milioni 50 kwa ajili ya kuanzisha na kukuza biashara ndogo za wanawake na vijana. Mbali na kutoa mikopo hiyo izunguke katika ngazi ya kijiji na mtaa, Dk Magufuli pia alisema Serikali yake itazuia kila aina ya usumbufu, unaofanywa kwa wafanyabiashara hao, ikiwemo kukamatwa kwa bodaboda na mama ntilie.
Kwa wakulima, alisema atahakikisha pembejeo sahihi zinatolewa kwa wakati na mazao yatakayovunwa, itakuwa marufuku kwa Serikali kukopa mazao yao kwa kuwa atahakikisha mbali na wakulima kupata bei nzuri ya mazao yao, watakapoiuzia Serikali itakuwa bidhaa kwa fedha taslimu. Aidha, aliahidi kuondoa ushuru unaosumbua wafanyabiashara wadogo na wakulima, ili wafanye biashara kwa uhuru wajipatie kipato halali.
Dk Magufuli pia alisema baada ya kusambaza umeme, atahakikisha viwanda vidogo, vya kati na vikubwa vinajengwa vijijini ili kusindika mazao ya kilimo shambani ili kutoka shambani bidhaa za mazao hayo ziuzwe katika masoko ya ndani na nje ya nchi. Kuhusu migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji, Dk Magufuli aliahidi kukabiliana na migogoro hiyo, ikiwa ni pamoja na kutoa ardhi zaidi kwaajili ya wakulima na wafugaji, ili kuondoa uhaba wa ardhi uliosababisha ugomvi wa maeneo ya kulishia mifugo na kulima.
Lakini pia aliahidi kunyang’anya mashamba ambayo yamehodhiwa na watu bila kutumiwa, na kuyagawa kwa wakulima na wafugaji wasio na maeneo ya kilimo. Katika elimu, alikuwa akiahidi kuhakikisha kuanzia mwakani, wanafunzi kutoka darasa la awali mpaka kidato cha nne, wanasoma bila kulipa ada, ili kuondolea wazazi usumbufu wa watoto wao kurudishwa nyumbani kwa kukosa ada.
Kwa wanafunzi wa elimu ya juu, aliwahakikishia kuwa hakutakuwa na usumbufu wa kupata mikopo na kuwataka wanahusika na kazi hiyo, kuwa tayari kwa kuwa atataka kila mwenye sifa ya kusoma elimu ya juu, apate mkopo. Katika sekta ya afya, aliahidi kujenga zahanati kwa kila kijiji na mtaa, kituo cha afya kwa kila kata na hospitali ya rufaa katika kila mkoa, na ameahidi kukomesha kero ya kukosekana dawa katika hospitali za Serikali.
Katika kero ya maji, alikuwa akisema kama amefanikiwa kujenga zaidi ya kilometa 17,700 za barabara ya lami, hatashindwa kujenga mabwawa na mtandao wa mabomba kwenda kwa wananchi ili kukomesha kero hiyo.
Pia aliahidi kujenga barabara mbalimbali za lami za kuunganisha wilaya na za mijini, huku akiahidi kuongeza mishahara ya wafanyakazi, ifanane na ya Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), taasisi aliyoianzisha na kuitetea, ambayo leo watu wengi wanatamani kuitumikia kutokana na maslahi mazuri na mafanikio yake.

Tuesday, 27 October 2015

WAKATI wakisubiri matokeo ya uchaguzi ya rais huku Tume ya Uchaguzi ikitangaza kura za wagombea wabunge na uwakilishi katika majimbo ya uchaguzi Zanzibar, Jeshi la Polisi limelazimika kuzima fujo na vurugu kutoka kwa wafuasi wa CUF waliotanda mitaa ya Mji Mkongwe na barabara kuu ya Darajani.
Vurugu zimezuka baada ya mgombea wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad kufanya tathmini na kutangaza matokeo ya ushindi wa chama chake katika uchaguzi wa juzi kwa asilimia 52.87. Maalim Seif alitoa tathmini hiyo mbele ya waandishi wa habari katika Ofisi Kuu ya CUF Mtendeni mjini Unguja na kuitaka Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kutangaza matokeo hayo.
Katika tathmini hiyo inaonesha kwamba mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kwa tiketi ya urais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein amepata ushindi kwa asilimia 47.13. Maalim Seif alidai matokeo waliyonayo yamekusanywa na mawakala waliopo katika vituo vya uchaguzi vilivyopo Unguja na Pemba kwa kufanya majumuisho. Hatua hiyo ilizusha shangwe na furaha kwa wafuasi wa CUF na kuanza kutembea barabarani huku gari zikipiga honi.
Baadhi ya mitaa ikiwemo Darajani na Mlandege, polisi waliweka vizuizi ambavyo vilisaidia kuwazuia wafuasi hao kuingia barabarani. Aidha, ofisi za Serikali zilizopo katika eneo la Mji Mkongwe pamoja na taasisi za kibenki, zilifungwa baada ya kuibuka kwa mazingira ya fujo na vurugu.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Mkadam Khamis Mkadam alithibitisha Jeshi la Polisi kudhibiti maeneo mbalimbali zaidi yaliyopo Mji Mkongwe pamoja na eneo la Darajani ambalo ni ngome ya upinzani.
“Tumefanikiwa kudhibiti vurugu za watu waliofanya fujo na vurugu katika maeneo mbali mbali ya mji wa Unguja na hali ni shwari kwa sasa,” alisema Mkadam. Kwa mujibu wa Sheria na Kanuni za Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ni kosa la jinai kwa mtu yeyote au mgombea wa chama cha siasa kutangaza matokeo ya urais. Mapema, CCM Zanzibar ililaani kitendo kilichofanywa na Maalim Seif kujitangazia ushindi katika uchaguzi huo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai alisema kitendo hicho ni sehemu ya vitendo na matukio ya uchochezi yanayotakiwa kudhibitiwa kwa ajili ya kuimarisha amani na utulivu. Vuai aliitaka ZEC kuchukua hatua za kisheria na kinidhamu kwa mgombea huyo kwa kauli zake ambazo lengo lake kuingiza nchi katika machafuko katika kipindi hiki kigumu cha uchaguzi.
Hata hivyo, viongozi watendaji wa ZEC hawakuwa tayari kulizungumzia suala hilo, ambapo maofisa wote walikuwa wapo katika mchakato wa kupokea na kutangaza matokeo ya uchaguzi wa majimbo.

WAKATI wakisubiri matokeo ya uchaguzi ya rais huku Tume ya Uchaguzi ikitangaza kura za wagombea wabunge na uwakilishi katika majimbo ya uchaguzi Zanzibar, Jeshi la Polisi limelazimika kuzima fujo na vurugu kutoka kwa wafuasi wa CUF waliotanda mitaa ya Mji Mkongwe na barabara kuu ya Darajani.
Vurugu zimezuka baada ya mgombea wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad kufanya tathmini na kutangaza matokeo ya ushindi wa chama chake katika uchaguzi wa juzi kwa asilimia 52.87. Maalim Seif alitoa tathmini hiyo mbele ya waandishi wa habari katika Ofisi Kuu ya CUF Mtendeni mjini Unguja na kuitaka Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kutangaza matokeo hayo.
Katika tathmini hiyo inaonesha kwamba mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kwa tiketi ya urais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein amepata ushindi kwa asilimia 47.13. Maalim Seif alidai matokeo waliyonayo yamekusanywa na mawakala waliopo katika vituo vya uchaguzi vilivyopo Unguja na Pemba kwa kufanya majumuisho. Hatua hiyo ilizusha shangwe na furaha kwa wafuasi wa CUF na kuanza kutembea barabarani huku gari zikipiga honi.
Baadhi ya mitaa ikiwemo Darajani na Mlandege, polisi waliweka vizuizi ambavyo vilisaidia kuwazuia wafuasi hao kuingia barabarani. Aidha, ofisi za Serikali zilizopo katika eneo la Mji Mkongwe pamoja na taasisi za kibenki, zilifungwa baada ya kuibuka kwa mazingira ya fujo na vurugu.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Mkadam Khamis Mkadam alithibitisha Jeshi la Polisi kudhibiti maeneo mbalimbali zaidi yaliyopo Mji Mkongwe pamoja na eneo la Darajani ambalo ni ngome ya upinzani.
“Tumefanikiwa kudhibiti vurugu za watu waliofanya fujo na vurugu katika maeneo mbali mbali ya mji wa Unguja na hali ni shwari kwa sasa,” alisema Mkadam. Kwa mujibu wa Sheria na Kanuni za Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ni kosa la jinai kwa mtu yeyote au mgombea wa chama cha siasa kutangaza matokeo ya urais. Mapema, CCM Zanzibar ililaani kitendo kilichofanywa na Maalim Seif kujitangazia ushindi katika uchaguzi huo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai alisema kitendo hicho ni sehemu ya vitendo na matukio ya uchochezi yanayotakiwa kudhibitiwa kwa ajili ya kuimarisha amani na utulivu. Vuai aliitaka ZEC kuchukua hatua za kisheria na kinidhamu kwa mgombea huyo kwa kauli zake ambazo lengo lake kuingiza nchi katika machafuko katika kipindi hiki kigumu cha uchaguzi.
Hata hivyo, viongozi watendaji wa ZEC hawakuwa tayari kulizungumzia suala hilo, ambapo maofisa wote walikuwa wapo katika mchakato wa kupokea na kutangaza matokeo ya uchaguzi wa majimbo.



Muaniaji kiti cha urais wa chama cha Republican nchini Marekani, Donald Trump, amesema kuwa dunia ingekuwa mahala salama zaidi kama tu Saddam Hussein wa Iraq na Maummar Gaddafi wa Libya wangelikuwa hai.
Bwenyenye huyo mbishi aliyasema hayo katika mahojiano na CNN baada ya kukashifu sera za kidiplomasia za rais Barrack Obama.
 
Trump alisema kuwa maafa yanayoendelea Mashariki ya Kati yalichangiwa asili mia mia moja na sera haribifu za rais Obama na bi Hillary Clinton.
''Japo tunamlaumu Maummar Gaddafi unadhani angekuwa hai magaidi wangekuwa huko ?La.'
'Angalia kwa makini hakuna Libya.'
'Libya tuliyoijua sasa imesambaratika kabisa'.
'Saddam Hussein alikuwa mtawala wa kiimla na tulijua kuwa hangeliwaruhusu magaidi kunawiri huko Iraq.'



Sasa Iraq ndio Havard ama chuo kikuu zaidi cha ugaidi duniani.
'Kama ni maswala ya ukiukaji wa haki za kibinadamu.'
'Kwa hakika hali ilivyo sasa ni mbaya zaidi kuliko tulivyodhania wakati huo.'
Bwenyenye huyo anayetarajiwa kutwaa tikiti ya kuwania urais ya chama hicho cha Republican amesema kuwa anapania kuimarisha hadhi ya Marekani.



Muaniaji kiti cha urais wa chama cha Republican nchini Marekani, Donald Trump, amesema kuwa dunia ingekuwa mahala salama zaidi kama tu Saddam Hussein wa Iraq na Maummar Gaddafi wa Libya wangelikuwa hai.
Bwenyenye huyo mbishi aliyasema hayo katika mahojiano na CNN baada ya kukashifu sera za kidiplomasia za rais Barrack Obama.
 
Trump alisema kuwa maafa yanayoendelea Mashariki ya Kati yalichangiwa asili mia mia moja na sera haribifu za rais Obama na bi Hillary Clinton.
''Japo tunamlaumu Maummar Gaddafi unadhani angekuwa hai magaidi wangekuwa huko ?La.'
'Angalia kwa makini hakuna Libya.'
'Libya tuliyoijua sasa imesambaratika kabisa'.
'Saddam Hussein alikuwa mtawala wa kiimla na tulijua kuwa hangeliwaruhusu magaidi kunawiri huko Iraq.'



Sasa Iraq ndio Havard ama chuo kikuu zaidi cha ugaidi duniani.
'Kama ni maswala ya ukiukaji wa haki za kibinadamu.'
'Kwa hakika hali ilivyo sasa ni mbaya zaidi kuliko tulivyodhania wakati huo.'
Bwenyenye huyo anayetarajiwa kutwaa tikiti ya kuwania urais ya chama hicho cha Republican amesema kuwa anapania kuimarisha hadhi ya Marekani.

Nahodha Mussa Hassan ‘Mgosi’ alisema tatizo la Simba wanaipima timu yao kwa mafanikio ya Yanga na hasa kuwa kwao kileleni, lakini wanashindwa kujua wapinzani wao wameshinda mechi zao wakiwa kwenye viwanja vipi.

Nahodha Mussa Hassan ‘Mgosi’ alisema tatizo la Simba wanaipima timu yao kwa mafanikio ya Yanga na hasa kuwa kwao kileleni, lakini wanashindwa kujua wapinzani wao wameshinda mechi zao wakiwa kwenye viwanja vipi.

johnTUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imetangaza matokeo ya awali ya urais kwa majimbo 26, yakionyesha mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli anaongoza akifuatiwa na Mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa.
Matokeo hayo yalitangazwa jijini Dar es Salaam jana kwa nyakati tofauti na Mwenyekiti wa NEC, Jaji Damian Lubuva kutoka kituo kikuu cha kutangazia matokeo kilichopo katika ukumbi wa mikutano wa Mwalimu Nyerere.
MAKUNDUCHI
Akitangaza matokeo ya Jimbo la Makunduchi lililoko Zanzibar, Jaji Lubuva alisema Dk. Magufuli alipata kura 8,406 sawa na asilimia 81.20 akifuatiwa na mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa, aliyepata kura 1,769 sawa na asilimia 17.9.
Katika jimbo hilo, alisema waliojiandikisha walikuwa ni 12,742 na waliojitokeza kupiga kura walikuwa 10,682 sawa na asilimia 81.24.
Aliwataja wagombea wengine waliofuatia na kura zao kwenye mabano kuwa ni Hashim Rungwe – Chaumma (68), Lutalosa Yemba – ADC (58), Kasambala Marick -NRA (23) Anna Mghwira – ACT-Wazalendo (22), Macmilan Lyimo -TLP (18) na Fahmi Dovutwa – UPDP (18).

PAJE
Kwa upande wa Jimbo la Paje, Jaji Lubuva alisema Dk. Magufuli alipata kura 6,035 sawa na asilimia 81.20, Lowasa kura 1,899 sawa na asilimia 23.60 na kufuatiwa na ACT kwa kura 36.
Chaumma walipata 28, ADC kura 21, TLP na NRA kila moja kura nane na UPDP kura 7.

LULINDI
Katika Jimbo la Lulindi, Dk. Magufuli alipata kura 31,603 sawa na asilimia 71.28 na Lowassa kura 11,543 sawa na asilimia 26.03 ya kura zote halali.
Wengine ni Mghwira aliyepata kura 528, Lutalosa Yemba kura 362, Rungwe kura 179, Kasambala kura 43, Lyimo kura 45 na Dovutwa kura 34.

CHAMBANI
Jimbo la Chambani, Lowassa ameongoza kwa kupata kura 5,319 sawa na asimilia 83.90 akifuatiwa na Dk. Magufuli aliyepata kura 818 sawa na asilimia 12.90.
Rungwe alipata kura 63, Chief Yemba kura 50, Dovutwa kura 36, Kasambala kura 20, Lyimo kura 19 na Mghwira kura 15.

KIWANI
Lowassa ameongoza kwa kupata kura 4,229 sawa na asilimia 68.51 akifuatiwa na Dk. Magufuli kura 1,661 sawa na asilimia 12.9.
Mgombea wa Chaumma alipata kura 96, ADC kura 71 UPDP kura 39, NRA kura 28, ACT kura 27 na TLP kura 22.

NSIMBO
Dk. Magufuli ameongoza kwa kupata kura 31,413, Lowassa kura 6,042, mgombea wa ACT kura 183, ADC kura 64, Chaumma kura 42, UPDP kura 15, TLP kura 14 na NRA kura 6.

NDANDA
Katika jimbo hilo, Dl. Magufuli alipata kura 33,699, Lowassa kura 19,017, mgombea wa ACT- Wazalendo kura 594, ADC kura 409, Chaumma kura 189, UPDP kura 49 na TLP kura 49.

DONGE
Dk. Magufuli alipata kura 5,592, Lowassa kura 1,019, mgombea wa Chaumma kura 23, ADC kura 22, NRA kura 10, UPDP kura 7, ACT kura 5 na TLP kura 4.

KIWENGWA
Mgombea wa CCM, Dk. Magufuli alipata kura 3,317, Lowassa kura 1,104, Chaumma kura 27, ADC kura 24, TLP kura 19, ACT kura 15, UPDP kura 10 na NRA kura 9.

BUMBULI
Dk. Magufuli alipata kura 35,310, Lowassa kura 7,928, mgombea wa ACT kura 447, ADC kura 188, UPDP kura 25, NRA kura 15 na TLP kura 13.

KIBAHA MJINI
Mgombea wa CCM, Dk. Magufuli alipata kura 34,604, Lowassa kura 25,448, ACT kura 314, Chaumma kura 77, ADC kura 59, TLP kura 17, NRA kura 15 na UPDP kura 11.

MKOANI
Lowassa ameongoza kwa kupata kura 7,368, akifuatiwa na Dk. Magufuli kura 3,341, Chaumma kura 87, ADC kura 60, NRA kura 44, TLP kura 33, UPDP kura 27 na ACT kura 20.

MTAMBILE
Latika jimbo hili, mgombea wa Chadema, Lowassa amepata kura 5,875, Dk. Magufuli kura 902, Chaumma kura 56, ADC kura 41, UPDP kura 25, NRA kura 22, TLP kura 18 na ACT kura 7.
GANDO
Mgombea wa Chadema alipata kura 5,903, CCM kura 881, ACT kura 11, ADC kura 23, Chaumma kura 49, NRA kura 14, TLP 11 na UPDP 25.
MTAMBILE
Mgombea wa Chadema alipata kura 6,903, CCM kura 428, ACT kura 9, ADC kura 28, Chaumma kura 58, NRA kura12 , TLP 21 na UPDP 37.
MGOGONI
Mgombea wa CCM alipata kura 710, Chadema kura 6,506, ACT kura 12 , ADC kura 31, Chaumma kura  45, NRA kura 12, TLP  8 na UPDP 37.
KISARAWE
Mgombea wa CCM alipata kura 24,886, Chadema kura 13,093,  ACT kura235 , ADC kura 19 , Chaumma kura 314, NRA kura 26, TLP kura 22 na UPDP kura 46.
MBINGA MJINI
Mgombea wa CCM alipata kura 29,225, Chadema kura 11,665,  ACT kura 329, ADC kura 131 , Chaumma kura 66, NRA kura 10, TLP 16 na UPDP 16.
NANYAMBA
Mgombea wa CCM alipata kura 24904, Chadema kura 16992,  ACT kura 361 , ADC kura 202 , Chaumma kura 172, NRA kura 39, TLP 48 na UPDP 64.
MOSHI MJINI
Mgombea wa CCM alipata kura 28,909, Chadema kura 49,379,  ACT kura 149, ADC 186 , Chaumma kura 1,154, NRA kura 8, TLP 7 na UPDP kura 6.
MKINGA
Mgombea wa CCM alipata kura 23,798, Chadema kura 11,291, ACT kura 228, ADC kura 186, Chaumma kura 351 , NRA kura 31, TLP 29 na UPDP 27.
PERAMIHO
Mgombea wa CCM kura 32,505, Chadema kura11,291, ACT kura 359, ADC kura  135, Chaumma kura 66, NRA kura 16, TLP 15 na UPDP 22.
NJOMBE MJINI
Mgombea wa CCM alipata kura 33,626, Chadema kura 20,368,  ACT kura 362, ADC kura111 , Chaumma kura 78, NRA kura 14, TLP 21 na UPDP 17.
SINGIDA MJINI
Mgombea wa CCM alipata kura 36,035, Chadema kura 19,007, ACT kura 235, ADC kura 87, Chaumma kura 64 , NRA kura 10, TLP kura 12 na UPDP kura 7.
LINDI MJINI
Mgombea wa CCM alipata kura 21,088, Chadema kura 17,607, ACT kura 123, ADC kura 103 , Chaumma kura 67, NRA kura 11, TLP 6 na UPDP kura 13.
WETE
Mgombea wa CCM alipata kura 958, Chadema kura 5,119,  ACT kura 18, ADC kura 22 , Chaumma kura 28, NRA kura 15, TLP 16 na UPDP kura 10.

johnTUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imetangaza matokeo ya awali ya urais kwa majimbo 26, yakionyesha mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli anaongoza akifuatiwa na Mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa.
Matokeo hayo yalitangazwa jijini Dar es Salaam jana kwa nyakati tofauti na Mwenyekiti wa NEC, Jaji Damian Lubuva kutoka kituo kikuu cha kutangazia matokeo kilichopo katika ukumbi wa mikutano wa Mwalimu Nyerere.
MAKUNDUCHI
Akitangaza matokeo ya Jimbo la Makunduchi lililoko Zanzibar, Jaji Lubuva alisema Dk. Magufuli alipata kura 8,406 sawa na asilimia 81.20 akifuatiwa na mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa, aliyepata kura 1,769 sawa na asilimia 17.9.
Katika jimbo hilo, alisema waliojiandikisha walikuwa ni 12,742 na waliojitokeza kupiga kura walikuwa 10,682 sawa na asilimia 81.24.
Aliwataja wagombea wengine waliofuatia na kura zao kwenye mabano kuwa ni Hashim Rungwe – Chaumma (68), Lutalosa Yemba – ADC (58), Kasambala Marick -NRA (23) Anna Mghwira – ACT-Wazalendo (22), Macmilan Lyimo -TLP (18) na Fahmi Dovutwa – UPDP (18).

PAJE
Kwa upande wa Jimbo la Paje, Jaji Lubuva alisema Dk. Magufuli alipata kura 6,035 sawa na asilimia 81.20, Lowasa kura 1,899 sawa na asilimia 23.60 na kufuatiwa na ACT kwa kura 36.
Chaumma walipata 28, ADC kura 21, TLP na NRA kila moja kura nane na UPDP kura 7.

LULINDI
Katika Jimbo la Lulindi, Dk. Magufuli alipata kura 31,603 sawa na asilimia 71.28 na Lowassa kura 11,543 sawa na asilimia 26.03 ya kura zote halali.
Wengine ni Mghwira aliyepata kura 528, Lutalosa Yemba kura 362, Rungwe kura 179, Kasambala kura 43, Lyimo kura 45 na Dovutwa kura 34.

CHAMBANI
Jimbo la Chambani, Lowassa ameongoza kwa kupata kura 5,319 sawa na asimilia 83.90 akifuatiwa na Dk. Magufuli aliyepata kura 818 sawa na asilimia 12.90.
Rungwe alipata kura 63, Chief Yemba kura 50, Dovutwa kura 36, Kasambala kura 20, Lyimo kura 19 na Mghwira kura 15.

KIWANI
Lowassa ameongoza kwa kupata kura 4,229 sawa na asilimia 68.51 akifuatiwa na Dk. Magufuli kura 1,661 sawa na asilimia 12.9.
Mgombea wa Chaumma alipata kura 96, ADC kura 71 UPDP kura 39, NRA kura 28, ACT kura 27 na TLP kura 22.

NSIMBO
Dk. Magufuli ameongoza kwa kupata kura 31,413, Lowassa kura 6,042, mgombea wa ACT kura 183, ADC kura 64, Chaumma kura 42, UPDP kura 15, TLP kura 14 na NRA kura 6.

NDANDA
Katika jimbo hilo, Dl. Magufuli alipata kura 33,699, Lowassa kura 19,017, mgombea wa ACT- Wazalendo kura 594, ADC kura 409, Chaumma kura 189, UPDP kura 49 na TLP kura 49.

DONGE
Dk. Magufuli alipata kura 5,592, Lowassa kura 1,019, mgombea wa Chaumma kura 23, ADC kura 22, NRA kura 10, UPDP kura 7, ACT kura 5 na TLP kura 4.

KIWENGWA
Mgombea wa CCM, Dk. Magufuli alipata kura 3,317, Lowassa kura 1,104, Chaumma kura 27, ADC kura 24, TLP kura 19, ACT kura 15, UPDP kura 10 na NRA kura 9.

BUMBULI
Dk. Magufuli alipata kura 35,310, Lowassa kura 7,928, mgombea wa ACT kura 447, ADC kura 188, UPDP kura 25, NRA kura 15 na TLP kura 13.

KIBAHA MJINI
Mgombea wa CCM, Dk. Magufuli alipata kura 34,604, Lowassa kura 25,448, ACT kura 314, Chaumma kura 77, ADC kura 59, TLP kura 17, NRA kura 15 na UPDP kura 11.

MKOANI
Lowassa ameongoza kwa kupata kura 7,368, akifuatiwa na Dk. Magufuli kura 3,341, Chaumma kura 87, ADC kura 60, NRA kura 44, TLP kura 33, UPDP kura 27 na ACT kura 20.

MTAMBILE
Latika jimbo hili, mgombea wa Chadema, Lowassa amepata kura 5,875, Dk. Magufuli kura 902, Chaumma kura 56, ADC kura 41, UPDP kura 25, NRA kura 22, TLP kura 18 na ACT kura 7.
GANDO
Mgombea wa Chadema alipata kura 5,903, CCM kura 881, ACT kura 11, ADC kura 23, Chaumma kura 49, NRA kura 14, TLP 11 na UPDP 25.
MTAMBILE
Mgombea wa Chadema alipata kura 6,903, CCM kura 428, ACT kura 9, ADC kura 28, Chaumma kura 58, NRA kura12 , TLP 21 na UPDP 37.
MGOGONI
Mgombea wa CCM alipata kura 710, Chadema kura 6,506, ACT kura 12 , ADC kura 31, Chaumma kura  45, NRA kura 12, TLP  8 na UPDP 37.
KISARAWE
Mgombea wa CCM alipata kura 24,886, Chadema kura 13,093,  ACT kura235 , ADC kura 19 , Chaumma kura 314, NRA kura 26, TLP kura 22 na UPDP kura 46.
MBINGA MJINI
Mgombea wa CCM alipata kura 29,225, Chadema kura 11,665,  ACT kura 329, ADC kura 131 , Chaumma kura 66, NRA kura 10, TLP 16 na UPDP 16.
NANYAMBA
Mgombea wa CCM alipata kura 24904, Chadema kura 16992,  ACT kura 361 , ADC kura 202 , Chaumma kura 172, NRA kura 39, TLP 48 na UPDP 64.
MOSHI MJINI
Mgombea wa CCM alipata kura 28,909, Chadema kura 49,379,  ACT kura 149, ADC 186 , Chaumma kura 1,154, NRA kura 8, TLP 7 na UPDP kura 6.
MKINGA
Mgombea wa CCM alipata kura 23,798, Chadema kura 11,291, ACT kura 228, ADC kura 186, Chaumma kura 351 , NRA kura 31, TLP 29 na UPDP 27.
PERAMIHO
Mgombea wa CCM kura 32,505, Chadema kura11,291, ACT kura 359, ADC kura  135, Chaumma kura 66, NRA kura 16, TLP 15 na UPDP 22.
NJOMBE MJINI
Mgombea wa CCM alipata kura 33,626, Chadema kura 20,368,  ACT kura 362, ADC kura111 , Chaumma kura 78, NRA kura 14, TLP 21 na UPDP 17.
SINGIDA MJINI
Mgombea wa CCM alipata kura 36,035, Chadema kura 19,007, ACT kura 235, ADC kura 87, Chaumma kura 64 , NRA kura 10, TLP kura 12 na UPDP kura 7.
LINDI MJINI
Mgombea wa CCM alipata kura 21,088, Chadema kura 17,607, ACT kura 123, ADC kura 103 , Chaumma kura 67, NRA kura 11, TLP 6 na UPDP kura 13.
WETE
Mgombea wa CCM alipata kura 958, Chadema kura 5,119,  ACT kura 18, ADC kura 22 , Chaumma kura 28, NRA kura 15, TLP 16 na UPDP kura 10.

Tazama mikoa ambayo CCM ameitesa UKAWA. Waswahili wanasema ni shiiidah

Tazama mikoa ambayo CCM ameitesa UKAWA. Waswahili wanasema ni shiiidah

Wednesday, 16 September 2015

MGOMBEA wa urais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kupitia Chadema, Edward Lowassa, amesema haitoshi kwa watu kuendelea kufurika katika mikutano yake pasipo kutia nia ya kumpigia kura ili aweze kuwa Rais wa Serikali ya Awamu ya Tano.
Lowassa anayeungwa mkono na vyama vingine vitatu vya CUF, NCCR- Mageuzi na NLD, alisema umati wa watu wanaojitokeza kumsikiliza kila mahali ikiwemo Morogoro Mjini hakutoshi iwapo hawataweza kumpigia kura nyingi za kuingia madarakani Oktoba 25, mwaka huu.
Lowassa aliyekuwa Waziri Mkuu wa kwanza katika Serikali ya Awamu ya Nne na kulazimika kuachia madaraka mapema mwaka 2008, alihutubia takribani kwa dakika kumi na baadaye kuwakaribisha na kuwatambulisha wagombea wa ubunge wa Jimbo la Morogoro Mjini na madiwani wa Kata mbalimbali ili kuwaombea kura kwa wananchi.
Alianza ziara yake kwa kuwahutubia wananchi wa kata ya Dumila, Turiani na kuwasili mjini Morogoro jioni ya saa kumi akiambatana na aliyekuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Tatu, Frederick Sumaye ambaye kama Lowassa, amejiengua CCM baada ya kukataliwa kuwania urais kwa tiketi ya chama hicho tawala.
Akihubutia katika mkutano huo uliofanyika katika uwanja wa Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege, Manispaa ya Morogoro, alisema mahudhurio hayo na kumshangilia huko kwa wingi kuonekane pia katika sanduku la kura.
Pia alitumia muda huo kuelezea azma yake endapo wananchi watamchagua kuwa Rais wa Tanzania, ataangalia namna ya kufufua viwanda vya Morogoro na ikiwezekana kuanzisha vipya ili kuwezesha upatikanaji wa ajira na kuuza bidhaa ghafi nje badala ya kuuza malighafi kama ilivyo kwa sasa.
Alisema, si dhambi viwanda kuendeshwa na serikali kwa kuwa jambo hilo linafanyika hata katika nchi nyingine za Ulaya na kutolea mfano Ufaransa ambako baadhi ya viwanda na mabenki yanamilikiwa na serikali.
Hivyo aliwataka wananchi kuwapigia kura wagombea wa Chadema kwa nafasi ya udiwani, ubunge ili aweza kupata timu atakayofanya nayo kazi endapo atachaguliwa kuwa rais.
Pamoja na hayo, alisema serikali yake atakayoiunda itakuwa rafiki wa mama lishe, bodaboda na wamachinga na kwamba ataanzisha benki itakayoshughulikia makundi hayo.
Pia alisema serikali yake itasimamia uboreshaji wa elimu, maslahi ya walimu na kutoa elimu bure kuanzia darasa la kwanza hadi chuo kikuu na kwamba endapo ataingia madarakani wanafunzi wote watasomba bure bila kulipa michango.

MGOMBEA wa urais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kupitia Chadema, Edward Lowassa, amesema haitoshi kwa watu kuendelea kufurika katika mikutano yake pasipo kutia nia ya kumpigia kura ili aweze kuwa Rais wa Serikali ya Awamu ya Tano.
Lowassa anayeungwa mkono na vyama vingine vitatu vya CUF, NCCR- Mageuzi na NLD, alisema umati wa watu wanaojitokeza kumsikiliza kila mahali ikiwemo Morogoro Mjini hakutoshi iwapo hawataweza kumpigia kura nyingi za kuingia madarakani Oktoba 25, mwaka huu.
Lowassa aliyekuwa Waziri Mkuu wa kwanza katika Serikali ya Awamu ya Nne na kulazimika kuachia madaraka mapema mwaka 2008, alihutubia takribani kwa dakika kumi na baadaye kuwakaribisha na kuwatambulisha wagombea wa ubunge wa Jimbo la Morogoro Mjini na madiwani wa Kata mbalimbali ili kuwaombea kura kwa wananchi.
Alianza ziara yake kwa kuwahutubia wananchi wa kata ya Dumila, Turiani na kuwasili mjini Morogoro jioni ya saa kumi akiambatana na aliyekuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Tatu, Frederick Sumaye ambaye kama Lowassa, amejiengua CCM baada ya kukataliwa kuwania urais kwa tiketi ya chama hicho tawala.
Akihubutia katika mkutano huo uliofanyika katika uwanja wa Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege, Manispaa ya Morogoro, alisema mahudhurio hayo na kumshangilia huko kwa wingi kuonekane pia katika sanduku la kura.
Pia alitumia muda huo kuelezea azma yake endapo wananchi watamchagua kuwa Rais wa Tanzania, ataangalia namna ya kufufua viwanda vya Morogoro na ikiwezekana kuanzisha vipya ili kuwezesha upatikanaji wa ajira na kuuza bidhaa ghafi nje badala ya kuuza malighafi kama ilivyo kwa sasa.
Alisema, si dhambi viwanda kuendeshwa na serikali kwa kuwa jambo hilo linafanyika hata katika nchi nyingine za Ulaya na kutolea mfano Ufaransa ambako baadhi ya viwanda na mabenki yanamilikiwa na serikali.
Hivyo aliwataka wananchi kuwapigia kura wagombea wa Chadema kwa nafasi ya udiwani, ubunge ili aweza kupata timu atakayofanya nayo kazi endapo atachaguliwa kuwa rais.
Pamoja na hayo, alisema serikali yake atakayoiunda itakuwa rafiki wa mama lishe, bodaboda na wamachinga na kwamba ataanzisha benki itakayoshughulikia makundi hayo.
Pia alisema serikali yake itasimamia uboreshaji wa elimu, maslahi ya walimu na kutoa elimu bure kuanzia darasa la kwanza hadi chuo kikuu na kwamba endapo ataingia madarakani wanafunzi wote watasomba bure bila kulipa michango.

Saturday, 5 September 2015

Mgombea Urais wa CC, Dk John Magufuli akihutubia wananchi wa Morogoro.MGOMBEA urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk John Magufuli ameahidi kunyang’any’a mashamba ambayo yamehodhiwa na watu bila kutumiwa kwa ufugaji wala kilimo, na kuyagawa kwa wakulima na wafugaji wasio na maeneo ya kilimo. Alisema hayo alipozungumza na wananchi wa wilaya za Ulanga na Kilombero mkoani Morogoro jana.
Dk Magufuli alisema akiwa rais, kuna mambo mengi anaweza kufanya, kukabiliana na migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji na mojawapo ni kutoa ardhi zaidi kwaajili ya wakulima na wafugaji, ili kuondoa uhaba wa ardhi, unaosababisha ugomvi wa maeneo ya kulishia mifugo na kulima.
Alisema kuna watu wanamiliki maelfu ya eka za ardhi bila kulima na kwamba atanyang’any’a mashamba hayo ambayo yamehodhiwa na watu hao bila kutumiwa kwa ufugaji wala kilimo. Akihutubia maelfu ya wananchi, pia Dk Magufuli alisema kuwa anajivunia uzoefu wa marais wastaafu wa Awamu ya Pili mpaka Awamu ya Nne na wa Zanzibar, kwamba ndio atakaowafuata kwa ushauri akikwama popote.
Alisema hiyo ni moja ya tofauti kubwa kati yake na wagombea wengine wa urais. “Nitaingia Ikulu nikiwa na washauri wazuri, nikikwama mahali nitakwenda kwa Rais Jakaya Kikwete, nikikwama nitaenda kwa mzee Benjamin Mkapa, nikikwama tena nakwenda kwa mzee Ali Hasan Mwinyi.
“Wako wengi, upo ushauri nitauchukua kutoka kwa mzee Salmin Amour (Rais Mstaafu wa Zanzibar), Dk Ali Mohamed Shein na kwa Amani Abeid Karume,” alisema. Kutokana na fursa hiyo ya kiuongozi aliyonayo ndani ya Chama Cha Mapinduzi, Dk Magufuli aliomba Watanzania wote bila kujali vyama vya siasa, makabila wala dini kumpa kura kwa wingi kwa kuwa atakuwa na washauri wazuri wenye uzoefu.
Alisema wagombea wengine, akiwemo wa Chadema anayeungwa mkono na vyama vinavyounda Ukawa, Edward Lowassa, hawataweza kupata ushauri wa washauri hao kama ilivyo rahisi kwake.
Kutokana na uhakika huo wa washauri wazoefu, Dk Magufuli alisema ndio maana baadhi ya wagombea hao wanaweza kuja na ahadi za uongo, ikiwemo ya kuondoa nyumba za tembe na za nyasi.
Aliwataka wananchi kuwapima wagombea hao katika ahadi zao, kwa kuwa baadhi walikuwepo ndani ya Serikali kwa muda mrefu, lakini walishindwa kuondoa nyumba hizo katika majimbo walikotokea.
Dk Magufuli alisema yeye hataahidi kuondoa nyumba hizo, bali anaahidi kushusha bei ya vifaa vya ujenzi hasa saruji, mabati na misumari, ili wananchi wanaofanya kazi wajenge nyumba bora.
Katika kuongeza idadi ya Watanzania wanaofanya kazi ili kufikia lengo hilo, Dk Magufuli alisema katika kila mtaa na kijiji, serikali yake itatoa Sh milioni 50 kwa ajili ya kuanzisha na kukuza biashara ndogo za wanawake na vijana.
Alisema atataka kila anayefanya kazi apate kipato kizuri kitakachomsaidia kukabiliana na mahitaji ya maisha yake, ikiwemo kujenga nyumba bora kutokana na kushushwa kwa bei za bidhaa za ujenzi. Kwa wakulima, alisema atahakikisha pembejeo sahihi zinatolewa kwa wakati na mazao yatakayovunwa, itakuwa marufuku kwa Serikali kukopa mazao yao.

Mgombea Urais wa CC, Dk John Magufuli akihutubia wananchi wa Morogoro.MGOMBEA urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk John Magufuli ameahidi kunyang’any’a mashamba ambayo yamehodhiwa na watu bila kutumiwa kwa ufugaji wala kilimo, na kuyagawa kwa wakulima na wafugaji wasio na maeneo ya kilimo. Alisema hayo alipozungumza na wananchi wa wilaya za Ulanga na Kilombero mkoani Morogoro jana.
Dk Magufuli alisema akiwa rais, kuna mambo mengi anaweza kufanya, kukabiliana na migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji na mojawapo ni kutoa ardhi zaidi kwaajili ya wakulima na wafugaji, ili kuondoa uhaba wa ardhi, unaosababisha ugomvi wa maeneo ya kulishia mifugo na kulima.
Alisema kuna watu wanamiliki maelfu ya eka za ardhi bila kulima na kwamba atanyang’any’a mashamba hayo ambayo yamehodhiwa na watu hao bila kutumiwa kwa ufugaji wala kilimo. Akihutubia maelfu ya wananchi, pia Dk Magufuli alisema kuwa anajivunia uzoefu wa marais wastaafu wa Awamu ya Pili mpaka Awamu ya Nne na wa Zanzibar, kwamba ndio atakaowafuata kwa ushauri akikwama popote.
Alisema hiyo ni moja ya tofauti kubwa kati yake na wagombea wengine wa urais. “Nitaingia Ikulu nikiwa na washauri wazuri, nikikwama mahali nitakwenda kwa Rais Jakaya Kikwete, nikikwama nitaenda kwa mzee Benjamin Mkapa, nikikwama tena nakwenda kwa mzee Ali Hasan Mwinyi.
“Wako wengi, upo ushauri nitauchukua kutoka kwa mzee Salmin Amour (Rais Mstaafu wa Zanzibar), Dk Ali Mohamed Shein na kwa Amani Abeid Karume,” alisema. Kutokana na fursa hiyo ya kiuongozi aliyonayo ndani ya Chama Cha Mapinduzi, Dk Magufuli aliomba Watanzania wote bila kujali vyama vya siasa, makabila wala dini kumpa kura kwa wingi kwa kuwa atakuwa na washauri wazuri wenye uzoefu.
Alisema wagombea wengine, akiwemo wa Chadema anayeungwa mkono na vyama vinavyounda Ukawa, Edward Lowassa, hawataweza kupata ushauri wa washauri hao kama ilivyo rahisi kwake.
Kutokana na uhakika huo wa washauri wazoefu, Dk Magufuli alisema ndio maana baadhi ya wagombea hao wanaweza kuja na ahadi za uongo, ikiwemo ya kuondoa nyumba za tembe na za nyasi.
Aliwataka wananchi kuwapima wagombea hao katika ahadi zao, kwa kuwa baadhi walikuwepo ndani ya Serikali kwa muda mrefu, lakini walishindwa kuondoa nyumba hizo katika majimbo walikotokea.
Dk Magufuli alisema yeye hataahidi kuondoa nyumba hizo, bali anaahidi kushusha bei ya vifaa vya ujenzi hasa saruji, mabati na misumari, ili wananchi wanaofanya kazi wajenge nyumba bora.
Katika kuongeza idadi ya Watanzania wanaofanya kazi ili kufikia lengo hilo, Dk Magufuli alisema katika kila mtaa na kijiji, serikali yake itatoa Sh milioni 50 kwa ajili ya kuanzisha na kukuza biashara ndogo za wanawake na vijana.
Alisema atataka kila anayefanya kazi apate kipato kizuri kitakachomsaidia kukabiliana na mahitaji ya maisha yake, ikiwemo kujenga nyumba bora kutokana na kushushwa kwa bei za bidhaa za ujenzi. Kwa wakulima, alisema atahakikisha pembejeo sahihi zinatolewa kwa wakati na mazao yatakayovunwa, itakuwa marufuku kwa Serikali kukopa mazao yao.

Wednesday, 2 September 2015

BAADA ya kutoweka hadharani tangu Julai 28, mwaka huu, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbrod Slaa amejitokeza hadharani na kuelezea kilichomsibu, akiweka wazi kwamba amestaafu siasa baada ya chama hicho kumpokea aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa ambaye amesisitiza hawezi kukwepa kashfa ya Richmond.
Dk Slaa aliwaambia waandishi wa habari katika mkutano uliodumu kwa takribani saa mbili katika Hoteli ya Serena, Dar es Salaam jana kuwa Lowassa si kiongozi anayefaa kuwa rais wa nchi kutokana na kuhusika na vitendo vya rushwa na kwamba ni mhusika namba moja katika kashfa ya Richmond, iliyomwondoa madarakani Februari 2008. Tangu Julai 28, wakati Lowassa alipoanza kuonekana katika vikao vya Chadema, Dk Slaa amekuwa haonekani katika vikao vya chama hicho ikiwemo Mkutano Mkuu uliomtangaza Lowassa kuwa mgombea urais wa chama hicho na umoja wa wapinzani (Ukawa) katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka huu.
Mbali ya Mkutano Mkuu, Dk Slaa hakuonekana katika matukio muhimu kama yale ya Lowassa kufika Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuchukua fomu ya kugombea urais na wakati wa kuirejesha, na pia katika mkutano wa uzinduzi wa kampeni kwenye Viwanja vya Jangwani, Agosti 29, mwaka huu.
Katika mkutano wa jana, Dk Slaa alieleza kwa kirefu kilichotokea na kumfanya kupotea katika harakati za Chadema huku akiweka wazi kuwa ujio wa Lowassa ulimfanya ajiuzulu nafasi ya Ukatibu Mkuu, tofauti na madai ya Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe kwamba alikuwa likizo. “Nimejitokeza leo, mimi sikuwa likizo.
Mengi yamesemwa na viongozi wangu, lakini ukweli ni kwamba sikupewa likizo na yeyote, nasisitiza sina barua yoyote ya likizo. “Kilichotokea ni kwamba niliamua kuachana na siasa tangu tarehe 28/7 majira ya saa 3 usiku, baada ya kuona yanayofanyika ndani ya chama changu na sikukubaliana nayo,” alisema Dk Slaa na kuongeza: “Wapo watu wanaosema Dk Slaa alishiriki kutoka mwanzo katika ujio wa Lowassa.
Nilishiriki kweli, lakini niliweka msingi tangu dakika ya kwanza kutaka kujua Lowassa anakuja Chadema kama mali au anakuja kama mzigo? Msimamo wangu huu haukupatiwa majibu na hadi sasa viongozi wa Chadema hawana majibu katika hili.”
Akisimulia mkasa mzima, padri huyo wa zamani wa Kanisa Katoliki alisema baada ya Lowassa kukatwa kwenye mchakato wa kumpata mgombea urais kupitia CCM mjini Dodoma, alipigiwa simu na Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima aliyemwita kuwa mshenga wa Lowassa, akimuarifu hatua hiyo ya kukatwa Lowassa ni mtaji kwa Chadema.
Alisema katika maelekezo yake, Askofu Gwajima alimuelekeza Dk Slaa awasiliane na Mwenyekiti wa Chadema, Mbowe kuhusu mpango huo na kumrejeshea majibu ya kile walichoafikiana na kwamba alitekeleza ombi hilo kwa kuwasiliana na Mbowe na baadaye walimkaribisha Askofu Gwajima ili kuzungumza kwa kina.
“Tangu wakati huo niliweka msimamo wangu. Unajua kwa kawaida ni vizuri kumsikia mtu ana nini na si kutomsikiliza kabisa. Chadema ni chama cha siasa haikatazwi kumpokea mtu. “Niliweka msimamo kwanza atangaze kutoka ndani ya CCM, baada ya kutangaza hilo atangaze pia ni chama gani anakwenda, halafu tatu atumie nafasi hiyo kujisafisha na tuhuma zake anazoshutumiwa.
Niliweka msimamo huo kwa kuamini kuwa Chadema ni chama kilichojijenga katika misingi ya uadilifu na iwapo asingefanya hivyo ni hatari,” alifafanua Dk Slaa aliyegombea urais kwa chama hicho mwaka 2010. Alisema kinyume cha msimamo aliouweka, Lowassa hakutangaza kujitoa CCM na kutangaza anakwenda chama gani kwa wakati huo, lakini pia hakujisafisha hadi alipokuwa katika kikao cha utambulisho Chadema ndipo alipozungumzia suala la Richmond baada ya kuulizwa na waandishi wa habari tena katika hali ya udikteta.
Alisema mbali ya msimamo huo, aliweka msimamo mwingine wa kutaka kujua, Lowassa anakwenda Chadema akiwa ni mali au mzigo, katika kile alichosema ilikuwa ni kutaka kutathmini kama ujio huo wa Lowassa kwa Chadema ungekuwa na manufaa au hasara. “Ujue kwenye biashara au siasa, anayejiunga leo ni lazima mfahamu, je, anakuja kama mali au kama mzigo?
Watu hapa wanasema nilipatwa na hasira kwa vile alipewa nafasi ya kugombea urais, suala si urais, hadi siku hiyo nilikuwa sijachukua fomu ya urais, kama ningekuwa nataka urais ningetangaza au kuchukua fomu kwani jina langu lilishapitishwa na vikao tangu Februari. “Hapa ukweli ni kwamba Slaa alikuwa anataka mgombea mwenye uwezo, sifa na anayeweza kuivusha Chadema kuiondoa CCM.
Hata mwaka 2010 sikujitokeza mimi kugombea urais, bali niliombwa. Urais si wangu, mimi binafsi ni kwa ajili ya watu,” alieleza akifafanua madai hayo ya kuwa alikasirika kwa kutoteuliwa kuwania urais. Alisema kutokana na swali hilo, alijibiwa kwamba Lowassa angekwenda Chadema na wabunge 50 waliokuwa wakimaliza muda wao, wenyeviti wa CCM wa mikoa 22, wenyeviti wa CCM wa wilaya 88, na hivyo aliamini kama ingekuwa hivyo nchi ingeweza kutetemeka.
“Niliweka sharti majina yatajwe, nilifanya vile kwa kuwa Katibu Mkuu makini wa chama hawezi kupokea tu watu, bila kujua ni akina nani na wanagombea wapi maana tulikuwa tayari na mfumo wa kuwaandaa wagombea ndani ya chama, hata hivyo majina hayo sikuyapata. Alisema ilipofika Julai 25, kilifanyika kikao ambacho aliagizwa kuitisha kikao cha Halmashauri Kuu na alipohoji nini kinaenda kuzungumzwa, hakupewa jibu.
Alisema Julai 25, alipigiwa simu na Mbowe ambapo katika mazungumzo yao kwa mara ya kwanza walitofautiana, ingawa alikubali kufika katika kikao alichowakuta Mbowe, Askofu Gwajima na Mwanasheria wao, Tundu Lissu. “Kikao kile kilianza saa 3 asubuhi hadi saa 9 jioni, na tulibishana sana, maana swali langu lilibakia kuwa lile lile, je Lowassa anakuja Chadema kama mali au kama mzigo?
Baada ya pale walisema twende nyumbani kwa Lowassa, lakini nilikataa kwani Lowassa ni mwanachama wa CCM hivyo mimi nisingeweza kwenda. “Tulirejea tena katika kikao kuanzia saa 9 jioni hadi saa 12.30, tukapumzika, lakini hatukuelewana. Wakaunda kamati ndogo ya kuzungumza na mimi na kunishauri, lakini nilikataa. Pale pale niliandika barua ya kujiuzulu nikampa Mwenyekiti wa kikao, Profesa Safari (Abdalah) lakini aliichana pale pale.
“Sikuridhika na hatua hiyo niliandika barua nyingine na kumkabidhi Makamu Mwenyekiti wa Zanzibar ambaye alinijibu kwamba Dk Slaa unajisumbua bure haya mambo yamepangwa. Hata hivyo, kesho yake niliandika barua rasmi ya kujizulu,” alieleza kiongozi huyo aliyeheshimika kwa misimamo yake ndani ya Chadema.
Akizungumzia nini kilifuata baada ya Lowassa kupokelewa Chadema; alisema alikwenda kama mzigo na si mali kwani yeye na wafuasi wake ni watu ambao ama walikataliwa na wananchi katika kura za maoni, au ni ambao wamekuwa wakituhumiwa katika masuala ya ufisadi na hawawezi kukubalika ndani ya jamii.
“Awali niliweka msimamo kwamba wale watakaokuja na Lowassa ni vizuri waje kabla ya kufanyika kura ya maoni, hilo halikuzingatiwa. Dk Mahanga (Makongoro, aliyekuwa Mbunge wa Ukonga na Naibu Waziri wa Kazi na Ajira) huyo ni mali au ni mzigo? Huyo amekataliwa na wananchi hivyo alikuwa anatafuta kichaka cha kujificha. “Hivi Sumaye (Frederick, Waziri Mkuu mstaafu) huyo ni mtu safi kweli. Watu wote wanamfahamu kwamba ni fisadi.
Nilimwita fisadi ndani ya Bunge wakati ule alipopokonya shamba la Magereza Kibaigwa. “Huyu Sumaye ndiye ambaye alisema CCM ikimteua Lowassa atahama chama. Watu wote mnajua Sumaye alikuwa anaitwa nani wakati ule… (kicheko). Leo makapi yametoka CCM yamekwenda Chadema.
Wenyeviti waliondoka ni mizigo, wote tunamjua Msindai (Mgana, aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida na Mwenyekiti wa Wenyeviti wa CCM). “Mimi namfahamu Msindai, alikuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali kabla yangu pale Bungeni alichokifanya ipo siku nitamuweka hadharani.
Mtu ambaye siwezi kumsema ni Mgeja (Khamis, aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Shinyanga)… huyo siwezi kumsema maana simfahamu,” alieleza Dk Slaa. “Kuna mtu anaitwa Chizi, hivi Chizi ni nani? Nilipofuatilia ili kumjua vizuri nikaambiwa eti alikuwa anapanga mipango ya wizi wa kura ndani ya CCM.
Yaani Chadema inampokea mtu kwa vile tu alikuwa mwizi wa kura? Kama tunataka Chadema kuiba kura kuna umuhimu gani wa kuiondoa CCM madarakani? Unaiondoa CCM kwa programu safi serious (makini) na watu serious (makini).”
Kuhusu Richmond, Dk Slaa alisema bado anaamini kuwa Lowassa hawezi kukwepa kashfa hiyo na alionesha na kusoma vielelezo na barua mbalimbali, alizosema zinadhihirisha Lowassa kuwa mpangaji mkuu wa mpango wa ufisadi wa Richmond na kwamba kupokelewa na Chadema, kumekifanya chama hicho kupoteza nguvu ya hoja ya kupambana na ufisadi, hoja aliyosema ilikuwa silaha pekee kwa Chadema.
Dk Slaa alimtaka Waziri Mkuu huyo wa zamani, kujitokeza na kueleza namna alivyohusika na sakata la Richmond, kwa kutaja Richmond ilikuwa kampuni ya nani, na ni wakubwa gani walioshinikiza kutolewa kwa zabuni hiyo ya kufua umeme wa dharura kama alivyodai na kuahidi kutoa taarifa zaidi ya umma kwa suala hilo.

BAADA ya kutoweka hadharani tangu Julai 28, mwaka huu, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbrod Slaa amejitokeza hadharani na kuelezea kilichomsibu, akiweka wazi kwamba amestaafu siasa baada ya chama hicho kumpokea aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa ambaye amesisitiza hawezi kukwepa kashfa ya Richmond.
Dk Slaa aliwaambia waandishi wa habari katika mkutano uliodumu kwa takribani saa mbili katika Hoteli ya Serena, Dar es Salaam jana kuwa Lowassa si kiongozi anayefaa kuwa rais wa nchi kutokana na kuhusika na vitendo vya rushwa na kwamba ni mhusika namba moja katika kashfa ya Richmond, iliyomwondoa madarakani Februari 2008. Tangu Julai 28, wakati Lowassa alipoanza kuonekana katika vikao vya Chadema, Dk Slaa amekuwa haonekani katika vikao vya chama hicho ikiwemo Mkutano Mkuu uliomtangaza Lowassa kuwa mgombea urais wa chama hicho na umoja wa wapinzani (Ukawa) katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka huu.
Mbali ya Mkutano Mkuu, Dk Slaa hakuonekana katika matukio muhimu kama yale ya Lowassa kufika Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuchukua fomu ya kugombea urais na wakati wa kuirejesha, na pia katika mkutano wa uzinduzi wa kampeni kwenye Viwanja vya Jangwani, Agosti 29, mwaka huu.
Katika mkutano wa jana, Dk Slaa alieleza kwa kirefu kilichotokea na kumfanya kupotea katika harakati za Chadema huku akiweka wazi kuwa ujio wa Lowassa ulimfanya ajiuzulu nafasi ya Ukatibu Mkuu, tofauti na madai ya Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe kwamba alikuwa likizo. “Nimejitokeza leo, mimi sikuwa likizo.
Mengi yamesemwa na viongozi wangu, lakini ukweli ni kwamba sikupewa likizo na yeyote, nasisitiza sina barua yoyote ya likizo. “Kilichotokea ni kwamba niliamua kuachana na siasa tangu tarehe 28/7 majira ya saa 3 usiku, baada ya kuona yanayofanyika ndani ya chama changu na sikukubaliana nayo,” alisema Dk Slaa na kuongeza: “Wapo watu wanaosema Dk Slaa alishiriki kutoka mwanzo katika ujio wa Lowassa.
Nilishiriki kweli, lakini niliweka msingi tangu dakika ya kwanza kutaka kujua Lowassa anakuja Chadema kama mali au anakuja kama mzigo? Msimamo wangu huu haukupatiwa majibu na hadi sasa viongozi wa Chadema hawana majibu katika hili.”
Akisimulia mkasa mzima, padri huyo wa zamani wa Kanisa Katoliki alisema baada ya Lowassa kukatwa kwenye mchakato wa kumpata mgombea urais kupitia CCM mjini Dodoma, alipigiwa simu na Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima aliyemwita kuwa mshenga wa Lowassa, akimuarifu hatua hiyo ya kukatwa Lowassa ni mtaji kwa Chadema.
Alisema katika maelekezo yake, Askofu Gwajima alimuelekeza Dk Slaa awasiliane na Mwenyekiti wa Chadema, Mbowe kuhusu mpango huo na kumrejeshea majibu ya kile walichoafikiana na kwamba alitekeleza ombi hilo kwa kuwasiliana na Mbowe na baadaye walimkaribisha Askofu Gwajima ili kuzungumza kwa kina.
“Tangu wakati huo niliweka msimamo wangu. Unajua kwa kawaida ni vizuri kumsikia mtu ana nini na si kutomsikiliza kabisa. Chadema ni chama cha siasa haikatazwi kumpokea mtu. “Niliweka msimamo kwanza atangaze kutoka ndani ya CCM, baada ya kutangaza hilo atangaze pia ni chama gani anakwenda, halafu tatu atumie nafasi hiyo kujisafisha na tuhuma zake anazoshutumiwa.
Niliweka msimamo huo kwa kuamini kuwa Chadema ni chama kilichojijenga katika misingi ya uadilifu na iwapo asingefanya hivyo ni hatari,” alifafanua Dk Slaa aliyegombea urais kwa chama hicho mwaka 2010. Alisema kinyume cha msimamo aliouweka, Lowassa hakutangaza kujitoa CCM na kutangaza anakwenda chama gani kwa wakati huo, lakini pia hakujisafisha hadi alipokuwa katika kikao cha utambulisho Chadema ndipo alipozungumzia suala la Richmond baada ya kuulizwa na waandishi wa habari tena katika hali ya udikteta.
Alisema mbali ya msimamo huo, aliweka msimamo mwingine wa kutaka kujua, Lowassa anakwenda Chadema akiwa ni mali au mzigo, katika kile alichosema ilikuwa ni kutaka kutathmini kama ujio huo wa Lowassa kwa Chadema ungekuwa na manufaa au hasara. “Ujue kwenye biashara au siasa, anayejiunga leo ni lazima mfahamu, je, anakuja kama mali au kama mzigo?
Watu hapa wanasema nilipatwa na hasira kwa vile alipewa nafasi ya kugombea urais, suala si urais, hadi siku hiyo nilikuwa sijachukua fomu ya urais, kama ningekuwa nataka urais ningetangaza au kuchukua fomu kwani jina langu lilishapitishwa na vikao tangu Februari. “Hapa ukweli ni kwamba Slaa alikuwa anataka mgombea mwenye uwezo, sifa na anayeweza kuivusha Chadema kuiondoa CCM.
Hata mwaka 2010 sikujitokeza mimi kugombea urais, bali niliombwa. Urais si wangu, mimi binafsi ni kwa ajili ya watu,” alieleza akifafanua madai hayo ya kuwa alikasirika kwa kutoteuliwa kuwania urais. Alisema kutokana na swali hilo, alijibiwa kwamba Lowassa angekwenda Chadema na wabunge 50 waliokuwa wakimaliza muda wao, wenyeviti wa CCM wa mikoa 22, wenyeviti wa CCM wa wilaya 88, na hivyo aliamini kama ingekuwa hivyo nchi ingeweza kutetemeka.
“Niliweka sharti majina yatajwe, nilifanya vile kwa kuwa Katibu Mkuu makini wa chama hawezi kupokea tu watu, bila kujua ni akina nani na wanagombea wapi maana tulikuwa tayari na mfumo wa kuwaandaa wagombea ndani ya chama, hata hivyo majina hayo sikuyapata. Alisema ilipofika Julai 25, kilifanyika kikao ambacho aliagizwa kuitisha kikao cha Halmashauri Kuu na alipohoji nini kinaenda kuzungumzwa, hakupewa jibu.
Alisema Julai 25, alipigiwa simu na Mbowe ambapo katika mazungumzo yao kwa mara ya kwanza walitofautiana, ingawa alikubali kufika katika kikao alichowakuta Mbowe, Askofu Gwajima na Mwanasheria wao, Tundu Lissu. “Kikao kile kilianza saa 3 asubuhi hadi saa 9 jioni, na tulibishana sana, maana swali langu lilibakia kuwa lile lile, je Lowassa anakuja Chadema kama mali au kama mzigo?
Baada ya pale walisema twende nyumbani kwa Lowassa, lakini nilikataa kwani Lowassa ni mwanachama wa CCM hivyo mimi nisingeweza kwenda. “Tulirejea tena katika kikao kuanzia saa 9 jioni hadi saa 12.30, tukapumzika, lakini hatukuelewana. Wakaunda kamati ndogo ya kuzungumza na mimi na kunishauri, lakini nilikataa. Pale pale niliandika barua ya kujiuzulu nikampa Mwenyekiti wa kikao, Profesa Safari (Abdalah) lakini aliichana pale pale.
“Sikuridhika na hatua hiyo niliandika barua nyingine na kumkabidhi Makamu Mwenyekiti wa Zanzibar ambaye alinijibu kwamba Dk Slaa unajisumbua bure haya mambo yamepangwa. Hata hivyo, kesho yake niliandika barua rasmi ya kujizulu,” alieleza kiongozi huyo aliyeheshimika kwa misimamo yake ndani ya Chadema.
Akizungumzia nini kilifuata baada ya Lowassa kupokelewa Chadema; alisema alikwenda kama mzigo na si mali kwani yeye na wafuasi wake ni watu ambao ama walikataliwa na wananchi katika kura za maoni, au ni ambao wamekuwa wakituhumiwa katika masuala ya ufisadi na hawawezi kukubalika ndani ya jamii.
“Awali niliweka msimamo kwamba wale watakaokuja na Lowassa ni vizuri waje kabla ya kufanyika kura ya maoni, hilo halikuzingatiwa. Dk Mahanga (Makongoro, aliyekuwa Mbunge wa Ukonga na Naibu Waziri wa Kazi na Ajira) huyo ni mali au ni mzigo? Huyo amekataliwa na wananchi hivyo alikuwa anatafuta kichaka cha kujificha. “Hivi Sumaye (Frederick, Waziri Mkuu mstaafu) huyo ni mtu safi kweli. Watu wote wanamfahamu kwamba ni fisadi.
Nilimwita fisadi ndani ya Bunge wakati ule alipopokonya shamba la Magereza Kibaigwa. “Huyu Sumaye ndiye ambaye alisema CCM ikimteua Lowassa atahama chama. Watu wote mnajua Sumaye alikuwa anaitwa nani wakati ule… (kicheko). Leo makapi yametoka CCM yamekwenda Chadema.
Wenyeviti waliondoka ni mizigo, wote tunamjua Msindai (Mgana, aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida na Mwenyekiti wa Wenyeviti wa CCM). “Mimi namfahamu Msindai, alikuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali kabla yangu pale Bungeni alichokifanya ipo siku nitamuweka hadharani.
Mtu ambaye siwezi kumsema ni Mgeja (Khamis, aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Shinyanga)… huyo siwezi kumsema maana simfahamu,” alieleza Dk Slaa. “Kuna mtu anaitwa Chizi, hivi Chizi ni nani? Nilipofuatilia ili kumjua vizuri nikaambiwa eti alikuwa anapanga mipango ya wizi wa kura ndani ya CCM.
Yaani Chadema inampokea mtu kwa vile tu alikuwa mwizi wa kura? Kama tunataka Chadema kuiba kura kuna umuhimu gani wa kuiondoa CCM madarakani? Unaiondoa CCM kwa programu safi serious (makini) na watu serious (makini).”
Kuhusu Richmond, Dk Slaa alisema bado anaamini kuwa Lowassa hawezi kukwepa kashfa hiyo na alionesha na kusoma vielelezo na barua mbalimbali, alizosema zinadhihirisha Lowassa kuwa mpangaji mkuu wa mpango wa ufisadi wa Richmond na kwamba kupokelewa na Chadema, kumekifanya chama hicho kupoteza nguvu ya hoja ya kupambana na ufisadi, hoja aliyosema ilikuwa silaha pekee kwa Chadema.
Dk Slaa alimtaka Waziri Mkuu huyo wa zamani, kujitokeza na kueleza namna alivyohusika na sakata la Richmond, kwa kutaja Richmond ilikuwa kampuni ya nani, na ni wakubwa gani walioshinikiza kutolewa kwa zabuni hiyo ya kufua umeme wa dharura kama alivyodai na kuahidi kutoa taarifa zaidi ya umma kwa suala hilo.

MGOMBEA urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk John Magufuli amesema Serikali atakayoiongoza baada ya kuchaguliwa, itapandisha mishahara ya watumishi wote wa umma ilingane na ile ya Wakala wa Taifa wa Barabara (Tanroads), ambayo aliianzisha na kuwapa wafanyakazi wake mishahara minono.
Hata hivyo, Dk Magufuli alisema baada ya kuongeza mishahara hiyo, wafanyakazi lazima wachape kazi na kuonya kuwa wasipofanya hivyo atapambana nao. Aidha, amesema Serikali atakayoiongoza, itapunguza bei ya vifaa vya ujenzi, hasa saruji na mabati.
Alisema hayo jana katika mikutano midogo aliyofanya njiani alikokuwa akisimamishwa na wananchi wakati alipokuwa akitoka Songea, kupitia Namtumbo na Tunduru kwenda Masasi mkoani Mtwara.
Dk Magufuli alisema mkoani Mtwara tayari ujenzi umeanza wa kiwanda cha saruji ambacho ndio kikubwa kuliko vyote Afrika Mashariki na Kati na kikikamilika, kitazalisha saruji nyingi na kupunguza bei ya bidhaa hiyo muhimu ya ujenzi.
Alisema kusudio la kushusha bei ya vifaa hivyo ni kusaidia wananchi wajenge nyumba nzuri na bora za makazi kwa ajili ya kuboresha maisha yao. Kuhusu kuboresha kipato cha wananchi ili wafanikishe azma ya kutumia punguzo la bei za bidhaa za ujenzi na kujenga nyumba bora, Dk Magufuli alisema umeme umeanza kufika katika maeneo hayo na Serikali yake itahakikisha vijijini kunajengwa viwanda vidogo vitakavyotoa ajira vijijini.
Mbali na ajira, pia aliahidi kutoa Sh milioni 50 kwa kila kijiji na kila mtaa, kwa ajili ya kuanzisha na kuendeleza miradi midogo midogo ya kujipatia kipato kwa ajili ya wanawake na vijana.

MGOMBEA urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk John Magufuli amesema Serikali atakayoiongoza baada ya kuchaguliwa, itapandisha mishahara ya watumishi wote wa umma ilingane na ile ya Wakala wa Taifa wa Barabara (Tanroads), ambayo aliianzisha na kuwapa wafanyakazi wake mishahara minono.
Hata hivyo, Dk Magufuli alisema baada ya kuongeza mishahara hiyo, wafanyakazi lazima wachape kazi na kuonya kuwa wasipofanya hivyo atapambana nao. Aidha, amesema Serikali atakayoiongoza, itapunguza bei ya vifaa vya ujenzi, hasa saruji na mabati.
Alisema hayo jana katika mikutano midogo aliyofanya njiani alikokuwa akisimamishwa na wananchi wakati alipokuwa akitoka Songea, kupitia Namtumbo na Tunduru kwenda Masasi mkoani Mtwara.
Dk Magufuli alisema mkoani Mtwara tayari ujenzi umeanza wa kiwanda cha saruji ambacho ndio kikubwa kuliko vyote Afrika Mashariki na Kati na kikikamilika, kitazalisha saruji nyingi na kupunguza bei ya bidhaa hiyo muhimu ya ujenzi.
Alisema kusudio la kushusha bei ya vifaa hivyo ni kusaidia wananchi wajenge nyumba nzuri na bora za makazi kwa ajili ya kuboresha maisha yao. Kuhusu kuboresha kipato cha wananchi ili wafanikishe azma ya kutumia punguzo la bei za bidhaa za ujenzi na kujenga nyumba bora, Dk Magufuli alisema umeme umeanza kufika katika maeneo hayo na Serikali yake itahakikisha vijijini kunajengwa viwanda vidogo vitakavyotoa ajira vijijini.
Mbali na ajira, pia aliahidi kutoa Sh milioni 50 kwa kila kijiji na kila mtaa, kwa ajili ya kuanzisha na kuendeleza miradi midogo midogo ya kujipatia kipato kwa ajili ya wanawake na vijana.

Thursday, 6 August 2015



Ama kweli Mbeya City msimu huu imepania, kwani imetangaza kula sahani moja na Yanga katika maandalizi yao ya Ligi Kuu Tanzania Bara. Unajua ikoje? Uongozi wa timu hiyo umesema unajua Yanga na Azam zimejifua vilivyo kupitia Kagame, lakini hiyo haiwapi shida kwani nao watatumia wiki zilizosalia kufanya yao mapema ili wafunike katika ligi.
Uongozi huo umesema moja ya mikakati yao ni kucheza mechi kadhaa za kimataifa na klabu toka nje ya nchi za Zesco ya Zambia na Bata Bullets ya Malawi ambazo zitacheza pia na Yanga hivi karibuni jijini Mbeya.
Kabla ya kucheza mechi hizo za kirafiki za kimataifa, Mbeya City itaanza na Yanga, Agosti 18, jijini Mbeya ambako Wanajangwani wataweka kambi kwa ajili ya kujiandaa na mechi ya Ngao ya Jamii dhidi ya Azam.
Katibu Mkuu wa timu hiyo, Emmanuel Kimbe alisema wapo kwenye mazungumzo na timu hizo ambazo pia zitacheza mechi za kirafiki na Yanga na kwamba wana asilimia kubwa ya kufanikisha mpango huo.
“Tunajua changamoto ambazo tutakabiliana nazo kwa Yanga na Azam, katika ligi maana hizo zimepata muda wa kujipima uwezo kwenye Kagame ndio maana tunataka kujifua kupitia timu zenye uwezo,” alisema.
Kimbe alisema pia katika mechi hizo zitawasaidia kujua uwezo wa wachezaji wao na kutambua kombeneshani, hivyo wanajifanya mazoezi kuhakikisha kile wanachokitarajia kinatimia.



Ama kweli Mbeya City msimu huu imepania, kwani imetangaza kula sahani moja na Yanga katika maandalizi yao ya Ligi Kuu Tanzania Bara. Unajua ikoje? Uongozi wa timu hiyo umesema unajua Yanga na Azam zimejifua vilivyo kupitia Kagame, lakini hiyo haiwapi shida kwani nao watatumia wiki zilizosalia kufanya yao mapema ili wafunike katika ligi.
Uongozi huo umesema moja ya mikakati yao ni kucheza mechi kadhaa za kimataifa na klabu toka nje ya nchi za Zesco ya Zambia na Bata Bullets ya Malawi ambazo zitacheza pia na Yanga hivi karibuni jijini Mbeya.
Kabla ya kucheza mechi hizo za kirafiki za kimataifa, Mbeya City itaanza na Yanga, Agosti 18, jijini Mbeya ambako Wanajangwani wataweka kambi kwa ajili ya kujiandaa na mechi ya Ngao ya Jamii dhidi ya Azam.
Katibu Mkuu wa timu hiyo, Emmanuel Kimbe alisema wapo kwenye mazungumzo na timu hizo ambazo pia zitacheza mechi za kirafiki na Yanga na kwamba wana asilimia kubwa ya kufanikisha mpango huo.
“Tunajua changamoto ambazo tutakabiliana nazo kwa Yanga na Azam, katika ligi maana hizo zimepata muda wa kujipima uwezo kwenye Kagame ndio maana tunataka kujifua kupitia timu zenye uwezo,” alisema.
Kimbe alisema pia katika mechi hizo zitawasaidia kujua uwezo wa wachezaji wao na kutambua kombeneshani, hivyo wanajifanya mazoezi kuhakikisha kile wanachokitarajia kinatimia.


Wachezaji saba; Jonas Mkude, Abdi Banda, Peter Mwalyanzi, Mwinyi Kazimoto, Said Ndemla, Awadh Juma na Emmanuel Mtambuka wote hawapumui huku wakiletewa tena Mzimbabwe Justine Majabvi ambaye inaelezwa kwamba muda wowote huenda akamwaga wino Msimbazi.

SIMBA inatarajiwa kurejea leo Alhamisi jijini Dar es Salaam baada ya wiki mbili za kujifua visiwani Zanzibar, lakini tayari wachezaji wa timu hiyo hasa viungo wakiwa kwenye vita kubwa ya kuwania namba.
Ushindani mkubwa uliopo katika nafasi hiyo umewafanya wachezaji hao kuwa macho kwa hofu kwamba mtu akizubaa tu, lazima ile kwake.
Wachezaji saba; Jonas Mkude, Abdi Banda, Peter Mwalyanzi, Mwinyi Kazimoto, Said Ndemla, Awadh Juma na Emmanuel Mtambuka wote hawapumui huku wakiletewa tena Mzimbabwe Justine Majabvi ambaye inaelezwa kwamba muda wowote huenda akamwaga wino Msimbazi.
Baadhi ya wachezaji hao wamekiri kwamba ndani ya Simba kwa sasa ni amsha amsha mwanzo mwisho na hakuna kulala kwa sababu ushindani ni mkubwa na kila mmoja anapenda kumridhisha kocha, Dylan Kerr.
Mkude ambaye ni miongoni mwa wanaocheza kati sambamba na Ndemla na Mtambuka, alisema Msimbazi kwa sasa hakulaliki kwa namna ushindani ulivyoongezeka huku viungo wa pembeni Mwalyanzi na Awadh Juma ambao wanamudu vyema kucheza kwenye nafasi mbalimbali za kiungo, nao wakisema hivyo hivyo.
“Haitakuwa rahisi kwa mchezaji yeyote kupata namba kama hatojituma kwenye mazoezi, hii ni kwa sababu kila mchezaji ana hamu ya kucheza kwenye kikosi cha kwanza cha Simba,” alisema Mkude.
Hata hivyo jambo hilo limemfurahisha Kerr aliyesema kuwa ushindani na uwepo wa viungo wengi, unampa nafasi ya kupata ushindi kwenye kila mchezo.
“Nina viungo wengi, hii ndiyo silaha yangu ya ushindi. Kwanza nataka ushindani, lakini pia nataka niwe na uwezo wa kutumia viungo nitakavyo ninapokuwa nikitumia mifumo mbalimbali tofauti. Kama mchezo utahitaji viungo watano basi nitakuwa nao, kama ni wanne au watatu basi natakiwa kuwa nao ambao ni imara,” alisema Kerr.
VIONGOZI WATIBUA
Katika hatua nyingine, Kocha wa Viungo wa timu hiyo, Mserbia Dusan Momcilovic akichukizwa na ongezeko la wachezaji wapya kwenye kikosi chake Kerr akisema hatamwonea haya yeyote atakayeshindwa kuonesha uwezo ndani ya kipindi hiki.
Kerr alisema: “Wachezaji wanazidi kuja, sijapendekeza yeyote, lakini niko tayari kuwaangalia na ambaye hataniridhisha sitamkubali.
“Mfano ikitokea yeyote akashindwa kuonesha uwezo sitaweza kuwa naye. Nataka mchezaji mwenye kiwango kizuri, mwenye uwezo mkubwa wa kuisaidia Simba na awe wa kuitendea haki jezi ya Simba.”
1 |


Wachezaji saba; Jonas Mkude, Abdi Banda, Peter Mwalyanzi, Mwinyi Kazimoto, Said Ndemla, Awadh Juma na Emmanuel Mtambuka wote hawapumui huku wakiletewa tena Mzimbabwe Justine Majabvi ambaye inaelezwa kwamba muda wowote huenda akamwaga wino Msimbazi.

SIMBA inatarajiwa kurejea leo Alhamisi jijini Dar es Salaam baada ya wiki mbili za kujifua visiwani Zanzibar, lakini tayari wachezaji wa timu hiyo hasa viungo wakiwa kwenye vita kubwa ya kuwania namba.
Ushindani mkubwa uliopo katika nafasi hiyo umewafanya wachezaji hao kuwa macho kwa hofu kwamba mtu akizubaa tu, lazima ile kwake.
Wachezaji saba; Jonas Mkude, Abdi Banda, Peter Mwalyanzi, Mwinyi Kazimoto, Said Ndemla, Awadh Juma na Emmanuel Mtambuka wote hawapumui huku wakiletewa tena Mzimbabwe Justine Majabvi ambaye inaelezwa kwamba muda wowote huenda akamwaga wino Msimbazi.
Baadhi ya wachezaji hao wamekiri kwamba ndani ya Simba kwa sasa ni amsha amsha mwanzo mwisho na hakuna kulala kwa sababu ushindani ni mkubwa na kila mmoja anapenda kumridhisha kocha, Dylan Kerr.
Mkude ambaye ni miongoni mwa wanaocheza kati sambamba na Ndemla na Mtambuka, alisema Msimbazi kwa sasa hakulaliki kwa namna ushindani ulivyoongezeka huku viungo wa pembeni Mwalyanzi na Awadh Juma ambao wanamudu vyema kucheza kwenye nafasi mbalimbali za kiungo, nao wakisema hivyo hivyo.
“Haitakuwa rahisi kwa mchezaji yeyote kupata namba kama hatojituma kwenye mazoezi, hii ni kwa sababu kila mchezaji ana hamu ya kucheza kwenye kikosi cha kwanza cha Simba,” alisema Mkude.
Hata hivyo jambo hilo limemfurahisha Kerr aliyesema kuwa ushindani na uwepo wa viungo wengi, unampa nafasi ya kupata ushindi kwenye kila mchezo.
“Nina viungo wengi, hii ndiyo silaha yangu ya ushindi. Kwanza nataka ushindani, lakini pia nataka niwe na uwezo wa kutumia viungo nitakavyo ninapokuwa nikitumia mifumo mbalimbali tofauti. Kama mchezo utahitaji viungo watano basi nitakuwa nao, kama ni wanne au watatu basi natakiwa kuwa nao ambao ni imara,” alisema Kerr.
VIONGOZI WATIBUA
Katika hatua nyingine, Kocha wa Viungo wa timu hiyo, Mserbia Dusan Momcilovic akichukizwa na ongezeko la wachezaji wapya kwenye kikosi chake Kerr akisema hatamwonea haya yeyote atakayeshindwa kuonesha uwezo ndani ya kipindi hiki.
Kerr alisema: “Wachezaji wanazidi kuja, sijapendekeza yeyote, lakini niko tayari kuwaangalia na ambaye hataniridhisha sitamkubali.
“Mfano ikitokea yeyote akashindwa kuonesha uwezo sitaweza kuwa naye. Nataka mchezaji mwenye kiwango kizuri, mwenye uwezo mkubwa wa kuisaidia Simba na awe wa kuitendea haki jezi ya Simba.”
1 |

Rais Jakaya Kikwete akiwa na majaji wapya 13 wa Mahakama Kuu na mmoja wa Mahakama ya Rufaa baada ya kuwaapisha Ikulu, Dar es Salaam jana. Kutoka kulia (wenye suti nyeusi) ni Waziri wa Sheria na Katiba, Dk Asha-Rose Migiro, Jaji Kiongozi, Shaban Lila, Jaji Mkuu, Mohamed Chande Othman na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue (kushoto). (Na Mpigapicha Wetu).
Rais Jakaya Kikwete akiwa na Majaji 13 wa Mahakama Kuu na mmoja wa Mahakama ya Rufaa  baada ya kuwaapisha Ikulu, Dar es Salaam jana. Kutoka kulia (wenye suti nyeusi) ni Waziri wa Sheria na Katiba, Dk Asha-Rose Migiro, Jaji Kiongozi, Shaban Lila, Jaji Mkuu, Mohamedi Chande Otman na Katibu Mkuu Kiongozi Omben Sefu.

JAJI Mkuu wa Tanzania, Mohammed Othman Chande amesema kitendo cha Rais Jakaya Kikwete kufanya uteuzi wa mara kwa mara wa majaji nchini, kimeongezea kwa kiasi kikubwa utendaji wa Idara ya Mahakama na hadi sasa kuna Majaji takribani 100, jambo ambalo halijawahi kutokea miaka ya nyuma.
Aidha, ameahidi kutokana na wingi wao, sasa wana uhakika wa kuongeza uchapaji kazi na kwa kuanzia, wameweka lengo kwamba, kesi zote katika Mahakama Kuu na Mahakama ya Biashara zisiendeshwe zaidi ya miezi 10.
Jaji Chande alikuwa akizungumza na waandishi wa habari Ikulu, Dar es Salaam jana mara baada ya Rais Kikwete kuapisha Majaji wa Mahakama Kuu 13 na Jaji mmoja wa Mahakama ya Rufani. “Tunamshukuru Rais kwa ongezeko hili la majaji ambalo sasa linaifanya Tanzania kuwa na majaji 100, hawa ni wengi haijawahi kutokea,” alisisitiza.
Alisema ongezeko hilo, litasaidia sekta hiyo kushughulikia tatizo la mlundikano wa kesi hasa katika kanda za Mahakama Kuu, ambazo kwa muda mrefu zimekuwa zikielemewa na kesi nyingi.
Alitaja kanda ambazo zina mzigo wa kesi nyingi, ambazo sasa zitapunguziwa mzigo huo kutokana na ongezeko hilo la majaji kuwa ni Kanda ya Mahakama Kuu ya Bukoba, ambayo Jaji mmoja alikuwa akishughulikia kesi 3,000 na Mwanza jaji mmoja kesi 600.
Aidha, alisema ongezeko hilo litasaidia maeneo mengine yenye kesi nyingi pia, ambayo ni Tabora na vitengo vya Mahakama Kuu kama vile Idara ya kazi, Ardhi na Biashara. Alisema tayari sekta ya Mahakama ilishajiwekea mikakati ya kushughulikia changamoto zinazoikabili sekta hiyo, ikiwa ni pamoja na kubadilisha ratiba, ambapo kwa upande wa Majaji walipangiwa Jaji mmoja sasa kusikiliza kesi 220, Hakimu Mkazi wa wilaya na Mkoa kesi 250 na Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo kesi 260.
“Kila Mahakama pia imewekewa malengo yake na lengo kubwa ni kuhakikisha kesi hazichukui muda mrefu kusikilizwa, kwa mfano kwa mujibu wa mabadiliko haya kitengo cha Biashara cha Mahakama Kuu kesi zake hazitosikilizwa kwa muda wa zaidi ya miezi 10 hadi mwaka mmoja,” alisisitiza.
Aliwataka majaji walioteuliwa na kuapishwa jana kutambua kuwa waliteuliwa katika nyadhifa hizo, kutokana na utendaji, uzoefu na uadilifu wao, hivyo wanapaswa kuhakikisha wanadumisha sifa hizo katika utendaji wao.
Alisema kabla ya majaji hao hawajaanza rasmi kazi, wataandaliwa mafunzo maalum ili waweze kuendana na utaratibu wa kimahakama kwa kuwa kati ya majaji hao, watano walikuwa mawakili wa kujitegemea, watano mawakili wa Serikali na watano walikuwa mahakamani.
Akizungumzia suala la uchaguzi, Chande, alisema tayari wamejipanga kuhakikisha kuwa kesi za uchaguzi zinasikilizwa kwa haki na muda ambapo hazitosikilizwa kwa zaidi ya miezi sita.
Kuhusu Majaji waliotuhumiwa kupatiwa mgawo wa fedha za akaunti ya Escrow, alisema tume iliyoundwa kufanya uchunguzi na upelelezi, tayari imekamisha upelelezi wake wa awali na itakapokamilisha kuuandaa, itaukabidhi rasmi kwa mamlaka ya uteuzi (Rais) kwa hatua zaidi.
Majaji hao ni Profesa Eudes Ruhangisa anayedaiwa kupata Sh milioni 400.25 na Aloysius Mujulizi Sh milioni 40.4. Awali, akizungumza na gazeti hili kuhusu uteuzi wake, Jaji wa Mahakama Kuu Ignas Kitusi, alisema kuna mipango mingi ya kuboresha huduma za Mahakama, ambapo aliahidi pamoja na wenzake kutekeleza mipango hiyo ikiwemo kurejesha imani ya wananchi dhidi ya Mahakama ambayo kwa sasa imepotea.
Jaji wa Mahakama Kuu, Rehema Kirefu, alisema uteuzi wa Rais wa majaji utasaidia haki kutendeka kwa haraka, kwani uchache wa majaji ulisababisha kesi nyingi kuchelewa kutokana na majaji waliopo kuzidiwa.
Jaji Salima Chikoyo alisema ana uzoefu wa muda mrefu na amefanikiwa kutumikia vitengo mbalimbali hivyo aliwataka wananchi wategemee kupata haki. Majaji wengine waliapishwa jana ni jaji wa Mahakama ya Rufani Richard Mziray na Majaji wa Mahakama Kuu ambao ni Lameck Mlacha, Wilfred Dysobera, Isaya Harufani, Julisu Malaba, Victoria Makani, Lucia Kairo, Benhaj Masoud, Issa Maige, Adam Mambi na Sirilius Matupa.

Rais Jakaya Kikwete akiwa na majaji wapya 13 wa Mahakama Kuu na mmoja wa Mahakama ya Rufaa baada ya kuwaapisha Ikulu, Dar es Salaam jana. Kutoka kulia (wenye suti nyeusi) ni Waziri wa Sheria na Katiba, Dk Asha-Rose Migiro, Jaji Kiongozi, Shaban Lila, Jaji Mkuu, Mohamed Chande Othman na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue (kushoto). (Na Mpigapicha Wetu).
Rais Jakaya Kikwete akiwa na Majaji 13 wa Mahakama Kuu na mmoja wa Mahakama ya Rufaa  baada ya kuwaapisha Ikulu, Dar es Salaam jana. Kutoka kulia (wenye suti nyeusi) ni Waziri wa Sheria na Katiba, Dk Asha-Rose Migiro, Jaji Kiongozi, Shaban Lila, Jaji Mkuu, Mohamedi Chande Otman na Katibu Mkuu Kiongozi Omben Sefu.

JAJI Mkuu wa Tanzania, Mohammed Othman Chande amesema kitendo cha Rais Jakaya Kikwete kufanya uteuzi wa mara kwa mara wa majaji nchini, kimeongezea kwa kiasi kikubwa utendaji wa Idara ya Mahakama na hadi sasa kuna Majaji takribani 100, jambo ambalo halijawahi kutokea miaka ya nyuma.
Aidha, ameahidi kutokana na wingi wao, sasa wana uhakika wa kuongeza uchapaji kazi na kwa kuanzia, wameweka lengo kwamba, kesi zote katika Mahakama Kuu na Mahakama ya Biashara zisiendeshwe zaidi ya miezi 10.
Jaji Chande alikuwa akizungumza na waandishi wa habari Ikulu, Dar es Salaam jana mara baada ya Rais Kikwete kuapisha Majaji wa Mahakama Kuu 13 na Jaji mmoja wa Mahakama ya Rufani. “Tunamshukuru Rais kwa ongezeko hili la majaji ambalo sasa linaifanya Tanzania kuwa na majaji 100, hawa ni wengi haijawahi kutokea,” alisisitiza.
Alisema ongezeko hilo, litasaidia sekta hiyo kushughulikia tatizo la mlundikano wa kesi hasa katika kanda za Mahakama Kuu, ambazo kwa muda mrefu zimekuwa zikielemewa na kesi nyingi.
Alitaja kanda ambazo zina mzigo wa kesi nyingi, ambazo sasa zitapunguziwa mzigo huo kutokana na ongezeko hilo la majaji kuwa ni Kanda ya Mahakama Kuu ya Bukoba, ambayo Jaji mmoja alikuwa akishughulikia kesi 3,000 na Mwanza jaji mmoja kesi 600.
Aidha, alisema ongezeko hilo litasaidia maeneo mengine yenye kesi nyingi pia, ambayo ni Tabora na vitengo vya Mahakama Kuu kama vile Idara ya kazi, Ardhi na Biashara. Alisema tayari sekta ya Mahakama ilishajiwekea mikakati ya kushughulikia changamoto zinazoikabili sekta hiyo, ikiwa ni pamoja na kubadilisha ratiba, ambapo kwa upande wa Majaji walipangiwa Jaji mmoja sasa kusikiliza kesi 220, Hakimu Mkazi wa wilaya na Mkoa kesi 250 na Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo kesi 260.
“Kila Mahakama pia imewekewa malengo yake na lengo kubwa ni kuhakikisha kesi hazichukui muda mrefu kusikilizwa, kwa mfano kwa mujibu wa mabadiliko haya kitengo cha Biashara cha Mahakama Kuu kesi zake hazitosikilizwa kwa muda wa zaidi ya miezi 10 hadi mwaka mmoja,” alisisitiza.
Aliwataka majaji walioteuliwa na kuapishwa jana kutambua kuwa waliteuliwa katika nyadhifa hizo, kutokana na utendaji, uzoefu na uadilifu wao, hivyo wanapaswa kuhakikisha wanadumisha sifa hizo katika utendaji wao.
Alisema kabla ya majaji hao hawajaanza rasmi kazi, wataandaliwa mafunzo maalum ili waweze kuendana na utaratibu wa kimahakama kwa kuwa kati ya majaji hao, watano walikuwa mawakili wa kujitegemea, watano mawakili wa Serikali na watano walikuwa mahakamani.
Akizungumzia suala la uchaguzi, Chande, alisema tayari wamejipanga kuhakikisha kuwa kesi za uchaguzi zinasikilizwa kwa haki na muda ambapo hazitosikilizwa kwa zaidi ya miezi sita.
Kuhusu Majaji waliotuhumiwa kupatiwa mgawo wa fedha za akaunti ya Escrow, alisema tume iliyoundwa kufanya uchunguzi na upelelezi, tayari imekamisha upelelezi wake wa awali na itakapokamilisha kuuandaa, itaukabidhi rasmi kwa mamlaka ya uteuzi (Rais) kwa hatua zaidi.
Majaji hao ni Profesa Eudes Ruhangisa anayedaiwa kupata Sh milioni 400.25 na Aloysius Mujulizi Sh milioni 40.4. Awali, akizungumza na gazeti hili kuhusu uteuzi wake, Jaji wa Mahakama Kuu Ignas Kitusi, alisema kuna mipango mingi ya kuboresha huduma za Mahakama, ambapo aliahidi pamoja na wenzake kutekeleza mipango hiyo ikiwemo kurejesha imani ya wananchi dhidi ya Mahakama ambayo kwa sasa imepotea.
Jaji wa Mahakama Kuu, Rehema Kirefu, alisema uteuzi wa Rais wa majaji utasaidia haki kutendeka kwa haraka, kwani uchache wa majaji ulisababisha kesi nyingi kuchelewa kutokana na majaji waliopo kuzidiwa.
Jaji Salima Chikoyo alisema ana uzoefu wa muda mrefu na amefanikiwa kutumikia vitengo mbalimbali hivyo aliwataka wananchi wategemee kupata haki. Majaji wengine waliapishwa jana ni jaji wa Mahakama ya Rufani Richard Mziray na Majaji wa Mahakama Kuu ambao ni Lameck Mlacha, Wilfred Dysobera, Isaya Harufani, Julisu Malaba, Victoria Makani, Lucia Kairo, Benhaj Masoud, Issa Maige, Adam Mambi na Sirilius Matupa.

Profesa Lipumba akizungumza na waandishi wa habari.
Profesa Lipumba akizungumza na waandishi wa habari.

MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi CUF, Profesa Ibrahim Lipumba amejiuzulu rasmi wadhifa wake huo ndani ya chama kwa kikle alichokitaja kuwa ni kukiukwa kwa Katiba ya chama hicho.
Kujiuzulu huko kunahitimisha wasiwasi wa muda sasa ndani ya chama chake kuhusu hatima yake kutokana na sababu ambazo hazikujulikana mara moja.Profesa Lipumba alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa chama mwaka 1999 na kugombea urais katika vipindi viinne ambavyo vyote alishindwa.
Tutawaletea habari kamili hivi punde.

Profesa Lipumba akizungumza na waandishi wa habari.
Profesa Lipumba akizungumza na waandishi wa habari.

MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi CUF, Profesa Ibrahim Lipumba amejiuzulu rasmi wadhifa wake huo ndani ya chama kwa kikle alichokitaja kuwa ni kukiukwa kwa Katiba ya chama hicho.
Kujiuzulu huko kunahitimisha wasiwasi wa muda sasa ndani ya chama chake kuhusu hatima yake kutokana na sababu ambazo hazikujulikana mara moja.Profesa Lipumba alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa chama mwaka 1999 na kugombea urais katika vipindi viinne ambavyo vyote alishindwa.
Tutawaletea habari kamili hivi punde.

Sunday, 2 August 2015

DR. SLAA WIFE IS A REASON FOR HIS RESIGNATION, Scholars described The rumors Saying Dr.. Slaa ... resignation in politics is allegedly his wife Pressure 
While rumors of resignation in title and left membership of the Party for Democracy and Development (Chadema), Dr. Wilbroad Slaa, having been circulating in social networks and newspapers, reports suggest that the reason to take such action is a pressure from his wife.

Information published by the newspaper quoting . Dr. Slaa himself, stated he left politics and left his post and will remain doing other activities.

. Dr. Slaa is alleged disagrees with the way his party welcomed a former Prime Minister Edward Lowassa.
Surely Infomation from our sources of information within Chadema claim, Dr. Dr. Slaa was involved in the process of welcoming and ratify Lowassa, stopped being a presidential candidate through the Citizens Constitutional Union (Ukawa).

However, another source of information claims to be the wife of . Dr. Slaa, Josephine Mashumbusi she pressured to resign after the husband of another candidate to allow the suspension (Lowassa).
"Josephine was sure her husband's presidential candidacy is one that stands on the side of Ukawa, the situation has changed, she was angry and told her husband either him or Chadema," the source added.

DR. SLAA WIFE IS A REASON FOR HIS RESIGNATION, Scholars described The rumors Saying Dr.. Slaa ... resignation in politics is allegedly his wife Pressure 
While rumors of resignation in title and left membership of the Party for Democracy and Development (Chadema), Dr. Wilbroad Slaa, having been circulating in social networks and newspapers, reports suggest that the reason to take such action is a pressure from his wife.

Information published by the newspaper quoting . Dr. Slaa himself, stated he left politics and left his post and will remain doing other activities.

. Dr. Slaa is alleged disagrees with the way his party welcomed a former Prime Minister Edward Lowassa.
Surely Infomation from our sources of information within Chadema claim, Dr. Dr. Slaa was involved in the process of welcoming and ratify Lowassa, stopped being a presidential candidate through the Citizens Constitutional Union (Ukawa).

However, another source of information claims to be the wife of . Dr. Slaa, Josephine Mashumbusi she pressured to resign after the husband of another candidate to allow the suspension (Lowassa).
"Josephine was sure her husband's presidential candidacy is one that stands on the side of Ukawa, the situation has changed, she was angry and told her husband either him or Chadema," the source added.

AZAM FC jana iliweka historia kwa kutwaa kwa mara ya kwanza taji la Kagame baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Gor Mahia ya Kenya katika fainali iliyopigwa kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
Ubingwa huo wa Azam FC umemaliza ubabe wa Yanga na Simba kwa Tanzania kutwaa taji hilo, ambalo limechukuliwa na wekundu wa Msimbazi mara sita huku vijana wa Jangwani wakilitwaa mara tano.
Mbali na kumaliza ubabe wa vigogo hivyo, Azam FC pia imeweka historia nyingine baada ya kumaliza mashindano hayo bila ya kufungwa bao hata moja kuanzia mwanzo wa mashindano hayo hadi mwisho.
Pia, Azam imemaliza ukame wa taji hilo ililonusurika kulitwaa mwaka 2012 ilipofungwa na Yanga 2-0 katika fainali iliyofanyika kwenye Uwanja wa Taifa. Katika mchezo huo, Azam FC ndio walikuwa wa kwanza kulifikia lango la Gor Mahia mara mbili mwanzoni kabisa mwa mchezo, kabla wapinzani wao hawajajibu wakati Medieval Kagere alipotaka kufunga.
Dakika ya 15 John Bocco aliipatia Azam bao la kwanza akimalizia krosi ya Kipre Tchetche. Muda mfupi kabla ya mapumziko, Azam FC ilionekana kupungukia nguvu na kuifanya Gor Mahia kufanya mashambulizi ya mara kwa mara katika lango la wapinzani wake hao.
Dakika ya 51 Azam nusura wapige bao la pili baada ya Tchetche kupiga shuti kali lililogonga mwamba wa pembeni na mpira kurudi uwanjani kabla haojaokolewa. Juhudi za Azam zilizaa matunda wakati Tchetche alipoipatia timu yake bao la pili baada ya kupiga mpira wa adhabu uliokwenda moja kwa moja wavuni ukimuacha kipa wa Gor Mahia Boniface Oluoch akidua bila la kufanya.
Mwamuzi alitoa adhabu hiyo baada ya Shomari Kapombe kuchezewa rafu na Aucho Khalid aliyeoneshwa kadi ya njano kwa mchezo huo mbaya. Azam FC wangeweza kufunga la tatu kama sio kukosa umakini kwa mchezaji wake, Didier Kavumbagu baada ya kukosa bao la wazi katika dakika ya 90 wakati alipopaisha mpira.
Vikosi: Azam FC: Aishi Manula, John Bocco, Aggrey Morris, Said Morad, Pascal Wawa, Jean Mugiraneza, Humid Mao, Farid Mussa/ Erasto Nyoni, Amme Ali/Frank Domayo, Shomari Kapombe na Kipre Tchetche. Gor Mahia: Boniface Oluoch, Mussa Mohamed, Sibomana Abouba, Harun Shakava, Karim Nizigayamana, Innocent Wafula, Such Khalid, Godfrey Walusimbi, Kagere Medie, Michael Olunga na Erick Ochieng.

AZAM FC jana iliweka historia kwa kutwaa kwa mara ya kwanza taji la Kagame baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Gor Mahia ya Kenya katika fainali iliyopigwa kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
Ubingwa huo wa Azam FC umemaliza ubabe wa Yanga na Simba kwa Tanzania kutwaa taji hilo, ambalo limechukuliwa na wekundu wa Msimbazi mara sita huku vijana wa Jangwani wakilitwaa mara tano.
Mbali na kumaliza ubabe wa vigogo hivyo, Azam FC pia imeweka historia nyingine baada ya kumaliza mashindano hayo bila ya kufungwa bao hata moja kuanzia mwanzo wa mashindano hayo hadi mwisho.
Pia, Azam imemaliza ukame wa taji hilo ililonusurika kulitwaa mwaka 2012 ilipofungwa na Yanga 2-0 katika fainali iliyofanyika kwenye Uwanja wa Taifa. Katika mchezo huo, Azam FC ndio walikuwa wa kwanza kulifikia lango la Gor Mahia mara mbili mwanzoni kabisa mwa mchezo, kabla wapinzani wao hawajajibu wakati Medieval Kagere alipotaka kufunga.
Dakika ya 15 John Bocco aliipatia Azam bao la kwanza akimalizia krosi ya Kipre Tchetche. Muda mfupi kabla ya mapumziko, Azam FC ilionekana kupungukia nguvu na kuifanya Gor Mahia kufanya mashambulizi ya mara kwa mara katika lango la wapinzani wake hao.
Dakika ya 51 Azam nusura wapige bao la pili baada ya Tchetche kupiga shuti kali lililogonga mwamba wa pembeni na mpira kurudi uwanjani kabla haojaokolewa. Juhudi za Azam zilizaa matunda wakati Tchetche alipoipatia timu yake bao la pili baada ya kupiga mpira wa adhabu uliokwenda moja kwa moja wavuni ukimuacha kipa wa Gor Mahia Boniface Oluoch akidua bila la kufanya.
Mwamuzi alitoa adhabu hiyo baada ya Shomari Kapombe kuchezewa rafu na Aucho Khalid aliyeoneshwa kadi ya njano kwa mchezo huo mbaya. Azam FC wangeweza kufunga la tatu kama sio kukosa umakini kwa mchezaji wake, Didier Kavumbagu baada ya kukosa bao la wazi katika dakika ya 90 wakati alipopaisha mpira.
Vikosi: Azam FC: Aishi Manula, John Bocco, Aggrey Morris, Said Morad, Pascal Wawa, Jean Mugiraneza, Humid Mao, Farid Mussa/ Erasto Nyoni, Amme Ali/Frank Domayo, Shomari Kapombe na Kipre Tchetche. Gor Mahia: Boniface Oluoch, Mussa Mohamed, Sibomana Abouba, Harun Shakava, Karim Nizigayamana, Innocent Wafula, Such Khalid, Godfrey Walusimbi, Kagere Medie, Michael Olunga na Erick Ochieng.

Mwenye kuelewa ataelewa habari ndo iyooo!

Mwenye kuelewa ataelewa habari ndo iyooo!

WAZIRI wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wasira (pichani), ameshinda kura za maoni za CCM, baada ya kupata kura 6,429 na kumshinda mpinzani wake wa karibu ambaye ni mjasiriamali, Robert Maboto aliyepata kura 6,206.
Akitangaza matokeo hayo jana katika ofisi ya CCM ya Wilaya ya Bunda, Mkurugenzi wa uchaguzi katika wilaya hiyo, Magreth Mtatiro, alisema Wassira alishinda kwa zaidi ya kura 223 kati ya kura zote zilizopigwa 15, 262.
Mtatiro alimtangaza mshindi wa tatu kuwa ni Mwenyekiti wa CCM mkoani Mara, Christopher Sanya aliyepata kura 1,140, ambapo wengine ni pamoja na Exavery Lugina aliyepata kura 846, Simon Odunga (547), Magesa Mugeta (446), Peres Magiri (385) na Burian Bitaa (263).
Kutokana na matokeo hayo, Mtatiro alimtangaza Waziri Wasira ambaye anatetea tena nafasi hiyo, kuwa mshindi katika kinyang’anyiro hicho cha kura za maoni. Wakati huohuo, mbunge aliyemaliza muda wake katika jimbo la Mwibara Kangi Lugola (pichani kulia), ameshinda uchaguzi katika kura za maoni za chama hicho na kumshinda kwa kura nyingi mpinzani wake wa karibu, Charles Kajege aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo hilo.

WAZIRI wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wasira (pichani), ameshinda kura za maoni za CCM, baada ya kupata kura 6,429 na kumshinda mpinzani wake wa karibu ambaye ni mjasiriamali, Robert Maboto aliyepata kura 6,206.
Akitangaza matokeo hayo jana katika ofisi ya CCM ya Wilaya ya Bunda, Mkurugenzi wa uchaguzi katika wilaya hiyo, Magreth Mtatiro, alisema Wassira alishinda kwa zaidi ya kura 223 kati ya kura zote zilizopigwa 15, 262.
Mtatiro alimtangaza mshindi wa tatu kuwa ni Mwenyekiti wa CCM mkoani Mara, Christopher Sanya aliyepata kura 1,140, ambapo wengine ni pamoja na Exavery Lugina aliyepata kura 846, Simon Odunga (547), Magesa Mugeta (446), Peres Magiri (385) na Burian Bitaa (263).
Kutokana na matokeo hayo, Mtatiro alimtangaza Waziri Wasira ambaye anatetea tena nafasi hiyo, kuwa mshindi katika kinyang’anyiro hicho cha kura za maoni. Wakati huohuo, mbunge aliyemaliza muda wake katika jimbo la Mwibara Kangi Lugola (pichani kulia), ameshinda uchaguzi katika kura za maoni za chama hicho na kumshinda kwa kura nyingi mpinzani wake wa karibu, Charles Kajege aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo hilo.

Jackson assesses each Reds player on the day.
HELSINKI, FINLAND - Friday, July 31, 2015: Liverpool's players line up for a team group photograph before a friendly match against HJK Helsinki at the Olympic Stadium. Back row L-R: James Milner, Joe Gomez, Dejan Lovren, Martin Skrtel, goalkeeper Simon Mignolet, Jordon Ibe. Front row L-R: Danny Ings, Adam Lallana, captain Jordan Henderson, Philippe Coutinho Correia, Nathaniel Clyne. (Pic by David Rawcliffe/Propaganda)
HJK Helsinki 0-2 Liverpool
Friendly – Olympic Stadium, Helsinki – Saturday, 1st August 2015
Goals: Origi (73), Coutinho (78)
Simon Mignolet — 6 (out of 10)
As has been the case so often this summer, the 27-year-old is barely worthy of a rating because he was barely called upon at any point. Six out of 10 seems fair though.
Nathaniel Clyne — 6
The former Southampton right-back has had a solid but unspectacular pre-season, and it was much of the same from the 24-year-old against Helsinki.
He was solid defensively, but didn’t offer a huge amount going forward.
Martin Skrtel — 6
Like Mignolet, Skrtel was never really tested at any point, but produced a reliable performance. Bigger tests will certainly come for the Slovakian.
Dejan Lovren — 6
The Croatian has taken plenty of flack lately, but he enjoyed a low-key and solid afternoon in Finland. The Britannia Stadium next Sunday will be a very different test, however, if he starts ahead of Mamadou Sakho.
Football - Liverpool FC Preseason Tour 2015 - HJK Helsinki v Liverpool FC
Joe Gomez — 6
The 18-year-old has had a fabulous summer, but he was less noticeable during a dull affair against Helsinki.
He didn’t get forward as effectively as in previous games, but never did anything wrong defensively at any point.
Jordan Henderson — 6.5
Liverpool’s new skipper was one of his side’s more energetic players, using the ball well and providing box-to-box running throughout. One of the best players at the club now.
James Milner — 7
The ex-Man City man was very impressive on the whole, offering typical industry in the middle of the park and playing a key role in Philippe Coutinho‘s goal.
He’s looking like a superb signing.
Philippe Coutinho — 7
It was great to see Coutinho back following an extended summer break, and unpredictably, he looked the most talented player on the pitch.
Although the 23-year-old didn’t necessarily produce huge amounts of note, he oozed class from start to finish. Scored the Reds’ second with a deflected shot.
Football - Liverpool FC Preseason Tour 2015 - HJK Helsinki v Liverpool FC
Jordon Ibe — 7
The exciting 19-year-old once again looked one of the Reds’ most formidable players, running at the Helsinki defence with pace, power and trickery.
He had the beating of the Helsinki left-back time and time again, and could have a massive 2015/16 season ahead of him.
Adam Lallana — 6
Lallana has been one of Liverpool’s most creative players this summer, but he was more subdued against Saturday’s opponents.
He flitted in and out of the game, without creating much of note.
Danny Ings — 6.5
The Englishman pressed very impressively throughout proceedings, and despite not looking a great threat, the 23-year-old looked a pest at all times.
Could prove to be be a very underrated signing.
Football - Liverpool FC Preseason Tour 2015 - HJK Helsinki v Liverpool FC
Substitutes
Divock Origi (on for Ings ’63) — 6.5
The Belgian was introduced midway through the second-half, and gave Liverpool the lead with a well-taken finish.
Joe Maguire (on for Gomez ’81) — n/a
No time to make an impact.
Pedro Chirivella (on for Coutinho ’81) — n/a
No time to make an impact.

Jackson assesses each Reds player on the day.
HELSINKI, FINLAND - Friday, July 31, 2015: Liverpool's players line up for a team group photograph before a friendly match against HJK Helsinki at the Olympic Stadium. Back row L-R: James Milner, Joe Gomez, Dejan Lovren, Martin Skrtel, goalkeeper Simon Mignolet, Jordon Ibe. Front row L-R: Danny Ings, Adam Lallana, captain Jordan Henderson, Philippe Coutinho Correia, Nathaniel Clyne. (Pic by David Rawcliffe/Propaganda)
HJK Helsinki 0-2 Liverpool
Friendly – Olympic Stadium, Helsinki – Saturday, 1st August 2015
Goals: Origi (73), Coutinho (78)
Simon Mignolet — 6 (out of 10)
As has been the case so often this summer, the 27-year-old is barely worthy of a rating because he was barely called upon at any point. Six out of 10 seems fair though.
Nathaniel Clyne — 6
The former Southampton right-back has had a solid but unspectacular pre-season, and it was much of the same from the 24-year-old against Helsinki.
He was solid defensively, but didn’t offer a huge amount going forward.
Martin Skrtel — 6
Like Mignolet, Skrtel was never really tested at any point, but produced a reliable performance. Bigger tests will certainly come for the Slovakian.
Dejan Lovren — 6
The Croatian has taken plenty of flack lately, but he enjoyed a low-key and solid afternoon in Finland. The Britannia Stadium next Sunday will be a very different test, however, if he starts ahead of Mamadou Sakho.
Football - Liverpool FC Preseason Tour 2015 - HJK Helsinki v Liverpool FC
Joe Gomez — 6
The 18-year-old has had a fabulous summer, but he was less noticeable during a dull affair against Helsinki.
He didn’t get forward as effectively as in previous games, but never did anything wrong defensively at any point.
Jordan Henderson — 6.5
Liverpool’s new skipper was one of his side’s more energetic players, using the ball well and providing box-to-box running throughout. One of the best players at the club now.
James Milner — 7
The ex-Man City man was very impressive on the whole, offering typical industry in the middle of the park and playing a key role in Philippe Coutinho‘s goal.
He’s looking like a superb signing.
Philippe Coutinho — 7
It was great to see Coutinho back following an extended summer break, and unpredictably, he looked the most talented player on the pitch.
Although the 23-year-old didn’t necessarily produce huge amounts of note, he oozed class from start to finish. Scored the Reds’ second with a deflected shot.
Football - Liverpool FC Preseason Tour 2015 - HJK Helsinki v Liverpool FC
Jordon Ibe — 7
The exciting 19-year-old once again looked one of the Reds’ most formidable players, running at the Helsinki defence with pace, power and trickery.
He had the beating of the Helsinki left-back time and time again, and could have a massive 2015/16 season ahead of him.
Adam Lallana — 6
Lallana has been one of Liverpool’s most creative players this summer, but he was more subdued against Saturday’s opponents.
He flitted in and out of the game, without creating much of note.
Danny Ings — 6.5
The Englishman pressed very impressively throughout proceedings, and despite not looking a great threat, the 23-year-old looked a pest at all times.
Could prove to be be a very underrated signing.
Football - Liverpool FC Preseason Tour 2015 - HJK Helsinki v Liverpool FC
Substitutes
Divock Origi (on for Ings ’63) — 6.5
The Belgian was introduced midway through the second-half, and gave Liverpool the lead with a well-taken finish.
Joe Maguire (on for Gomez ’81) — n/a
No time to make an impact.
Pedro Chirivella (on for Coutinho ’81) — n/a
No time to make an impact.