HATUTAKUBALI UCHAGUZI 2015 UFANYIKE KWA KATIBA YA SASA
Ni maneno yaliyokaririwa na viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA),
wamesema hawako tayari kushiriki Uchaguzi Mkuu ujao wa mwaka kesho huku
nchi ikiwa na Katiba ya zamani, hivyo Jumatatu wanatarajiwa kuingia
katika mazungumzo kunusuru mchakato mzima wa Katiba.
Wameeleza
kuwa, kwa kutambua muda mfupi uliobaki kati ya mchakato wa Katiba
kumalizika na Uchaguzi Mkuu, watafanya mazungumzo hayo kwa faida ya
Taifa na wananchi waliojitokeza kwa
wingi kuwasihi warejee katika Bunge Maalumu la Katiba linalotarajiwa
kurejea kwa siku 60 kuanzia Agosti 5, mwaka huu.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, mmoja wa viongozi wa umoja huo ambaye
ni Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, Freeman Mbowe alisema nina yasema
haya kwa niaba ya Mchumi bingwa duniani Prof Ibrahim Lipumba na James
Mbatia wana imani kuwa taifa linahitaji Katiba mpya hivyo watajadili
katika mazungumzo hayo ya Jumatatu ili kuwawezesha kupata njia mbadala
iwapo mchakato huo utakwama.
“Napenda kuwataarifu wananchi kuwa
Ukawa tuko tayari kwa mazungumzo kwa nia ya kunusuru mchakato wa Katiba
kuendelea kama walivyotusihi watu mbalimbali, lakini tutaenda katika
mazungumzo hayo Jumatatu kwa kuhakikisha mchakato huo hautanajisiwa,”
alisema Freeman Mbowe.
Saturday, 19 July 2014
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment